sky soldier
JF-Expert Member
- Mar 30, 2020
- 5,408
- 19,026
Nyumbani kwangu hapa naishi na mke na watoto wangu wawili pamoja na binti wa kazi na ndugu wawili.
Sasa kuna kipindi kuna paka mdogo alikutwa maeneo ya karibu na mtoto wangu basi mtoto wangu huyo akamleta.
Ni kipaka cheupe chenye madoa ya brown kwa mbali, kilikuwa kidogo sana, Binafsi nilikataa kufuga paka nyumbani kwangu ila basi nikakubali kishingo upande baada ya wife kuwa upande wa mtoto wangu kwamba wamfuge.
Sikua na muda na huyo paka kabisa japo yeye nlikuwa namuona anavyokazana kufosi nimzoee, mfano alikuwa anapenda kupita pita chini ya miguu na hata napomfukuza alikuwa anarudi, Nlikuwa nashangaa inakuwaje paka hakazani kujenga mazoea na watu waliomzoea kama wife na watoto ila huku ambako hajaliwi yeye ndio anakutaka.
Kuhusu kumlisha wala hapakuwa na shida, Nlikuwa nashangaa sana jinsi anayvyojaliwa na watoto na wife, maziwa anapewa na kuna wakati mwengine ananunuliwa samaki.
Sasa kuanzia juzi sijui alipatwa na nini ila niliskia tu anaumwa, nikapotezea maana hanihusu sana, mtoto alikuja kuniasa nimwite daktari wa mifugo ila nikaona hii ni kuchezea pesa sasa maana huyu paka anakufa kama paka wengine tu, Ila alipoenda kwa mama yake naona daktari aliletwa sijui hata kilichoendelea.
Leo nipo nje hapa napumzika akaja analia lia nyau, nyau, nyau anapita pita kwenye miguu, namtoa anarudi, namtoa anarudi, basi nikamwacha tu, sasa naamka kwene kiti ile namwangalia nakuta katulia tuli, kumtikisa naona hamna response, nikajua tu huyu kashakata roho.
Anyway haikunistua sana ila jambo nalojiuliza hivi viumbe vikikufia karibu je kuna tatizo hasa katika ulimwengu wa kiroho?
Ni salama kuwazika kwenye eneo lako au ni bora kuwazikia mbali kabisa na kwako?
Sasa kuna kipindi kuna paka mdogo alikutwa maeneo ya karibu na mtoto wangu basi mtoto wangu huyo akamleta.
Ni kipaka cheupe chenye madoa ya brown kwa mbali, kilikuwa kidogo sana, Binafsi nilikataa kufuga paka nyumbani kwangu ila basi nikakubali kishingo upande baada ya wife kuwa upande wa mtoto wangu kwamba wamfuge.
Sikua na muda na huyo paka kabisa japo yeye nlikuwa namuona anavyokazana kufosi nimzoee, mfano alikuwa anapenda kupita pita chini ya miguu na hata napomfukuza alikuwa anarudi, Nlikuwa nashangaa inakuwaje paka hakazani kujenga mazoea na watu waliomzoea kama wife na watoto ila huku ambako hajaliwi yeye ndio anakutaka.
Kuhusu kumlisha wala hapakuwa na shida, Nlikuwa nashangaa sana jinsi anayvyojaliwa na watoto na wife, maziwa anapewa na kuna wakati mwengine ananunuliwa samaki.
Sasa kuanzia juzi sijui alipatwa na nini ila niliskia tu anaumwa, nikapotezea maana hanihusu sana, mtoto alikuja kuniasa nimwite daktari wa mifugo ila nikaona hii ni kuchezea pesa sasa maana huyu paka anakufa kama paka wengine tu, Ila alipoenda kwa mama yake naona daktari aliletwa sijui hata kilichoendelea.
Leo nipo nje hapa napumzika akaja analia lia nyau, nyau, nyau anapita pita kwenye miguu, namtoa anarudi, namtoa anarudi, basi nikamwacha tu, sasa naamka kwene kiti ile namwangalia nakuta katulia tuli, kumtikisa naona hamna response, nikajua tu huyu kashakata roho.
Anyway haikunistua sana ila jambo nalojiuliza hivi viumbe vikikufia karibu je kuna tatizo hasa katika ulimwengu wa kiroho?
Ni salama kuwazika kwenye eneo lako au ni bora kuwazikia mbali kabisa na kwako?