Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,890
- 6,896
[*=1]Speaker, Naibu na wenyeviti bungeni wanatabia ya kuwapendelea wabunge wa CCM
[*=1]Speaker, Naibu na wenyeviti wanawakandamiza wabunge wa upinzani
[*=1]Bunge sasa ni Chuo Kikuu cha matusi
[*=1]Ufisadi sasa imegeuzwa taaluma ya ajira serikalini
Spika Makinda, Ndugai walipuliwa
Padri Baptiste Mapunda wa Kanisa Katoliki Tanzania amewataka Spika wa Bunge, Anne Makinda, Naibu wake, John Ndugai na wenyeviti kuacha tabia ya kuwapendelea wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kuwakandamiza wa upinzani wakati wa vikao, hali ambayo imesababisha Bunge kuwa chuo kikuu cha matusi na kuhatarisha mustakabari wa usalama wa nchi.
Aidha, amesema hivi sasa nchi imejaa ufisadi ambao sasa imekuwa kama taaluma ambayo watu wanakweda kuisomea ili wanapoingia madarakani wajichotee fedha huku Watanzania wakiendelea kuwa maskini wa kutupwa.
Padri Mapunda alitoa kauli hiyo jana wakati akihubiri katika misa ya Jumapili kwenye Parokia ya Manzese ya Kanisa Katoliki jijini Dar es Salaam.
"Taifa limefika mahali pabaya sana, hivi sasa chuo kikuu cha matusi kimekuwa ni bungeni na kimsingi hayo yoye yanasababishwa na Spika na wasaidizi wake ambao wanaonyesha upendeleo wa wazi kwa wabunge wa CCM," alisema Mapunda na Padri Mapunda ambaye pia ni Mkurugenzi wa Shirika la Faidika Afrika Mashariki.
Huku akishangiliwa na mamia ya waumini wa kanisa hilo, Padri Mapunda alisema wakati wa uongozi wa Rais wa Awamu ya Kwanza Mwalimu Julius Nyerere nchi ilikuwa na heshima na amani, lakini hivi sasa wameingia madarakani viongozi wasio na maadili mema ambao wamepandikiza virusi na kuifanya nchi isiwe na amani.
Alisema viongozi wengi wa serikali wamekuwa mstari wa mbele kuhubiria amani, lakini wanasahau kutenda haki kwani nchi isiyokuwa na umoja ni hatari kwa usalama.
"Nyerere alikuwa nabii na mchungaji mwema aliyeweza kufanikisha kuyaunganisha makabila 120 nchini ambapo nchi kipindi hicho ilikuwa na amani, lakini leo hii wamekuja watu wamepandikiza virusi na sasa nchi haina amani kila siku ni matukio mabaya," alisema Padri Mapunda.
Alivishutumu vyombo vya usalama kuwa kimsingi vimeshindwa kulinda usalama wa wananchi hali ambayo imesababisha kuwepo kwa maovu mengi na kusababisha watu kuishi kwa hofu.
Alisema kwa mfano tukio la kutekwa na kuteswa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk. Stephen Ulimboka, vyombo vya dola vimeonyesha udhaifu mkubwa sana kwa kushindwa kuwakamata wahusika wakuu wa tukio hilo na ndiyo maana kumekuwa na uongo mwingi sana unaofanywa viongozi wa Jeshi la Polisi na Serikali kwa lengo la kuficha ukweli.
"Manyanyaso katika nchi yetu yamekuwa mengi sana kwa mfano Dk. Ulimboka kutekwa na kung'olewa meno na kucha ni hatari, mimi nitaendelea kumuombea Dk. Ulimboka apone arudi hapa nchini ili aje amwage ukweli hapa wa tukio hilo," alisema Mapunda. "Serikali ya CCM ihakikishe wananchi wanakuwa salama, lakini kwa sasa Tanzania siyo salama, Jeshi la Polisi linaonyesha upendeleo katika utendaji wake wa kazi, kimsingi tumefika pabaya miaka 50 tangu uhuru, tunahitaji manabii wa kuiongoza nchi," alisema Padre Mapunda.
