Papa Francisco aridhia ombi la Askofu Telesphor Mkude wa Jimbo Katoliki Morogoro kung'atuka kutoka madarakani

Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
1,813
4,544
Baba Mtakatifu Francisco ameridhia ombi la Kung'atuka kutoka madarakani lililowasilishwa na Askofu Telesphor Mkude wa Jimbo Katoliki Morogoro.Awali mwaka 2019 Baba Mtakatifu alimteua Monsinyori Lazarus Vitalis Msimbe, S.D.S kuwa msimamizi wa Kitume wa jimbo hilo akiwa na majukumu ya kufundisha, kuongoza na kuwatakatifuza watu wa Mungu ili kutoa nafasi kwa Mhashamu Askofu Mkude kushughulikia afya yake ambayo ilianza kuteteleka. Askofu Telesphor Mkude alizaliwa tarehe 30 Novemba 1945 huko Pinde wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro.

Julai 16 1972 Askofu Telesphor Mkude alipata daraja Takatifu la Upadre wa Jimbo Katoliki Morogoro huku 18 Januari 1988 Mtakatifu Yohane Paulo II akamteua kuwa Askofu wa Jimbo Katoliki Tanga ambapo 26 April 1988 aliwekwa wakfu na Hayati Kardinali Laurean Rugambwa.

5 Aprili 1993 Mtakatifu Yohane Paulo II alimteua kuwa Askofu wa Jimbo Katoliki Morogoro ambapo amedumu mpaka 30/12/20 Baba Mtakatifu Francisko aliporidhia ombi lake la kung'atuka madarakani.

#Kanisakatolikitanzania
 
Namtakia mapumziko mema.
Mwishoni wa utumishi wake katika kanisa umekua changamoto kwake kwa kweli.
Kule kuwa askofu aise na mamlaka yoyote hupelekea hate kutokupata heshima ilio mstahilikia.

Alipata skendo kubwa kidogo japo wameficha sababu za kumweka kando au za kumvua nyadhifa za kiuaskofu lakini ni Kama kashfa Fulani hivi aliipata.


Yote ya yote alikua ni askofu mzuri kwakweli tena mzuri haswa ila mwisho was utumishi wake umekua mbaya kidogo.

Sent from my TECNO RA7 using JamiiForums mobile app
 
Namtakia mapumziko mema.
Mwishoni wa utumishi wake katika kanisa umekua changamoto kwake kwa kweli.
Kule kuwa askofu aise na mamlaka yoyote hupelekea hate kutokupata heshima ilio mstahilikia.

Alipata skendo kubwa kidogo japo wameficha sababu za kumweka kando au za kumvua nyadhifa za kiuaskofu lakini ni Kama kashfa Fulani hivi aliipata.


Yote ya yote alikua ni askofu mzuri kwakweli tena mzuri haswa ila mwisho was utumishi wake umekua mbaya kidogo.

Sent from my TECNO RA7 using JamiiForums mobile app
Scandal ipi mkuu? Unaweza changanua kwa manufaa ya wanajukwaa
 
Alicho kitakasa Mungu usikiite Najisi. Kutakatfuza
 
Mungu amjalie Mapumziko mema, kwa kweli ile ilikuwa ni changamoto kubwa sana kwake lakini Mungu ni Mwema. Iliyobakia tuzidi kumuombea Matashi mema kwa Mungu na amjalie afya na Baraka daima.
 
Alipata skendo kubwa kidogo japo wameficha sababu za kumweka kando au za kumvua nyadhifa za kiuaskofu lakini ni Kama kashfa Fulani hivi aliipata.


Yote ya yote alikua ni askofu mzuri kwakweli tena mzuri haswa ila mwisho was utumishi wake umekua mbaya kidogo.

Sent from my TECNO RA7 using JamiiForums mobile app


Umekuwa mbaya kwa sababu ya kushughulika na afya yake au nini?na hiyo scandal ni kuhusu afya yake au ndo kujifanya kumjua mtu kuliko anavyojijua mwenyewe?

Fafanua!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
I wish him all the best

Sijawahi kuonana naye personal lakini nimewahi kumsikia kwa miaka kadhaa akitoa huduma ya kiroho kupitia redio Ukweli Morogoro miaka ile.
 
Namtakia mapumziko mema.
Mwishoni wa utumishi wake katika kanisa umekua changamoto kwake kwa kweli.
Kule kuwa askofu aise na mamlaka yoyote hupelekea hate kutokupata heshima ilio mstahilikia.

Alipata skendo kubwa kidogo japo wameficha sababu za kumweka kando au za kumvua nyadhifa za kiuaskofu lakini ni Kama kashfa Fulani hivi aliipata.


Yote ya yote alikua ni askofu mzuri kwakweli tena mzuri haswa ila mwisho was utumishi wake umekua mbaya kidogo.

Sent from my TECNO RA7 using JamiiForums mobile app
Kwa hio wewe unajua sana ila na wewe unaficha sasa kwa nini ulete kama huna uhakika?
 
Namtakia mapumziko mema.
Mwishoni wa utumishi wake katika kanisa umekua changamoto kwake kwa kweli.
Kule kuwa askofu aise na mamlaka yoyote hupelekea hate kutokupata heshima ilio mstahilikia.

Alipata skendo kubwa kidogo japo wameficha sababu za kumweka kando au za kumvua nyadhifa za kiuaskofu lakini ni Kama kashfa Fulani hivi aliipata.


Yote ya yote alikua ni askofu mzuri kwakweli tena mzuri haswa ila mwisho was utumishi wake umekua mbaya kidogo.

Sent from my TECNO RA7 using JamiiForums mobile app
Huna ulijualo, zaidi ya kuokoteza plus chuki/&wivu 'kwa kanisa/watu wa Mungu'

Askofu kafikia muda wa kupumzika/ama kustaafu 'miaka 75'
 
Huna ulijualo, unaokoteza plus chuki

Askofu kafikia muda wa kupumzika (ama kustaafu) - miaka 75
Ni kweli boss kafikia muda wa kustaafu Kama inavyotakikana, unajua ni kwanini alikuwepo msimamizi wa kutumia jimboni morogoro Padre msimbe anaesimamia masuala yote yakichungaji Kama askofu miaka karibu miwili kabla ya huyo askofo kustaafu?

Sent from my TECNO RA7 using JamiiForums mobile app
 
Ni kweli boss kafikia muda wa kustaafu Kama inavyotakikana, unajua ni kwanini alikuwepo msimamizi wa kutumia jimboni morogoro Padre msimbe anaesimamia masuala yote yakichungaji Kama askofu miaka karibu miwili kabla ya huyo askofo kustaafu?

Sent from my TECNO RA7 using JamiiForums mobile app
Bishop Telesphor Mkude alipumzishwa katika majukumu ya kuongoza, kutakatifuza na kuwafundisha watu wa Mungu Jimbo Katoliki la Morogoro ili kushughulikia zaidi afya yake

Hayo mengine ni yako aroo
 
Umekuwa mbaya kwa sababu ya kushughulika na afya yake au nini?na hiyo scandal ni kuhusu afya yake au ndo kujifanya kumjua mtu kuliko anavyojijua mwenyewe?

Fafanua!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
Pamoja na afya lakini kuna la ziada boss haliwezi kusemwa. Jana tu kwenye maziko ya askofu banzi Kama uliona happy alikuwepo lakini kwenye utambuzi alisahaulika mpaka askofu Alie kua karibu na Padre kitima alimkumbusha ndio akatambua uwepo wake.
Kwa mtu Kama askofu mkude ambae alimuachia kiti askofu banzi, na ambae pia wote walitoka Jimbo moja la morogoro ilikua sio mtu was kusahaulika kwenye utambulisho.

Sent from my TECNO RA7 using JamiiForums mobile app
 
Bishop Telesphor Mkude alipumzishwa katika majukumu ya kuongoza, kutakatifuza na kuwafundisha watu wa Mungu Jimbo Katoliki la Morogoro ili kushughulikia zaidi afya yake

Hayo mengine ni yako aroo
Ni kweli mbona Sasa hivi yupo imara kuliko wakati wakimsimamisha?

Sent from my TECNO RA7 using JamiiForums mobile app
 
Pamoja na afya lakini kuna la ziada boss haliwezi kusemwa. Jana tu kwenye maziko ya askofu banzi Kama uliona happy alikuwepo lakini kwenye utambuzi alisahaulika mpaka askofu Alie kua karibu na Padre kitima alimkumbusha ndio akatambua uwepo wake.
Kwa mtu Kama askofu mkude ambae alimuachia kiti askofu banzi, na ambae pia wote walitoka Jimbo moja la morogoro ilikua sio mtu was kusahaulika kwenye utambulisho.

Sent from my TECNO RA7 using JamiiForums mobile app
Na mie najua alipadrisha mashemasi Vimeo.... Ndio akaliwa kichwa na Mamlaka.
 
Back
Top Bottom