Pascal Mayalla na Maulid Kitenge ni watu wa kitengo? Story za Ngorongoro na ukimya wa mahojiano bungeni ni alert tu

seedfarm

JF-Expert Member
Feb 9, 2020
260
2,654
Kwa wale wanaoangalia mambo kwa jicho la tatu, siyo kila ukionacho kwa macho ya kawaida ndivyo kilivyoumbwa. Hakuna utabiri katika hii dunia, kila kitu ni mipango inakuwa imepangwa na watu iwe mizuri au mibaya, ya muda mfupi au mirefu.

Katika kila jambo linalotokea kuna nguvu ya uvutano nyuma yake, kuna msukumo na nguvu kubwa sana. Usikubali mtu akasema voice from within au nimeoteshwa, mara nyingi wanakuwa na taarifa kamili za mipango husika iwe mipango ya muda mrefu au mfupi.

Kuna watu wanataarifa classified lini Israel itaanzisha mashambulizi tena Gaza, kuna watu wana taarifa wabunge gani hawatapata nafasi 2025. Watu kama Kigogo Twitter hakuwa mtabiri au anaoteshwa mambo wakati wa JPM bali kuna watu walikuwa na taarifa za miaka miwili au mitatu zaidi na ni watu wa kitengo.

Kuna watu maisha yao yana utata sana, wanaongea na kutenda tofauti na mioyo yao. Wanatumika kupima upepo na nguvu kwa kigezo cha uwanahabari. Kuna kundi kubwa hapa Jf ni wapiga filimbi na wapima upepo.

Makala za Pascal mara nyingi ni zenye utata sana na ikapelekea mtu asiyejua mambo kumuita bungeni, yaliyotokea huko ni siri. Lakini akina Gwajima na Polepole walituambia waliambiwa kitu gani kwenye kamati ya Bunge, Pascal yeye amekaa kimya. Je, alijitambulisha yeye ni kitengo?

Maulidi Kitenge, Huyu ndio ana utata zaidi na siyo kidogo, ana mambo mengi huwa anatumika kupunguza upepo. Hata wakati ule wa kusisitiza kujifukiza alitumika sana. Ishu ya Ngorongoro anapitia mipango ile ile huku wengi hawamuelewi, hafanyi Propaganda hata kidogo kwenye ishu za kupima upepo.

Kuna listi ya wanamuziki kama Mwana FA na Wengine wana mambo mengi sana. Huyu wakati taarifa za JPM kufariki ni siri aliweka ujumbe wenye utata wa kumuaga JPM kwa lugha ya Fasihi lakini wengi walimuhoji akaupiga kimya.

Watu mliozoea kwenda kuchart PM na kutoa namba zenu za simu muwe makini sana, Kama huna madhara wewe toa namba yako lakini kama una madhara achana na kutoa namba PM.

Hii dunia ina watu wengi lakini inaongozwa na kakikundi ka watu wachache. Tanzania tupo wengi lakini kuna kundi lina taarifa classified na limetawanyika, wengi wakijiita manabii na wanahabari za uchunguzi. Wote hawa husingizia wameoteshwa ndoto au wana sauti ndogo ndani inawasumbua yaani voice from within ya kujua ya kesho au miaka mitatu baadae.​
 
Paskali.
Baba yake mzee mayala alikuwa polisi na madaraka ya juu kuyatumikia alikuwa RCO. P anasema alikuwa mtumishi pia wa idara ya usalama.
Mama yake p, amefarik majuz na alikuwa anakula pensio 80% ya makachelo waandami sana. P anasema mishara ya waandamiz sana anaifaham ya wengi. Alijuaje, atajibu kwa kuwa ni mwanahabr.

Pasi ni maj general.
 
Paskali.
Baba yake mzee mayala alikuwa polisi na madaraka ya juu kuyatumikia alikuwa RCO. P anasema alikuwa mtumishi pia wa idara ya usalama.
Mama yake p, amefarik majuz na alikuwa anakula pensio 80% ya makachelo waandami sana. P anasema mishara ya waandamiz sana anaifaham ya wengi. Alijuaje, atajibu kwa kuwa ni mwanahabr.

Pasi ni maj general.
RSO ni tofauti na RCO!
 
Kitenge ghafla tu alijitokeza mbele ya Nape na mshika bastola,akaanza kumwambia "namna gani wewe bwana,utaharibu" huku akimvuta pembeni mshika benduki,hapo hapo walikua sambamba na vijana wengine mapandikizi,ujasiri gesture aliyokua nayo wakati wa tukio inaweza kukupa picha kamili!!

Mayala wazazi wake walikuaga kitengo enzi za Nyerere na nafikiri hadi Mwinyi na nyadhifa kazaa!!

Maandiko yake yote,kiundani utayaona ni ya kiCCM ila ana akili nyingi za kujifanya kama hahusiki kuipalilia CCM!!

Wengi hatukumbukagi mambo ama hatuyasomagi kwa umakini,ni Mayala huyu huyu alieanziaga hapa jukwaani na makala mflululizo la kumchongea Erick Kabendera,kwa wale waliosahau ama hawakuona hilo warejee makala zake kadhaa akilishutumu gazeti la "The economist" kua maandishi wake ana mtusi Magufuli!!

Infact tips zinasema moja ya hao Wana habari ndio alieenda kutaja mwandishi wa makala zile ni nani kwa Tanzania,maana zilikua hazina majina ya mwandishi!! Haikuchukua kitambo sana na Erick yakamkuta,tukashuhudia mama yake mzazi kwa huzuni kabisa akimuomba mkubwa fulani amsamehe mwanae!!!

Mama alifariki huku kijana akinyimwa hata ruksa ya kuhudhuria mazishi japo alikua rumande tu!! Na hao ndio wazalendo wetu!!
 
Ipo siku utasikiw GL yupo mapumziko huko ng'ambo baada ya kutimiza majukumu yake akiwa huku.
Utabaki kutafakari kati ya kukubali au kuamini jamaa yupo uhamushoni.

Ni mfano lakini siyo halisi.
 
Humu JF, huko mitaani, mashuleni, maofisini, masokoni, stendi, kwenye daladala, mabasi na mwendokasi, internet-world, n.k kote huko wapo watu wenye vinasaba na kitengo.
Lakini muhimu ni kuishi kwa kusimamia principles na misimamo.
Ukiwa jasiri utakufa. Ukiwa muoga utakufa.
Ila ukiwa jasiri utaishi miaka mingi!
 
Haitusadii lolote wawe sijui wa nini, sie Mungu tunasema twende tu ,ku kalibu kukucha, tuliyasema maneno Kama aya kipindi Cha mwendazake , tukachukuliwa mapopoma,

Sikia laana za roho miambili sio za kubeza swala nikutafute suluhu,

Ona Sasa

Machinga ,mama ntilie wanalia bomolewa vibanda vyao

Juzi nikamsikia mbuge anasema vipelekwe vifaru,washawasha kuondoa watu Ngorongoro,

Nami nasema wakafanye ,maana ngozi nyeusi mpaka dam zitoke masikion ,ndo utasikia kelele, ACHA wafanye ,
 
Back
Top Bottom