Elections 2015 Operesheni Zinduka: Uamuzi Sahihi 2015

Mzee anzisha opereshen.... Kuna samaki wengi sana utawavua.. Wanaoshabikia kwa upepo tuu

Ni movement nzuri nimeipenda sana itatusaidia sisi mtaani kupata pa kuanzia kuwaelimisha waliochanganywa na mafuriko.


Wasiwasi wangu inaishia mitandaoni tena jamiiforums ambapo wengi hawafiki ingefika mitaani watu wangeelewa sana. Angalieni namna ya kuifikisha mitaani bila hivyo ni kazi bure.
 
NB: Video Inafuata

Operesheni Zinduka imeanza kama nilivyoahidi (jana haikuwezekana kwa sababu moja tu ya heshima ya Mch. Mtikila na haihusiani na mipango ya watu wengine). Nitajitahidi kuwa na onesho hili kila siku (ukiondoa mwisho wa Juma) na nitazungumzia mada mbalimbali. Wiki hii ya kwanza zaidi nitagusia hoja nyingi zilizoibuliwa kutushangaa tunaomkataa Lowassa kama mgombea Urais kwa tiketi ya upinzani.

La pili nitajitahidi hasa wiki ile inayokuja kutoa nafasi kwa wagombea wa CHADEMA kwenye Ubunge (ambao tutaweza kuwafikia) ili wajiuze kwani ninaamini Bunge lenye nguvu lililoundwa na watu waliolelewa na kukomaa katika upinzani na wenye kuelewa hasa ajenda ya upinzani ndio chachu ya kweli ya mabadiliko tuyatakayo. Hivyo, wiki ile inayokuja tutatoa nafasi hii kwa wote tutakaoweza kuwapata.

Tatu, kwa vile nina uhakika wapo wengi ambao hawajakubaliana na uamuzi wangu huu (ambao naamini ni sahihi) basi nitatoa nafasi pia kwa watu wengine kutoa hoja zao dhidi ya ninachosema (sikiliza onesha hili juu ya 'mashart kuzingatiwa'). Kwa barua pepe anuani yangu ipo chini na namna nyingine ya mawasiliano nitawajulisha siku chache zijazo.

Nitajitahidi kuweka shows zote kwenye uzi huu huu kila siku, na video zitafuata chini toka ya zamani zaidi hadi mpya zaidi.

Mwisho, ninaamini na nina uhakika kuwa kwa atakayeamua kunisikiliza kuanzia sasa hadi kuamkia Uchaguzi Mkuu hatoweza kumpigia Lowassa kura ya Urais. Ni kwa sababu hiyo wale ambao tayari wameshaamua kuwa haijalishi nini kitasemwa juu ya Lowassa nawaomba au kuwashauri wasisikilize mada hizi wasije kujikuta wanabadili mawazo. Mada hizi ni kwa wale tu ambao bado hawajaamua au wale ambao wameamua lakini bado wanajikuwa wanavuta na upepo wa 'nyomi' kiasi kwamba bado hawajathibitika katika msimamo wao.

"Uamuzi Makini, Uamuzi wa Lazima, Uamuzi Sahihi"

MMM

ONESHO 1. "Baada ya Kelele Sauti za Hoja Zitashinda"


Wabunge wa upinzani wanaenda kusimamia ajenda hipi kama vyama vyao vimeuwa misingi na kanuni zao kwasababu ya masrahii ya watu wachache?
 
Last edited by a moderator:
Huyu Jamaa sijui anataka kutuaminisha nini, nashindwa kuelewa kama kweli huyu jamaa ni Diaspora, maana anafurahia sisi kuishi maisha magumu kama haya, Yaani eti tuchaguwe wabunge wa upinzani alafu uraisi tumpe Magufuri, Kwa nini tusiwapige chini hawa jamaa ili wawe wapinzani maana naamini CCM wakiwa wapinzani Nchi itakwenda kwa kasi ya ajabu sana
 
Mwanakijiji ulipoleta bandiko lako kuhusu Dr. Slaa -Kwamba CDM ikae na Dr. Slaa ili kuridhia matakwa ya Dr. Slaa aliyoyaweka kuhusu kumpokea EL. Katika bandiko lile nilikueleza wazi kwamba wewe na genge lako huna nafasi ya ushawishi tena kwenye mbio za MABADILIKO. Tafuta njia nyingine ya kurudisha heshima yako ila hii unayotumia si sahihi mkuu. CDM ni zaidi ya hoja zako ambazo ni myopic unazotaka kuaminisha wanajamvi. I wrote ''they will cut you down like grass"

Jipange upya mkubwa
 
Huyu mwanakijiji ni moja ya watu wanaotumiwa na ccm. Mlungula umeshampitia, ndio maana kaanza porojo. Ikimsikiliza kwa makini utakugundua kuwa maneno yake yamejaa unafiki. Njaa mbaya sana, kaona wenzake wanavuna kaamua kuchangamkia fursa naye aweze kushibisha tumbo lake.
 
Kashindwa Slaa, Lipumba, Mtikila, Wasira, Nape, kinana na Mwigulu utaweza wewe mwanakijiji? Unapoteza muda wako wa kufanya production wakati ungeenda Step entertainment ungepata ajira nzuri ya kuwa director wa bongo muvii
 
mzee mwanakijiji unanichanganya it is in the middle of campaign alafu unatuambia tusimchague lowasa je tuendeee na CCM hiyo hiyo? mpaka 2020 ?

kwanini usiwapigie debe wabunge na wmadiwani wa upinzani ili tuwe na bunge ambalo litakuwa na wapinzani wengi so we can challenge the goverment? kuliko kuelekeza nguvu nyingi kumpinga lowasa bcs at the end of the day ameshapitishwa na chama/UKAWA sijui kama inasaidia sana sasa ivi kushutumu sana tungojee uchaguzi ukiisha then tuamue kama kuna haja ya kuangalia kwa nini BAADHI YA VIONGOZI WA CDM/UKAWA WALIAMUA HAYO MAAMUZI YA KUMPITISHA LOWASA AS A CANDIDATE FOR UKAWA.
 
NB: Video Inafuata

Operesheni Zinduka imeanza kama nilivyoahidi (jana haikuwezekana kwa sababu moja tu ya heshima ya Mch. Mtikila na haihusiani na mipango ya watu wengine). Nitajitahidi kuwa na onesho hili kila siku (ukiondoa mwisho wa Juma) na nitazungumzia mada mbalimbali. Wiki hii ya kwanza zaidi nitagusia hoja nyingi zilizoibuliwa kutushangaa tunaomkataa Lowassa kama mgombea Urais kwa tiketi ya upinzani.

La pili nitajitahidi hasa wiki ile inayokuja kutoa nafasi kwa wagombea wa CHADEMA kwenye Ubunge (ambao tutaweza kuwafikia) ili wajiuze kwani ninaamini Bunge lenye nguvu lililoundwa na watu waliolelewa na kukomaa katika upinzani na wenye kuelewa hasa ajenda ya upinzani ndio chachu ya kweli ya mabadiliko tuyatakayo. Hivyo, wiki ile inayokuja tutatoa nafasi hii kwa wote tutakaoweza kuwapata.

Tatu, kwa vile nina uhakika wapo wengi ambao hawajakubaliana na uamuzi wangu huu (ambao naamini ni sahihi) basi nitatoa nafasi pia kwa watu wengine kutoa hoja zao dhidi ya ninachosema (sikiliza onesha hili juu ya 'mashart kuzingatiwa'). Kwa barua pepe anuani yangu ipo chini na namna nyingine ya mawasiliano nitawajulisha siku chache zijazo.

Nitajitahidi kuweka shows zote kwenye uzi huu huu kila siku, na video zitafuata chini toka ya zamani zaidi hadi mpya zaidi.

