rodrick alexander
JF-Expert Member
- Feb 12, 2012
- 15,183
- 20,137
Katika msimu ambao Simba wameandwamwa na vyombo vya habari kuwa wanabebwa na waamuzi ni msimu huu.Waandishi bila kujadili maadili yao ya kazi waliweka ushabiki mbele kuwa Simba inashindwa kwa kubebwa bila kuangalia upande wa pili ambao mechi zao nyingi zimekuwa na maamuzi yenye utata.
Ilifikia kipindi simba imecheza badala ya kuelezea mpira ulivyokuwa walijikita kujadili waamuzi hali ambayo ilijenga uwoga kwa waamuzi waliokuwa wanachezesha mechi za Simba na kupelekea Simba kunyimwa penati au magoli ya wazi kwa hofu ya kisakamwa au kufungiwa.
Kwa wale walioangalia mechi ya juzi kati ya Azam na Yanga walishuhudia waamuzi wakikataa magoli mawili ya wazi pamoja na kunyimwa penati baada ya Mchezaji wao kuangushwa ndani ya eneo la penati.
Vyombo vingi vya habari vilikaa kimya lakini timu ya Azam iliamua kuandika barua bodi ya ligi na kupeleka clip za mchezo huo kuonyesha jinsi waamuzi walivyoihujumu.
Bodi ya ligi imethibitisha kupokea malalamiko yao na kuahidi kuyatolea maamuzi pamoja na matukio mengine yaliyotokea toka ligi ianze baada ya kusimamishwa kwa janga la Corona.
Huu ni wakati wa kujulikana ni nani anatumia pesa ili apate matokeo
Ilifikia kipindi simba imecheza badala ya kuelezea mpira ulivyokuwa walijikita kujadili waamuzi hali ambayo ilijenga uwoga kwa waamuzi waliokuwa wanachezesha mechi za Simba na kupelekea Simba kunyimwa penati au magoli ya wazi kwa hofu ya kisakamwa au kufungiwa.
Kwa wale walioangalia mechi ya juzi kati ya Azam na Yanga walishuhudia waamuzi wakikataa magoli mawili ya wazi pamoja na kunyimwa penati baada ya Mchezaji wao kuangushwa ndani ya eneo la penati.
Vyombo vingi vya habari vilikaa kimya lakini timu ya Azam iliamua kuandika barua bodi ya ligi na kupeleka clip za mchezo huo kuonyesha jinsi waamuzi walivyoihujumu.
Bodi ya ligi imethibitisha kupokea malalamiko yao na kuahidi kuyatolea maamuzi pamoja na matukio mengine yaliyotokea toka ligi ianze baada ya kusimamishwa kwa janga la Corona.
Huu ni wakati wa kujulikana ni nani anatumia pesa ili apate matokeo