Elections 2010 Pamoja na kujipa ushindi CCM mbona iko kwenye bumbuazi?

Chakaza

JF-Expert Member
Mar 10, 2007
39,759
71,139
Wote tunaifahamu CCM na tambo zake pale inapopata ushindi wowote hata uwe mdogo kiasi gani. Ni TOT, taarabu,ngoma na kejeli kwenda mbele. Sasa wamepatwa na nini hawa jamaa? maana pamoja na kujitangaza ushindi sura zao kuanzia viongozi wa juu hadi wanachama zinaonyesha kuduwaa na kama aina fulani ya aibu, lile bashasha lao la tambo limepotea kabisa.
Jee ni kwa vile wanaijua siri ya ushindi wao? au ni hofu kuwa wapinzani safari hii hawatakubali kuburuzwa? au wanaogopa kuwa ya Kenya yanaweza kutokea na mwishowe ni wahusika kupelekwa The Hague?
 
Niliishawahi kusema hapa kuwa kuna haina tatu za watu ndani ya CCM

1. Wenye dhamira hai
2. Wenye dhamira zinazoelekea kufa
3. Wenye dhamira mfu

Wachache wamefikia kwenye dhamira mfu na hao ndo unawaona kwenye vyombo vya habari wakiishabikia CCM eti imeshinda huku wakijua si kweli lakini kwa kuwa dhamira zao ni mfu hawaoni haya.

Kwa kuwa wengi wa CCM wako kwenye kundi la 1 na 2 na wanajua nini kimefanyika mpaka wanajiita washindi, naomba uudhurie mojawapo ya sherehe zao za ushindi utangundua kuwa wengi roho zao zinasononeka maana hawasherekei ushindi wa kweli, ni suhindi wa hira na dhamira zao zinawasuta!

Anayeiba hawezi sahau aliyemwibia hata siku moja!

Naomba siku moja mnipe mwonekano wa watu wa ssm katika sherehe zao na hasa subiri siku ya kuapishwa rahisi utaona atakavyokuwa akiongea, uso wake utakuwa kioo cha madhambi aliyoyatenda!
 
Niliishawahi kusema hapa kuwa kuna haina tatu za watu ndani ya CCM

1. Wenye dhamira hai
2. Wenye dhamira zinazoelekea kufa
3. Wenye dhamira mfu

Wachache wamefikia kwenye dhamira mfu na hao ndo unawaona kwenye vyombo vya habari wakiishabikia CCM eti imeshinda huku wakijua si kweli lakini kwa kuwa dhamira zao ni mfu hawaoni haya.

Kwa kuwa wengi wa CCM wako kwenye kundi la 1 na 2 na wanajua nini kimefanyika mpaka wanajiita washindi, naomba uudhurie mojawapo ya sherehe zao za ushindi utangundua kuwa wengi roho zao zinasononeka maana hawasherekei ushindi wa kweli, ni suhindi wa hira na dhamira zao zinawasuta!

Anayeiba hawezi sahau aliyemwibia hata siku moja!

Naomba siku moja mnipe mwonekano wa watu wa ssm katika sherehe zao na hasa subiri siku ya kuapishwa rahisi utaona atakavyokuwa akiongea, uso wake utakuwa kioo cha madhambi aliyoyatenda!
mkuu Paul jk nahisi yuko ktk kundi la 3.nahisi kwa upeo wake hata siku ya kuapishwa atafurahi tu maana hana upeo na utu wa kuona aibu kwa mabaya yaliotendeka.
 
Mzimu wa madhambi yao unawaandama na utaendelea kuwaandama kwa kadri matatizo ya nchi hii yanavyoongezeka.
 
Ile badget ya TOT ilihamishiwa kwenye kuwahonga wasimamizi wa uchaguzi na usalama wa taifa! PESA YOTE KUSA ISA!!
 
Unajua raha ya mashindano ni kushinda hata kwa kura moja utashangilia sana na kufurahia.
Ila ukichakachua ushangilie nini ,ni kama kujifanyia mazingaombwe
 
Amakweli mchuma janga hula na wakwao,naona wapinzani mnavyopeana moyo baada ya kukosa ushindi,Slaa alisha ahidi kuwa hakunakulala mpaka kieleweke ndio kimeeleweka.Poleni sana
 
Back
Top Bottom