Nkwesa Makambo
JF-Expert Member
- Aug 26, 2011
- 4,763
- 1,314
Kona ya Karugendo kwenye Gazeti la Raia Mwema 'Tujadili suala la Ushoga,linajadilika'
Nimesoma makala ya Padri wa zamani Privatus Karugendo yenye kichwa cha habari tajwa hapo juu,nimesoma kwa kuirejea mara mbili huku nikijaribu kuhusianisha kichwa cha habari na makala hausika,Kwa kusema kweli nimeshindwa kuelewa si tu huyu Padri wa zamani nini alikusudia katika makala hii.
Ametoa maelezo mazuri juu ya tamasha ya Jinsia lililofanyika mwezi uliopita na uhusiano uliokuwepo kati ya tamasha na mashoga na madhumuni halisi ya tamasha husika,katika maelezo yake amaejitahidi sana kuhusisha mmomonyoko wa maadili katika jamii yetu na jinsi jamii ilivypotoka katika huo mmomonyoko wa maadili,juhudi zake zote za kueleza juu ya mmomonyoko wa maadili zilijikita katika kueleza matokeo yake akihusianisha na mambo mengi machafu katika jamii huku ushoga ukiwekwa mbali bali akielezea juu juu kwamba ni matokeo ya uharibifu wa maadili.
kilichonistua sana ni Mtizamo wake mbaya dhidi ya waandishi wa habari ambao mwenyewe amewaita 'waandishi wa habari wenye mtizamo finyu na wenye malengo yao binafsi waliyaacha mengine yote na kuliwekea mkazo hili la ushoga' kwake yeye mwandishi wa habari asiyekubaliana na ushoga au watu wasiokubaliana na ushoga ni wale wenye nia ya kubinafsisha katiba.
Pamoja na kujieleza kidogo kwamba 'nia si kuunga mkono ushoga;bali uelewa wa kulishughulikia jambo lililopo (ushoga ni ukweli ulio katika jamii yetu,tunataka tusitake)'
Baada ya kupitia makala yake nimeshindwa kuelewa huyu x-padre ni SHOGA ANAYETAFUTA UHURU WA USHOGA WAKE au ni binadamu mwenye huruma kwa mashoga, naomba wanaJF hasa waliopitia makala yake wale wenye nia ya kulinda uhuru na haki za binadamu tujadili hoja zake ili tuweze kumtambua,sina uhakika sana na nini kilicholichefua kanisa katoliki kufikia kumtema padri huyu,Je ushoga waweza kuwa sehemu ya uovu wake kwenye kanisa uliosababisha atemwe?
Nawakilisha...
Nimesoma makala ya Padri wa zamani Privatus Karugendo yenye kichwa cha habari tajwa hapo juu,nimesoma kwa kuirejea mara mbili huku nikijaribu kuhusianisha kichwa cha habari na makala hausika,Kwa kusema kweli nimeshindwa kuelewa si tu huyu Padri wa zamani nini alikusudia katika makala hii.
Ametoa maelezo mazuri juu ya tamasha ya Jinsia lililofanyika mwezi uliopita na uhusiano uliokuwepo kati ya tamasha na mashoga na madhumuni halisi ya tamasha husika,katika maelezo yake amaejitahidi sana kuhusisha mmomonyoko wa maadili katika jamii yetu na jinsi jamii ilivypotoka katika huo mmomonyoko wa maadili,juhudi zake zote za kueleza juu ya mmomonyoko wa maadili zilijikita katika kueleza matokeo yake akihusianisha na mambo mengi machafu katika jamii huku ushoga ukiwekwa mbali bali akielezea juu juu kwamba ni matokeo ya uharibifu wa maadili.
kilichonistua sana ni Mtizamo wake mbaya dhidi ya waandishi wa habari ambao mwenyewe amewaita 'waandishi wa habari wenye mtizamo finyu na wenye malengo yao binafsi waliyaacha mengine yote na kuliwekea mkazo hili la ushoga' kwake yeye mwandishi wa habari asiyekubaliana na ushoga au watu wasiokubaliana na ushoga ni wale wenye nia ya kubinafsisha katiba.
Pamoja na kujieleza kidogo kwamba 'nia si kuunga mkono ushoga;bali uelewa wa kulishughulikia jambo lililopo (ushoga ni ukweli ulio katika jamii yetu,tunataka tusitake)'
Baada ya kupitia makala yake nimeshindwa kuelewa huyu x-padre ni SHOGA ANAYETAFUTA UHURU WA USHOGA WAKE au ni binadamu mwenye huruma kwa mashoga, naomba wanaJF hasa waliopitia makala yake wale wenye nia ya kulinda uhuru na haki za binadamu tujadili hoja zake ili tuweze kumtambua,sina uhakika sana na nini kilicholichefua kanisa katoliki kufikia kumtema padri huyu,Je ushoga waweza kuwa sehemu ya uovu wake kwenye kanisa uliosababisha atemwe?
Nawakilisha...