Padri Mapunda taabani, anahitaji msaada

kilimasera

JF-Expert Member
Dec 2, 2009
3,068
266
Wednesday, 01 December 2010 21:50
0
digg

Joyce Joliga, Songea
WAUMINI wa Kanisa Katoliki wa Parokia ya Matogoro, Manispaa ya Songea, wamelazimika kuendesha mchango kwa ajili ya Padri Alphonce Mapunda, ili aweze kupata matibabu ya mgongo Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam.

Hatua hiyo ilifikiwa juzi baada ya kuguswa na tatizo linalomkabili kiongozi wao, huku wakiombwa na watu wengine wenye mapenzi mema ya kumsaidia kupata matibabu.

Muumini mmoja, Grace Joram, alisema wananchi wote wenye mapenzi mema wanaombwa kumsaidia mtumishi huyo ili apatiwe matibabu kwani, anakabiliwa na tatizo hilo kwa wiki tatu sasa.
Joram alisema kabla ya kukumbwa na ugonjwa wa uti wa mgongo, Padri Mapunda alikuwa mstari wa mbele katika kutoa huduma za maombezi kwa waumini na wananchi, bila kujali dini wala kabila na kwamba, aliweza kusuluhisha migogoro mbalimbali ya wana ndoa.

"Jamani tumsaidieni Padri wetu kwani, amekuwa mtu mwema sana kwetu, maumivu aliyonayo sasa ni makali na anahitaji msaada wetu ili aweze kupata matibabu kumsaidia kupata matibabu kutamrejeshea tumaini jipya," alisema Grace.

Naye Jane Mbawala alisema ameguswa na tatizo hilo na ana imani wananchi na waumini wa kanisa hilo, watamsaidia kiongozi huyo fedha za matibabu na mahitaji mengine muhimu.
.
Alisema waumini wengi wameguswa na tatizo hilo kwani, licha ya kuonekana kuwa ni dhaifu na kuanguka mara tatu akitoa huduma ya kiroho Kanisa la Mateka, aliweza kuendelea kusaidia waumini hali ambayo iliwafanya kuguswa na jambo hilo.
Kwa upande wake, Padri Nicodems Luambano, aliwaomba waumini na watu wenye mapenzi mema kumsaidia mtumishi huyo ili aweze kupata matibabu.
Watakaoguswa wampigie simu au kutuma fedha kwenye namba 0713 33 17 22 na 0754 66 17 22
 
Unamaanisha amekosa pesa ya matibabu ama.....MAOMBI ZAIDI?
Haiingii akilini faza na kanisa kukosa pesa ya matibabu kiasi cha kuombaomba kwa wananchi, kuna watu wengi sana wasio na msaada wowote wanateseka! Pole sana faza-sisi mm na familia yangu tunakuombea ulinzi wa mungu! Amen
 
Pole sana Mtumishi wa Mungu, naamini atasaidiwa tu maadamu kuna namba umeweka hapo, poleni sana.

Hivi hawana majina mengine zaidi ya majina ya wanyama, Mapunda akamwambia Mbawala????? Just kidding
 
huku ni kudhalilisha kanisa katoliki.kulingana na maelezo hayo nina shaka kama padri huyo bado ni mhudumu wa kanisa katoliki.tuambieni vizuri.MARIA MATER INFIRMORUM ORA PRO PADRE MAPUNDAE
 
Kanisa langu hilo nilipopatia Komunio ya kwanza mwaka 1985. wakati huo yupo pale Father Hunja, akiwa ndo paroko wa pale, palikuwa na neema sana sasa nashangaa watu wanatembeza bakuli kuomba msaada duh patakuwa pamebakia kitu kweli jamani?
 
Pole sana Mtumishi wa Mungu, naamini atasaidiwa tu maadamu kuna namba umeweka hapo, poleni sana.

Hivi hawana majina mengine zaidi ya majina ya wanyama, Mapunda akamwambia Mbawala????? Just kidding

Mkuu Elli majina ya kawaidfa hayo hata Ulaya wapo akina JOhn BULL, John Deere, Glen Antelope. unashangaa Mapunda na Mbawala, mkuu kuna akina Mbuzi, Nguruwe, Tembo na kadhalika.
 
Insha'Allah Mwenyezi Mungu atamjaalia apate matibabu ili apone haraka!
 
kanisa katoliki huwa halina tabia ya kutelekeza mapadre hata siku moja...

nadhani huyo alisha kuwa x-communicated na kanisa na hatoi huduma yoyote
 
Jamani huyu padri ni yule aliyekuwa hapa manzese catholic ambaye alikuwa anaiponda sana ccm?
 
Pole sana fadha na mi ntakuchangia japo kidogo na ni siri yangu ila kwa tigo pesa.nasubiri kucheka utumbo utakaoporomoshwa na malaria komavu.
 
Hii kweli ni aibu na siamini kabisa Father atembezewe bakuli la mchango kwa ajili ya matibabu. Jimbo kwanza linafanya nini? kila mwezi vigango vinawapelekea pesa kama mchango wa kuendesh jimbo ,hawawezi kulipia matibabu ya mtumishi wa Mungu huyu ama labda kuna uhasama na haijii akilini kabisa .
 
waliopost tunawaomba watupe status ya pd mapunda kuk kanisa kwa sasa,kwani bila hivyo mimi binafsi naona tunataka kuibiwa. Na kwanini tutume fedha kwenye cm za watu binafsi? Waweke akaunti ya parokia.je hakuna mapadri wanaomhudumia hadi taarifa ziwe hivyo? Kusema padre mgonjwa kutawaharibia zaidi,labda mueleze kama hayuko tena na kanisa hiyo ni case nyingine.nataka kuchangia milioni moja lakini naomba maelezo hayo.katoliki siyo kama kwa lwakatare yule mchungaji fisadi na feki
 
Katoliki kuna kanisa la mateka?? Mbona jina la kanisa hilo limekaa kilokole zaidi!!!!!
 
kardinali pengo amchotee zile za memorundum of understanding
 
Jamani huyu padri ni yule aliyekuwa hapa manzese catholic ambaye alikuwa anaiponda sana ccm?

we nae maswala ya siasa yametokea wapi?
Toa msaada wa mawazo au fedha kama umeguswa sio kutaka kumjua ni wa wapi.
 
Jamani huyu padri ni yule aliyekuwa hapa manzese catholic ambaye alikuwa anaiponda sana ccm?
NDUGU, mAPUNDA WAPO WENGI.................Yule wa Manzese kwa sasa anaishi Uganda, na huyu Mapunda mwingine ni wa Matogoro kule Songea. Hivyo ni Mapunda mbili tofauti
 
huku ni kudhalilisha kanisa katoliki.kulingana na maelezo hayo nina shaka kama padri huyo bado ni mhudumu wa kanisa katoliki.tuambieni vizuri.MARIA MATER INFIRMORUM ORA PRO PADRE MAPUNDAE

This is not acceptable. Roman Catholic is very respected and can not allow this to happen.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom