PAMBA YAICHAPA POLISI MARA 3-2 DIMBA LA CCM KIRUMBA, Ubingwa DARAJA la KWANZA TZ

nngu007

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
15,862
5,797

[h=3][/h]





NA ALBERT G. SENGO:MWANZA


Ikitumia Vyema uwanja wake wa nyumbani Pamba Fc ya Mwanza leo imeanza vyema mchezo wake wa kwanza kundi C ya Ligi ya soka Daraja la kwanza ya Tanzania bara kwa kuichapa Polisi Mara kwa mabao 3-2.




Magoli ya Pamba yalifungwa na Mathayo William dakika ya 3, Shahban Makoba dakika ya 61 na Mashaka Kiumba dakika ya 70.


Upande wa timu ya Polisi Mara magoli yake yalifungwa na Kaichi Kaichi kwenye dakika ya 4, na Athumani Matutu aliyefunga bao la pili dakika ya 90.

Makocha wa timu zote mbili walipata fursa kuzungumza na Sports Xtra juu hali ya mchezo na nini matarajio kwa mechi zinazofuata za kundi C, Ligi soka Daraja la kwanza Tanzania bara.



Msikilize Wa kwanza ni kocha wa timu ya Pamba ya jijini Mwanza Ibrahim Mulumba..





Naye kocha wa Polisi mara Hafidh Salim amewaumu wachezaji wake kuingiwa kitete na mchezo huo wakiacha maelekezo yake na kucheza kila mmoja kimpango wake...




MWISHO

SOURCE; G SENGO
 
Back
Top Bottom