tatanyengo
JF-Expert Member
- Mar 30, 2011
- 1,134
- 280
Katika utaratibu wa kawaida wabunge wa vyama vya siasa wanakuwa na mkutano uitwao Party Caucus. Lengo la mkutano wa aina hii ni kwa ajili ya pengine kupendekeza na kupitisha majina ya wagombea wa nafasi mbalimbali kulingana na mahitaji au kujadili namna ya kupitisha sera iliyo katika mchakato. Lakini katika hali isiyo ya Kawaida, Party Caucus ya CCM imekuwa ni kwa ajili ya kupanga mikakati ya kupitisha na kuunga mkono hotuba za bajeti ambazo hazina maslahi kwa wananchi mfano ile ya wizara ya elimu. Tunawaomba ndugu wabunge mnapokuwa bungeni jaribuni kutetea maslahi ya wananchi zaidi kuliko serikali na vyama vyenu. Tafadhali rejeeni majukumu ya Bunge: Kutunga sheria na kuisimamia serikali.