fikirikwanza
JF-Expert Member
- Jan 25, 2012
- 7,452
- 3,065
Hivi karibuni takribani mwaka huu wote hadi tulipo leo TBC1 na Komedi ya Masanja, Choti etc haina mvuto kabisa kwa watazamaji kiasi cha watu kukimbilia EATV kule kwa bambo ambao wanaonekana kuziba pengo la kifo cha mende cha komedi ya kinaMjuni.
Utafiti usio na gharama kubwa kwenye maeneo ya starehe wadau wamekuwa wakiomba sehemu za bar kuhamisha chanel kutoka TBC1 kwenda EATV ili kupata ujumbe wenye maudhui ya kuelemisha, burudani na vichekesho.
Ni dhahiri Masanja na wenzake ama wamekwisha au ndo uongozi wa TBC1 umeshindwa kuwasaidia inavyohitajika ili kuendelea kukalia usukani wa komedi TZ; Ni ama warudie kwenye fomu au tuwaage rasmi ktk fani hiyo na tuwakaribishe makundi yenye ujumbe na kuelimisha wakati ujumbe unafikishwa kwa kutoa burudani EATV/StarTV-Futuhi japo hawako serious sana na kazi pia.
Mlitulisha mua sasa ni wakati wa kutema makapi ya mua, hakuna utamu tena.
Utafiti usio na gharama kubwa kwenye maeneo ya starehe wadau wamekuwa wakiomba sehemu za bar kuhamisha chanel kutoka TBC1 kwenda EATV ili kupata ujumbe wenye maudhui ya kuelemisha, burudani na vichekesho.
Ni dhahiri Masanja na wenzake ama wamekwisha au ndo uongozi wa TBC1 umeshindwa kuwasaidia inavyohitajika ili kuendelea kukalia usukani wa komedi TZ; Ni ama warudie kwenye fomu au tuwaage rasmi ktk fani hiyo na tuwakaribishe makundi yenye ujumbe na kuelimisha wakati ujumbe unafikishwa kwa kutoa burudani EATV/StarTV-Futuhi japo hawako serious sana na kazi pia.
Mlitulisha mua sasa ni wakati wa kutema makapi ya mua, hakuna utamu tena.
Habari zenu
Tukiwa hapa kijiweni Bamaga, tukipiga story mbili tatu anakuja jamaa Mshikaji wetu anayefanyia TBC ambapo Ni mmoja kati ya waendesha kipindi fulani...Baada ya kupiga story mbili tatu tumejikuta tunamwuliza kuhusu hili kundi baada ya kupotea ghafla katika ramani ya vichekesho.
Naye alichotujibu ni anasikia kundi limevunjika Kimyakimya kila mtu anapiga issue zake..
Kuna mwenye habari zaidi kuhusu Kuvunjika Kwa Group Hili???