Pamoja na kutosafirisha makinikia Migodi wa Buzwagi waapa kukamilisha miradi ya jamii

tramadol

JF-Expert Member
Oct 10, 2015
5,383
4,317
Zikiwa zimepita siku 91 tangu Rais John Magufuli apige marufuku usafirishaji wa mchanga wa madini Nje ya nchi bado hatima ya suala hilo haijafahamika.

Hata hivyo uamuzi huo haujaathiri mgodi wa dhahabu wa Buzwagi uliopo Kahama kwa kutoendelea kutekeleza miradi ya jamii.

Meneja wa mgodi huo Stewart Hamilton amesema wataendelea kutekeleza miradi hiyo bila kujali mgogoro uliopo kati yao na Serikali.

Akikabidhi vifaa vya ujenzi wa bweni la wasichana ktk Sekondari ya Mwendakulima Meneja huyo alisema miradi itatekelezwa yote kwasababu haina uhusiana na suala la makinikia.

Mkuu wa Wilaya ya Kahama Fadhili Nkurlu aliupongeza mgodi huo kwa kukamilisha miradi ya wanainchi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya mji wa Kahama Anderson Msumba alisema kati ya migodi 4 iliyopo kanda ya ziwa Buzwagi ni mgodi mdogo lakini ndiyo unaofanya mambo makubwa ya maendeleo Katika wilaya hiyo.

Chanzo:Mwanainchi
 
Wanasubiri kwa hamu kubwa report ya Tume ya pili.

Miradi ya maendeleo ni just peanut kwa faida kubwa wanazopata hawa jamaa
 
Wanasubiri kwa hamu kubwa report ya Tume ya pili.

Miradi ya maendeleo ni just peanut kwa faida kubwa wanazopata hawa jamaa
Ukijengewa choo cha matundu kumi itatangazwa kwenye kila TV hapa nchini. Uliwahi kujiuliza thamani ya choo hicho na ukalinganisha na thamani ya madini wanayovuna pale Buzwagi? Hakika utashangaa ukijua hivyo.
 
Ukijengewa choo cha matundu kumi itatangazwa kwenye kila TV hapa nchini. Uliwahi kujiuliza thamani ya choo hicho na ukalinganisha na thamani ya madini wanayovuna pale Buzwagi? Hakika utashangaa ukijua hivyo.
Kuna haja kubwa ya kureview mikataba hii ya madini ni kweli tunachopata ktk sekta ya madini ni sawa sawa na hakuna.
 
Back
Top Bottom