Paji la uso na siri ya jicho la tatu

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,633
697,536
f6e63668ac1c4a88887ca94b0bd11c01.jpg


Hutaamini utakachogundua hapa kuhusu paji lako la uso...hapa ndio asili ya neno kipaji ilipatikana..hapa napo ni lango hapa ndio penye njia ya kuingilia mlango wa sita baada ya ile mitano. Hili ni jicho la ndani jicho lisioonekana.lango kuu la kiroho.

Tutaenda kwa mitazamo yote ya kidini na kiimani, kisayansi, kihisia na hata kwenye nguvu za giza.

1. Third Eye - Thalamus - Eye of Horus
c028b8f6365bdd2fb44aaf6796fdf17f.jpg


Hapa ni kwa mtazamo wa kisayansi nafikiri ni kwenye somo la anatomy kuhusu ubongo, jicho la tatu linaonekana katikati ya ubongo (zingatia katikati) vertebrate brain hapo ndio zinapozalishwa homoni za kulaza au kuamsha hisia maono usingizi nk.

2. Mathematics
22f4856d4325c03356542c3c19a96824.jpg


Katika ulimwengu wa mahesabu na hesabu, wanamahesabu kwenye ishu za ratio cos na tan watatusaidia hapa.

3. Tahjud (Meditation)
1a3f1076a0eecca2d21fb8771039a216.gif


Kwenye tahajudi wale waliosoma chakra na habari za milango nane, ukiangalia vizuri huo mchoro chakra ya sita ndio ya kuingilia mlango wa sita wa fahamu.

4. Baptism & Sijda
b23bbe047b4fed53bc8acd968bfbde9f.jpg
7581aaa5dd84dc3d74104360bf95c259.jpg


Kiimani katika ukristo, kwenye ubatizo alama ya msalaba kwenye paji la uso ndio hukamilisha tendo na kuwa Mkristo kamili sasa.. Lakini pia ukisoma kitabu cha ufunuo na habari za kutiwa Muhuri katika paji la uso utafahamu zaidi..

Kwenye Uislam tunajua nini maana na umuhimu wa swala tano na kuthibitisha uchaji wako katika swala tano ni sigida kwenye paji la uso.

5. A kiss on the Forehead
95e4888b95b1f04ef937618e752fd13d.jpg


Kwenye mahusiano busu kwenye paji la uso ni tofauti kabisa na mabusu ya sehemu nyingine yoyote.

6. FREEMASONRY
2eaa591e515e975051f9640238953750.jpg

Kwenye imani za mpinga Kristo freemason satanism nk alama yao kubwa ni jicho la tatu

7. SEVERE PUNISHMENTS (WATERBOARD)
8654ca9f3d106b3012aa7228ab664632.jpg


Kwenye adhabu na mateso mbalimbali paji la uso hutumika kuleta adha ya ajabu mwilini... Mateso ya water board ni mfano mmojawapo. Unalazwa chini unafunikwa kitambaa usoni kisha unamwagiwa maji.. Ni aina ya adhabu isiyoumiza mwili bali inayoumiza hisia.

8. Michezoni:
Kwenye mchezo wa ngumi alama za juu ni zile ambazo zinaangukia kwenye paji la uso.

Nimejaribu kwenda na picha kuokoa ufafanuzi wa maneno mengi... Tunaishi kwenye ulimwengu wa ajabu mno.. Tunashiriki kitu hicho hicho lakini kwa maana matumizi na mitizamo tofauti. Tunafundishwa kutolala chali kuepuka ndoto za mauzauza na majinamizi kumbe siri ni jicho la tatu jicho la maono.

Manabii na watenda miujiza hupenda kuwapuliza ama kuwashika watu penye paji la uso na kifuatacho hapo ni mzinga kama si kupiga kelele... Baadhi ya tiba mbadala hutumia paji la uso kama lango la uponyaji.

Wahindi na wahindu kwenye imani zao hujipaka rangi katikati ya macho kama sehemu ya ibada nk.

Jaribu kutafakari kwa hatua hiki kinachoitwa jicho la tatu, paji la uso, imani yako na maisha yako ya kila siku... Mwishowe tunaweza kujikuta tunaabudu paji la uso kwa muktadha tusiojua.
 
Kuna kitu nimeanza kukielewa hapo hasa nilivyosoma hicho kitabu cha KUTOKA 13:16 kwenye Biblia.

Ngoja tuanze sasa kufukunyua nondo za huu uzi taratibu.

Ipi ni athari ya kulala chali, na kwa nini watawala wengi wa zamani walikuwa hawalali kifudi fudi??

Ukiangaliakumbu kumbu za mafarao wa misri walikuwa wanawekewa kabisa mto wa kulaliaambao ulikuwa hauwaruhusu kugeuza vichwa wakati wa kulala, na wote walikuwa wanalala chali.

Kuna siri gani hapa.??
 
Kuna kitu nimeanza kukielewa hapo hasa nilivyosoma hicho kitabu cha KUTOKA 13:16 kwenye Biblia.

Ngoja tuanze sasa kufukunyua nondo za huu uzi taratibu.

Ipi ni athari ya kulala chali, na kwa nini watawala wengi wa zamani walikuwa hawalali kifudi fudi??

Ukiangaliakumbu kumbu za mafarao wa misri walikuwa wanawekewa kabisa mto wa kulaliaambao ulikuwa hauwaruhusu kugeuza vichwa wakati wa kulala, na wote walikuwa wanalala chali.

Kuna siri gani hapa.??
Hata maiti halazwi kifudifudi
 
Naamini tuna wanafunzi wengi wa Buddhism humu ndani hasa kwenye kipengele cha spiritual awakening.

dc556203657c470dbe63ccbc7d5602a4.jpg


Unaposoma hiyo topic na ukaja kulinganisha na huu mchoro unapata mtiririko wenye kuleta uhalisia wa ajabu kabisa.

c19a91f68d318dd66366655ef11060a7.jpg


Lakini pia kuna baadhi ya mimea hutumika kiimani kama stimuli/stimulas ya jicho la kiroho... Ni kama shortcut ya meditation au ya kuingia mlango wa sita kupitia moshi.

f0ae1602a46f2fb9ece65cbd9be7812f.jpg


Ndio maana mijadala haiishi kuhusiana na mmea... Shida moja ya mmea ni kwamba huamsha pande mojawapo kati ya zile mbili za mawasiliano ya kiroho ndani ya nafsi upande wa hasi na upande wa chanya... Inategemea kichocheo kipi kitawahi.

Kuna hii kitu mtu akifanya mambo yasiyoeleweka anaambiwa ni madhara ya bhangi za kuvutia chooni, ni kama mzaha vile lakini chooni panajulika kama mlango wa kuzimu na makazi ya roho wachafu...

Sasa bhangi inaamsha mlango wa sita kupitia jicho la tatu halafu unalivutia chooni, hapa unachanganya hasi na chanya. Matokeo yake lazima kichwa kipate moto.
 
I liked it jinsi nilivyokuwa na meditate baada ya kula ganja,it was such an awesome moment. nilikuwa naweza kuyapanga na kuyapangua mambo yangu na yakaenda fresh kabisa...badae ikawa Kila nikivuta najuta sanaaa,yani hata kosa la mwaka 2000 nalikumbuka looote af najuta sanaaa, basi nkaiacha. Ila ntairudia after 4 years if God wishes.

Nakufuatilia mkuu @ mshana jr.
 
kuna jamaa kitaani akivuta bangi anasema anawasiliana na akina Obama , bush , putin n.k hiyo inakuwa kweli?
imebidi nicheke kwa kujibana hapa nilipo unajua ile kitu inaamsha hisia za mlango wa sita kupitia hilo jicho la tatu
Lakini katika mlango ule wa hisia alishajenga mawazo ya kuonana na hao watu kwahiyo kinachotokea ni kama tu mlango wa hisia kubeba ujumbe na kuupeleka kama ulivyo kwenye mlango wa sita
 
I liked it jinsi nilivyokuwa na meditate baada ya kula ganja,it was such an awesome moment. nilikuwa naweza kuyapanga na kuyapangua mambo yangu na yakaenda fresh kabisa...badae ikawa Kila nikivuta najuta sanaaa,yani hata kosa la mwaka 2000 nalikumbuka looote af najuta sanaaa,basi nkaiacha.
ila ntairudia after 4 years if God wishes.

nakufuatilia mkuu @ mshana jr
Minds tricks and inner creation in two phases
First phase all things related to positive states
Second phase all things related to negative state
Sometimes they work simultaneously and sometimes they work periodically
 
Back
Top Bottom