Pata ufahamu na elimu dhidi ya ugonjwa wa Mafindofindo (Tonsils)

Mahesabu

JF-Expert Member
Jan 27, 2008
5,972
3,830
1603606438357.png


BAADHI YA MASWALI YALIYOULIZWA KUHUSU UGONJWA HUU
Ugonjwa huu ambao kwa kiswahili zoelefu unajulikana kama "Mafindofindo" hivi sasa umevamia watu wengi nikiwemo na mimi mwenyewe.

Dalili nilizoanza nazo ni homa,kichwa kuuma,mwili kuuma,uchovu mkubwa na usingizi usioisha,koo kuuma(madonda kooni) mi nilidhani ni dalili za malaria.

Nikaja kuta si mimi tu niliyekuwa naugua ugonjwa huu.Kila nimfahamuye anaponambia anaumwa ukimuuliza anakwambia ni "TONSES"

Mpaka sasa ni zaidi ya watu 7(saba) wakiwa sehemu tofauti wanaugua ugonjwa huu.

Japo onyo nililopokea ni kwamba usinywe vitu vya baridi lakini siku zote nimekuwa nikinywa kwa miaka sasa bila kupata dalili hizo.

Hapa ndio nafikia kujiuliza na kuuliza umma, Je ugonjwa huu ni maambukizi?
---
Heshima mbele wana JF.

Naomba kuuliza swali:

Hivi mtu anapofanyiwa upasuaji "operation" ya tonsils halafu akang'olewa je kuna uwezekano wa ugonjwa kurudi tena? make kuna rafiki yangu alifanyiwa upasuaji mwezi wa nne kufika mwezi wa 7 zikarudi ikabidi akafanyiwe upasuaji tena.

Je, inawezekana hiyo?
---
Habari wanajamvi,
Kijana wangu ana umri wa miaka mitano. Amekuwa akisumbuliwa na tatizo la tonsils kuvimba mara kwa mara. Tatizo hili lilianza kujitokeza akiwa na miezi takribani sita hivi. Wakati linaanza tatizo hili alikuwa akisumbuliwa na homa kali, mafua, kikohozi na pia alikuwa akikoroma sana usiku akiwa amelala (alikuwa anapata taabu sana ya kupumua).

Nimekuwa nikimpeleka kwa wataalamu wa magonjwa ya watoto na baadhi yao wamekuwa wakishauri yaondolewe kwa surgery lakini wengine wameshauri si vema kumfanyia surgery kwani hayajafikia hatua mbaya sana.

Kwa ushauri wa daktari bingwa kabisa wa magonjwa ya watoto amesema dalili za kuwa ugonjwa huo umefikia critical point ni pamoja na kucha kubadilika kuwa za rangi ya kibuluu, dalili ambayo kijana huyu hajafikia. Na pia kwa utaalamu na uzoefu wa bingwa huyo ni kuwa akifikia umri wa miaka 10-14 kuna uwezekano wa tatizo hilo kutoweka lenyewe.

Sasa tatizo hili limekuwa likijirudia mara kwa mara. Na mara zote daktari bingwa amekuwa akimpatia dawa ambazo akitumia tatizo linapungua kwa takribani 80%. Lakini huwa linajirudia katika kipindi cha wiki 2-4 baada ya kumaliza dawa.

Sasa naombeni ushauri wenu:
1. Nini suluhisho la tatizo hili?
2. Je ni kweli akifikisha umri huo uliotajwa tatizo hili linaweza kuisha?
3. Nini prons & cons za kufanya au kutofanya surgery?
4. Je surgery ya ugonjwa huu inachukua muda gani kupona? (Ukitilia maanani kidonda kipo katika njia ya chakula/hewa so kinakuwa katika disturbance ya mara kwa mara).

Natanguliza shukrani zangu za dhati.
Habari wanajamvi,
Kijana wangu ana umri wa miaka mitano. Amekuwa akisumbuliwa na tatizo la tonsils kuvimba mara kwa mara. Tatizo hili lilianza kujitokeza akiwa na miezi takribani sita hivi. Wakati linaanza tatizo hili alikuwa akisumbuliwa na homa kali, mafua, kikohozi na pia alikuwa akikoroma sana usiku akiwa amelala (alikuwa anapata taabu sana ya kupumua).

