Pakistani yasitisha uhusiano na India kutokana na mzozo katika eneo la Kashmir

Influenza

JF-Expert Member
Jul 1, 2018
1,438
3,333
Pakistan imetangaza hatua ya kumfurusha mwanadiplomasia wa ngazi ya juu wa India na kusitisha biashara kati yake na India kufuatia mzozo wa eneo la Kashmir.

Wakati huo huo Umoja wa Mataifa, UN umeelezea hofu yake kufuatia hatua ya hivi karibuni ya India kuiondolea Jimbo la Kashmir, mamalaka ya kujitawala ikisema "itachangia ukiukwaji wa haki za binadamu".

Msemaji wa UN amegusia hatua ya kukatiza huduma za mawasiliano, kuwazuilia viongozi wa jimbo hilo na kupiga marufuku mikutano ya kisiasa baadhi ya mambo yanayoweza kuchangia hali ya taharuki katika eneo hio.

maelfu ya maafisa wa usalama wamekuwa wakishika doria katika barabara za eneo hilo.

Visa vya maandamano na makabiliano ya mawe vimeripoti, licha ya kukatizwa kwa mawasiliano na kuwekwa kwa amri ya kutotoka nje.

Wakashmir katika maeneo mengine nchini humo wamesema kuwa hawana njia ya kuwasiliana na familia zao. Baadhi ya viongozi wa eneo hilo pia wamezuiliwa

India na Pakistan - huko nyuma zilishawahi kupigana vita kutokana na mzozo wa eneo hilo, je dunia inaelekea kushuhudia tena mapambano ya nchi hizo ambazo tayari zinajihami na silaha nzito za nyukilia?

Kwanini Kashmir ni eneo tata?
Kashmir ni eneo lililopo kwenye safu za milima ya Himalaya na nchi zote mbili India na Pakistani zinadai kuwa ni eneo lao.

Katika kipindi cha ukoloni wa Mwingereza jimbo la Jammu na Kashmir lilikuwa na hadhi ya kujitawala kupitia kiongozi wa makabila, lakini likajiunga na India mwaka 1947 katika kipindi ambacho Bara Hindi lilipatiwa uhuru na kugawanywa katika mataifa mapya ya India na Pakistani.

Nchi hizo mbili huenda zikatumbukia vitani na kujikuta kila mmoja akishikilia sehemu ya eneo hilo baada ya makubaliano ya kusimamisha mapigano yalipoafikiwa.

Kumekuwa na ghasia katika upande wa jimbo hilo utakaotawaliwa na India kwa kipindi cha miaka 30 iliyopita.

Makundi ya wanaharakati wanaotaka kujitenga na India yamekuwa yakishinikiza kupewa uhuru wao.

Mwanzoni mwa mwezi wa Agosti, kulikuwa na dalili kuwa kuna jambo kubwa lingetokea katika jimbo la Kashmir.

Makumi ya maelfu ya wanajeshi wa ziada wa India yalipelekwa kwenye eneo hilo.

Shughuli kubwa ya kuhiji ya kihindu ilikatazwa na mamlaka, shule na vyuo viliamriwa kufungwa.

Watalii waliamriwa kuondoka mara moja na huduma za simu na mtandao wa intaneti kufungwa.

Viongozi wote maarufu wa kisiasa wa eneo hilo waliwekwa katika vizuizi kwenye nyumba zao.

Lakini wakati hayo yote yakiendelea, hofu kubwa ilikuwa ni kwamba ibara ya 35A ya katiba ya India ingelifutiliwa mbali.

Ibara hiyo ndiyo inayoipa Kashmir upekee na hadhi ya kujitawala.

Serikali ikashangaza kila mmoja kwa kufuta ibara nzima ya 370 ambapo 35A ni ibara ndogo, na sehemu hiyo ya katiba ndiyo imekuwa mwongozo wa sera za nchi hiyo juu ya Kashmir kwa miongo saba iliyopita.
 
Wahindi wapumbavu sana, eneo lote mlilonalo still mnataka na kashmir! Kwanza jina lenyewe la mji/kashmir haliendani na wala pilipili.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom