Mgongo wa paka
JF-Expert Member
- Oct 3, 2011
- 485
- 36
Kwa mujibu wa waziri lukuvi alipoongea ktk moja ya sherehe zina zokaribisha sherehe kuu ya kutimiza miaka 50 ya uhuru. Anasema wakati tukipata uhuru mtanzania alipata shilingi 770 kwa mwaka huyo mtanzania wa chini. Leo mtanzania anapata anapata shilingi laki saba na sabini elfu. Kwa kujiamini na akionekana akifurahia kuwa pato la mtanzania limeongezeka. Sasa shilingi 770 wakati huo ilikuwa sawa na dola 770. Kwa mahesabu ya haraka mtanzania alipata shilingi milioni moja na lakimbili na hamsini elfu. Kabla ya uhuru na wakati wa uhuru. Lakini leo mtanzania anapata shilingi laki saba na sabini elfu halafu lukuvi anafurahi patao la mtanzania kushuka jamani nivema tuwe wakweli ili tutatue hili tatizo la kushuka kipato cha mtanzania tujiulize wapi tumejikwaa ili tuongeze hilo pato la mtanzani tuwe wazalendo.