Wakudadavuwa
JF-Expert Member
- Feb 17, 2016
- 17,506
- 15,997
Tundu Lissu ni nani ndani ya CHADEMA? nani wanaomuunga mkono ndani ya CHADEMA? Pengine nianze kwa kujibu maswali hayo hapo juu. Tundu Lissu ni Mwanachama na Mwanasheria wa CHADEMA na kwa sasa amejijenga kwa kuibua utata kila uchao si tu dhidi ya serikali bali utata wake ni mkubwa sana ndani ya chama chake cha CHADEMA husuasani kwa viongozi na wafadhili wakuu.
Tundu Lissu ndani ya CHADEMA anaungwa mkono kwa dhati kabisa na wafuasi wasiofungamana na kundi la Mbowe na marafiki wa EL kwa lugha rahisi Tundu Lissu anaungwa mkono na wanachadema wanaotaka Mbowe na EL waondoke CHADEMA kwa sababu ya makandokando yao.
Kundi la marafiki wa EL, kundi hili kamwe haliwezi kumuaini Tundu Lissu japo wanamtumia katika harakati za kuwasafisha na kuwatafutia huruma ya wananchi. Ikumbukwe kuwa hawa ni wana-CCM kindakindaki ila wametafuta pahala pa kuuguza ''vidonda vyao''.
Japo Tundu Lissu alinukuliwa akiwananga miaka kadhaa iliyopita huku akitamani serikali ya JK iwafunge gerezani bila hata kuwafungulia mashitaka kwani Tundu alijigamba kuwa na ushahidi ndani na nje ya bunge dhidi ya watu hawa.
Kundi hili linamtumia Tundu Lissu kama fimbo lakini kamwe halimwamini na wala hawamshirikishi kwenye mipango yao ya siri kwa sababu wanajua ni kigeu geu, siku wakikosana hubadilisha maneno na kuongea hadharani. Kwa kifupi hawawezi kukubali Tundu Lissu awe Mkuu wa Chama.
Kundi la ''Kamanda'' Mbowe, kwa mnaofuatilia mambo mtagundua kundi la wafuasi wa Mbowe limekaa kimya likitafakari jinsi ambavyo Mwenyekiti akipingwa mitandaoni na kwenye media, hawa hawakubali. Kundi hili wamo akina Lema, Msigwa nk...hawa muda ukifika wataongoza mapambano dhidi ya Tundu Lissu kuhakikisha hapati fursa ya kuwa mwenyekiti.
Watahakikisha anasomewa mashitaka kwa hati za uongo na kutolewa hukumu. Hawa dhumuni lao kubwa ni kubaki na ''status quo'' kuhakikisha chama kinashiriki uchaguzi na kujihakikishia ruzuku na si kutwaa madaraka. Kwa kundi hili endapo Tundu Lissu akifanikiwa kuwa Mwenyekiti huenda wakakosa ushawishi kwani kundi kubwa la watu wasio mrengo wa Mbowe au Lowassa ndio watapata madaraka ya Chama ndio watakao kuwa na sauti na watchukua nafasi za uongozi hivyo hawataruhusu Tundu apenye.
Muda ndio jibu, Mustakabali wa Tundu Lissu ndani ya CHADEMA haswa katika harakati za kuukwaa uenyekiti huenda ukasababisha kuundiwa zengwe na kufurushwa chamani kama Zitto Kabwe.
Tundu Lissu ndani ya CHADEMA anaungwa mkono kwa dhati kabisa na wafuasi wasiofungamana na kundi la Mbowe na marafiki wa EL kwa lugha rahisi Tundu Lissu anaungwa mkono na wanachadema wanaotaka Mbowe na EL waondoke CHADEMA kwa sababu ya makandokando yao.
Kundi la marafiki wa EL, kundi hili kamwe haliwezi kumuaini Tundu Lissu japo wanamtumia katika harakati za kuwasafisha na kuwatafutia huruma ya wananchi. Ikumbukwe kuwa hawa ni wana-CCM kindakindaki ila wametafuta pahala pa kuuguza ''vidonda vyao''.
Japo Tundu Lissu alinukuliwa akiwananga miaka kadhaa iliyopita huku akitamani serikali ya JK iwafunge gerezani bila hata kuwafungulia mashitaka kwani Tundu alijigamba kuwa na ushahidi ndani na nje ya bunge dhidi ya watu hawa.
Kundi hili linamtumia Tundu Lissu kama fimbo lakini kamwe halimwamini na wala hawamshirikishi kwenye mipango yao ya siri kwa sababu wanajua ni kigeu geu, siku wakikosana hubadilisha maneno na kuongea hadharani. Kwa kifupi hawawezi kukubali Tundu Lissu awe Mkuu wa Chama.
Kundi la ''Kamanda'' Mbowe, kwa mnaofuatilia mambo mtagundua kundi la wafuasi wa Mbowe limekaa kimya likitafakari jinsi ambavyo Mwenyekiti akipingwa mitandaoni na kwenye media, hawa hawakubali. Kundi hili wamo akina Lema, Msigwa nk...hawa muda ukifika wataongoza mapambano dhidi ya Tundu Lissu kuhakikisha hapati fursa ya kuwa mwenyekiti.
Watahakikisha anasomewa mashitaka kwa hati za uongo na kutolewa hukumu. Hawa dhumuni lao kubwa ni kubaki na ''status quo'' kuhakikisha chama kinashiriki uchaguzi na kujihakikishia ruzuku na si kutwaa madaraka. Kwa kundi hili endapo Tundu Lissu akifanikiwa kuwa Mwenyekiti huenda wakakosa ushawishi kwani kundi kubwa la watu wasio mrengo wa Mbowe au Lowassa ndio watapata madaraka ya Chama ndio watakao kuwa na sauti na watchukua nafasi za uongozi hivyo hawataruhusu Tundu apenye.
Muda ndio jibu, Mustakabali wa Tundu Lissu ndani ya CHADEMA haswa katika harakati za kuukwaa uenyekiti huenda ukasababisha kuundiwa zengwe na kufurushwa chamani kama Zitto Kabwe.