Mwisho, ninaamini na nina uhakika kuwa kwa atakayeamua kunisikiliza kuanzia sasa hadi kuamkia Uchaguzi Mkuu hatoweza kumpigia Lowassa kura ya Urais. Ni kwa sababu hiyo wale ambao tayari wameshaamua kuwa haijalishi nini kitasemwa juu ya Lowassa nawaomba au kuwashauri wasisikilize mada hizi wasije kujikuta wanabadili mawazo. Mada hizi ni kwa wale tu ambao bado hawajaamua au wale ambao wameamua lakini bado wanajikuwa wanavuta na upepo wa 'nyomi' kiasi kwamba bado hawajathibitika katika msimamo wao.

"Uamuzi Makini, Uamuzi wa Lazima, Uamuzi Sahihi"

MMM

ONESHO 1. "Baada ya Kelele Sauti za Hoja Zitashinda"
Wewe babu tulia tulishaamua kumchagua Lowassa hiyo zinduka fanya na vigagula wenzio
 
Last edited by a moderator:
Wabunge wa upinzani wanaenda kusimamia ajenda hipi kama vyama vyao vimeuwa misingi na kanuni zao kwasababu ya masrahii ya watu wachache?

Sikuwai kutegemea nitakuja kuichagua ccm katika maisha yangu ila kwa waliyotufanyia ukawa sioni wa kuchagua zaidi ya Magufuli na mbunge wa ccm na diwani.


Bado tunaendelea kusubiri mabadiliko ya kweli.
 
Huyu ni Mzee Mwanakijiji;

Nimeomba kadi karibu miaka miwili iliyopita; hivi majuzi nikafikiri wananipatia lakini wakawa wanataka vithibitisho utadhani nataka kujiunga CIA.. Mwishoni wananiambia "tumesikia una mpango wa kutusafisha... CCM safi haiitaji kusafishwa"..

Pasco akamfariji;

.
Pole Mzee, kadi is nothing but a piece of paper, kinachomater ni ile genuine desire deep down your heart to see Tanzania change for the better. Japo wamekukatalia hiyo kadi, amini maneno yangu, utafikia wakati CCM watapata busara za uoni wa ndani jinsi unavyowasaidia, watakuita, watakubembelezea kadi, na utaitwa Magogoni na kuobwa 'tusaidiane'!.

[FONT=century gothic [USER=118]Mzee Mwanakijiji[/USER] akamjibu;[/FONT]

hahaha Pasco.. usiumie sana; kadi wamenikatalia ati nitakuwa pandikizi; ...

.leo hii anataka tuamini kwa miaka 20 alikuwa upinzani? Ninachojua - na kuamini- ni kuwa muda wote huo akiwa mwanachama wa ccm amekuwa akijua na kuona kuwa hawatendi sawasawa na ahadi zao na hili amekuwa akilipigia kelele tangu enzi hizo. Leo unataka kutuaminisha fikra zako ni huru (ilhali uliomba kadi ya uanachama)!???

Hivi unawachukuliaje Watanzania kwa mfano? Yani mimi shida yangu kwako ni kutudanganya tu! Nisigekuona muongo na mfitini kama ungeacha kutumia sifa hiyo ya 'mwandishi huru' useme tu wewe ni ccm na ndiyo sababu ya kutomtaka Lowassa! .
 
Last edited by a moderator:
Sikuwai kutegemea nitakuja kuichagua ccm katika maisha yangu ila kwa waliyotufanyia ukawa sioni wa kuchagua zaidi ya Magufuli na mbunge wa ccm na diwani.


Bado tunaendelea kusubiri mabadiliko ya kweli.

Ukiyakosa mwaka huu labda kama huko kuzimu kuna mabadiliko, au wajukuu zako! Maana kwa miaka ya hivi karibuni sahau mabadiliko!
 
