Ufugaji wa Samaki: Pata ushauri, mawazo na michango kuhusu ufugaji samaki. Jifunze changamoto, utaalamu na masoko ya Samaki

Habari wadau je zile nylon za kufugia samaki kuna aliyewahi zitumia, kuna changamoto zozote ukilinganisha na kuchimba na kujengea. Nilitaka kuanza ufugaji mdogo kwa kutumia liner badala ya kujengea. Ushauri please
 
Habari wadau je zile nylon za kufugia samaki kuna aliyewahi zitumia, kuna changamoto zozote ukilinganisha na kuchimba na kujengea. Nilitaka kuanza ufugaji mdogo kwa kutumia liner badala ya kujengea. Ushauri please

Kwanza kwa wadau wote wa huu uzi waliotamani field tour wanisamehe kwa sasa nimekwama kidogo ,nimekutana na changamoto ya upatikanaji wa maji na ardhi inanyonya maji sana.

Tumetumia pesa nyingi sana(karibia 30m)so far na bado project iko utotoni kabisa.Na mara ya kwanza i never thought this project was huge(mabwawa 6 ya square meter 400 kila moja).

So im looking for partners now wa kusonga nao mbele zaidi sababu hapo nahitaji either liner au kujengea kwa cement which are both equally expensive.Na pia kuchimba maji(sio changamoto sana)

Lakini unaweza kutumia nylon za kawaida(Sisi wa Itabagumba Sengerema tunaita kavelo)ila uwe makini na zile pindo inapopita uzi na overlap za hizo nylon zisipitishe maji na zinakaa for at least 2 years, wakati zile zenyewe special zinakaa kama miaka 10 hivi ila zina bei balaa,Balton Tanzania wanazo.
 
Kwanza kwa wadau wote wa huu uzi waliotamani field tour wanisamehe kwa sasa nimekwama kidogo ,nimekutana na changamoto ya upatikanaji wa maji na ardhi inanyonya maji sana.

Tumetumia pesa nyingi sana(karibia 30m)so far na bado project iko utotoni kabisa.Na mara ya kwanza i never thought this project was huge(mabwawa 6 ya square meter 400 kila moja).

So im looking for partners now wa kusonga nao mbele zaidi sababu hapo nahitaji either liner au kujengea kwa cement which are both equally expensive.Na pia kuchimba maji(sio changamoto sana)

Lakini unaweza kutumia nylon za kawaida(Sisi wa Itabagumba Sengerema tunaita kavelo)ila uwe makini na zile pindo inapopita uzi na overlap za hizo nylon zisipitishe maji na zinakaa for at least 2 years, wakati zile zenyewe special zinakaa kama miaka 10 hivi ila zina bei balaa,Balton Tanzania wanazo.
asante sana miaka 2 ni tosha kwa kuanzia project ikikua nitatumia hizo za balton. Kkoo nilikuta 12x4m ni 150,000 nitajitaidi kuleta feedback nikifanikiwa
Kwanza kwa wadau wote wa huu uzi waliotamani field tour wanisamehe kwa sasa nimekwama kidogo ,nimekutana na changamoto ya upatikanaji wa maji na ardhi inanyonya maji sana.

Tumetumia pesa nyingi sana(karibia 30m)so far na bado project iko utotoni kabisa.Na mara ya kwanza i never thought this project was huge(mabwawa 6 ya square meter 400 kila moja).

So im looking for partners now wa kusonga nao mbele zaidi sababu hapo nahitaji either liner au kujengea kwa cement which are both equally expensive.Na pia kuchimba maji(sio changamoto sana)

Lakini unaweza kutumia nylon za kawaida(Sisi wa Itabagumba Sengerema tunaita kavelo)ila uwe makini na zile pindo inapopita uzi na overlap za hizo nylon zisipitishe maji na zinakaa for at least 2 years, wakati zile zenyewe special zinakaa kama miaka 10 hivi ila zina bei balaa,Balton Tanzania wanazo.
 
UFUGAJI WA SAMAKI

Tasnia ya ufugaji wa samaki inajumuisha ukuzaji wa viumbe vya kwenye maji (bahari na maji baridi) katika mazingira tofauti na yale ya asili. Lengo kuu ni kukuza kwa muda mfupi ili kujipatia lishe, kipato na kutunza mazingira ya bahari, mito, maziwa nk.
Ufugaji unagusa viumbe vya kwenye maji kuanzia mimea kama vile mwani, samaki wasio na mapezi (kaa-crabs, kambamiti-prawns, chaza-oyster, majongoo bahari nk) na samaki wenye mapezi (perege/sato, kambale, kibua, trout, chewa nk).

