Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,466
- 113,543
Wanabodi,
Ule msemo wa " Kunguru mwoga, hukimbiza bawa lake!" leo umeendelea kwa Chama Cha Mapinduzi, kumuopa kada wake RA kana kwamba ni mungu mtu, hivyo sasa kinamtishia nyau kumpeleka mahakamani!.
Uoga huo umetangazwa rasmi na Katibu Uenezi, Nape Mnauye kwa waandishi wa habari.
Kwa mujibu wa TBC-1 news za saa 2:00, Nape ameonekana amelishika gazeti la Mtanzania na kutishia nyau kuwa watalifikisha mahakamani kwa madai ya kuvujisha siri za vikao vya CC kwenye gazeti hilo!.
Kutendo hicho ni ishara dhahiri ya uoga kama kunguru dhidi ya RA ambaye ni kada wao, wanamjua ndie mmiliki wa gazeti hilo, wanaogopa kumkabili na sasa kujidai kutaka kuitumia mahakama kumwajibisha!.
Nadhani CCM inawanasheria wazuri tuu ambao wangeishauri CCM against hiyo wastage of time kufungua useless case ambayo itakuwa thrown out on the first hearing!.
Nadhani CCM bado iko kwenye ile njozi ya "chama dola" hivyo inajiaminisha documents za vikao vyao ni state secrets hivyo mahakama itawalazimisha Mtanzania wafanye 'disclosure' ya source wao ili afungwe kwa possessio ya ' state secrets'!.
Ukiona chama kinakimbilia mahakamani kutafuta mchawi miongoni mwa makada wake, ujue hizo ni dalili za mfa maji haachi kutapata sasa kinataka hata kudandia chelewa ili kujiokoa!.
All the best CCM kwenye kesi dhidi ya kada wake!.
Wasalaam.
Pasco (wa jf)
Ule msemo wa " Kunguru mwoga, hukimbiza bawa lake!" leo umeendelea kwa Chama Cha Mapinduzi, kumuopa kada wake RA kana kwamba ni mungu mtu, hivyo sasa kinamtishia nyau kumpeleka mahakamani!.
Uoga huo umetangazwa rasmi na Katibu Uenezi, Nape Mnauye kwa waandishi wa habari.
Kwa mujibu wa TBC-1 news za saa 2:00, Nape ameonekana amelishika gazeti la Mtanzania na kutishia nyau kuwa watalifikisha mahakamani kwa madai ya kuvujisha siri za vikao vya CC kwenye gazeti hilo!.
Kutendo hicho ni ishara dhahiri ya uoga kama kunguru dhidi ya RA ambaye ni kada wao, wanamjua ndie mmiliki wa gazeti hilo, wanaogopa kumkabili na sasa kujidai kutaka kuitumia mahakama kumwajibisha!.
Nadhani CCM inawanasheria wazuri tuu ambao wangeishauri CCM against hiyo wastage of time kufungua useless case ambayo itakuwa thrown out on the first hearing!.
Nadhani CCM bado iko kwenye ile njozi ya "chama dola" hivyo inajiaminisha documents za vikao vyao ni state secrets hivyo mahakama itawalazimisha Mtanzania wafanye 'disclosure' ya source wao ili afungwe kwa possessio ya ' state secrets'!.
Ukiona chama kinakimbilia mahakamani kutafuta mchawi miongoni mwa makada wake, ujue hizo ni dalili za mfa maji haachi kutapata sasa kinataka hata kudandia chelewa ili kujiokoa!.
All the best CCM kwenye kesi dhidi ya kada wake!.
Wasalaam.
Pasco (wa jf)