OR-TAMISEMI, Kama Idara za Mipango zitawezeshwa, tutafikia Maono ya Rais Samia

Robert S Gulenga

JF-Expert Member
Jan 3, 2013
2,160
1,492
Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan maono yake ni kuhakikisha Watanzania wanapata huduma zilizo bora , Mh Rais amekuwa akipigana usiku na mchana kuhakikisha Watanzania wote wanapata huduma za Afya, Maji, Umeme, Watoto wote wenye umri wa kwenda Shule wanaenda shule bila ada, barabara zinazopitika wakati wote pamoja na huduma nyingine muhimu.

Katika kusaidia kupatikana kwa huduma zilizo bora kwa Watanzania na kufikia malengo na matamanio ya Mheshimiwa Rais, OR- TAMISEMI iwekeze katika kuimarisha Idara za Mipango, Takwimu na Ufiuatiliaji katika Halmashauri zote Nchini.

Idara za Mipango, Takwimu na Ufiuatiliaji ni engine inayoweza kutoa dira wa utoaji wa huduma kwa Wananchi, ndio inayoweza kutoa muelekeo wa kufikia malengo ya Halmashauri katika ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri, utoaji wa huduma kwa Wananchi, utekelezaji wa miradi ya Maendeleo na kuweza kuitafsiri Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi kwa vitendo.

Halmashauri ziweze kuweka bajeti ya kuhakikisha inatenga bajeti ya kuwapeleka Watalaamu wa Idara za Mipango katika mafunzo ya muda mfupi ili kuongeza ujuzi na weredi katika kuibua miradi mipya ya maendeleo, kujifunza namna ya kubuni vyanzo vipya vya mapato na kuanda bajeti bora zinazotekelezeka.

Halmashauri zote zimekuwa zikiandaa Mpango Mkakati wa Halmashauri wa miaka 5 ( Strategic Planning), SP ni roho ya kila Taasisi katika utekelezaji wa Taasisi zote (Iwe Taasisi ya Serikali au ya Mtu binafsi), Watalaamu wa Idara ya Mipango wawezeshwe kwa kupewa mafunzo namna bora ya kuandaa Mpango Mkakati unaotekelezeka, hii itasaidia sana Halmashauri zote kujiwekea malengo. Bila kuwapeleka Wataalamu hawa wa Idara za mipango kwenye mafunzo ya muda mfupi, Halmashauri zitaendelea kutekeleza bajeti zile zile kila mwaka japokuwa kuna ufanisi lakini tunaweza pata ufanisi zaidi kwa KUZIWESHA HALMASHAURI KUWA NA WATAALAMU WENYE UELEWA NA UZOEFU MKUBWA KATIKA MAMBO YA MIPANGO.

OR-TAMISEMI, Idara ya Mipango ina Watalaam wazuri na bobezi katika mambo ya uandaaji wa Mpango Mkakati, Watumike kutoa elimu kwa Watalaam wa Halmashauri ili kila Halmashauri iwe na Mpango Mkakati unaotekelezeka, hili litawezekana kama Halmasahuri zitaweka bajeti ya Uwezeshaji mafunzo haya kwa Watalaamu wake.

Ukitembelea Taasisi za Elimu (VYUO VIKUU) vina Wataalamu special kwa ajili ya kusimamia Mpango Mkakati wa Taasisi zao, Taasisi za Elimu zinafanikiwa katika utekelezaji wa Mipango Mikakati yao kwa Sababu Wamewekeza katika Idara za Mipango.


Mungu Ibariki Tanzania.

Mungu Mbariki Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan.

KAZI IENDELEE
 
Kaka
Umeandika Thesis yenye uchambuzi mzuri haswa.

Bahati mbaya nchi hii ilipoteza mwelekeo pale watu walipoanza kuzitazama Halmashauri kwa jicho la husda!
Halmashauri zikapachikwa kila aina ya lawama - ufisadi, ukabila, wizi, umaarufu nk.

Siasa ndio zikaingizwa humo hadi zikabakizwa kuwa vyombo vya kusafisha masoko na barabara hahaha!!
Tunachekwa kila upande
 
Kaka
Umeandika Thesis yenye uchambuzi mzuri haswa.
Bahati mbaya nchi hii ilip
Mkuu mavumbi Kuna umuhimu mkubwa wa kuzifanyia "OVERHAUL" Halmashauri ili ziweze kukizi malengo yakuazishwa kwake, pasipofanyika maboresho lawama na kunyosheana vidole hakutaisha, Halmashauri nyingi zitaendelea kutegemea OC ya Serikali Kuu katika kujiendesha.
 
Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan maono yake ni kuhakikisha Watanzania wanapata huduma zilizo bora , Mh Rais amekuwa akipigana usiku na mchana kuhakikisha Watanzania wote wanapata huduma za Afya, Maji, Umeme, Watoto wote wenye umri wa kwenda Shule wanaenda shule bila ada, barabara zinazopitika wakati wote pamoja na huduma nyingine muhimu.
 
OR-TAMISEMI ni lidudu likubwa sana ambalo lina dis-economies of scale. Kulimanage vizuri imekuwa shida, hata mawaziri wanageuzwa mara kwa mara. Pili kuna mahitaji tofauti kati ya eneo moja na lingine na Dodoma wanaweza wasitambue hili.

Tatu kwa mamlaka makubwa ya Rais anaweza kuamua wapi awape huduma na wapi asipeleke (hili tumeliona).

Kuna faida ya kufanya maamuzi mengine sehemu husika. Hii inanipelekea kufikiria kwa nini tusi ingie kwenye mfumo wa Serikali za majimbo ambao hutumika na nchi ambazo ni kubwa kidney kama Africa kusikia, DRC, Nigeria, Sudani etc. Hata ndugu zetu wa Kenya wa me ingia huko.
 
Utaratibu mzima na utekelezaji wa mipango unatia mashaka sana. Kwa muda mfupi nimeweza kuona mambo yafuatayo ambayo hayaridhishi na hayawezi kusukuma utekelezaji kwa kuhusisha wadau wote wa elimu. Mambo hayo ni pamoja na:
1. Viongozi kujikita zaidi kwenye kutengeneza mipango na siyo kwenye kutekeleza mipango hiyo.
2 Mipango mingi huandaliwa katika muundo wa kutoka juu kuja chini "top-down, technocratic way" jambo ambalo wakati mwingine linawafanya watekekelezaji kushindwa kujua malengo ya wanachopaswa kutekeleza. Ingawa mipango inaweza kuandaliwa na wataalamu lakini wanaowajibika kutekeleza ni wadau wote na jambo hili huhitaji kila mmoja kuwa na utayari.
3.Kutokuyapa mabadiliko ya mazingira uzito. Mipango mingi ya elimu imendaliwa kana kwamba walioindaa wana taarifa zote na mbinu zinazohitajika katika utekelezaji.

Ushauri wangu
Huu ni wakati muafaka kabisa wa kuachana na utaratibu wa zamani wa kupanga na kuanza kuweka  mpangomkakati "strategic planning" Kwa sababu utaratibu huu husaidia kupongeza ufanisi kwa kuhakikisha wahusika wote wanashiriki kikamilifu kutimiza malengo ya taasisi kwa kuifanya taasisi iendane na mabadiliko hitajifu ya mazingira. Pamoja na hayo mpangomkakati una sifa kama:
1.Unajikita kwenye kupata matokeo
2. Unahusisha ushirikiahwaji
3.Unasadifu mabadiliko
4 .Unahusisha ufutiliaji wa ufanisi
5. Unasisitiza kwenye utekelezaji wa mpango
6.Unahususha upangaji changamani...
..............................................................................................
It is our high time to focus on plan implementation.
 
Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan maono yake ni kuhakikisha Watanzania wanapata huduma zilizo bora , Mh Rais amekuwa akipigana usiku na mchana kuhakikisha Watanzania wote wanapata huduma za Afya, Maji, Umeme, Watoto wote wenye umri wa kwenda Shule wanaenda shule bila ada, barabara zinazopitika wakati wote pamoja na huduma nyingine muhimu.

Katika kusaidia kupatikana kwa huduma zilizo bora kwa Watanzania na kufikia malengo na matamanio ya Mheshimiwa Rais, OR- TAMISEMI iwekeze katika kuimarisha Idara za Mipango, Takwimu na Ufiuatiliaji katika Halmashauri zote Nchini.

Idara za Mipango, Takwimu na Ufiuatiliaji ni engine inayoweza kutoa dira wa utoaji wa huduma kwa Wananchi, ndio inayoweza kutoa muelekeo wa kufikia malengo ya Halmashauri katika ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri, utoaji wa huduma kwa Wananchi, utekelezaji wa miradi ya Maendeleo na kuweza kuitafsiri Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi kwa vitendo.

Halmashauri ziweze kuweka bajeti ya kuhakikisha inatenga bajeti ya kuwapeleka Watalaamu wa Idara za Mipango katika mafunzo ya muda mfupi ili kuongeza ujuzi na weredi katika kuibua miradi mipya ya maendeleo, kujifunza namna ya kubuni vyanzo vipya vya mapato na kuanda bajeti bora zinazotekelezeka.

Halmashauri zote zimekuwa zikiandaa Mpango Mkakati wa Halmashauri wa miaka 5 ( Strategic Planning), SP ni roho ya kila Taasisi katika utekelezaji wa Taasisi zote (Iwe Taasisi ya Serikali au ya Mtu binafsi), Watalaamu wa Idara ya Mipango wawezeshwe kwa kupewa mafunzo namna bora ya kuandaa Mpango Mkakati unaotekelezeka, hii itasaidia sana Halmashauri zote kujiwekea malengo. Bila kuwapeleka Wataalamu hawa wa Idara za mipango kwenye mafunzo ya muda mfupi, Halmashauri zitaendelea kutekeleza bajeti zile zile kila mwaka japokuwa kuna ufanisi lakini tunaweza pata ufanisi zaidi kwa KUZIWESHA HALMASHAURI KUWA NA WATAALAMU WENYE UELEWA NA UZOEFU MKUBWA KATIKA MAMBO YA MIPANGO.

OR-TAMISEMI, Idara ya Mipango ina Watalaam wazuri na bobezi katika mambo ya uandaaji wa Mpango Mkakati, Watumike kutoa elimu kwa Watalaam wa Halmashauri ili kila Halmashauri iwe na Mpango Mkakati unaotekelezeka, hili litawezekana kama Halmasahuri zitaweka bajeti ya Uwezeshaji mafunzo haya kwa Watalaamu wake.

Ukitembelea Taasisi za Elimu (VYUO VIKUU) vina Wataalamu special kwa ajili ya kusimamia Mpango Mkakati wa Taasisi zao, Taasisi za Elimu zinafanikiwa katika utekelezaji wa Mipango Mikakati yao kwa Sababu Wamewekeza katika Idara za Mipango.


Mungu Ibariki Tanzania.

Mungu Mbariki Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan.

KAZI IENDELEE
WIZARA YAO IMEPIGA MABILIONI YA FEDHA KWA SEMINA BADALA YA KUZIPELEKA KWENYE IDARA ZAKE
Screenshot_20230203-031633.jpg
 
Back
Top Bottom