Sasa hilo jicho la tatu na haya mawili ya gorori lipi linaona mbali zaidi katika kutafakari na yaani lenye upeo mkubwa!! 2 au 3?Karibu bila shaka
Elezea zaidi mkuuAnza na meditation
Jitenge na dunia ya siasa
Jitenge na dunia ya starehe
Acha kabisa kutumia vilevi na nyama
Je umewai kujiuliza kabla hujazaliwa ulikuwa wapi? Usinisimulie kuhusu biology nazungumzia kiroho (spiritually). Ukifa unarudi ulipokuwepo kabla hujazaliwa (nyumbani) kumbuka roho haifi sasa kule utapata matokeo yako namna ulivyoishi Duniani.Ok, nimekupata mkuu, je huko nyumbani ndio wapi sasa?
Nitajuaje kama hapa nilipo sasa ndio nyumbani au ndio nimezaliwa upya? Hiyo evidence ya mimi kuja kuwa paka au mtoto wa tajiri we umeijuaje kwa kutumia methodology ipi? Swali Langu lipo palepale kwa nini tupo hapa duniani, tunaishi na tunakufa? Lengo la kuja hapa duniani ni nini? Je umewahi kufikiri usingekuwa binadamu ungekuwa kiumbe gani labda? Je madhumuni ya haya maisha ni kitu gani?Je umewai kujiuliza kabla hujazaliwa ulikuwa wapi? Usinisimulie kuhusu biology nazungumzia kiroho (spiritually). Ukifa unarudi ulipokuwepo kabla hujazaliwa (nyumbani) kumbuka roho haifi sasa kule utapata matokeo yako namna ulivyoishi Duniani.
Kama uliishi vizuri Duniani muendelezo wako utakuwa mzuri unaweza kuzaliwa tena kama binadamu chini ya wazazi matajiri wakati kabla walikuwa maskini.
Kama uliishi vibaya Duniani muendelezo wako utakuwa mbaya pia unaweza kuzaliwa kama paka au mbwa au kiumbe chochote cha ajabu.
Well said.Nimepitia thread yako naanza kuunganisha matukio. Nilichokielewa Ni kwamba jicho la tatu linahusiana sana na power of meditation. So it depends on what you meditate.
Kama muda mwingi una meditate neno la Mungu hata Yale yatakayokujia yatakuwa ya kimungu zaidi. Ukikaa Ku meditate habari za kiganga na kichawi kwa mfano muda wote movies unazotazama zikawa na uhusiana na mambo ya kichawi lazima reflection ya jicho la tatu itakupeleka kwenye mambo ya kutisha.
hakuna shida kabisa, hiyo ni normal muscle twitchingNakukubali sana mkuu mshana mimi jicho langu la kulia linachezacheza sana hivi kwa linafanya hivyo naomba ufafanuzi wako mkuu maana linanipa fikra sana naomba Msaada wako mkuu
Asante na pole sana jitahidi uanze na tahajudi huo ndio msingi wa kuelekea kufungua jicho la tatuNimepitia mara nyingi kusoma post zako zimenivutia sana na sasa nataka kuona mambo tofauti nimechoka kuona mambo yale yale kila siku kibaya zaidi nimehangaika sana kwa waganga lakini sikumuamini hata mmoja kwa kifupi na mengi sana ya kueleza ila naomba ufafanuzi kuhusu ipi ya kuanzia baina ya tahajudi na jicho la tatu nataka kujua na kuelewa mambo yalionizunguka nimechoka kuwaza naamini hapa ndio mahali sahihi na mtu sahihi naomba Msaada wako
Asalaam wakuu
Nimefuatilia bandiko la Mshana Jr kwa umakini mkubwa maana mada kama hizi ni chakula ya ubongo.
Kwanza napenda kukiri kuwa jicho la tatu sio jambo la kufikirika, ni lango ambalo likifunguka basi binadamu unakuwa na ufahamu mkubwa kuliko kawaida.
Pia kwa wajuzi wa mambo ya auras na chakras wakina Rakims wanaweza kuongelea zaidi ushiriki wa jicho la tatu katida meditation.
Ni muhimu kufahamu elimu kama hizi maana zinafungua cells za ubongo zilizokuwa zimelala.
