Oral exminations at college/university level

Ninachosema mimi ni kuboresha elimu yetu kuanzia elimu ya msingi hadi chuo kikuu. Na njia niliyoipendekeza inamsaidia mwanafunzi kujenga uwezo wa kujifunza, kuelezea alichojifunza kwa kuandika na kuongea. Kwa ujumla ni njia nzuri zaidi ya kumjengea mwanafunzi 'learning skills' - uwezo zaidi.

Nilisema mwanafunzi anapimwa kuanzia kushiriki kwake darasani, 'class presentation', 'written assignments', 'tests', 'written exams' na 'oral exams'. Vyote hivi vitamsaidia mwanafunzi kuongeza maarifa kwa kujenga uwezo wa kujieleza kwa maandishi na kuongea.

Wanafunzi wengi na hata watu wengine kwa kukosa nafasi ya kujenga uwezo wa namna hiyo wanashindwa kujadili hoja kikamilifu na ndiyo maana hata kama mtu anajua kitu fulani anashindwa kukijadili au kuwafanya wengine wakielewe vizuri. Ndiyo maana baadhi ya watu hawajui kujadili hoja. Wanajua kusema na wanategemea anayelezwa 'kumeza' kila kitu na akiulizwa anachukia.

Mkuu Magobe,
Nafikiri unachoonglea ni sawa kabisa kama unashauri kuwa isiwe ni mtihani tu bali iwe ni ushiriki wa ujumla kwa wanafunzi katika mijadala darasani, debate clubs n.k. ikiwa ni sehemu ya corse work yao. Kwa hilo nakubaliana na wewe.

Lakini kama hatutakuwa na waalimu walio na elimu nzuri, hatutaweza kuwa na wanafunzi walio na elimu bora likewise. Pia mfumo mzuri wa uhakiki wa waalimu na ufundishaji unahitajika. Mwalimu angepaswa kupimwa kulingana na kiwango cha kufaulisha wanafunzi, badala ya kuwa na waalimu wenye uhakika wa mishahara yao bila kujali ufaulu wa wanafunzi wake.
 
Mkuu Magobe,
Nafikiri unachoonglea ni sawa kabisa kama unashauri kuwa isiwe ni mtihani tu bali iwe ni ushiriki wa ujumla kwa wanafunzi katika mijadala darasani, debate clubs n.k. ikiwa ni sehemu ya corse work yao. Kwa hilo nakubaliana na wewe.

Lakini kama hatutakuwa na waalimu walio na elimu nzuri, hatutaweza kuwa na wanafunzi walio na elimu bora likewise. Pia mfumo mzuri wa uhakiki wa waalimu na ufundishaji unahitajika.

Mwalimu angepaswa kupimwa kulingana na kiwango cha kufaulisha wanafunzi, badala ya kuwa na waalimu wenye uhakika wa mishahara yao bila kujali ufaulu wa wanafunzi wake.

Ni kweli unachosema na kwa bahati mbaya sana kupima waalimu kwa kufaulisha ndilo tatizo linalofanya baadhi waonyeshe mitihani. Mimi nashauri upimaji wa mwanafunzi usilenge kufaulisha tu bali pia ushiriki mzima wa mwanafunzi darasani.

Nina imani waalimu wakipewa motisha kutakuwa na mabadiliko na ikishatokea hivyo kuwe pia na 'inspection' kama ilivyokuwa inafanyika miaka ya nyuma. Tuwe na 'inspectors' wanaotembelea shule zote kupima ufundishaji wa waalimu na jinsi wanafunzi wanavyoshiriki darasani.

Naomba nitumie mfano huu: shule nyingi za seminari zinafaulisha vizuri hasa kwa kutokana na mfumo ambao binafsi naona unazingatia ushauri kama ninaoutoa. Ni vizuri waalimu wakuu wasione aibu kujifunza 'learning skills' kutoka shule hizi.

Hivi ni kweli shule hizi zinafaulisha kwa vile zina idadi ndogo ya wanafunzi tu au kuna pia jitihada za ziada zinazofanyika ambazo kama shule nyingine zingejifunza huenda kungeleta mabadiliko katika 'performance' nzima.

Shule nyingi za siku hizi na hasa zile za elimu ya watu wazima (Two Years in One) zina matatizo makubwa sana. Waalimu wanafundisha lakini hakuna uangalizi wowote kwani shule hizi na zingine zenye udhaifu kama huo wanafunzi wanafundishwa tu waelewe au wasielewe mradi wameshalipa ada ni juu yao.

Na wenye hela kwa kawaida huwa hawakubali kushindwa kwani inakuwa aibu kwao na ndio maana wanafanya juu-chini watoto wao hata kama hawajui wanafaulu.

Kwa kweli ni aibu kubwa kuona kuwa hata wanafunzi wa chuo kikuu wanafanyiwa 'assignments'. Na swali ambalo najiuliza ni kwamba kama 'assignments' tu wanaibia, je, kwa majaribio na mitihani inakuwaje? Yaani, inatisha!
 
Ni kweli unachosema na kwa bahati mbaya sana kupima waalimu kwa kufaulisha ndilo tatizo linalofanya baadhi waonyeshe mitihani. Mimi nashauri upimaji wa mwanafunzi usilenge kufaulisha tu bali pia ushiriki mzima wa mwanafunzi darasani.

Nina imani waalimu wakipewa motisha kutakuwa na mabadiliko na ikishatokea hivyo kuwe pia na 'inspection' kama ilivyokuwa inafanyika miaka ya nyuma. Tuwe na 'inspectors' wanaotembelea shule zote kupima ufundishaji wa waalimu na jinsi wanafunzi wanavyoshiriki darasani.

Naomba nitumie mfano huu: shule nyingi za seminari zinafaulisha vizuri hasa kwa kutokana na mfumo ambao binafsi naona unazingatia ushauri kama ninaoutoa. Ni vizuri waalimu wakuu wasione aibu kujifunza 'learning skills' kutoka shule hizi.

Hivi ni kweli shule hizi zinafaulisha kwa vile zina idadi ndogo ya wanafunzi tu au kuna pia jitihada za ziada zinazofanyika ambazo kama shule nyingine zingejifunza huenda kungeleta mabadiliko katika 'performance' nzima.

Shule nyingi za siku hizi na hasa zile za elimu ya watu wazima (Two Years in One) zina matatizo makubwa sana. Waalimu wanafundisha lakini hakuna uangalizi wowote kwani shule hizi na zingine zenye udhaifu kama huo wanafunzi wanafundishwa tu waelewe au wasielewe mradi wameshalipa ada ni juu yao.

Na wenye hela kwa kawaida huwa hawakubali kushindwa kwani inakuwa aibu kwao na ndio maana wanafanya juu-chini watoto wao hata kama hawajui wanafaulu.

Kwa kweli ni aibu kubwa kuona kuwa hata wanafunzi wa chuo kikuu wanafanyiwa 'assignments'. Na swali ambalo najiuliza ni kwamba kama 'assignments' tu wanaibia, je, kwa majaribio na mitihani inakuwaje? Yaani, inatisha!

Mkuu Magobe,
Nafikiri bado wazo la kumpima mwalimu kulingana na kiwango cha kufaulisha kwake ni zuri hasa ukilinganisha hali ya kutowiana ya shule zetu. Adjustment inaweza kufanyika kulingana na mazingira ya shule ilipo na facilities kwa mfano, shule ya msingi ya manispaa ya Morogoro inaweza kulinganishwa na ya manispaa ya Ilala, Dar, au Ifakara na Kilwa n.k. Baada ya hapo suala la kuonyesha mitihani linaweza kushughulikiwa ikiwa ni pamoja na adhabu kali kwa wahusika. Lakini kwa kipimo hicho itajulikana nani anafanya kazi na nani hafanyi.

Seminari zinafaulisha sana kwa sababu moja tu, uwajibikaji wa waalimu ikiwa ni pamoja na ufuatiliaji wa karibu wa kila wanachofanya wanafunzi wao.

Hata hivyo, nakubaliana na wewe kabisa kuwa kuna matatizo mengi sana kwenye shule zetu; mishahara midogo, inspection pungufu n.k., na ndio maana nimependekeza kuwepo na kipimo kinachowalinganisha waalimu wote, wakati hayo mengine yakiendelea kushughulikiwa.

Matatizo mengine kama ya kufanyiwa assignment n.k., nafikiri sio ubiquitous na hayataisha. La muhimu ni kuwepo kwa standards za kupima waalimu, against wenzao wa shule/vyuo vingine, kama ilivyo kwa wanafunzi, ili kuwafanya wawajibike zaidi na pia wao wenyewe kujua kama wanafanikiwa au la.
 
Nafikiri anachokisema gombe ni

wanafunzi wafanye presentation mfano ana present topic ya Atom mbele ya wanafunzi harafu profesa naye anakua kama mwanafunzi anamsikiliza na wanafunzi wengine pamoja na prof wanamuuliza maswali,hii ina eliminate uwezekano wa kughushi kwa aina yoyote ile.

Pili wanafunzi wanafanya Oral yani mbele ya kabineti la ma prof wasomo ma prof wawili watatu kwenda mbele ,mfano mwanafunzi anaelezea topic mbili tatu ,hii pia inatoa nafasi makini.

Tatu mwanafunzi wakati wa tutorial mfano anakua anatoka mbele anakwenda kukokotoa swali na kuelezea kwanini kakokotoa vile na sivinginevyo hapo pia anapata maksi zake.
Mwisho anaingia mtihani wa kuandika pia anapata maksi zake inapigwa jumla inatafutwa wastani anapata maksi zake.

Hii inamaana mwanfunzi anaanza kukusanya maksi tangu mwanzo wa term hadi mwisho,ni uonezi ama kuwahadaa watu kwa kumu jaji mwanafunzi aliyosoma miezi sita anayaandika kwa saambili ama moja.
 
Nafikiri anachokisema gombe ni

wanafunzi wafanye presentation mfano ana present topic ya Atom mbele ya wanafunzi harafu profesa naye anakua kama mwanafunzi anamsikiliza na wanafunzi wengine pamoja na prof wanamuuliza maswali,hii ina eliminate uwezekano wa kughushi kwa aina yoyote ile.

Pili wanafunzi wanafanya Oral yani mbele ya kabineti la ma prof wasomo ma prof wawili watatu kwenda mbele ,mfano mwanafunzi anaelezea topic mbili tatu ,hii pia inatoa nafasi makini.

Tatu mwanafunzi wakati wa tutorial mfano anakua anatoka mbele anakwenda kukokotoa swali na kuelezea kwanini kakokotoa vile na sivinginevyo hapo pia anapata maksi zake.
Mwisho anaingia mtihani wa kuandika pia anapata maksi zake inapigwa jumla inatafutwa wastani anapata maksi zake.

Hii inamaana mwanfunzi anaanza kukusanya maksi tangu mwanzo wa term hadi mwisho,ni uonezi ama kuwahadaa watu kwa kumu jaji mwanafunzi aliyosoma miezi sita anayaandika kwa saambili ama moja.

Asante sana Mkamap. Kwanza, chuo nilichosoma mimi tulikuwa tunafanya hayo niliyoyaeleza hapo juu. Mwanzoni nilipata shida sana kwa 'oral examinations' lakini baadaye niliona ilinijengea uwezo na niliweza kupata maksi nyingi zaidi hata kuzidi 'essays' na 'written examinations'.

Naamini hata kwa wanafunzi wengine itakuwa vigumu mwanzoni tu kwa vile hawajazoea lakini kwa baadaye ni njia nzuri sana ya kumjengea mwanafunzi uwezo wa kujieleza, kuondoa woga wa kuzungumza au kueleza kitu mbele ya wengine (public speaking) na pia atakuwa na uwezo wa kujieleza kwa kuandika na kuongea.

Tatu, chuo chetu kilikuwa kinawafikiria 'mara mbili' wale waliokuwa wanafaulu sana au kupata maksi za chini. Yaani, kazi zao zilikuwa zinasahihishwa tena na 'external examiners' ili kuhakikisha kuwa mtu anapata maksi ambazo ni zake kweli. Hii iliweza kuwasaidia wanafunzi waliolalamika wameonewa na pia iliweza kubaini wenye tabia ya kuibia.

Nne, waalimu wetu tulikuwa tunawafanyia 'evaluation'. Kama wanafunzi wengi watampa mwalimu fulani alama za chini sana (wakati wa 'evaluation') basi uongozi wa chuo baada ya kuridhika na 'evaluation' hiyo waliweza kusitisha mkataba wa mwalimu huyo kufundisha au waliweza kumshauri kurekebisha namna yake ya ufundishaji. Hali hii iliwafanya waalimu wetu kuwa waangalifu sana na kweli walikuwa wakifanya kazi kwa bidii na maarifa. Mfumo mzima wa utowaji maksi au 'evaluation' ya waalimu, kwa maoni yangu, ulikuwa 'fair'.

Tano, mwanafunzi alikuwa anapewa nafasi ya ku'present' 'paper' yake ya mwisho mbele ya jopo la waalimu (internal & external examiners) na kuulizwa maswali kadhaa kuhusiana na paper yake hiyo. Kila mwalimu aliweka alama zake kwa yale maswali aliyouliza.

Maksi alizopata mwanafunzi pamoja na maksi zingine zote, ziliwekwa pamoja kwa mgawanyo, mfano: Class presentation (5 marks), Class participation (10 marks), assignments (15 marks), tests (20 marks), written examinations
(25 marks) na oral examinations (25 marks). Maksi hizi zote zilitafutiwa wastani na kisha kuchukua, mfano, alama 40% na ile paper ya mwisho alama 60%. Alama hizi zote ndizo zilizomwezesha mwanafunzi kupata diploma au digrii ya kiwango fulani.

Haya niliyojifunza naona yote au baadhi yake kutegemea na mahitaji yetu yanaweza kusaidia, kama yatafuatwa, kuboresha elimu yetu kwa 'levels' zote hapa kwetu Tanzania. Mimi naamini Watanzania wakifundishwa vizuri watafanikiwa kabisa na kwa hiyo hakuna cha kusingizia lugha au nini. Tatizo ni moja tu mfumo wa ufundishaji ni mbaya, tuna waalimu ambao hawana maandilizi mazuri na hawana motisha katika kazi yao.
 
huu utaratibu upo muslim university of morogoro...course work inajengwa na
1: seminar presentation n paper,
2: take home assignment
3:test 1
4:test 2
5:pANNEL DISCUSSION/ORAL TEST kwa kila somo ....
N:B HAKUNAGA "UE" ZA MULTIPLE CHOICE pale
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom