Elections 2010 Pamoja na CCM kuchakachua matokeo, sheria hii kuitesa Chadema.......

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,467
911,172
Majimbo mengi ambayo CCM imeishinda Chadema tofauti ya kura ni ndogo lakini tofauti ya uwakilishi bungeni itakuwa kubwa kwa sababu viti maalumu vinagawiwa kwa kuzingatia idadi ya wabunge Bungeni badala ya idadi ya kura kila Chama ilizozipata....

Hii ni shubiri nyingine ambayo itajitokeza bungeni mara litakapozinduliwa...........kati ya kazi ya wabunge wa upinzani wanazopaswa kuzifanya ni kuandaa muswada wa kuibadilisha sheria hiyo ili kura za wapigakura ndizo zitumike kugawa nafasi za viti maalumu ili kuongeza hamasa ya wapigakura kushiriki kuchagua viongozi wao........

Utaratibu uliopo unazuia wapigakura wasiweze sauti yao kusikika bungeni kwa vyama ambavyo havikushinda moja kwa moja jimbo...........huu ni uonezi na unatia dosari demokrasia yetu................
 
mmmmmmh,nahisi watafanyia kazi wazo lako,ni zuri for sure ila binafsi sitaki viti maalumu na vya kuteuliwa sioni maana yake
 
Back
Top Bottom