Nawasilisha.
Jicho la tatu hilo... Una foreseen vision jiendelezeUkiwa unaota Image inatokea kwenye Ubongo(Bila shaka kupitia third eye)..Mr Mshana hivi inakuaje Mtu anaona Matukio ambayo hayajawahi kutokea katika maisha ya muda flani,mfano mimi nimewahi kuona matukio kama mawili mwaka jana kabla ya kutokea physically mwaka huu hadi nikaogopa..kwa sasa Nina mpango wa kuwa na Diary kuandika Ndoto..
Haya yote yamefichwa na Vatican city
Hutaamini utakachogundua hapa kuhusu paji lako la uso...hapa ndio asili ya neno kipaji ilipatikana..hapa napo ni lango hapa ndio penye njia ya kuingilia mlango wa sita baada ya ile mitano. Hili ni jicho la ndani jicho lisioonekana.lango kuu la kiroho.
Tutaenda kwa mitazamo yote ya kidini na kiimani, kisayansi, kihisia na hata kwenye nguvu za giza.
1. Third Eye - Thalamus - Eye of Horus
Hapa ni kwa mtazamo wa kisayansi nafikiri ni kwenye somo la anatomy kuhusu ubongo, jicho la tatu linaonekana katikati ya ubongo (zingatia katikati) vertebrate brain hapo ndio zinapozalishwa homoni za kulaza au kuamsha hisia maono usingizi nk.
2. Mathematics
Katika ulimwengu wa mahesabu na hesabu, wanamahesabu kwenye ishu za ratio cos na tan watatusaidia hapa.
3. Tahjud (Meditation)
Kwenye tahajudi wale waliosoma chakra na habari za milango nane, ukiangalia vizuri huo mchoro chakra ya sita ndio ya kuingilia mlango wa sita wa fahamu.
4. Baptism & Sijda
Kiimani katika ukristo, kwenye ubatizo alama ya msalaba kwenye paji la uso ndio hukamilisha tendo na kuwa Mkristo kamili sasa.. Lakini pia ukisoma kitabu cha ufunuo na habari za kutiwa Muhuri katika paji la uso utafahamu zaidi..
Kwenye Uislam tunajua nini maana na umuhimu wa swala tano na kuthibitisha uchaji wako katika swala tano ni sigida kwenye paji la uso.
5. A kiss on the Forehead
Kwenye mahusiano busu kwenye paji la uso ni tofauti kabisa na mabusu ya sehemu nyingine yoyote.
6. FREEMASONRY
Kwenye imani za mpinga Kristo freemason satanism nk alama yao kubwa ni jicho la tatu
7. SEVERE PUNISHMENTS (WATERBOARD)
Kwenye adhabu na mateso mbalimbali paji la uso hutumika kuleta adha ya ajabu mwilini... Mateso ya water board ni mfano mmojawapo. Unalazwa chini unafunikwa kitambaa usoni kisha unamwagiwa maji.. Ni aina ya adhabu isiyoumiza mwili bali inayoumiza hisia.
8. Michezoni:
Kwenye mchezo wa ngumi alama za juu ni zile ambazo zinaangukia kwenye paji la uso.
Nimejaribu kwenda na picha kuokoa ufafanuzi wa maneno mengi... Tunaishi kwenye ulimwengu wa ajabu mno.. Tunashiriki kitu hicho hicho lakini kwa maana matumizi na mitizamo tofauti. Tunafundishwa kutolala chali kuepuka ndoto za mauzauza na majinamizi kumbe siri ni jicho la tatu jicho la maono.
Manabii na watenda miujiza hupenda kuwapuliza ama kuwashika watu penye paji la uso na kifuatacho hapo ni mzinga kama si kupiga kelele... Baadhi ya tiba mbadala hutumia paji la uso kama lango la uponyaji.
Wahindi na wahindu kwenye imani zao hujipaka rangi katikati ya macho kama sehemu ya ibada nk.
Jaribu kutafakari kwa hatua hiki kinachoitwa jicho la tatu, paji la uso, imani yako na maisha yako ya kila siku... Mwishowe tunaweza kujikuta tunaabudu paji la uso kwa muktadha tusiojua.