Nimekuwa nikimpeleka kwa wataalamu wa magonjwa ya watoto na baadhi yao wamekuwa wakishauri yaondolewe kwa surgery lakini wengine wameshauri si vema kumfanyia surgery kwani hayajafikia hatua mbaya sana.

Kwa ushauri wa daktari bingwa kabisa wa magonjwa ya watoto amesema dalili za kuwa ugonjwa huo umefikia critical point ni pamoja na kucha kubadilika kuwa za rangi ya kibuluu, dalili ambayo kijana huyu hajafikia. Na pia kwa utaalamu na uzoefu wa bingwa huyo ni kuwa akifikia umri wa miaka 10-14 kuna uwezekano wa tatizo hilo kutoweka lenyewe.

Sasa tatizo hili limekuwa likijirudia mara kwa mara. Na mara zote daktari bingwa amekuwa akimpatia dawa ambazo akitumia tatizo linapungua kwa takribani 80%. Lakini huwa linajirudia katika kipindi cha wiki 2-4 baada ya kumaliza dawa.

Sasa naombeni ushauri wenu:
1. Nini suluhisho la tatizo hili?
2. Je ni kweli akifikisha umri huo uliotajwa tatizo hili linaweza kuisha?
3. Nini prons & cons za kufanya au kutofanya surgery?
4. Je surgery ya ugonjwa huu inachukua muda gani kupona? (Ukitilia maanani kidonda kipo katika njia ya chakula/hewa so kinakuwa katika disturbance ya mara kwa mara).

Natanguliza shukrani zangu za dhati.
1582091364453.png


BAADHI YA MAONI NA MAJIBU YALIYOTOLEWA NA WADAU
Pole emecka kwa kuchelewa kuja hapa...unajua tena internet mpaka ofisini! Madaktari 'choka-mbaya'!​

Tonsils zinapotolewa kwa upasuaji (Tonsilectomy) zinapaswa kutoka/kung'olewa zote pande zote mbili....huwa haibaki hata moja. Na kwa sababu ziko kwenye kama kifuko hivi (sac) ni rahisi basi kuzichomoa nzima nzima isibaki hata kidogo. Na zinapotolewa, basi huwezi tena pata ugonjwa wa kuvimba na kuuma Tonsils yaani 'Tonsilitis'.

Kwa kweli sijui ilitokeaje kwa rafiki yako akaugua tena na kulazimika kufanya operation kwa mara ya pili (sijawahi kuona hilo katika uDaktari wangu). Labda hiyo operation ya kwanza haikuwa Tonsilectomy...sijui...check uwe na uhakika. Na kama ilikuwa tonsilectomy, ina maana Daktari alitoa tonsil moja akaacha nyingine? au alitoa zote but not completely?...Highly unlikely!
---

Mahesabu, NDIO,MAFINDOFINDO NI AMBUKIZI

HOW?

Tonsilitis usually spread from person to person by contact with throat or nasal fluid of someone already infected.

HOW TO AVOID?
1.make sure to keep your sick person's drinking glasses and eating utensils separate ans wash them in hot,soapy water
2.All family members should wash their hands frequently.


Tonsil husababishwa na sababu nyingi tu . Pia husababishwa na upungufu wa white blood cells katika mwili ambazo cells hizi ndio hupigana na vidudu vyote venye kuleta maradhi ndani ya mwili sasa vinaposhindwa kufanya kazi lymph zinavimba na husababisha Tonsils.

Kila mtu na ukuwaji wake wa mwili, wapo ambao wanapata tonsils kwa kunywa maji ya baridi ambayo maji ya baridi huwa ni moja katika chanzo cha kupata tonsils, mavumbi huchangia vile vile pilipili na vitu vikali kama vile embe mbichi limau pia huwa ni sababu kuu ya kupata tonsil.