Mwanakijiji umemdharirisha sana Mtikila kuimba nyimbo ya Tanzania Tanzania nakupenda kwa moyo wote. Mtikila mpaka anafariki alikua haitambui Tanzania yeye alikua anaitambua Tanganyika. Ningekushauri ungeimba wimbo wowote unaohusina na Tanganyika kama upo. Pia ningekushauri urekebishe yafuatayo unapokuja kwa mara ya pili
1. Maneno kama NINGE, NITA, etc usiyatumie sababu inaonesha unapenda kutukuzwa
2. Tuna wagombea tayari, unatushauri nini sisi wapiga kura ie nani anafaa kua urisi ?
3. Maoni yako yanamlenga zaidi Lowasa, kwanini usifanye uchambuzi wako kwa wagombea wote ili sisi wapiga kura tuweze kuchuja yupi anafaa na yupi hafai?
4. Kwa hii clip inaonesha unachuki zaidi kwa Lowasa, huoni kwamba kuna kitu kimefichika nyuma ya pazia kinachokusukuma kwenye hili.

Asante

Mkuu achana kabisa na mambo ya muamala!

Ungeweza kuamini huko zamani, mtu kama Slaa angekuwa ndembendembe kama hivi?
 
mi sihitaji kusikiliza opresheni zinduka ili kufanya maamuzi nilishaamua kutompa kura lowassa bila kujali anagombea chama gani pia kukinyima kura chama chochote atakachogombea lowassa
 
Huu ushabiki tena kutoka kwa wakongwe wa humu ambao wameshiriki kikamilifu mijadala ya ufisadi inanifanya nihisi akili yangu labda haiko sawa. Wajanja waliovuruga kule na tunajua vyema historia yao wanaibukia kwetu tunawakabidhi kila kitu!! Huu uchaguzi utakuwa na matokeo hasi kwa upinzani kuliko hata 2010..
 
Wewe Mzee mwanakijiji huko ulipo kama unaishabikia CCM nachelea kusema wewe biashara yako huko ulipo ni ya kuuza madawa ya kulevya na hapo unatetea haki zako za msingi katika biashara yako na si vinginevyo kwani CCM ndio kimbilio na mafichoni kwa walanguzi wa dawa za kulevya.
 
UKAWA tukishinda uchaguzi huu. MM na Dr Mihogo habari yenyu ndio kwishilia mbali!
 
Kumekucha tena makamamda operesheni Zinduka hiyo.

huyo hana lolote kazi kuandika mabandiko huku kichwa kakiingiza kwenye keyboard.

operation zinduka wakati hata avatar yake kaweka picha feki atamzinduwa nani?
 
Huyu ni Mzee Mwanakijiji;



@pasco akamfariji;



[FONT=century gothic [B]Mzee Mwanakijiji[/B] akamjibu;[/FONT]



.leo hii anataka tuamini kwa miaka 20 alikuwa upinzani? Ninachojua - na kuamini- ni kuwa muda wote huo akiwa mwanachama wa ccm amekuwa akijua na kuona kuwa hawatendi sawasawa na ahadi zao na hili amekuwa akilipigia kelele tangu enzi hizo. Leo unataka kutuaminisha fikra zako ni huru (ilhali uliomba kadi ya uanachama)!???

Hivi unawachukuliaje Watanzania kwa mfano? Yani mimi shida yangu kwako ni kutudanganya tu! Nisigekuona muongo na mfitini kama ungeacha kutumia sifa hiyo ya 'mwandishi huru' useme tu wewe ni ccm na ndiyo sababu ya kutomtaka Lowassa! .

Hii ni hatari, kumbe uyu mzee ni CCM damu. Ajitokeze ajibu
 
UKAWA kwa moto, CCM kwa moto!

Naweza kuelewa unavyopata tabu katika fikra. Unashindwa kui support CCM na Magufuli waziwazi kwa sababu unaogopa kula matapishi yako lakini pia unashindwa kuisupport UKAWA/CDM kwa sababu wamemweka msiyemtaka, wamekataa kufuata 'masharti' mliyowapa (ili mkubaliane nao).

Muhimu ni kuwa watanzania wengi tayari wanajua wanachotaka.....Mabadiliko. Unachoweza kufanya kwa sasa ni kuwaambia ni vipi watayapata kutoka CCM else watayatafuta kutoka UKAWA!

Pole sana MMM.
 
Back
Top Bottom