Aina ya ufugaji

Zifuatazo ni aina/level za ufugaji ambazo mkulima anaweza kufanya kulingana na malengo na uwezo wake:

1. Huria (Extensive farming)

• Idadi ya samaki wanaopandikizwa: samaki 2-3 kwa mita ya mraba
• Samaki hutegemea chakula cha asili (mimea ya majini-phytoplankton, wadudu/viumbe vidogo vya majini-zooplankton)
• Hauitaji ubadilishaji wa maji
• Hauihitaji huduma ya ziada ya hewa

2. Kati ya huria na nusu shadidi (Modified extensive)  Idadi ya samaki, 4-7 kwa mita ya mraba

• Chakula cha asili na chakula cha ziada huitajika
• Maji hubadilishwa sentimenta 10-20 kila baada ya 3-4weeks kulingana na hali ya samaki na maji yako
• Huduma ya hewa ya ziada sio ya ulazima

3. Nusu shadidi (Semi-intensive)

• Idadi ya samaki kwa mita ya mraba ni 10-25
• Chakula cha asili na cha ziada
• Huduma ya hewa ya ziada lazima
• Maji hubadilishwa kila siku au kila baada ya siku kadhaa (15-25 cm)

4. Shadidi (Intensive)

• Idadi ya samaki ni zaidi ya 25 kwa mita ya mraba
• 100% chakula cha kutengenezwa
• Maji ni kuingia na kutoka
• Hewa ya ziada masaa yote
• Eneo linalotumika ni dogo ukilinganisha na mifumo mingine

Miundombinu ya ufugaji

Samaki wanaweza kufugwa katika miundombinu mbalimbali kama ifuatayo:

• Bwawa
• Kina 0.8-1.5m
• Ukubwa 100 mita za mraba- 1ha

• Matanki

Umbo-mstatili au mviringo nk
Kina 1-1.5m
Kipenyo kwa lile la mduara 3-10m
Ukubwa kwa la mstatili inategemea na uwezo lakini lisiwe kubwa ili kuhimili nguvu ya maji
Materials: Plastic, cement, chuma nk
NB: Simtank linafaa( Faida inapatikana kama utalitumia kwa intensive system)

Vizimba (Fish cages)
Huwekwa katika maji ya asili kama vile ziwani, baharini au katika bwawa. Vipo vinavyoundwa kwa local materials kama mianzi na vipo vya aluminium.

Eneo linalofaa kwa ufugaji

Baadhi ya maeneo yanayofaa ni yale mashamba ya mpunga, na maeneo yaliyo karibu na vyanzo vya maji. Zifuatazo ni sifa za maeneo yanayofaa:

1. Udongo: Mfinyanzi husaidia kupunguza gharama za ujenzi wa bwawa na maji kwakuwa linaweza kutuamisha maji na kuruhusu maji yasipotee. Likiwa la kichanga bwawa ni lazima lijengewe au kuwekwa nylon sheet ili kuzuia upotevu wa maji. Unaweza ukahamisha udongo wa mfinyanzi kutoka sehemu moja hadi nyingine ili kuzuia upotevu wa maji (muone mtaalamu kwa ushauri zaidi juu ya mbinu ya kuhamisha udongo).

2. Chanzo cha maji ya uhakika
Eneo liwe na maji ya uhakika. Vyanzo vya maji ni kama vile mito, bahai, maziwa, chem chem., kisima, maji ya dawasco na mvua. Maji yasiwe na kemikali hatarishi kwa viumbe.

3. Miundombinu ya barabara: Inasaidia kwa ajili ya usafirishaji wa bidhaa na samaki wakati wa kuvuna.
4. Eneo lisiwe na historia ya mafuriko ili kuzuia athari za mafuriko kwa miundombinu yako. Utatumia gharama nyingi katika kuimarisha miundombinu yako.Jamii/aina ya samaki
5. Eneo lenye mwinuko wa wastani husaidia katika ujenzi wa bwawa.
6. Miundombinu ya umeme ni sifa ya ziada hususan kwa mkulima wa kati na wajuu kwa ajili ya kutumika katika kuendesha visambaza hewa.
7. Ulinzi muhimu

Note: Aina ya eneo lako ndilo linaweza kukufanya uchague muundombinu gani wa kufugia utumie

Aina ya samaki unaoweza kufuga Tanzania kwa sasa
Maji baridi

Sato/perege, Kambale, Kambamiti wa maji baridi na Trout (maeneo ya baridi kama vile Iringa, Kilimanjaro Arusha na Mbeya) na samaki wa mapambo.

Maji bahari

Kambamiti wa maji bahari, mwatiko, chewa, kaa, chaza wa lulu

Upatikanaji wa Vifaranga vya samaki husika

Vyanzo vya vifaranga ni kutoka katika mito, bahari, maziwa na wale wa kuzalishwa katika vituo vya kuzalishia vifaranga.

Sato na Kambale

Vituo vya serikali Utapata sato wa kike na kiume mixed sex). Kingolwira –Morogoro, LuhiraSongea, Mbegani-Bagamoyo . Kifaranga huuzwa Tsh. 50-100 kwa kifaranga.

Vituo binafsi kama vile Faith aquaculture-Kibamba (DSM) (utapata monosex sato), PeramihoSongea (mixed sex). Monosex huuzwa Tsh. 200 kwa kifaranga, na mixed ni 100 kwa kifaranga.

Trout

Mayai huagizwa toka Marekani, Israel
Kambamiti wa baharini Alphakrust –Mafia.

Chakula cha samaki

Chakula cha asili

Hurutubishwa kwa mbolea ya wanyama kama vile kuku, ngombe, mbuzi nk. Kwa kiwango cha 1000kg/ha. Mbolea ya kuku ni kali hivyo unaweza punguza ikawa 250-500kg/ha.

Chakula cha kutengeneza

Samaki huitaji protein ili akuwe na kila samaki ana mahitaji yake hivyo ni species specific. Formula zipo kwa wale wanaotaka kutengeneza. Tanzania hakuna kiwanda kinachotengeneza. Ingredients zake ni kama vile dagaa, pumba, soya, unga wa ngano, unga wa muhongo nk.

Uvunaji

Kwa kawaida ni miezi 4-6 amabapo unapata 250-400g kulingana na ulishaji wako. Kwa prawns ni miezi 3-6 wanafikia 30-50g ambayo ni ukubwa wa soko.

Tathmini ya uchumi

Perege/sato Mfano:

Ukubwa wa bwawa ni 20m by 30m= 600 mita za mraba
Idadi ya samaki (7 kwa mita ya mraba) kwa monosex tu= 600 x 7=4200 fish
Uzito hadi kuvuna (4-6months)- 250g= 4200 x 250g= 1050kg (Nimesha convert gram to kg) Bei kwa kilo ni 6000-8000 kulingana na mahali=6milion-8milion.

Gharama unazoweza kutumia
Ujenzi wa bwawa
Kuchimba kwa vibarua ni 500,000-600,000
Kuchimba kwa machine ni 1,000,000-1,500,000 kulinganana mahali ulipo

Kama udongo ni kichanga itabidi ujengee (kujengea ni gharama na inaweza ikafika 3.5-4m kwa gharama zote kuanzia kuchimba hadi kujengea).

Chakula
cha kutengeneza tani 1 inaweza kugharimu laki 7-9. Hapa ili uweze kuzalisha tani 1 ya samaki aina ya perege utahitaji tani 1-1.5 ya chakula.
Gharama ya vibarua 150,000-250,000 kwa mwezi.
Utakuwa na gharama ya chokaa kwa ajili ya kuua vidudu (laki 100,000-200,000), mbolea kuzalisha chakula cha asili (gharama ni 50,000).

Jinsi ya kuhudumia bwawa, kuandaa chakula nitaandaa tips zingine.
Ha Muji
 
Ndugu mwanajamii,
Karibu sana mimi nafuga Samaki na ninao utakaaa wa kutosha juu ya ufugaji wa Samaki aina ya sato(Tilapia) Karibu sana tunaweza share.
 
Uchimbaji wa bwana unategemea na ukubwa wa bwawa,ukitaka kazi na bwawa likae vizuri inakuhitaji uwe na excavators ila pia wapo watu wanachimba ila wanachukua mda mrefu sana. Kwa mfano nimechimba na excavator size ya 43mx15m kwa shilling 700,000 arusha.
Aisee ARUSHA maeneo gani nije kujifunza kwasababu na mimi nahitaji sana hiyo biashara.Mimi nipo Moshi.
 
Samaki tunafuga kwenye mabwawa yetu

ImageUploadedByJamiiForums1462458459.196065.jpg
 
1. Unahitaji uwe na eneo lenye maji ya kutosha au uwe na kisima kirefu ambacho kina uwezo wa kutoa maji masaa yote.

2.Upate mtalaamu mzuri wa kuchimba Kisima chenye Urefu wa mita 1.5 ( pref excavator).

3. Ukishachimba inategemea aina ya udongo uliopo ( soil texture) kama sehemu ina chemi chemi ni nzuri unaweza tengeneza matuta tu halafu maji yakajaa yenyewe

4. Unapaswa kupata mbegu nzuri iliyoandaliwa vizuri na yenye kukua.

5.ulishaji wa hao Samaki ni muhimu kuangalia sana hasa kipindi wanavyokuwa bado vifaranga
Hayo ndiyo muhimu kwanza
 
Hawa wana gm 480-500 tumewafuga miezi 8 sasa lakini hawa ni wazazi ndio maana wanakua taratibu kwa sababu tunavuna mayai Ili tupate vifaranga, kwa hiyo kila mara wiki wanasumbuliwa ingekuwa madume kwa ajili ya mboga yamkini wangekuwa wana uzito mkubwa hata gm 800 au zaidi
 
Back
Top Bottom