Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,422
- 911,172
Ngeleja: Hoja si kujiuzulu
Imeandikwa na Lucy Lyatuu;
Tarehe: 8th December 2010
WAZIRI wa Nishati na Madini, William Ngeleja amesema tatizo sio kujiuzulu, bali ni jinsi ya kutatua kero za umeme na kuhakikisha mgawo wa umeme unakwisha nchini.
Ngeleja alitoa kauli hiyo Dar es Salaam jana wakati akijibu maswali ya waandishi wa habari kuhusiana na madai ya kutakiwa kufanya hivyo kama ambavyo Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), David Kafulila alivyodai kupeleka hoja binafsi bungeni ya kutokuwa na imani naye.
Ngeleja alisema hayo ni mawazo ya Mbunge huyo na kamwe hawezi kuzuia mtu kutoa maoni yake kwa kuwa ana hisia kali kama ambavyo yeye (Ngeleja) anazo.
Madai ya Kafulila aliyatoa wakati alipotangaza kuwa anakusudia kupeleka hoja binafsi katika Mkutano wa Pili wa Bunge, Februari mwakani kutaka serikali iwajibike kwa kuliingizia Taifa hasara kwenye sekta ya umeme, kutokana na hukumu ya kesi ya Dowans na Tanesco ambayo Tanesco inapaswa kulipa Sh bilioni 185.
Kafulila pia anakusudia katika hoja hiyo, kulitaka Bunge liazimie kupiga kura ya kutokuwa na imani na Waziri wa Nishati na Madini, kwa madai kuwa ameshindwa kusimamia utekelezaji wa Sera ya Nishati na Mpango Kabambe wa Usambazaji wa Umeme nchini.
"Tatizo sio kujiuzulu, bali tatizo ni kufuatilia na kutatua kero za umeme zinazowasumbua wananchi.
Aliyosema Kafulila yanatokana na adha ambayo anakutana nayo kama ambavyo na mimi inanikumba," alisema Waziri huyo aliyerejeshwa na Rais Jakaya Kikwete kuongoza tena wizara hiyo.
"Nayaheshimu mawazo ya mheshimiwa mbunge.., siwezi kuzuia yeye kutoa maoni yake, ila aelewe kuwa serikali inaendelea kutatua tatizo hilo kwa nguvu kubwa," alisema Ngeleja.
Kuhusu Dowans, alisisitiza kuwa liko mikononi mwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambapo yeye ndiye atakayeshauri na kuamua kama kampuni hiyo italipwa ama halipwi.
Alisema Tanzania ni nchi inayoongozwa kwa misingi ya sheria na maoni ya watu binafsi hayawezi kuongelewa.
"Kwanza sitaki kufungua ukurasa wa suala hili, nchi hii inajielekeza katika misingi ya sheria, hivyo sheria zilizopo zitatumika pamoja na kupata ushauri wa Mwanasheria Mkuu," alisema Ngeleja.
Alisema kwa sasa faili liko kwa Mwanasheria Mkuu ili aweze kulipitia kutoa mawazo na ushauri wake juu ya suala hilo ila ifahamike kuwa nchi inaongozwa kwa misingi ya sheria na utawala bora.
Kwa mujibu wa Ngeleja, kwa sasa serikali haiwezi kuzungumzia hisia za watu, bali hatima yake itaamuliwa na Mwanasheria Mkuu na kukanusha taarifa iliyoandikwa katika moja ya vyombo vya habari nchini, kuwa serikali yajivua zigo la deni la Dowans na kusema endapo Mwanasheria Mkuu akitoa maoni ya Dowans kulipwa, watakaa na kulitazama zaidi na kama Tanesco inaweza kubeba mzigo huo.
Imeandikwa na Lucy Lyatuu;
Tarehe: 8th December 2010
WAZIRI wa Nishati na Madini, William Ngeleja amesema tatizo sio kujiuzulu, bali ni jinsi ya kutatua kero za umeme na kuhakikisha mgawo wa umeme unakwisha nchini.
Ngeleja alitoa kauli hiyo Dar es Salaam jana wakati akijibu maswali ya waandishi wa habari kuhusiana na madai ya kutakiwa kufanya hivyo kama ambavyo Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), David Kafulila alivyodai kupeleka hoja binafsi bungeni ya kutokuwa na imani naye.
Ngeleja alisema hayo ni mawazo ya Mbunge huyo na kamwe hawezi kuzuia mtu kutoa maoni yake kwa kuwa ana hisia kali kama ambavyo yeye (Ngeleja) anazo.
Madai ya Kafulila aliyatoa wakati alipotangaza kuwa anakusudia kupeleka hoja binafsi katika Mkutano wa Pili wa Bunge, Februari mwakani kutaka serikali iwajibike kwa kuliingizia Taifa hasara kwenye sekta ya umeme, kutokana na hukumu ya kesi ya Dowans na Tanesco ambayo Tanesco inapaswa kulipa Sh bilioni 185.
Kafulila pia anakusudia katika hoja hiyo, kulitaka Bunge liazimie kupiga kura ya kutokuwa na imani na Waziri wa Nishati na Madini, kwa madai kuwa ameshindwa kusimamia utekelezaji wa Sera ya Nishati na Mpango Kabambe wa Usambazaji wa Umeme nchini.
"Tatizo sio kujiuzulu, bali tatizo ni kufuatilia na kutatua kero za umeme zinazowasumbua wananchi.
Aliyosema Kafulila yanatokana na adha ambayo anakutana nayo kama ambavyo na mimi inanikumba," alisema Waziri huyo aliyerejeshwa na Rais Jakaya Kikwete kuongoza tena wizara hiyo.
"Nayaheshimu mawazo ya mheshimiwa mbunge.., siwezi kuzuia yeye kutoa maoni yake, ila aelewe kuwa serikali inaendelea kutatua tatizo hilo kwa nguvu kubwa," alisema Ngeleja.
Kuhusu Dowans, alisisitiza kuwa liko mikononi mwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambapo yeye ndiye atakayeshauri na kuamua kama kampuni hiyo italipwa ama halipwi.
Alisema Tanzania ni nchi inayoongozwa kwa misingi ya sheria na maoni ya watu binafsi hayawezi kuongelewa.
"Kwanza sitaki kufungua ukurasa wa suala hili, nchi hii inajielekeza katika misingi ya sheria, hivyo sheria zilizopo zitatumika pamoja na kupata ushauri wa Mwanasheria Mkuu," alisema Ngeleja.
Alisema kwa sasa faili liko kwa Mwanasheria Mkuu ili aweze kulipitia kutoa mawazo na ushauri wake juu ya suala hilo ila ifahamike kuwa nchi inaongozwa kwa misingi ya sheria na utawala bora.
Kwa mujibu wa Ngeleja, kwa sasa serikali haiwezi kuzungumzia hisia za watu, bali hatima yake itaamuliwa na Mwanasheria Mkuu na kukanusha taarifa iliyoandikwa katika moja ya vyombo vya habari nchini, kuwa serikali yajivua zigo la deni la Dowans na kusema endapo Mwanasheria Mkuu akitoa maoni ya Dowans kulipwa, watakaa na kulitazama zaidi na kama Tanesco inaweza kubeba mzigo huo.