Orodha ya maneno ambayo ukiambiwa unahisi utapeli au yanakupa uoga moyoni

Good Father

JF-Expert Member
Feb 28, 2014
10,272
18,334
Wakuu kuna jambo ukilisikia au ukiambiwa unahisi unataka kutapeliwa, pia maneno mengine ukiambiwa unajisikia uoga fulani moyoni.
Angalia orodha yangu hapa kisha weka maneno yanayokupa uoga/kuhisi unatapeliwa.

1. Muuza bidhaa akisema yupo Kariakoo aisee nahisi muda wowote naibiwa

2. Mfanyabiashara akisema "na mikoani tunatuma ukilipa atleast nusu ya bei ya bidhaa".

3.Mwana jf akisema bei ya bidhaa nimfuate inbox

4.Earn monye online

5. Dawa za nguvu za kiume
6.Pete ya bahati
7.Pesa za majini
8.Kumfanya mpenzi wako akupende
Aisee waganga mnazingua kinyama
cc:Brother Mshana Jr.

9.Kuunganisha vifurushi vya Azam na DSTv kwenye dishi la Star Times

Ongeza maneno yako...
 
1.Enzi hizo unakuta jamaa arusha anakuuzia BlackBerry mpya elf15 ukijichanganya umebeba sabuni
2.unafika ubungo sa12;30 mkata tiketi anakwambia gari yake ndio ya mbele
3.kwetu kwetu tarime nafika kariakoo mtu cmjui ananiambia karibu mgosi
4.unashuka tu manseze unakutana na mdada mremboo anakwambia kaka nmevutiwa na wewe af ukichek ndio nmetoka mkoani na raizon langu, ata kama lazima nimkemee
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom