OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 49,080
- 103,312
Kwa kweli mgombea Tundu Lissu anasikitisha sana kutoa matusi mazito kabisa na kudhalilisha wenzie. Kwa haraka haraka nimeyanyaka baadhi ya matusi yake ambayo yanalalamikiwa sana:
- Ujenzi wa uwanja wa ndege wa Chato ambao haukufuata utaratibu na haukupitishwa na bunge
- Wafanyakazi kutopata nyongeza ya mshahara kwa miaka mitano
- Kukosekana kwa uhuru wa kutoa maoni kulikopelekea kutungwa sheria kandamizi
- Kujali maendeleo ya vitu badala ya watu
- Kunyima vyama vya siasa uhuru wa kikatiba wa kufanya siasa
- Matumizi mabaya ya fedha za mifuko ya bima ya afya na hifadhi, matumizi kinyume na malengo. Zikikopwa hazirudishwi
- Ongezeko kuuuubwa la makato ya Bodi ya Mikopo toka 8% mpaka 15%
- Elimu duni isiyowajenga watoto wetu kujitegemea
- Kutokufanyika uchunguzi wa kina wa mauaji, utekaji na kupigwa kwake risasi
- Mbinyo kwa vyombo vya habari
- Ongeza na wewe matusi mengine, mi nimeweka machache tu