Part 1: TISS bado safari ngumu

My Son drink water

JF-Expert Member
Nov 30, 2016
4,932
13,283
Kuna watu wanadhani kuondoka kwa mzee wangu wa Kanisa,TISS ndugu Kipilimba basi mambo yanaenda kubadilika na kuifanya idara hiyo ifanye kazi nzuri la hasha.

TISS bado ina safari ndefu mno ili iwe idara bora Kama zingine, recruitment ya TISS imejaa viroja na maajabu, tofauti na mashirika mengi ya kijasusi Duniani.

TISS imejaa kina "kamlete ",yaani watu wanaopewa ajira na ndugu zao kwa sababu ya ugumu wa maisha ya Bongo, hakuna usahili wa uhakika, madhara yake kumejaa ma agent ambao wakiona post Kama hii wanatamani wamkamate mtoa mada na kumpoteza.
Haina watu wazalendo kwa Taifa lao bali wazalendo wa chama tawala cha CCM chenye ndoto za kutawala Tanzania milele.

TISS haiwezi kumwajiri mwanachama wa CHADEMA au mpinzani yoyote bali Lazima awe mfia CCM na siyo mfia Tanzania.

Kazi kubwa za idara za kijasusi ni kuhakikisha nchi iko salama wakati wote na kuhakikisha hakuna umaskini ktk nchi kwa gharama yoyote ile.

Hongera zenu CIA, MI6, MOSSAD nyie ndo mnaipeleka Dunia puta kwa maslahi ya mataifa yenu, hamna muda na siasa.

Kazi ya idara ya usalama wa taifa ni kuwa loyal kwa nchi na si kwa wanasiasa...

INAENDELEA










 
Idara nyeti inapaswa kuwa na watu ambao brains zao zinacharge kweli kweli
Watu wenye upeo mkubwa kiakili na kinidhamu.

Idara inapaswa iwe na cream of the cream ya nchi

Siyo unachukua watu kwa milengo ya kisiasa matokeo yake hata analysis simple tu za mambo yanayojiri nchini hawawezi na hawana inputs zozote za maana!

Siyo lazima wachukue wenye madigrii tu bali wachukue watu bright kisha wawaendeleze, maana kuna watu hawakwenda shule za madarasani lakini wana akili kishenzi!

Kiukweli mambo yaliyokuwa yakifanyika nchini ndani ya miaka minne iliyopita utadhani yanapangwa na kufanywa na amateurs, kuanzia scripts za matukio feki ambazo raia siku hizi wanacheka tu!

Wewe imagine mtu anapiga picha kijijini kakaa na Jiwe anajifanya eti na yeye ni mmoja wa wazee masikini wa huko Chato kumbe ni.mmoja wa waambata wa Jiwe kwenye matukio mengine na picha zake zipo!

Eti mwanamama yuko hospitali anajifanya kumuomba raisi hela ya kukomboa maiti, halafu eti yuko peke yake na hakuwa cleared njiani anapopita rais, umewahi kuona wapi hii zaidi ya script?

Eti mtu anaenda bandarini na kisha kuokota vichwa vya treni

Vijana kufuatiliwa facebook kwa comment za maoni yao tu ya kisiasa na kupewa msoto mkali!

Unaenda kuandaa script ya maandamano kwenye ubalozi wa nchi nyingine kinyume cha protokali za Kidiplomasia duniani eti kushinikiza nchi iingilie mchakato wa madai yaliyoko mahakamani

Mambo gani haya ya ajabu kabisa!

TUNATAKA IDARA SMART, SHARP, JUST na YENYE KULINDA USALAMA WA NCHI KWANZA SIYO POLITICAL ambitions za MTU
 
TISS ina matatizo makubwa sana tofauti na watu wengi wanavyofikiri.

Tatizo kubwa kabisa linaloifanya TISS kuonekana kuwa ni taasisi ya hovyo, isiyofaa NA kuonekana kuwa ni taasisi ambayo ni adui mkubwa wa umma wa Tz ni kutokana na Sheria anzilishi ya Taasisi hii, pamoja na Sheria zingine, kanuni, na Miongozo mbalimbali inayotumika ktk kuendesha shughuli za kila siku za taasisi yenyewe.

Sheria na Kanuni zinazosimamia TISS ni mbaya, zimepitwa NA wakati, hazilengi ktk kuikomboa nchi hii na wananchi wake wote KWA ujumla kutokana na vitisho mbalimbali vya kiusalama pamoja na kuikomboa nchi na watu wake kutoka kwenye janga kubwa LA umaskini KWA kufanya UJASUSI wa Kiuchumi.

Kutokana na Sheria na Kanuni zilizopo, TISS inalazimika kuwa ni taasisi ya Kumlinda Rais, Urais, Viongozi wa Serikali, hasa wa nyadhifa za juu tu pamoja Serikali yenyewe, pamoja na Chama Tawala kilichopo Madarakani, basi.Hivyo basi, hata akiajiriwa nani ndani ya taasisi hii ya TISS anajikuta analazimika kutii kwa lazima matwaka haya ya Sheria ya Kulinda NA kutetea maslahi ya Viongozi wa Serikali tu na ya Chama Tawala kilichopo madarakani badala ya Kulinda NA Kuitetea Maslahi Mapana ya Umma wa wananchi wa Tz.
 
😆😆😆
Act like you CAN’T afford bread until they find out you own a bakery.. _joy_... Hel.jpg
 
153 Reactions
Reply
Back
Top Bottom