Pamoja na yote: Hivi kweli mafuta yakiwapo ziwa Nyasa/Malawi visima vya mafuta vichimbwe?

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Mgogoro wa mpaka katika ziwa kati ya Tanzania na Malawi wengi wanasema unatokana na uwezekano wa kuwapo mafuta ndani ya hilo ziwa. Hivi kweli hata mafuta yakiwapo ni busara kuyachimba toka ziwa hili linalotegemewa na maelfu ya watu kwa ajili ya maji ya kunywa, mifugo, uvuvi, kuoga, kilimo na maisha kwa ujumla?

Fikiria ikitokea kuvuja kwa mafuta kama ilivyotokea Marekani, watu wangapi wataathirika? Tuna uwezo wa kuwapa watu maji mbadala wakati tukisubiri ziwa lisafishwe, kama kweli litasafishwa? Na pia hili ni ziwa la fresh water, sio maji ya chumvi kama ya bahari yenye uwezo wa kujisafisha. Kweli tuko tayari watumiaji wa hili ziwa walishwe au kunyweshwa takataka za "oil rigs"?

Angalia picha za inavyokuwa ikitokea kisima cha mafuta ziwani au baharini kikavuja.

View attachment Oil spill katika ziwaau bahari.docx
 
Tathmini ya Athari za Kimazingira (Environment Impact Assessment) ndiyo itakayotoa ufafanuzi wa kina kufanya uamuzi wa ama kuchimba au kutokuchimba mafuta kutoka ziwa Nyasa, kama yapo.
 
mgogoro wa mpaka katika ziwa kati ya tanzania na malawi wengi wanasema unatokana na uwezekano wa kuwapo mafuta ndani ya hilo ziwa. Hivi kweli hata mafuta yakiwapo ni busara kuyachimba toka ziwa hili linalotegemewa na maelfu ya watu kwa ajili ya maji ya kunywa, mifugo, uvuvi, kuoga, kilimo na maisha kwa ujumla?

Fikiria ikitokea kuvuja kwa mafuta kama ilivyotokea marekani, watu wangapi wataathirika? Tuna uwezo wa kuwapa watu maji mbadala wakati tukisubiri ziwa lisafishwe, kama kweli litasafishwa? Na pia hili ni ziwa la fresh water, sio maji ya chumvi kama ya bahari yenye uwezo wa kujisafisha. Kweli tuko tayari watumiaji wa hili ziwa walishwe au kunyweshwa takataka za "oil rigs"?

Angalia picha za inavyokuwa ikitokea kisima cha mafuta ziwani au baharini kikavuja.

View attachment 62266

huna akili kabisa . Aani huna akili hata moja
 
hata wakifanya EIA, watapeleka nchi zote 2? Maana athari za kimazingira zitagusa nchi zote 2.

Na huu mgogoro ni mafuta tu kweli?? Uraniuma je?? Maana uranium ya mkuju inaweza kwenda hadi huko.
 
Back
Top Bottom