Pamba imenasa sikioni

Ommydee

Member
May 10, 2016
18
13
Jmn habari zenu naomba msaada wenu nilikuwa nasafisha sikio kwa Banat mby pamba imenasa ndani hata kuonekana haionekani icho kipamba msaada ndugu zng
 
ilisha wahi kunitokea, usiweke maji sikioni mkuu, nilikuwa kijijini, kituo cha afya yule mama alichukua hizi sindano za kawaida za hospitali akaikunja kidogo mezani kule kwenye ncha, haikuchukua sekunde 15 akanionesha pamba aliyoitoa kwa ile sindano, niliogopa sana maana nilihisi anaweza toboa ngoma ya sikio, ndo ivo tena juzi niliporudi pale bush nikaambiwa yule mama karudi kwao magu kamtumbua vyeti feki
 
Jmn habari zenu naomba msaada wenu nilikuwa nasafisha sikio kwa Banat mby pamba imenasa ndani hata kuonekana haionekani icho kipamba msaada ndugu zng
muda wa kupost humu unautoa wapi badala ya kwenda hospitali?unatafuta kiki?nenda kwa bodaboda wenzio ukae na yule vehicle!
 
Acha upoyoyo, Kata sikio ondoa pamba faster.

Kama unaogopa hebu mwambie Mkurya au Masai hapo jirani afanye vyake.

Mwisho, ndiyo ukome kutumia pamba za wachina kutolea uchafu masikioni.
 
Hiyo iliwahi kunitokea...Mwanzo nikatia maji sikioni alafu nikaruka ruka shingo ikiwa upande haikusaidia kitu.

kesho yake asubuhi nikaenda mahabara...Dokta akachungulia sikioni akasema haoni kitu nikaaza kuogopa huoni kitu namna gani wakati mi nakwambia pamba imenasia humo ebooo.

Mi nikawa nime-panic uoga umenishika Dokta nae anasisitiza humu sikioni hakuna kitu Hiyo pamba labda ilitoka usingizini bila wewe kujua.

Basi nikaanza kulia pale Nikim-bembeleza Dokta aangalie tena kwa umakini maana sikio lilikuwa zito na nalisikia kabisa linalia nzeeeeeeeee yule Dokta kwa huruma akaniambia lala tena akachukua bomba la sindano akalitia maji alafu akayatia sikioni baada ya dakika 5 akachukua kibanio akaingiza sikioni chokoa sekunde 20 katoa nayo.

pale pale kelele sikioni zikaisha na nikapona kabisa huu mwaka 5 sijawahi kutia pamba sikioni zaidi ya kutia njiti ya kibiriti...wahi hospital ukapate tiba
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom