Ufugaji wa Samaki: Pata ushauri, mawazo na michango kuhusu ufugaji samaki. Jifunze changamoto, utaalamu na masoko ya Samaki

Ok basi naweza kufanya mautundu Kutengeneza la simtank.. Nitakata hata mara bili.....!
Inawezekana pia, au waweza chimba kibwawa chako ukubwa unaotaka, badala ya kusakafia unatumia zile plastic liner ili kutoruhusu maji kunyonywa na udongo.

Hizi karatasi za plastic waweza zipata kwa urahisi zipo maduka mengi mjini
 
Nimesikia ufugaji wa Samaki kwa kutumia bwawa dogo la plastiki nyumbani ni mkombozi tosha wa Maisha. Nahitaji msaada wenu wadau. Je bwawa hilo la plastic liwe na vipimo gani? Hayo maplastic yanauzwa bei gani?

Ni kweli samaki wanafugika kwenye tank za plastic; ila plastic pekee halitoshi, maana hewa iliyomo kwenye maji inakwisha kadri samaki wanavyoinyonya kama sehemu ya upumuaji.

Pia maji ya kwenye tank yatachafuliwa taratibu kwa kinyesi cha hao samaki.
Utahitajika ama uwe unabadili maji mara kwa mara ili ipatikane hewa mpya kwenye maji hayo mapya ambayo pia yatakuwa hayana kinyesi cha samaki.

Kuna utaratibu wa aina mbili wa kutumia maji hayo hayo (na nyongeza kidogo nadhani---bado najifunza kwa kusoma tu). Utaratibu huu unatoa uchafu wa kinyesi na unarudisha hewa safi kwenye maji.

Ingia Youtube, halafu tafuta 1. RAS---Recirculating Aquaculture System na 2. Aquaponic System.
Ni mafunzo marefu na nadhani magumu kwa sisi ambao ndio kwanza tunawaza kuingia katika ufugaji wa samaki kwa njia ya ma-tank. Lakini hakuna wepesi pale unapotaka kujiletea maendeleo, lazima kupambana.
 
Mkuu mleta mada naomba kujua kwanini vifaranga vya kambare vinabei kubwa yaani 500?wakati sato ni 300?
 
Wana JF

Tanzania imebarikiwa kuwa na vyanzo vya maji ya asili ikiwemo mito, mabwawa, maziwa, bahari, chemchem nk. Kutokana na vyanzo hivi tunapata samaki wa aina mbalimbali wakiwemo perege/sato, kambale, kambamiti (prawns), vibua, changu, kaa n.k.

Samaki ni chanzo cha lishe, kipato na ajira, tunaweza tukatengeneza vito kutokana na lulu wa chaza. Nimejaribu kuzungukia katika soko letu la fery pale nikagundua akina mama na wadau wengi wanafaidika sana na biashara ya samaki nadhani tunawaona mitaani kwetu lakini wanalalamika bei imekuwa juu na upatikanaji wake ni wa shida sana kulingana na msimu.

Nilijaribu kufuatilia kwa undani suala hili kwa wizara husika nikaelezwa ni kweli bei ya samaki iko juu na upatikanaji wake ni mgumu kutokana na samaki wamepungua kwa kiasi kikubwa na wanapungua kwa kasi ya ajabu...Hali hii inatokana na mabadiliko ya hali ya hewa, uharibifu wa mazingira, nguvu kubwa ya uvuvi iliyopo kwa mfano samaki sangara kutoka ziwa victoria wamepungua sana na wanaopatikana kwa sasa ni wadogo. Pia wizara ililazimika kufunga uvuvi wa prawns kwa meli kubwa kubwa kutokana na hali kuwa mbaya. Hata perege wanaopatikana ni wadogo na kwa uchache.

Ili kuokoa suala hili, njia pekee ni kuhamasisha UFUGAJI WA SAMAKI kwa ajili ya kipato, ajira na chakula. Nimevutiwa na suala hili nikaona niwashirikishe wana JF. Nchi za asia china, ufilipino, japan, indonesia fani hii imekuwa sana na wananchi wanajikwamua kiuchumi kutokana na ufugaji wa samaki.

Bado ninafanya ufuatiliaji wa karibu kuhusu suala hili la ufugaji samaki na jinsi tunavyoweza kufaidika nalo. Ninaamini tunaweza kufuga na kupata faida kubwa pia tukatunza mazingira yetu ya asili.

Wakati naendelea kufuatilia suala hili naomba mwenye taarifa basi tushirikiane hapa JF. Nitarudi tena kwa maada hii mara nitakapokusanya taarifa ndani ya siku chache.

Nawasilisha kwa michango yenu.

Nteko Vano Maputo

Penye nia pana njia

--------------------------

Uvuvi%2Bbusega%2B4.jpg



-----------------------------






*Nakala na vitabu juu ya Ufugaji wa Samaki DOWNLOAD Attachments
Ati sehemu kama Mbeya Kwenye Baridi baridi waeza funga samaki aina ya Sato.!?
 
Ati sehemu kama Mbeya Kwenye Baridi baridi waeza funga samaki aina ya Sato.!?
NDIO UNAFUGA VIZURI TU, NIMEONA KWA MACHO YANGU KAMBALE PALE TUKUYU MWAKA JANA, WAKATI ZAMANI NILIAMINI KUWA KAMBALE NI WA MAJI JOTO.
 
natamani sana kufuga samaki,je maeneo ya rufiji yanafaa?na upatikanaji wa maji vibali naazaje?na mtaji wa wastani sh ngapi ili uweze uza kwa faida angalau?
 
  • gharama kwa ujumla kama mimi nataka kufuga kulimo cha biashara . gharama average(general) zinakuwaje?
  • na sehemu ninapoweza pata hao samaki wa kuanzia? nipo morogoro.
 
Back
Top Bottom