Outstanding Performance

Njowepo

JF-Expert Member
Feb 26, 2008
9,710
2,226
KIKOSI cha wachezaji 16 wa soka walio chini ya umri wa miaka 17, ‘Copa Coca-Cola Dream Team’, waliopatikana kupitia fainali za taifa katika michuano ya Copa Coca-Cola, juzi walifanikiwa kutwaa ubingwa wa mashindano maalumu yaitwayo Coca-Cola Inter-Tournament yaliyofikia tamati juzi, nchini Brazil.
Mashindano hayo yaliyokwenda sambamba na mafunzo, yalifanyika katika kituo cha michezo cha Brazil cha BSA, kinachomilikiwa na kocha maarufu, Alberto Pereirra, yalifanyika katika Uwanja wa Maracana yakishirikisha vijana wa umri huo kutoka nchi mbalimbali.
Timu hiyo iliyo chini ya makocha - Mbrazili Marcio Maximo na Marsh Sylvestre - katika mechi ya kwanza iliifunga Peru mabao 5-0, hivyo kutinga hatua ya robo fainali.
Katika hatua hiyo, vijana hao walitoka sare ya bila kufungana na Chile kabla ya kuitungua Argentina 2-0 katika mechi ya nusu fainali, hivyo kufanikiwa kufika fainali ya mashindano hayo.
Juhudi za vijana hao hazikuishia hapo, kwani walizidi kujituma hata katika mechi ya fainali dhidi ya Chile na kufanikiwa kuwafunga bao 1-0 na kutwaa ubingwa wa mashindano hayo ya kimataifa.
Keep it up!
 
Habari nzuri kama hizi kwenye nchi yetu yenye mabaya mengi zingepaswa zitoke magazetini angalau kuwapa watu tabasamu. Congra boys.
 
Sasa linganisha maandalizi ya hawa vijana na ile SHORTCUT ya kutuletea kocha kutoka nje kufundisha Taifa stars.
Kuna mwanajeshi nilimwona akihojiwa kwenye TV wiki chache zilizopita. Huyu bwana anafundisha vijana wadogo NIDHAMU pamoja na kucheza mpira. (Huyu jamaa ana elimu ya michezo kutoka chuo kikuu). Kabla nilidhani wataalam kama huyu mwanajeshi hawapo nchini. Sijui nani alitoa ushauri kwamba tuanze kwanza kumleta kocha kutoka nje.





.
 
Sasa linganisha maandalizi ya hawa vijana na ile SHORTCUT ya kutuletea kocha kutoka nje kufundisha Taifa stars.
Kuna mwanajeshi nilimwona akihojiwa kwenye TV wiki chache zilizopita. Huyu bwana anafundisha vijana wadogo NIDHAMU pamoja na kucheza mpira. (Huyu jamaa ana elimu ya michezo kutoka chuo kikuu). Kabla nilidhani wataalam kama huyu mwanajeshi hawapo nchini. Sijui nani alitoa ushauri kwamba tuanze kwanza kumleta kocha kutoka nje.





.
Kwani hao vijana wanafundishwa na nani?
kama siyo kocha wa kigeni?
 
kuna baadhi ya waandishi wanasema ni maximo wengine Marsha wengine wote wawili, ili mradi tu wanaandika wanachojisikia ili kupotosha umma wa wanganyika.
Sasa huyu kocha.
Swli ni kuwa ni kuwa je viongozi na wapenzi wa huo mchezo mko tayari kuwatunza hawa vijana hadi waingie timu ya taifa?
Manake msianze: serikali itusaidie, mara viongozi wa taifa sijui nini.
swala libaki kwa wapenzi wa mchezo wenyewe, ili mpate raha zenu, shughulikieni watayarishaji wa raha zenu.
Mbona hatusikii mamisi wakiomba msaada serikalini?
 
Back
Top Bottom