Padre Dkt. Kitima: Aliyemuua Kibao tunamlaani, amefanya kosa baya, ni chukizo kwa Mungu

Waufukweni

JF-Expert Member
May 16, 2024
1,552
4,169
Padre Dkt. Charles Kitima, Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki Tanzania (TEC), ametoa kauli nzito akisema kuwa viongozi wa dini lazima waonyeshe wazi kwamba aliyehusika katika mauaji ya Ally Mohamed Kibao amefanya kosa kubwa na ni laana kwa Mwenyezi Mungu.

Pia, Soma: Dar: Ali Mohamed Kibao, kiongozi wa CHADEMA auawa na mwili kutelekezwa Ununio ukiwa umeharibika sana

Akizungumza kuhusu tukio hilo, Padre Kitima alisisitiza kuwa, "Aliyemuua Kibao amefanya kosa baya na ni laana kwa Mwenyezi Mungu. Kama viongozi wa dini, lazima tuseme hili. Tunalaani vikali vitendo vya uhalifu kama hivi."

Aliongeza, "Unafikiri watoto wa Mzee Kibao, aliyeuawa kinyama, wataonana vema na wale wanaohisiwa? Hii imejenga chuki kubwa kati ya familia na jamii. Tunapiga vita, tuna laani, na tunahitaji aliyemuua Kibao atubu kwa Mungu wake au achukuliwe hatua na sheria."

Padre Kitima alisisitiza kuwa, kama viongozi wa dini, ni jukumu lao kutoa ujumbe wa haki na amani, na kuonya dhidi ya vitendo vya kinyama vinavyovuruga jamii na kuleta machafuko.
Soma:
 
Padre Dkt. Charles Kitima, Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki Tanzania (TEC), ametoa kauli nzito akisema kuwa viongozi wa dini lazima waonyeshe wazi kwamba aliyehusika katika mauaji ya Ally Mohamed Kibao amefanya kosa kubwa na ni laana kwa Mwenyezi Mungu.

Pia, Soma: Dar: Ali Mohamed Kibao, kiongozi wa CHADEMA auawa na mwili kutelekezwa Ununio ukiwa umeharibika sana

Akizungumza kuhusu tukio hilo, Padre Kitima alisisitiza kuwa, "Aliyemuua Kibao amefanya kosa baya na ni laana kwa Mwenyezi Mungu. Kama viongozi wa dini, lazima tuseme hili. Tunalaani vikali vitendo vya uhalifu kama hivi."

Aliongeza, "Unafikiri watoto wa Mzee Kibao, aliyeuawa kinyama, wataonana vema na wale wanaohisiwa? Hii imejenga chuki kubwa kati ya familia na jamii. Tunapiga vita, tuna laani, na tunahitaji aliyemuua Kibao atubu kwa Mungu wake au achukuliwe hatua na sheria."

Padre Kitima alisisitiza kuwa, kama viongozi wa dini, ni jukumu lao kutoa ujumbe wa haki na amani, na kuonya dhidi ya vitendo vya kinyama vinavyovuruga jamii na kuleta machafuko.
Soma:
Kama kanisa inafaa kuiombea Neema na Baraka za Mungu familia ya Mzee Kibao..

Lakin zaid sana kumuombea huruma ya Mungu muuaji wa Mzee Kibao.

Mengine nadhani sio wajibu wa kanisa bali inaweza kua uchochezi zaidi 🐒
 
Huruma ya Mungu kwa tukio km hilo kwa muuaji ina gharama kubwa kuliko gharama ya kumuua Mzee Kibao..usidhani ni vyepesi km maigizo!
Ndiyo maana nasema ni huruma ya Mungu pekee ndio inaweza kumpatia ahuweni muuaji yeyeto yule na sio mbambamba nyinginezo 🐒
 
.Kama kanisa inafaa kuiombea Neema na Baraka za Mungu familia ya Mzee Kibao..

Lakin zaid sana kumuombea huruma ya Mungu muuaji wa Mzee Kibao.

Mengine nadhani sio wajibu wa kanisa bali inaweza kua uchochezi zaidi 🐒
Wamepewa funguo za mbinguni na duniani .Watakemea ,watabariki na wataponya .CCM na serikali walimuua KIBAO walaaniwe .Kila aliyeshiriki alaaniwe
 
Ndiyo maana nasema ni huruma ya Mungu pekee ndio inaweza kumpatia ahuweni muuaji yeyeto yule na sio mbambamba nyinginezo 🐒
..ahueni ipi??? Yuda iskariote alipata ahueni, au kwenda kuzimu kwako ndio ahueni! labda km ni hivyo uko sawa kulingana na unavyofahamu, lkn hiyo si ahueni! ahueni ni kuungama na kutubu kwa Mungu na kwa wanadamu hasa kwa familia ya Mzee Kibao!
 
adre Dkt. Charles Kitima, Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki Tanzania (TEC), ametoa kauli nzito akisema kuwa viongozi wa dini lazima waonyeshe wazi kwamba aliyehusika katika mauaji ya Ally Mohamed Kibao amefanya kosa kubwa na ni laana kwa Mwenyezi Mungu.
Amina. Na laana ya Mwenyezi Mungu ikaandamane nao na uzao wao!
 
Mungu mlinde Padri Kitima ili naye asitekwe
Hahahaa nimecheka kwanza hiyo haiwezekani hata kidogo ndugu mfumo wa kanisa Katoriki ni wa kimafia hujapata ona ,waone vile vile wale Vatican ina sikio kila jumba kubwa lolote mpaka Iran wakikaa kupanga tu washajua , labda tu yaratibiwe kigaidi gaidi lakini kupitia wasiojulikana uongo
 
Padre Dkt. Charles Kitima, Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki Tanzania (TEC), ametoa kauli nzito akisema kuwa viongozi wa dini lazima waonyeshe wazi kwamba aliyehusika katika mauaji ya Ally Mohamed Kibao amefanya kosa kubwa na ni laana kwa Mwenyezi Mungu.

Pia, Soma: Dar: Ali Mohamed Kibao, kiongozi wa CHADEMA auawa na mwili kutelekezwa Ununio ukiwa umeharibika sana

Akizungumza kuhusu tukio hilo, Padre Kitima alisisitiza kuwa, "Aliyemuua Kibao amefanya kosa baya na ni laana kwa Mwenyezi Mungu. Kama viongozi wa dini, lazima tuseme hili. Tunalaani vikali vitendo vya uhalifu kama hivi."

Aliongeza, "Unafikiri watoto wa Mzee Kibao, aliyeuawa kinyama, wataonana vema na wale wanaohisiwa? Hii imejenga chuki kubwa kati ya familia na jamii. Tunapiga vita, tuna laani, na tunahitaji aliyemuua Kibao atubu kwa Mungu wake au achukuliwe hatua na sheria."

Padre Kitima alisisitiza kuwa, kama viongozi wa dini, ni jukumu lao kutoa ujumbe wa haki na amani, na kuonya dhidi ya vitendo vya kinyama vinavyovuruga jamii na kuleta machafuko.
Soma:
Padre Kitima yuko sahihi kabisa, mauaji hayo yamesababisha chuki kubwa sana kati ya Wananchi wa kawaida ambao ni wapenda haki dhidi ya Serikali na CCM, hususani kuibuka kwa chuki kati ya raia dhidi ya Jeshi la Polisi na TISS ambao kwenye mkasa huu wanashukiwa Moja kwa Moja kuhusika na mauaji hayo ya kinyama.

Kama kanisa inafaa kuiombea Neema na Baraka za Mungu familia ya Mzee Kibao..

Lakin zaid sana kumuombea huruma ya Mungu muuaji wa Mzee Kibao.

Mengine nadhani sio wajibu wa kanisa bali inaweza kua uchochezi zaidi 🐒
Kabisa Lina wajibu wa kukemea uovu mbaya kama huo.
Je, wewe binafsi ungejisikiaje endapo kama huyo mzee aliyeuawa kwenye mkasa huu angekuwa baba yako mzazi?
 
Back
Top Bottom