DR SANTOS
JF-Expert Member
- Mar 11, 2019
- 10,509
- 21,399
Hutaki auMi ni miongoni mwa Wana CCM ambao sikupendezwa na Mheshimiwa Tundu Lissu Kupigwa risasi ,
Mimi ni Miongoni mwa Wana CCM ambao hatukukubaliana na jinsi nchi ilivyokuwa inaendeshwa na Bwana Magufuli, Mimi na akina Kagasheki, Mwandosya, January Makamba na Butiku tulikuwa hatukubaliani na hayo,
Mimi ni Mwana CCM ambaye Sikubali na sijawai kuamini Kama Mbowe ni Gaidi , labda anaweza akawa na tuhuma nyingine za kuchochea vurugu na kutotii amri za Mamlaka ila si Kwa kiwango cha ugaidi!
Mimi ni Mwana CCM ambaye sikukubaliana na jinsi wanaharakati na waandishi walivyoshughulikiwa Kipindi cha Magufuli na wengine wenye mawazo mbadala wakatishiwa Kama bwana Evarist Chahali na kukimbia nchi, Mama yake Kabendera Erik akatiweka kisa Mwanaye kabambikiwa kesi, Wazee wa Ben saanane wanalia hawajui alipo,
Mimi ni Mwana CCM ninayependa KATIBA mpya, siyo katiba ya maslahi ya wanaotaka kutawala bali wananchi Kwa ujumla, na cha kushangaza zaidi ni Mwana CCM nayeamini kwamba Tanganyika tunaonewa ndani ya Muungano japo wengi mnaona Zanzibar ndo wanaonewa tu!
Mimi ni Mwana CCM nayependa ushindani wa hoja na siasa za Utani refter kwa Nape Vs Mbowe 2011, Wassira Vs Chadema !!!
Mimi ni CCM ambaye siamini katika kuhama hama vyama kwakuwa ukianza kuhama utavimaliza vyote!!!!!
Mimi ni Mwana CCM nayeamini katika kusameheana kwa makosa madogo mfano Membe anao uwezo wa Kumsamehe Musiba wakayamaliza na niliwai kusema kwamba Cyprian Musiba anakosea sana!!!
Mimi ni Mwana CCM nayependa uhuru wa kutoa maoni na uwazi na kuwepo freedom of expression napenda kuandika na Kuongea!!!
Mimi ni Mwana CCM nayeamini Samia Rais na Mwenyekiti wetu bado anayo nafasi ya Kuyarekebisha makosa madogo Kama kuleta maridhiano!!!
Pia mimi ni Mwana CCM nayependa kuwashuri vijana kutotumika kisiasa
KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
BRITANICCA ENCYCLOPEDIA