Pamoja na yote huenda Tundu Lissu akafukuzwa CHADEMA kama Zitto

Chadema wanamuunga mkono Mwanasheria Mkuu wa Chadema Tundu Lissu katika vita vya kupinga udikteta uchwara kwenye nchi yetu kila mtanzania mwenye akili timamu tunatakiwa kumuunga mkono Tundu Lissu. Hayo mambo ya kufukuzana ningeanza huyo mwenyekiti wenu huko lumumba ameshindwa kila kitu mpaka sasa amebakia kutafuta kiki

Francis12, unajua maana ya Udikteta uchwara!. Au kwa maana ya Lissu ambaye anataka uhuru usio na mipaka, lakini wakati uleule:
1) Uhuru alionao wa kutisha vyombo vya habari na kuropoka hovyo na akarudi nyumbani kwake salama, ati hautoshi!
2) Uhuru tulionao humu JF wa kuandika upuuzi, kutukana na kubandika picha za hovyo, na tukabaki salama, pia hautoshi!

Wahenga walinenena ALIYESHIBA HAMJUI MWENYE NJAA, bali anataka wengine wasipate kabisa. Uhuru aliokuwa nao Lissu, kwa nafasi zake kama kiongozi, hajui uhitaji wa uhuru wa watu wengine japo kero zao zitekelezwe na Serikali iliyoko madarakani. Lissu, atembelee vijijini aone hali halisi ya maisha ili apate cha kuikosoa Serikali - UZEMBE, RUSHWA, UFISADI, na wanasiasa uchwara kama yeye Lissu, ambaye yanayomgusa apate umaarufu ndiyo utawala usio wa kidikteta. Anataka uhuru wa kuzunguka nchi nzima kwa mikutano na maandamano awalishe wananchi maneno, huku matumbo yao yakibaki na njaa!

Pia imeandikwa kwenye maandiko matakatifu, Methali 27:7 Aliyeshiba hata asali huikataa, lakini kwa mwenye njaa kila kichungu ni kitamu. Kwamba ajuaye maumivu ya kiatu ni yule aliyekivaa. Lissu hajui shida na kero za wananchi bali umaarufu wake kisiasa. Watu hawatashiba kwa kuwa na uhuru wa kuongea usio na mipaka.

Kitabu hicho hicho cha Methali 27:1,2 imeandikwa 1Usijisifie ya kesho, hujui nini kitatokea leo mpaka kesho. 2Acha watu wengine wakusifu, kuliko mdomo wako wewe mwenyewe. Lissu amesema sana mazuri, mabaya, uwongo na ukweli, uzushi na umbea. Imefika wakati sasa, kama msomi kiongozi, kutafakari matokeo ya kidomodomo chake.
 
Ngoja nifunge break ...nichanganye na zangu!hivi Lissu amesema /tamani kugomvea uenyekiti CDM?bila shaka unaweza ukadai pia hii kamatwa kamatwa yake pengune ametamani urais wa Tz baada ya kuonja ladha ya urais wa TLS!


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ngoja nifunge break ...nichanganye na zangu!hivi Lissu amesema /tamani kugomvea uenyekiti CDM?bila shaka unaweza ukadai pia hii kamatwa kamatwa yake pengune ametamani urais wa Tz baada ya kuonja ladha ya urais wa TLS!


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Francis12, unajua maana ya Udikteta uchwara!. Au kwa maana ya Lissu ambaye anataka uhuru usio na mipaka, lakini wakati uleule:
1) Uhuru alionao wa kutisha vyombo vya habari na kuropoka hovyo na akarudi nyumbani kwake salama, ati hautoshi!
2) Uhuru tulionao humu JF wa kuandika upuuzi, kutukana na kubandika picha za hovyo, na tukabaki salama, pia hautoshi!

Wahenga walinenena ALIYESHIBA HAMJUI MWENYE NJAA, bali anataka wengine wasipate kabisa. Uhuru aliokuwa nao Lissu, kwa nafasi zake kama kiongozi, hajui uhitaji wa uhuru wa watu wengine japo kero zao zitekelezwe na Serikali iliyoko madarakani. Lissu, atembelee vijijini aone hali halisi ya maisha ili apate cha kuikosoa Serikali - UZEMBE, RUSHWA, UFISADI, na wanasiasa uchwara kama yeye Lissu, ambaye yanayomgusa apate umaarufu ndiyo utawala usio wa kidikteta. Anataka uhuru wa kuzunguka nchi nzima kwa mikutano na maandamano awalishe wananchi maneno, huku matumbo yao yakibaki na njaa!

Pia imeandikwa kwenye maandiko matakatifu, Methali 27:7 Aliyeshiba hata asali huikataa, lakini kwa mwenye njaa kila kichungu ni kitamu. Kwamba ajuaye maumivu ya kiatu ni yule aliyekivaa. Lissu hajui shida na kero za wananchi bali umaarufu wake kisiasa. Watu hawatashiba kwa kuwa na uhuru wa kuongea usio na mipaka.

Kitabu hicho hicho cha Methali 27:1,2 imeandikwa 1Usijisifie ya kesho, hujui nini kitatokea leo mpaka kesho. 2Acha watu wengine wakusifu, kuliko mdomo wako wewe mwenyewe. Lissu amesema sana mazuri, mabaya, uwongo na ukweli, uzushi na umbea. Imefika wakati sasa, kama msomi kiongozi, kutafakari matokeo ya kidomodomo chake.
Umenena vema
 
vita ya uwenyekiti chadema haitamuacha TUNDU LISSU salama.... mfano halisi ni wazee wa mpango mkakati ZITTO,KITILA,MWIGAMBA hawakubaki salama
Hao wote uliowataja hapo juu ccm mnajua mlichowafanya ninyi. Mliwashawishi wakashawishika sasa ulifikiri chadema ni kama ccm wakugundisha minofu kwenye mifupa ya zamani? Chadema iliwaondoa mapandikizi yote ya ccm ndani ya chama. Mf angalia mnachokifanya sasa hivi ndani ya cuf kwa pandikizi lenu Lipumba ila mwisho wake ni aibu tupu.

ccm badala mhangaike na changamoto za maisha ya Watz mnahangaika na vyama vya upinzani. Kama mnafikiri kuvivuraga vyama ndio suluhisho la matatizo ya Watz mnapoteza muda. Hata mkifanikiwa kuvuruga cuf kwa lengo la kudhoofisha UKAWA pia mnapoteza muda ukawa tayari ulishakomaa ndani ya mioyo ya Watz.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Chadema ni Taasisi sio mtu mmoja mmoja, kama ccm waliweza kumkata lowasa basi hata lisu akizingua chadema watamtoa tu

Chadema ni taasisi? Kakudanganya nani? CHADEMA kina wenyewe na wenyewe ni wenye pesa walio ndani ya CHADEMA Lisu na wengineo wasio na hela ni wasindikizaji tu na wachangamsha chama.Matajiri wenyewe wenye pesa wala hawapigi yowe kama akina LIsu.Wenye chama huongea kwa nadra mno.

Lisu sio mfadhili wa chama ndio maana si rahisi akapata uenyekiti ,umakamu au ukatibu mkuu au uweka hazina.Akithubutu kuchukua fomu kugombea uenyekiti au uraisi wanamtimua mchana kweupe jua linawaka.

Yaani mfano chukulia LISU ndiye awe mgombea uraisi halafu Sumaye na LOWASA na matajiri rafiki zao ,na matajiri wa kichaga marafiki wa MBowe wamwage pesa zao kumsaidia LIsu kumkodia helikopta za kuzunguka nchi nzima na ndege za kukod kwa kampeni zakei!!!???? Hilo jambo halipo.

Anayeamua nani awe mwenyekiti ,mgombea uraisi au mweka hazina wa CHADEMA ni wenye pesa ambao ndio wanakiweka chadema mjini.Lisu hayumo kwenye kundi la wenye nazo yuko kwenye kundi la wapiga dede na kelele wa chama.KUNDI ambalo halina nguvu kwenye maamuzi makubwa ya chama.
 
Zito ni mfanyakazi wa serikali ya CCM ...na yuko kazini kuitumikia serikali yake...Lissu ni mwanasiasa wa Upinzani na mwanachama wa CHADEMA HEBU USIMLINGANISHE NA HAYO MALAPULAPU YAKO
 
Kweli kawashika pabaya, sasa hivi mnamuombea afukuzwe Chadema?

Inaitwa Precedency kijana.Zitto alianza hivhiv na yaliomkuta ulikuja kuyafahamu naamini......
Mungu akijaalia tutakua hapa kukumbusha yakitimia..kama makaburi mengine mengi yanyofukuliwa sasa!
 
Inaitwa Precedency kijana.Zitto alianza hivhiv na yaliomkuta ulikuja kuyafahamu naamini......
Mungu akijaalia tutakua hapa kukumbusha yakitimia..kama makaburi mengine mengi yanyofukuliwa sasa!

Pambaneni na rushwa kwanza uko kwenye chama chenu.
 
Pambaneni na rushwa kwanza uko kwenye chama chenu.

Kwenye chama sasa hakuna rushwa.imeshughulikiwa accordingly na mapambano ni endelevu.

Sijui kama unakumbuka vugu vugu lilivyoanza mpaka Zitto kuvuliwa uanachama,bet u were still a kid with no access to internet wala habari huko Katavi uliko so huwezi elewa kinachosemwa hapa juu ya Lissu na uwezekano wa kufukuzwa
 
Propaganda za kuchonganisha ni jadi ya ccm. hata siku moja hamjawahi kuamka salama kuona jinsi Lissu anavyo wachachafya, hasa boss wenu.
 
Hakuna hoja ni pumba tuu umeandika una umri gani?
Umri wangu! Ndiyo hoja yako? Wa kwako je! Ukijenga hoja jibu kwa hoja unapojibiwa. Huna tofauti na Lissu anayepayuka kuliko mtoto pamoja na umri, elimu na madaraka aliyokuwa nayo.
 
Hivi unafikri utapata ubunge wa kuchaguliwa na wananchi kwa kuinanga Chadema, Mbowe na Tundu Lissu huku mitandaoni? Wacha ramli chonganishi huku, nenda Songwe ukajijenge kwa wapiga kura, kwani vitu maalum safari hupewi.
Jielekeze kwenye hoja bila kejeli kwa mtoa hoja. Hata ya kuuzwa Chadema yalianzia humu JF mkaarisha matusi.
 
Back
Top Bottom