KUHUSU AJALI
Padri Mapunda alisema Tanzania imekuwa kama nchi ya majanga ambayo kila siku ajali za barabarani, majini na angani zimekuwa zikitawala na kuongezeka kuwa hali hiyo ni matokeo ya kushindwa kwa waliopewa madaraka ya kusimamia maeneo hayo.
Aidha, amesema hivi sasa nchi imejaa ufisadi ambao sasa imekuwa kama taaluma ambayo watu wanakweda kuisomea ili wanapoingia madarakani wajichotee fedha huku Watanzania wakiendelea kuwa maskini wa kutupwa.
Padri Mapunda alitoa kauli hiyo jana wakati akihubiri katika misa ya Jumapili kwenye Parokia ya Manzese ya Kanisa Katoliki jijini Dar es Salaam.
"Taifa limefika mahali pabaya sana, hivi sasa chuo kikuu cha matusi kimekuwa ni bungeni na kimsingi hayo yoye yanasababishwa na Spika na wasaidizi wake ambao wanaonyesha upendeleo wa wazi kwa wabunge wa CCM," alisema Mapunda na Padri Mapunda ambaye pia ni Mkurugenzi wa Shirika la Faidika Afrika Mashariki.
Huku akishangiliwa na mamia ya waumini wa kanisa hilo, Padri Mapunda alisema wakati wa uongozi wa Rais wa Awamu ya Kwanza Mwalimu Julius Nyerere nchi ilikuwa na heshima na amani, lakini hivi sasa wameingia madarakani viongozi wasio na maadili mema ambao wamepandikiza virusi na kuifanya nchi isiwe na amani.
Alisema viongozi wengi wa serikali wamekuwa mstari wa mbele kuhubiria amani, lakini wanasahau kutenda haki kwani nchi isiyokuwa na umoja ni hatari kwa usalama.
"Nyerere alikuwa nabii na mchungaji mwema aliyeweza kufanikisha kuyaunganisha makabila 120 nchini ambapo nchi kipindi hicho ilikuwa na amani, lakini leo hii wamekuja watu wamepandikiza virusi na sasa nchi haina amani kila siku ni matukio mabaya," alisema Padri Mapunda.
Alivishutumu vyombo vya usalama kuwa kimsingi vimeshindwa kulinda usalama wa wananchi hali ambayo imesababisha kuwepo kwa maovu mengi na kusababisha watu kuishi kwa hofu.
Alisema kwa mfano tukio la kutekwa na kuteswa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk. Stephen Ulimboka, vyombo vya dola vimeonyesha udhaifu mkubwa sana kwa kushindwa kuwakamata wahusika wakuu wa tukio hilo na ndiyo maana kumekuwa na uongo mwingi sana unaofanywa viongozi wa Jeshi la Polisi na Serikali kwa lengo la kuficha ukweli.
"Manyanyaso katika nchi yetu yamekuwa mengi sana kwa mfano Dk. Ulimboka kutekwa na kung'olewa meno na kucha ni hatari, mimi nitaendelea kumuombea Dk. Ulimboka apone arudi hapa nchini ili aje amwage ukweli hapa wa tukio hilo," alisema Mapunda. "Serikali ya CCM ihakikishe wananchi wanakuwa salama, lakini kwa sasa Tanzania siyo salama, Jeshi la Polisi linaonyesha upendeleo katika utendaji wake wa kazi, kimsingi tumefika pabaya miaka 50 tangu uhuru, tunahitaji manabii wa kuiongoza nchi," alisema Padre Mapunda.
KUHUSU AJALI
Padri Mapunda alisema Tanzania imekuwa kama nchi ya majanga ambayo kila siku ajali za barabarani, majini na angani zimekuwa zikitawala na kuongezeka kuwa hali hiyo ni matokeo ya kushindwa kwa waliopewa madaraka ya kusimamia maeneo hayo.