Tila-lila2
JF-Expert Member
- Oct 20, 2019
- 653
- 1,058
Paskali fahamu kuwa hata kabla sijaamua kujiunga rasmi JF nimekuwa nikisoma sana nyuzi zako. Mara nyingi umekuwa ukianzisha nyuzi ambazo na mimi nakuwa nimezifikiri na hivyo unakuwa umeniwasilishia kwa hakika. Lakini sio zile nyuzi ambazo sometimes zinafanya usieleweke.
Leo Paskali naona nikukumbushe tu kwa uzi wenye mtindo wa swali kwa sababu najua wewe ni "msoma trend" wa mambo ambayo huyaandika. Vipi tukiangalia suala la chuki katika nchi yetu - trend yake inaendaje? Paskali hujaandika kuhusu hili! Kwa nini? Unaogopa ama?
Anyway - Nakuuliza Paskali vipi mwelekeo wa jamii yetu kushikana na kuwa wamoja na kuipinga chuki dhidi yetu trend yake ikoje tangu uongozi huu uingie?
Paskali unaonaje matendo ya kwa mfano kupotea kwa wananchi na Serikali kuwa kimya kimya kimya kimya kimya sana - hayakuzi chuki katika nchi yetu?
Paskali matukio kutopepelezwa ya watu kupigwa risasi na mengine kutangazwa kufanyiwa upelelezi fasta ya watu kuhisiwa kupewa sumu - hayaleti chuki ya kuonesha upendeleo dhidi yetu?
Paskali vipi utaratibu kwa mfano wa kuijali jamii yetu mfano kuongeza mishahara kwa wafanyakazi - hii haijaleta chuki dhidi ya jamii yetu?
Paskali - vipi uendeshwaji wa siasa zetu ulivyo - Uchaguzi wa Serikali za mitaa ulivyofanyika mwaka jana na kupiga pin shughuli za kisiasa za wazi kwa upinzani tu wakati wa chama tawala wakijimwambafai - hii haijaleta chuki dhidi yetu?
Paskali - kubwa kuliko unaonaje kitendo cha Chama Tawala kwenda kumtoa yule Mwanachama wao aliyecross kutoka Chadema kwa kumlipia faini na kisha Polepole kuongea kwa Kiingereza kuitangazia dunia kuwa nao mwanachama wao alikuwa kafungwa - hii haijaleta chuki katika nchi yetu?
Paskali - unaonaje pia undugunaizesheni uliiooneshwa na Rais kwa Mheshimiwa Msigwa wakati akijua yeye Rais ni baba wa WaTanzania wote, haashirii kuwa wengine wakome wenyewe huko jela ila Ndugu yake Msigwa atoke - hii haijaleta chuki katika jamii yetu?
Paskali - ukiwa kama Mwanasheria unaonaje pia kuwa Hakimu angeweza tu kutamka kuwa kama wahukumiwa katika adhabu waliyopewa wanaamua kulipa faini awape muda wa kulipa faini na wakishindwa ndiyo wakamatwe kwenda jela na yeye akaamua waende kwanza jela na kisha walipe faini wakiwa huko huko jela ni kama wametumikia adhabu zote hizo kwa pamoja - yaani wameenda jela siku kadhaa halafu na wamelipa faini yote - hili halizidishi chuki katika jamii yetu?
Ndugu yangu Paskali ni mengi yanafanyika ambayo yanaashiria kukuza chuki badala ya kuleta amani na upendo katika nchi yetu. Hata kama kuna mipango mizuri ya kukuza uchumi wetu inatekelezwa lakini jamii inayojaa chuki ndani ya mioyo yao ni hatari sana huko mbeleni.
Kwangu mimi wewe ni kama unaongoza kujadili hoja rahisi na za maana katika Jukwaa hili lakini naona katika kuangalia mambo ya amani na upendo katika nchi yetu kwa kiasi kikubwa unakwepa kujadili.
Kazi njema Kaka Paskali!
Tila Lila2
Leo Paskali naona nikukumbushe tu kwa uzi wenye mtindo wa swali kwa sababu najua wewe ni "msoma trend" wa mambo ambayo huyaandika. Vipi tukiangalia suala la chuki katika nchi yetu - trend yake inaendaje? Paskali hujaandika kuhusu hili! Kwa nini? Unaogopa ama?
Anyway - Nakuuliza Paskali vipi mwelekeo wa jamii yetu kushikana na kuwa wamoja na kuipinga chuki dhidi yetu trend yake ikoje tangu uongozi huu uingie?
Paskali unaonaje matendo ya kwa mfano kupotea kwa wananchi na Serikali kuwa kimya kimya kimya kimya kimya sana - hayakuzi chuki katika nchi yetu?
Paskali matukio kutopepelezwa ya watu kupigwa risasi na mengine kutangazwa kufanyiwa upelelezi fasta ya watu kuhisiwa kupewa sumu - hayaleti chuki ya kuonesha upendeleo dhidi yetu?
Paskali vipi utaratibu kwa mfano wa kuijali jamii yetu mfano kuongeza mishahara kwa wafanyakazi - hii haijaleta chuki dhidi ya jamii yetu?
Paskali - vipi uendeshwaji wa siasa zetu ulivyo - Uchaguzi wa Serikali za mitaa ulivyofanyika mwaka jana na kupiga pin shughuli za kisiasa za wazi kwa upinzani tu wakati wa chama tawala wakijimwambafai - hii haijaleta chuki dhidi yetu?
Paskali - kubwa kuliko unaonaje kitendo cha Chama Tawala kwenda kumtoa yule Mwanachama wao aliyecross kutoka Chadema kwa kumlipia faini na kisha Polepole kuongea kwa Kiingereza kuitangazia dunia kuwa nao mwanachama wao alikuwa kafungwa - hii haijaleta chuki katika nchi yetu?
Paskali - unaonaje pia undugunaizesheni uliiooneshwa na Rais kwa Mheshimiwa Msigwa wakati akijua yeye Rais ni baba wa WaTanzania wote, haashirii kuwa wengine wakome wenyewe huko jela ila Ndugu yake Msigwa atoke - hii haijaleta chuki katika jamii yetu?
Paskali - ukiwa kama Mwanasheria unaonaje pia kuwa Hakimu angeweza tu kutamka kuwa kama wahukumiwa katika adhabu waliyopewa wanaamua kulipa faini awape muda wa kulipa faini na wakishindwa ndiyo wakamatwe kwenda jela na yeye akaamua waende kwanza jela na kisha walipe faini wakiwa huko huko jela ni kama wametumikia adhabu zote hizo kwa pamoja - yaani wameenda jela siku kadhaa halafu na wamelipa faini yote - hili halizidishi chuki katika jamii yetu?
Ndugu yangu Paskali ni mengi yanafanyika ambayo yanaashiria kukuza chuki badala ya kuleta amani na upendo katika nchi yetu. Hata kama kuna mipango mizuri ya kukuza uchumi wetu inatekelezwa lakini jamii inayojaa chuki ndani ya mioyo yao ni hatari sana huko mbeleni.
Kwangu mimi wewe ni kama unaongoza kujadili hoja rahisi na za maana katika Jukwaa hili lakini naona katika kuangalia mambo ya amani na upendo katika nchi yetu kwa kiasi kikubwa unakwepa kujadili.
Kazi njema Kaka Paskali!
Tila Lila2