Papa Francis atoroka Vatican usiku

Very dangerous. Anaweza kutekwa au kukumbwa na kashfa. Pili mimi sio muumini sana wa kutoa misaada kwa maskini. Tushughulikie matatizo yanayosababisha watu kuwa maskini hasa umaskini wa kulazimishwa. Sina uhakika kama Vatican kuna vijiji. Ni nchi ya wakazi kama 1000 fu

Mimi si muumini pia, lakini natambua juhudi za makanisa kukusanya pesa kutoka kwa waumini wenye nafuu na kwenda kuwasaidia maskini wasio na kitu. Kazi ya kushughulikia matatizo yanayosababisha umaskini ni ya wanasiasa, makanisa yanasaidia kuamsha wananchi kwa kutoa elimu, pia wanalijnda afya ya jamii, nadhani unatambua kuwa hospitali zinazomilikiwa na mashirika ya kidini zilivyo kimbilio kubwa kwa sasa!
 
Hata Yesu aliwatoroka sana wanafunzi wake mpaka siku moja wakati wanamtafuta wakamkuta kisimani na yule mama msamaria na inaonekana wanafunzi wali- doubt kwamba alikua anamuimbisha yule mama

We Bibilia unasoma au umehadithiwa?
 
Hapo unaji "contradict" na habari iliyopo post #1 :

Kwanza usome mada na kuielewa. Mwandishi ameeleza historia ya huyu Papa alipokuwa askofu Mkuu na kardinali huko Ajentina alikuwa na mazoea ya kwenda vijijini akiambatana na msaidizi wake kwenda kutoa misaada kwa maskini nk. Huko Rome alienda mitaani kutoa misaada kwa maskini. Jadili na kutoa hoja kwa uelewa wa kuelewa ulichokisoma si kudandia maana mambo mengine huyajui, na kama huyajui tuulize tunaojua tukufahamishe badala ya kuvimbishia mishipa kitu usichokijua.
 
Kwanza usome mada na kuielewa. Mwandishi ameeleza historia ya huyu Papa alipokuwa askofu Mkuu na kardinali huko Ajentina alikuwa na mazoea ya kwenda vijijini akiambatana na msaidizi wake kwenda kutoa misaada kwa maskini nk. Huko Rome alienda mitaani kutoa misaada kwa maskini. Jadili na kutoa hoja kwa uelewa wa kuelewa ulichokisoma si kudandia maana mambo mengine huyajui, na kama huyajui tuulize tunaojua tukufahamishe badala ya kuvimbishia mishipa kitu usichokijua.

Wacha uongo, kafute na sentensi hii kama unataka iwe kama wewe utakavyo. "kuwapa misaada maskini maeneo ya vijiji, mjini Vatican."

Vatican iko Ajentina?

Ni kweli kabisa anasaidia masikini usiku, wakati wa kulala! hilo wala silipingi. Ndivyo Ilivyo.
 
Wacha uongo, kafute na sentensi hii kama unataka iwe kama wewe utakavyo. "kuwapa misaada maskini maeneo ya vijiji, mjini Vatican."

Vatican iko Ajentina?

Ni kweli kabisa anasaidia masikini usiku, wakati wa kulala! hilo wala silipingi. Ndivyo Ilivyo.

Ya Vatican utayaweza wewe wakati huijui biblia, sembuse Canon Law inayoongoza Vatican? Nikugeuzia upande wa mwongozo na sheria za uchungaji ndo kabisa hutajua kitu, pale kila kitu kina utaratibu na mwongozo wake, haya huyajui unadandia gari usilojua linakoelekea we unakazana kupungia mkono na unalikimbiza tu litakupoteza na katu halitageuza kukushushia ulikolidandia na utashtukia umepoteza muda wako bure.
 
We Bibilia unasoma au umehadithiwa?

kwa taarifa yako mimi biblia nimeshaisoma na kuimaliza yote (Mwanzo - ufunuo) kwa kutumia biblia tofauti tofauti mara tatu bila kuhesabu kusoma bila mpangilio maalum na mpaka sasa najifunza kierebrania na kgiriki ili niweze kuelewa maana katika original manuscripts. biblia ina siri nyingi sana(tafsiri) kama unaisoma kwa kumaanisha acha hizi za kusoma kutafuta miujiza au ulinzi

(John 4:27 [KJV])
And upon this came his disciples, and marvelled that he talked with the woman: yet no man said, What seekest thou? or, Why talkest thou with her?

