Pamoja na mapungufu yake mengi, katika hili heko mbunge lameck o. Airo

Galapagos

JF-Expert Member
Nov 26, 2012
251
39
Habari wana Jamvi, Mbunge wa jimbo la Rorya mh.Lameck Airo ni miongoni mwa wale waheshimiwa ambao ni nadra sana kusikia michango yao bungeni, haya ni mapungufu yake. Nimesikitika kusoma habari kuwa jirani yake mbunge wa Tarime mh.Nyambari Nyangwine ameshindwa hata kusaidia ktk ukarabati wa vyoo vya shule ya sekondari Nkende iliyo karibu na nyumbani kwake hadi kupelekea shule kufungwa, kisa na mkasa eti hakupata kura maeneo hayo, huyu ni tofauti na mh. Lameck ambaye husaidia bila kujali ili mradi tukio liko ndani ya jimbo lake, katika hili napenda kumpa heko mh. Lameck Airo
 
Airo ni sawa tu na kivuli ndani ya Rorya. Kujenga choo cha shule hata wewe unaweza. Aongee matatizo ya Rorya bungeni!
 
Tunamsubiri Nyangwine atuongoze na mapanga kwenda kweny mgodi ili waje kutujengea choo hapo Nkende. Kama hakupata kura maeneo hayo ndo alipize kisasi? Je hakusikia kwamba majimbo ya upinzani ndo barabara nzuri zinajengwa na kwa wana CCM pako hoi! Yeye asubirie 2015, anunue rim nyingi tu atunge vitabu kuelezea shule zisizo kuwa na vyoo akianza na ya Nkende,

Mura waitu fita ni fita mpa kiereweke, Mura kura nimekura pa kurara je.


 
airo ni sawa tu na kivuli ndani ya rorya. Kujenga choo cha shule hata wewe unaweza. Aongee matatizo ya rorya bungeni!

Ataje vyoo alivyojenga na shule gani...sisi wanaRorya tunashida sana, boda ya Kirongwe hakijajengwa wakati wakenya walishajenga upande wao sisi bado wala airo hana habari ya kukumbushia serikali wala sijamsikia akiulizia sera ya serekali kuhusu kupandikiza samaki wapya kwenye ziwa victoria kwani sangara wamemaliza samaki wa aina nyingi sana.

Airo ajawatendea wana Rorya haki kabisa
 
Ataje vyoo alivyojenga na shule gani...sisi wanaRorya tunashida sana, boda ya Kirongwe hakijajengwa wakati wakenya walishajenga upande wao sisi bado wala airo hana habari ya kukumbushia serikali wala sijamsikia akiulizia sera ya serekali kuhusu kupandikiza samaki wapya kwenye ziwa victoria kwani sangara wamemaliza samaki wa aina nyingi sana. Airo ajawatendea wana Rorya haki kabisa
Mnamulaumu nani sasa? kwanini mlikubali kudanganywa na pilau? ndio laana ya mungu hiyo sasa, 2015 atakuja kivingine na mtampa tu.
 
Huu uzi nao unastahili kujadiliwa? Who is Lameck Airo anyway? Matatizo ya elimu yanaeleweka kuwa yalipandwa na CCM kisha yakamea, wakatilia mbolea, wakapitisha palizi na sasa wanavuna walichokipanda!!! Mfumo mzima wa Serikali ya CCM ndiyo chanzo cha Umasikini, Elimu Duni, Maradhi, Ujinga Mwingi, Umasikini na sasa UFISADI umetamaliki kiasi cha kuandika kwenye Rasimu ya Katiba eti Tunavutia uwekezaji kwenye Rasilimali zetu badala ya kutamka wazi wazi ni jinsi gani Rasilimali zetu zitawanufaisha watanzania kwanza na kwa kufuata taratibu zipi...CCM ni Janga kwa vizazi vya sasa na vijavyo...
 
Hahahah...kweli Watanzania sisi ni waduanzi, yaani kujenga vyoo hadi mbunge asaidie??...mnashindwa hata kufyatua matofali kwa kutumia udongo na baadaye kuyachoma matofali hayo?
 
Mnamulaumu nani sasa? kwanini mlikubali kudanganywa na pilau? ndio laana ya mungu hiyo sasa, 2015 atakuja kivingine na mtampa tu.

Walimchagua Baba Airo kwa sababu ako na pesa! Aliwapatia ugali wa udaga kwa Kamongo wakashiba na kushushia gongo, huku wakisema ero kamano Baba Airo. Tunachagua viongozi wasiyofaa baada ya kurubuniwa kwa vitu vya kijinga kabisa!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom