Ndugu zangu,
Hata mwezi haujapita, niliweka hoja hii mezani kwenye ukurasa wangu wa FB. Kuna ambao walinielewa, lakini kuna ambao hawakunielewa mpaka kufikia kunijadili mtoa hoja badala ya hoja iliyokuwa mezani. Ni haki yao.
Upinzani katika hali ya sasa umesambaratika. Kuna kosa kubwa lilifanywa na UKAWA, tunalijua.
Nitakuwa mtu wa mwisho kutaka turudi kwenye mfumo wa chama kimoja, maana naamini katika pluralism.
Hata hivyo, naiona haja ya uwepo wa mbadala wa vyama vya upinzani vilivyopo sasa. Ni kwa vile, tofauti na CCM, ambacho ni Chama Itikadi na Wanachama, vilivyopo ni vyama Kiongozi/Viongozi (Wenye navyo) na Itikadi Holela.
Si kazi nyepesi, kujenga chama cha siasa chenye misingi ya itikadi na kilicho chini ya wanachama.
Kunahitajika uwepo wa demokrasia ya ndani ya vyama ( Intra Party Democracy). Madhara ya kutafuta njia za mkato hupelekea msambaratiko kama tunaoushuhudia sasa.
Nini kinafuata?
Kuelekea 2020 Wabunge wa upinzani wenye kukubalika kwenye majimbo yao wanaweza kuanzia sasa kufikiri kwenda kugombea tena kwa tiketi za CCM kwa kuhofia jahazi walilomo sasa linaelekea kuzama.
Inasikitisha
Maggid Mjengwa.
0688 37 36 52 ( Whatsapp)
Hata mwezi haujapita, niliweka hoja hii mezani kwenye ukurasa wangu wa FB. Kuna ambao walinielewa, lakini kuna ambao hawakunielewa mpaka kufikia kunijadili mtoa hoja badala ya hoja iliyokuwa mezani. Ni haki yao.
Upinzani katika hali ya sasa umesambaratika. Kuna kosa kubwa lilifanywa na UKAWA, tunalijua.
Nitakuwa mtu wa mwisho kutaka turudi kwenye mfumo wa chama kimoja, maana naamini katika pluralism.
Hata hivyo, naiona haja ya uwepo wa mbadala wa vyama vya upinzani vilivyopo sasa. Ni kwa vile, tofauti na CCM, ambacho ni Chama Itikadi na Wanachama, vilivyopo ni vyama Kiongozi/Viongozi (Wenye navyo) na Itikadi Holela.
Si kazi nyepesi, kujenga chama cha siasa chenye misingi ya itikadi na kilicho chini ya wanachama.
Kunahitajika uwepo wa demokrasia ya ndani ya vyama ( Intra Party Democracy). Madhara ya kutafuta njia za mkato hupelekea msambaratiko kama tunaoushuhudia sasa.
Nini kinafuata?
Kuelekea 2020 Wabunge wa upinzani wenye kukubalika kwenye majimbo yao wanaweza kuanzia sasa kufikiri kwenda kugombea tena kwa tiketi za CCM kwa kuhofia jahazi walilomo sasa linaelekea kuzama.
Inasikitisha
Maggid Mjengwa.
0688 37 36 52 ( Whatsapp)