Wakati unapokuwa na tonsils muhimu zaidi kuacha maji ya baridi na vitu vyote vikali, zaidi utumie maji ya moto

Dawa za tonsils ni : kama ni mtumiaji wa dawa za chemicals basi epincilin inasaidia sana kuondosha tonsils.

Dawa nyengine ambayo mimi binafsi naipendelea hii zaidi kwani inafanya kazi mara moja : Kamua ndimu moja katika glass yako kisha tia maji ya Uvuguvugu (warm water) na baadae tia vijiko vinne vidogo vya asali na kijiko robo cha chumvi kuroga uzuri na unywe pole pole

Au Dawa hii Jaribu pia Dawa ya TONSILS ni kusukutuwa maji yaliokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala Tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto.

Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia.

Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako.

Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya kazi na mdomo uko wazi basi pia unaweza kuumwa na Tonsils.

Vile vile kutoka nje kwenye joto kisha ukaingia pahala baridi huwa inasababisha Tonsils na maradhi mengine kama flu na kuumwa na kichwa..n.k
---
inategemea na sababu gani iliyokusababisha upate haya maradhi ya Mafindofindo (Tonsilitis). Ushauri mzuri ni kumwona daktari, hii ni kwasababu it is caused by many organisms including bacteria. Ni daktari ambaye anaweza

kutofautisha. Pia inategema kama ni mara ya kwanza au ni chronic. Nikiwa kama daktari wa magonjwa mimi sikushauri tu ule dawa tu au unywe maji moto. Kama yalivyo magonjwa ya njia za juu ya hewa ni vizuri kujiepusha kunywa Vitu

baridi. Ushauri mzuri ni kumwona daktari.

Pia unaweza kujaribu.

Hii dawa ya kienyeji mie naita five in one.

1) Glasi moja ya maji Safi ya kunywa.

2) Kijiko 1 cha Asali Safi ya nyuki wakubwa.

3) Kijiko 1 cha Uwatu iliyosagwa (Hilba) kwa lugha ya kiingereza inaitwa Fenugreek

4) Tangawizi (fresh)

5) Kipande cha ndimu

kisha zichanganye pamoja halafu chemsha kama unavyo chemsha chai, ngojea ipoe moto kidogo kisha unywe kama unavyo kunywa chai kutwa mara 3 kwa muda wa siku 3 au siku 7. ukipona nipatie ]
mafindo.JPG
---
938454e6214c6da24da6bd2355215750.jpg


Kumekuwa na uelewa mdogo wa suala la vidonda vya koo maarufu kama mafindofindo katika jamii zetu. Watu wengi wamekuwa wakiamini uognjwa huu unasababishwa na utumiaji wa vitu vya baridi kama vile ice cream na barafu.

Dhana hii potofu imesababisha wazazi wengi kuwapiga marufuku watoto wao kutumia wakidhani ndio chanzo kikuu. Leo nitaelezea ugonjwa huo wa mafindo findo ama kwa kitaalamu tonsillitis.

Mafindofindo ni mjibizo wa tezi iitwayo tonsil, ambayo husaidiana na tezi nyingine katika mwili kupambana na vimelea mbalimbali vya magonjwa kwa kutengezea askari mwili. Tezi hizi ziko mbili na zinapatikana pande zote mbili mbele na nyuma ya koo. Zina rangi ya pinki na mara zinapovimba baada ya maambukizi hubadilika na kuwa nyekundu.

Mafindofindo ni ugonjwa ambao huambukizwa kwa njia za hewa, ambapo vimelea vya magonjwa kama vile bakteria na virusi huenezwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia mbalimbali.

Moja wapo ni kupiga chafya, kukohoa, kugusa zana zenye vimelea na kughusisha midomoni au masikioni, ugonjwa huu huwapata watoto zaidi ingawa huweza huwaathiri pia na watu wa rika nyingine.
Dalili kuu za ugonjwa huu ni vidonda kooni, mara nyingi mgonjwa hulalamika kuwa na vidonda kooni ambavyo huambatana na maumivu makali wakati wa kumeza chakula.

Dalili nyingine zinazoambatana na vidonda kooni ni uvimbe wa tezi unaodhihirika mbele ya shingo, homa kali, kichwa kuuma, mafua, harfu mbaya kinywani, kufifia au kupotea kwa sauti na mwili kuchoka. Vidonda kooni ambavyo huambatana na dalili nyingine kama vile mafua, kupiga chafya na kikohozi mara nyingi husababishwa na virusi.

Kwa sababu hiyo, matibabu ya dawa katika hali hiyo si ya lazima kwa sababu mwili unaweza kupambana katika kuondoa vijidudu hivyo. Endapo vidonda vya koo havitaambatana na dalili yoyote kama nilizozitaja, moja kwa moja kinachodhaniwa ni maambukizi ya bakteria.

Njia mbadala za kutibu ugonjwa huu ni pamoja na kupumzika, kusukurua kinywa kwa kutumia maji vuguvugu yenye chumvi na kunywa maji mengi.
Dawa za maumivu na homa hutolewa na wakati mwingine sawa za vijaviuasumu (antibiotic) huweza kutumika iwapo maambukizi ni ya bakteria.

Endapo ugonjwa hautapatiwa tiba ya haraka madhara mbalimbali huweza kujitokeza kama vile homa ya rheumatic, magonjwa ya sikio, figo, tezi nyingine pia katika mwili zaweza kuathiriwa pia kwa kutengeneza usaha.
Mwendelezo wa maambukizi ya tezi hizi za koo, huweza kusababisha mafindofindo sugu. Hii ni kutokana na kuendelea kuzaliana kwa bakteria ambao hutengeneza vifuko vidogo vidogo kwenye tezi hizo.

Ndani ya vifuko hivi hutengenezwa mawe madogo yaliyo na mchanganyiko wa salfa ambayo huleta harufu mbaya ya kinywa. Mara nyingi mafindofindo sugu hutibiwa kwa njia ya upasuaji. Hii huamriwa na daktari endapo maambukizi hayo yatakuwa yameendelea kumsumbua mgonjwa kwa kipindi kirefu. Upasuaji utamsaidia mgonjwa kuepuka madhara kwenye mifumo mingine.

Ili kuepuka kupata maambukizi katika mfumo wa hewa ni vyema kuzingatia usafi wa mwili na mikono.
Epuka sehemu ambazo utakaa muda mrefu ambazo zina vihatarishi kama vile msongamano wa watu na vumbi.
Villky_J
---
Matibabu za tonsilitis (Mafindofindo)
inategemea the cause. The best option ni kumwona daktari, hii ni kwasababu it is caused by many organisms including bacteria. Ni daktari ambaye anaweza kutofautisha. Pia inategema kama ni mara ya kwanza au ni chronic. Nikiwa kama daktari wa magonjwa I dont advice ule to dawa tu au unywe maji Moto. Kama yalivyo magonjwa ya njia za juu ya hewa ni vizuri kuepuka vitu baridi. The best option ni kumwona Daktari.

Pia unaweza kujaribu,

Hii dawa ya kienyeji mie naita five in one,

1) gilasi moja ya maji

2) kijiko 1 cha asali

3) Kijiko 1 cha Uwatu iliyo sagwa (Hilba)

4) Tangawizi (fresh)

5) Kipande cha ndimu

kisha zichanganye pamoja halafu chemsha kama unavyo chemsha chai, ngojea ipungue moto kidogo kisha inywe kama unavyo kunywa chai.
---
Tonsil husababishwa na sababu nyingi tu . Pia husababishwa na upungufu wa white blood cells katika mwili ambazo cells hizi ndio hupigana na vidudu vyote venye kuleta maradhi ndani ya mwili sasa vinaposhindwa kufanya kazi lymph zinavimba na husababisha Tonsils.

Kila mtu na ukuwaji wake wa mwili, wapo ambao wanapata tonsils kwa kunywa maji ya baridi ambayo maji ya baridi huwa ni moja katika chanzo cha kupata tonsils, mavumbi huchangia vile vile pilipili na vitu vikali kama vile embe mbichi limau pia huwa ni sababu kuu ya kupata tonsil.

Wakati unapokuwa na tonsils muhimu zaidi kuacha maji ya baridi na vitu vyote vikali, zaidi utumie maji ya moto

Dawa za tonsils ni : kama ni mtumiaji wa dawa za chemicals basi epincilin inasaidia sana kuondosha tonsils.

Dawa nyengine ambayo mimi binafsi naipendelea hii zaidi kwani inafanya kazi mara moja : Kamua ndimu moja katika glass yako kisha tia maji ya Uvuguvugu (warm water) na baadae tia vijiko vinne vidogo vya asali na kijiko robo cha chumvi kuroga uzuri na unywe pole pole

Au Dawa hii Jaribu pia Dawa ya TONSILS ni kusukutuwa maji yaliokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala Tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto.

Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia.

Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako.

Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya kazi na mdomo uko wazi basi pia unaweza kuumwa na Tonsils.

Vile vile kutoka nje kwenye joto kisha ukaingia pahala baridi huwa inasababisha Tonsils na maradhi mengine kama flu na kuumwa na kichwa..n.k

Tumia kisha unipe FeedBack. P.h.D. MziziMkavu
---
Mkuu Baba mtata,

Tonsils ni moja wapo ya tissue zinazopatikana mwilini, kwa kawaida huwa zinakuwa nne..yaani katika Kinywa na Koo.Tissue hizi husaidia katika mfumo wa kuukinga mwili(hasa kinywa, koo) na magonjwa.

Tonsilitis, (yaani MAKORORO) hii ndiyo hasa tatizo na mara nyingi imekuwa ikiitwa kama visivyo kama vile "Tonsis, Tonsils, n.k" kumaanisha kuugua kwa Tonsils.

Tatizo la tonsilitis, inaweza kusababishwa kwa vitu mbalimbali zaidi ni vyema kujua umri, na utumiaji wa vyakula/maji , n.k

Si kila "kuumwa kwa koo" humaanisha tatizo la Tonsilitis, hata hivyo pamoja na kuwa na shida katika umezaji wa mate, huambatana na homa, kujisikia vibaya, pia inawezakana kubadilika kwa sauti(kuambatana kwa mafua n.k)

Kwa kufika hospitali,itajulikana hasa ni nini na kupata matibabu sahihi.
---
pole mkuu,

Nilikuwa nasumbuliwa sana na ugonjwa huu hata dawa za antibiotic za kumeza hazikusaidia nikawa napata sindano za mishipa nikaagiziwa dawa za asili ambayo ni pilipili manga na binzari jinsi ya kutumia:
  • kijiko cha chai 1 binzari
  • kijiko cha chai 1 Pilipili manga
  • maziwa fresh 1/2 glass yenye moto
unachanganya unakoroga halafu unakunywa kama chai inaukali/ uchungu kiasi unatakiwa kunywa taratibu
nimekunywa kwa muda wa wiki 2 asubuhi na jioni.

kwa kweli imenisaidia angalau nimefikisha mwaka bila kupata hayo makitu na wakati mwengine nikisikia dalili nakoroga dawa yangu nakunywa.
 
Mahesabu, NDIO,MAFINDOFINDO NI AMBUKIZI

HOW?

Tonsilitis usually spread from person to person by contact with throat or nasal fluid of someone already infected

HOW TO AVOID?
1.make sure to keep your sick person's drinking glasses and eating utensils separate ans wash them in hot,soapy water
2.All family members should wash their hands frequently.

============

Tonsil husababishwa na sababu nyingi tu . Pia husababishwa na upungufu wa white blood cells katika mwili ambazo cells hizi ndio hupigana na vidudu vyote venye kuleta maradhi ndani ya mwili sasa vinaposhindwa kufanya kazi lymph zinavimba na husababisha Tonsils.

Kila mtu na ukuwaji wake wa mwili, wapo ambao wanapata tonsils kwa kunywa maji ya baridi ambayo maji ya baridi huwa ni moja katika chanzo cha kupata tonsils, mavumbi huchangia vile vile pilipili na vitu vikali kama vile embe mbichi limau pia huwa ni sababu kuu ya kupata tonsil.

Wakati unapokuwa na tonsils muhimu zaidi kuacha maji ya baridi na vitu vyote vikali, zaidi utumie maji ya moto

Dawa za tonsils ni : kama ni mtumiaji wa dawa za chemicals basi epincilin inasaidia sana kuondosha tonsils.

Dawa nyengine
ambayo mimi binafsi naipendelea hii zaidi kwani inafanya kazi mara moja : Kamua ndimu moja katika glass yako kisha tia maji ya Uvuguvugu (warm water) na baadae tia vijiko vinne vidogo vya asali na kijiko robo cha chumvi kuroga uzuri na unywe pole pole

Au Dawa hii Jaribu pia Dawa ya TONSILS ni kusukutuwa maji yaliokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala Tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto.

Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia.

Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako.

Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya kazi na mdomo uko wazi basi pia unaweza kuumwa na Tonsils.

Vile vile kutoka nje kwenye joto kisha ukaingia pahala baridi huwa inasababisha Tonsils na maradhi mengine kama flu na kuumwa na kichwa..n.k

 
Nao hilo ni jibu la kidaktari. Mimi sio daktari, ila naweza sema ugonjwa huo ni ambukizi kwa watu wanaoambukizika kutokana na mambo ya kigenetiki. Nina watoto 5, wawili wa mama mmoja na watatu wengine wa mama mwingine. Hawa wawili mama mmoja ndio ambao hupata tonses na wala hawaambukizi hawa watatu wengine na wakiumwa hatuchukui tahadhari zozote.

Hawa ambao hawapati ndio kiboko kwa kula barafu, tena mmoja anatafuna kama peremende na kumeza mabonge lakini hapati. utafiti binafsi, sio wa kidakitari, nikagundua hawa wanaoumwa kwa mama yao ugonjwa huu upo, na hawa wasioupata kwao haupo kabisa. Ni sawa na magonjwa kama ulcers, pressure, mvi na upara, yatatokana na ukoo.

Nimegundua kumbe hata uzee pia ni kuoo, ukiangalia kuna koo hawazeeki, na kuna koo just at 60 ni mzee wakutupa. Ila pia in every case, there is exceptionals.
 
Pasco

kama ulivyosema kuwa wewe sio daktari,lakini kauli yako kuwa mafindofindo uweza ambukiza watu ambao wanafanana vinasaba ni sahihi,zipo reseach zilifanywa na kuthibitisha hilo,lakini hali hiyo haimanishi kwamba wale wenye vinasaba tofauti kama vya wale wanaougua hawawezi ambukizwa.Kama nilivyoeleza hapo juu,tunatakiwa tuchukue hizo taadhari ili kuepukana na maambukizi ya mafindofindo.
 
Ndio unaambukiza na zipo njia nying za maambukizi moja ni busu la kubadilishan mate kwa wapenzi aka denda kama mmoja wapo ana umwa anaumwa mafundofundo basi mwenzi wake ni rahisi kuupata
 
Tonsilitis ni ugonjwa kuvimba kwa tezi za shingo (tonsils) ambao unaletwa na bacteria pamoja na virusi. Asilimia kubwa inaletwa na bacteria wanaoitwa Streptococcus pyogenes.

Bacteria hawa hushambulia tezi ambazo huvimba , kuwa nyekunde na kuwa na usaha. Kwa sababu unaletwa na vijidudu basi huambukizwa kwa njia ya droplets (vimajimaji) vilivyo na hawa bacteria. Kwa kawaida ni ugonjwa wa watoto lakini inaweza kuwapata watu wazima.

Willy
 
Tonsilitis ni ugonjwa kuvimba kwa tezi za shingo (tonsils) ambao unaletwa na bacteria pamoja na virusi. Asilimia kubwa inaletwa na bacteria wanaoitwa Streptococcus pyogenes. Bacteria hawa hushambulia tezi ambazo huvimba , kuwa nyekunde na kuwa na usaha. Kwa sababu unaletwa na vijidudu basi huambukizwa kwa njia ya droplets ( vimajimaji) vilivyo na hawa bacteria. Kwa kawaida ni ugonjwa wa watoto lakini inaweza kuwapata watu wazima.
Willy

Mbona hamsemi dawa nyie.....?
 
Mbona hamsemi dawa nyie.....?

Dawa yake ni kunywa warm tea au unaweza tengeneza lemon juice na kunywa. mafindo findo hata mie huwa napata mara kwa mara.Kama unasikia maumivu sana unaweza kunywa panadol kwa kutuliza maumivu.
 
Matibabu za tonsilitis inategemea the cause. The best iption ni kumwona daktari, hii ni kwasababu it is caused by many organisms including bacteria.

Ni daktari ambayeanaweza kutofautisha. Pia inategema kama ni mara ya kwanza au ni chronic. Nikiwa kama daktari wa magonjwa I dont advice ule to dawa tu au unyem maji moto. Kama yalivyo magonjwa ya njia za juu ya hewa ni vizuri kuavoid vitu baridi.

Tonsilitis inazo complication zake pamoja na kuaffect moyo (Rheumatic fever) ndiyo maana unahitaji kumwona daktari. Naona nikomee hapa.
Willy
 
Willy,
Hapa WILLY umenena. kwa mbali najisikia MOYO UNAUMAna mara chache KULIPUKA......!
dawa niliyopewa mimi ni AZYWOK CAPSULES(azythromicin)
ASANTENI WACHANGIAJI KWA DARASA NILILOLIPATA JUU YA UGONJWA HUU!
JE UGONJWA HUU NI MLIPUKO(kama kipindupindu)?
 
Hapa WILLY umenena. kwa mbali najisikia MOYO UNAUMAna mara chache KULIPUKA......!
dawa niliyopewa mimi ni AZYWOK CAPSULES(azythromicin)
ASANTENI WACHANGIAJI KWA DARASA NILILOLIPATA JUU YA UGONJWA HUU!
JE UGONJWA HUU NI MLIPUKO(kama kipindupindu)?

Zimekusaidia?
 
ZIMENISAIDIA...lakini dozi mbili, kwani ya kwanza baada ya kuisha zikaanza kurudi tena....ikabidi niji-prescribe dozi ya pili!
 
Dr. Heshima Mbele na wana JF

Dokta tonses(mafindofindo) yakizidi yana madhara gani??

kwa upande wangu ninayo hayo mafindofindo sasa yananisumbua sana muda na kila asubuhi nikipiga mswaki natema damu, na nikiwa nakula nashindwa kumeza napaliwa sana na msosi mpaka niweke maji pembeni. bado sijaenda hospital na nikiangalia yamevuimba sana.

msaada wakuu nijue madhara niwahi kutibu ila nilishawahi kujaribu PEN V ikadunda hii inaponesha kwa muda. na kazini ni AC sasa sijui ni hii AC
 
pole sana.
jaribu kusukutua na maji ya chumvi angalau mara 3 kwa siku yanasaidia sana.
pia epuka kula vitu vya baridi kama maji yabaridi, na vyakula vinayowekwa kwenye jokofu,


maumivu yakizidi pata ushauri kwa dakitari
 
pole sana.
jaribu kusukutua na maji ya chumvi angalau mara 3 kwa siku yanasaidia sana.
pia epuka kula vitu vya baridi kama maji yabaridi, na vyakula vinayowekwa kwenye jokofu,


maumivu yakizidi pata ushauri kwa dakitari

Maneno hayo. Nimeshasikia wengine hufanyiwa operesheni ya kuyaondoa kabisa, lakini usithubutu kufanya hivyo maana nimeshasikia matukio machache ambapo wagonjwa waliokubali kufanyiwa operesheni kufariki.
 
Pole pastor. Mimi nilisumbuliwa sana na hii kitu,mwishowe nikafanyiwa operation ya kuyatoa.It si a quick one,nadhani technolojia imeshakuwa safi. Tell u what,yatoe tu,ni mateso bila sababu take it from me.Na ukifikia umri flani hayatolewi tena coz the earlier the better.Madhara yake ni pamoja na magonjwa ya moyo (congenital heart diseases) na figo_Onana na ENT coz yanatabia ya kufanya sudden fatal attack,i lost my cousin with these!Kila la kheri
 
Back
Top Bottom