Pamoja na kutakiwa kujiuzulu; Ngeleja agoma...

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,422
911,172
Ngeleja: Hoja si kujiuzulu

Imeandikwa na Lucy Lyatuu;
Tarehe: 8th December 2010



WAZIRI wa Nishati na Madini, William Ngeleja amesema tatizo sio kujiuzulu, bali ni jinsi ya kutatua kero za umeme na kuhakikisha mgawo wa umeme unakwisha nchini.

Ngeleja alitoa kauli hiyo Dar es Salaam jana wakati akijibu maswali ya waandishi wa habari kuhusiana na madai ya kutakiwa kufanya hivyo kama ambavyo Mbunge wa Jimbo la
Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), David Kafulila alivyodai kupeleka hoja binafsi bungeni ya kutokuwa na imani naye.

Ngeleja alisema hayo ni mawazo ya Mbunge huyo na kamwe hawezi kuzuia mtu kutoa maoni yake kwa kuwa ana hisia kali kama ambavyo yeye (Ngeleja) anazo.


Madai ya Kafulila aliyatoa wakati alipotangaza kuwa anakusudia kupeleka hoja binafsi katika Mkutano wa Pili wa Bunge, Februari mwakani kutaka serikali iwajibike kwa kuliingizia Taifa hasara kwenye sekta ya umeme, kutokana na hukumu ya kesi ya Dowans na Tanesco ambayo Tanesco inapaswa kulipa Sh bilioni 185.


Kafulila pia anakusudia katika hoja hiyo, kulitaka Bunge liazimie kupiga kura ya kutokuwa na imani na Waziri wa Nishati na Madini, kwa madai kuwa ameshindwa kusimamia utekelezaji wa Sera ya Nishati na Mpango Kabambe wa Usambazaji wa Umeme nchini.


"Tatizo sio kujiuzulu, bali tatizo ni kufuatilia na kutatua kero za umeme zinazowasumbua wananchi.


Aliyosema Kafulila yanatokana na adha ambayo anakutana nayo kama ambavyo na mimi inanikumba," alisema Waziri huyo aliyerejeshwa na Rais Jakaya Kikwete kuongoza tena wizara hiyo.


"Nayaheshimu mawazo ya mheshimiwa mbunge.., siwezi kuzuia yeye kutoa maoni yake, ila aelewe kuwa serikali inaendelea kutatua tatizo hilo kwa nguvu kubwa," alisema Ngeleja.


Kuhusu Dowans, alisisitiza kuwa liko mikononi mwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambapo yeye ndiye atakayeshauri na kuamua kama kampuni hiyo italipwa ama halipwi.


Alisema Tanzania ni nchi inayoongozwa kwa misingi ya sheria na maoni ya watu binafsi hayawezi kuongelewa.


"Kwanza sitaki kufungua ukurasa wa suala hili, nchi hii inajielekeza katika misingi ya sheria, hivyo sheria zilizopo zitatumika pamoja na kupata ushauri wa Mwanasheria Mkuu," alisema Ngeleja.


Alisema kwa sasa faili liko kwa Mwanasheria Mkuu ili aweze kulipitia kutoa mawazo na ushauri wake juu ya suala hilo ila ifahamike kuwa nchi inaongozwa kwa misingi ya sheria na utawala bora.


Kwa mujibu wa Ngeleja, kwa sasa serikali haiwezi kuzungumzia hisia za watu, bali hatima yake itaamuliwa na Mwanasheria Mkuu na kukanusha taarifa iliyoandikwa katika moja ya vyombo vya habari nchini, kuwa serikali yajivua zigo la deni la Dowans na kusema
endapo Mwanasheria Mkuu akitoa maoni ya Dowans kulipwa, watakaa na kulitazama zaidi na kama Tanesco inaweza kubeba mzigo huo.
 
Kujiuzulu ni lazima bse umekabiziwa wizara ambayo for the last 5 years imekushinda.
Kila siku mwatudanganya kuwa mgao utakuwa historia.
 
"Tatizo sio kujiuzulu, bali tatizo ni kufuatilia na kutatua kero za umeme zinazowasumbua wananchi.

sasa hapa huyu braza ngeleja anaamanisha nini??? tunajua swala nikutatua kero za wananchi kwenye sekta ya umeme ambayo wewe for the last 5 yrs umeshindwa kuitatua thus y imeonekana ni vzr ukajiuzulu ili nafasi hy apewe mwingine ambaye possibly wihin 3 yrs anaweza kuja na changes za kutosha kwenye hii sekta....Why cant u feel guilty???? is t hard 4 u to realize this bro?????
 
wana jf ile petition mpaka sasa watu wangapi wamesha saini?siku zake za hesabika,wananchi wanaomba hard copy wazisaini
 
Wajameni, i'm getting so disappointed when i read the international news and see Tanzania is facing power rationing as a result of serious power shortages while i am aware of numerous energy resources the land is endowed with! From geothermal to windpower to solarpower to natural gas to coal to hydropower to nuclear power to ocean current power you name it; Tanzania has them all! But, what is the problem then?

As things seem, the whole reason behind the imminent power cuts, emanates from the lack of that acute but compassionate sense of urgency and will upon
individuals bestowed with that sensitive responsibility to provide reliable power, a vital component to stir up country`s economic growth. While our President keeps yapping of his efforts to give the country an upper hand on business environment in the region, his efforts get wasted since five years down the line nothing has been done to improve energy availability situation. Interestingly, this comes after the president and his unusual entourage spent huge amount of money to undertake business trips abroad in the name of promoting investments while knowing in advance simple things like power supply remain a nightmare on the ground. As a matter of fact to salt-en the unhealed wound; an 18% hike on cost per unit of electricity has been slapped on the face of the poor Tanzanians and those manufacturers the government has just managed to attract. More provoking, all this is happening 2 months down the election pledges HE JK strongly campaigned for...!?

Though our minister of Energy and Mineral Resources Hon. Ngeleja believes has a strong case to make and excuse himself from the shambles of the current energy woos (i.e. the Pan African energy's gas wells not being able to supply enough gas to run the machines and produce the legally assigned
180 MW of electricity contracted by TANESCO); his rhetoric demonstrates of a man that has lost focus and lacks capability to rescue this nation from further economic deterioration the country is to suffer. If at all the legal procedures are observed, the pan African Energy has to be charged with sabotaging the economy by not providing the legally bound energy quota as stated in the contract, but lack of true leadership at the ministry in-charged continues to pile up tolls on lives of normal people!

This ministry that to-date lacks clear policies and
execution of plans to turn things around and provide permanent solutions on energy availability, needs nothing more than its top leaders' resignation for failing the Tanzanians while daring a nation with a 'lip-service' on promises that by "2013" energy shortages will be a history as if we have never heard of that before. It's high time now that HE Kikwete stops awarding the cabinet positions to incompetent individuals that have shown failure in his last government, if at all the interests of this country are the main agenda of his Government in power.

The perplexing and inexcusable
repetitive explanations on the failures to deliver at ones duties need not be tolerated anymore by the Commander in chief considering the economic harmful ways the country is exposed to e.g. the current situation rises production costs (for Tanzania often "irreversibly") that trigger a multiplicative series of market responses that cummulatively yield to an overhead inflation on consumer price that devalues our currency and leads to a rise in general cost of living affecting every citizen. When one looks at the Performance check list, its obvious Hon. Ngeleja does not fit at the current job that entails high work ethics while directly influences the competitiveness of country's economy. Therefore as my opinion; experienced, hard worker and God fearing individuals with integrity and track records should be given that ministry portfolio if at all things are to change i.e. the current top three plus the commissioners should be sent home!

Heri ya Noeli na mwaka Mpya gizani!

 
You have said it all. Tuna matatizo ya uongozi kwenye nchi yetu. Mitambo kuharibika, maintenance or whatever ni mambo ya kawaida lakini serikali ilipashwa kuhakikisha kwamba kuna back up arrangements in case one of the power supplies inakwama kufanya kazi ama kwa sababu moja au nyingine, back up inafanya kazi na kuzalisha umeme. Serikali haiwezi kukwepa lawama kwa uzembe wa kutokuwa na back up.

Halafu eti tunaita wawekezaji!!!! Shame on us.

Tiba
 
"Is Ngeleja a right man for the energy and mineral resources ministry?" Hell NO!!! Ngeleja is good for nothing!!! Even a kid can see that!! The thing is... JK doesn't seem to notice that as he is always suffering from a very malicious disease!!!...... "NEPOTISM!!!!"
 
"Is Ngeleja a right man for the energy and mineral resources ministry?" Hell NO!!! Ngeleja is good for nothing!!! Even a kid can see that!! The thing is... JK doesn't seem to notice that as he is always suffering from a very malicious disease!!!...... "NEPOTISM!!!!"

Ngeleje yupo hapo sio kwa matakwa ya Jakaya bali yupo hapo kwa shinikizo la Rostam ili alinde maslshi yake ya madini na nishati!! The guy is DUMB!!
 
Your questiona is very very fun! I can read your mind!

JK once was in the same ministry he did NOTHING! Kikwete huyu

Asking if Ngeleja is right man is ignoring the fact that even Kikwete is not right at all at all!! having some who seem good ministers does not nullify the fact that Kikwete is bogus and we are having good ones by chance!
 
we have a Finance minister with a FAKE DEGREE and he's back in the new cabinet. Not only mwenyewe harefute hizi claims...hata ofisi yake haisemi kitu kuhusu hili, let alone mwajiri wake

Ukistaajabu ya musa utashangaa ya Firauni
 
As things stands now in Tanzania, it is Extremly difficult to know if there is anyone who is fit enough to hold the position is occupying. That this is so is due to the fact that, currently the government seem to be pre-occupied mainly by two things; first self-aggrendizement on the part of those in power, and secondly, to put in place the neccessary safeguards to ensure that the right person succeeds JK, come 2015. Apart from these, everything else seem to be of no consequence.
 
Nimetafakari sana tamko la waziri Ngeleja la kutaka kampuni tata ya Dowans ilipwe,kwa hali ilivyo hata ndani ya chama chake ni kwamba wabunge hawakubaliani na swala hilo,na zaidi watanzania wengi hawakubaliani na swala hilo,sasa nauliza ataficha wapi uso wake asipojiuzulu?hasa kwa kuwa alisimamia kidete ilipwe kama vile yeye ni agent wa hawa wadai tata au pesa zinatoka mfukoni mwake.
 
unajiuliza km ni agent?kwn hujui km ngeleja alikua mwajiriwa wa RA ndugu yangu?hyo ni agent wa kudumu kwn hta kampen zake hyo ndo mdhamini...na kama ujuavyo RA ndio EL wch minz JK nae yumo na hata hyn wizara wadau wanadai kapewa purposly kulinda maslah!
 
unajiuliza km ni agent?kwn hujui km ngeleja alikua mwajiriwa wa RA ndugu yangu?hyo ni agent wa kudumu kwn hta kampen zake hyo ndo mdhamini...na kama ujuavyo RA ndio EL wch minz JK nae yumo na hata hyn wizara wadau wanadai kapewa purposly kulinda maslah!
hiyo nilikua sijui kweli kinachotakiwa ni katiba mpya ili kuhakikisha 2015 hawa watu hawarudi,kumbe ndio maana huwa hachukui maamuzi ya maana nyakati zote,asante mkuu
 
hawa wa2 ni kuwanyima kura 2,me nawaza yan hpa ndo kwnz tunaanza awamu ya 2 ya JK,mambo ni mabaya na mabovu km haya!cjui km cabinet hii nayo itatek ol 5 yrz...!ngeleja kuficha uso co kaz xana km kwa mh prezoo
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom