Tindo
JF-Expert Member
- Sep 28, 2011
- 58,981
- 103,354
Quran imeingiaje tena Chadema bana, hivi Waislam waliwakosea nini?
Acha dhihaka na post zenye kukejeli imani za watu wengine. Nchi yetu imefikia kufanya maamuzi au kuchagua viongozi kwa kuangalia dini zao na wala si weledi wa kazi husika. Hapa jukwaani mara nyingi unakuja kuitetea ccm huku ukitumia uislamu kama kinga kwa hoja za kipuuzi. Unaonekana hujui ama unafanya maksud kama hapa jf imekuwa sehemu ya kushinda viongozi wa siasa ambao sasa wamejikuta hawana uwezo wa kimaamuzi bali kutoa maamuzi na kuteua viongozi kwa mitazamo ya kidini. Leo hii mmefanya propaganda za kipuuzi kwa kutumia dini kama kinga mpaka kupelekea kufanya kwamba ccm ianze kuonekana ya kiislam na cdm ya kikristo. Upuuzi huo mnaoufanya hapa jukwaani umepelekea waislim kujiona hawatendewi haki na mfumo huu dhaifu mpaka wanajikuta wanadai mahakama ya kadhi, badala ya kupambana kuibana serekali iwapelekee waumini wao maji safi, umeme, elimu na afya bora inajitahidi serekali iwapatie mahakama ili washitakiane waache kudai huduma bora za kijamii. Sasa upuuzi wenu utawafanya waislamu wajivunie taasisi ya mashitaka kana kwamba waislam ni watu wasio na maadili huku ukiacha wakristu na wengineo wakikazana kuleta huduma muhimu za kijamii, kwani waisilamu watakuwa mahakamani kushitakiana.
Nikukanye kabisa, ukiingia hapa jukwaa la siasa changia kisiasa na sio kutumia uislamu kuharibu mada na kuleta fitina za kidini kwa maslahi ya kisiasa.