(John 4:27 [TR])
και επι τουτω ηλθον οι μαθηται αυτου και εθαυμασαν οτι μετα γυναικος ελαλει ουδεις μεντοι ειπε τι ζητεις; η τι λαλεις μετ αυτης;
 
The Catholic Mafioso are going to poison this guy very soon, he goes against everything they believe.
 
Mi naona itakuwa michezo km ile ya Saudia na Oman

Saudia na Oman kucheza mipira usiku ni very popular kwani huko mchana ni joto kali sana. Wala sikupingi kwa hilo.

Sasa fikiri kibaridi cha Europe mwezi huu kilivyo kikali, kuchezea mipira usiku kunanoga kweli.
 
Saudia na Oman kucheza mipira usiku ni very popular kwani huko mchana ni joto kali sana. Wala sikupingi kwa hilo.

Sasa fikiri kibaridi cha Europe mwezi huu kilivyo kikali, kuchezea mipira usiku kunanoga kweli.
Ukitaka kumsoma mtu udhaifu wake angalia mwelekeo wake anakoelekeza mada hata kama haiongelei maudhui hayo ni dalili tosha yu dhaifu ya anachojaribu kutushawishi kwa vile kama ni mpishi kila muongeleachoa hatakosa kugusa mapishi, ndicho anachokijadili FaizaFox.
 
Mi naona itakuwa michezo km ile ya Saudia na Oman

Tatizo ninyi hamuujui ukatoliki, unaona wenyewe wanaojua wanaeleza wanachokijua na wasiojua wameamua kuwa wasomaji wa kujifunza kinachoendelea.

Je, unajua kwamba pope ni mtawa? Kama huwajui watawa, jaribu kuagnalia masister na mabrother ndo utajua ninachokiongelea hiyo ndiyo status na maisha ya Pope kabla ya uaskofu na hadi sasa yuko vile. Kwa wengine wanashangaa kwa nini hataki kuishi apartment ya kifahari na kuamua kuishi hostel kwa walala hoi sababu wengi wetu tunaojadili humu hatujui hulka na mfumo wa maisha ya kimoki, yaani maisha ya kitawa. Yule ni mtawa tofauti na wale ambao wametokana na secular priest wanaopenda ufahari. Usishangae ukiona pope analala sakafuni kama wafanyavyo watawa wafransiskani, huo ndio mtindo wa maisha yake kwani cheo cha upapa hakimwondolei sifa, na mazingira ya wito wake wa kitawa.

Watawa ni watu wanaojali sana maskini na watu wasiojiweza, na historia ya maisha yake hata huko alikokuwa askofu na kisha kuwa kardinali alikuwa na mazoea hayo ya kuwatembelea maskini. Mchana mngejua ratiba ya pope ilivyobanwa na shughuli za ofisi na watalii pale Vatican. Kumbuka watawa si watu wa kulala masaa mengi, nisehemu ya kufunga, kusali, kuwatembea na kuwasaidia maskini. Nimejaribu kuwafungua akili kidogo maana wengine hapa wanafikiria na kutafsiri kwa misingi na taratibu za maisha yao bila kujua uwanja na nafsi ya tunayemjadili.
 
Ukitaka kumsoma mtu udhaifu wake angalia mwelekeo wake anakoelekeza mada hata kama haiongelei maudhui hayo ni dalili tosha yu dhaifu ya anachojaribu kutushawishi kwa vile kama ni mpishi kila muongeleachoa hatakosa kugusa mapishi, ndicho anachokijadili FaizaFox.

Soma post vizuri ujuwe zinajibu nini, wacha papara. Naona umeanza kujifunza kuandika ipasavyo. Taratibu tutafika.
 
Soma post vizuri ujuwe zinajibu nini, wacha papara. Naona umeanza kujifunza kuandika ipasavyo. Taratibu tutafika.
Sababu hukijui tunachokijadili, we unadandia hoja, na mambo ya ndani ya nyuma isiyo yako utabaki kuhangaika nayo kwa vile ni yao hayakuhusu na hutayaelewa, utabaki kuumiza kichwa kwa mambao yasiyokuhusu na kutoyaelewa. Wenye kuyafahamu na kuyaelewa ni wale waliomo ndani ya nyumba yao.
 
Back
Top Bottom