Kudo
JF-Expert Member
- Nov 2, 2017
- 1,809
- 6,081
- Thread starter
- #41
RIWAYA; OPERESHENI KUKU (KUFA KUPONA)
NA; BAHATI MWAMBA
SIMU; 0758573660
SEHEMU YA SITA
--EAGLE WING HOUSE-DAR—
Mwanamke aliependeza kwenye sare zake za jeshi alishusha mkonga wa simu ya mezani huku uso wake ukiwa umejikunja na mdomo wake akiwa ameupeleka mbele kama kalambishwa konyagi.
Akakalia kiti chake cha kuzunguka na kuweka miguu juu ya meza iliokuwa mbele yake huku mikono yake akiufumbata pamoja na kuilaza juu kidogo ya kinena kisha macho yake yakatua juu ya ukuta na kukutana na picha ya rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania.
Mwanamama yule mabegani mwake alikuw na kola yenye ngao (bibi na bwana) kisha nyota tatu kumaanisha cheo chake kilikuwa Brigedia Jeneral na juu kidogo ya mfuko wa vazi lake la juu kulikuwa kuna jina lake.
Alikuwa ni Brigedia Jeneral Hawa Maiga.
Muda huo alikuwa ametoka kuwasiliana na simu mbili huku simu ya kwanza ikiwa ni kutoka nchini Congo kwenye vikosi vya umoja wa mataifa na kuarifiwa kuwa mkubwa wa waasi Chepe alikuwa amegoma kuzungumza nao hivyo walikuwa hawajui ni nini shida yake kwa waandishi wale.
Bi Hawa Maiga alishindwa kuelewa kama Chepe alishindwa kuzungumza ni kwa kuwa amejua aina ya watu aliowateka ama anahisi tu.
Bi. Hawa Maiga alimtambua vyema Chepe kuliko mtu yeyote na alijua ni lazima Chepe atakuwa amejua wale ni Zedi na Mina kutoka kwenye kitengo chake cha MI chini ya mwamvuli wa special operations..
“Lakini nimekutengeneza mimi Chepe na huwezi kushindana na mimi hata kidogo, uliowaua wanatosha, familia zao zimelia vya kutosha nisingependa tena damu imwagike ni lazima nikutie mikononi hata kwa kuingia mi mwenyewe” Brigedia Jeneral Hawa Maiga alijisemea huku akitikisa mguu wake wa kulia na kwa waliomfahamu hapo walijua yupo kwenye kiwango cha mwisho cha hasira na hata ukimzingua unaweza kuchezea risasi ama mbata za kutosha.
Bi Hawa pia alikuwa amepiga Simu kwa Kamishina Zenge wa Zenge ambae nae alikuwa ni msimamizi wa operesheni maalumu upande wa jeshi la polisi huku yeye akiwa ni msimamizi wa operesheni maalumu upande wa jeshi yani Military intelligence (MI).
Kwa nini walishirikiana?
Kwa sababu vijana wa special operations walikuwa ni wale wale huku wakijigawa kimajukumu kulingana na uzito wa kazi kila pande hivyo wakiwa chini ya Zenge wa Zenge walipaswa kufanya kazi za kipolisi na wakiwa chini ya Hawa Maiga wanafanya kazi za jeshi kikamilifu kwa kuwa wote walikuwa ni makomando waliofuzu kila idara na pia walikuwa wameiva kwenye mafunzo ya ujasusi na upelelezi.
Simu aliopiga ilimhitaji Kamishina afike makao makuu yao wote kwa kikao chao cha dharura kuhusu jambo lile.
Na kikao kile ndicho kilizaaa balaa na kizaaa zaa kikubwa ndani ya Dar na nchini Congo na ikawa ni operesheni kufa kupona iwe jua iwe mvua.
****
Kamishina Zenge wa Zenge aliingia kwenye ofisi ya Bi Hawa Maiga zikiwa zimebaki sekunde chache kutimia saa moja tangu alipopokea simu ya wito kutoka kwa Bi Hawa Maiga wa kitengo cha special operations ndani ya idara ya MI katika jeshi la wananchi.
Alikaa kwenye kiti bila kukaribishwa huku akitupa bareti yake karibu na miguu ya Brigedia Jenerali Hawa Maiga.
“Usiniambie kama hii ni priority Red!!” Kamishina Zenge wa Zenge alianzisha mazungumzo huku salamu ikiwa si kipaumbele chao wakati huo.
“Yes!! Ni priority red Kamishina!!” Hawa alijibu huku akishusha miguu kwenye meza na kumtazama Kamishina Zenge wa Zenge.
“So!!” Zenge alihoji hivyo..
“Rescue team!! Nadhani ndo kipaumbele chetu kwa sasa kwa sababu spies are blacked!!” Brigedia Hawa Maiga alimwambia Kamishina Zenge wa Zenge.
“Why!?” Kamishina aliuliza.
“Kila wanaokanyaga maguu kule Beni wanarudi vichwa chini kwa kifo ama vilema,idara ipo hoi sasa!!” Brigedia alijibu.
“Unataka kusema nini juu ya Mina na Zedi?” Kamishina aliuliza huku akiwa ametoa jicho kuashiria hakupenda kusikia habari mbaya kuwahusu.
“Mitambo ilitoa taarifa ya kuwa wao wapo matatizoni na ni ngumu kupona!!” Hawa Maiga alijibu.
“What!!!” Zenge wa Zenge alishangaa.
“Kompyuta ya malkia ilitoa mlio kuashiria moja ya vijana wa special op,yupo matatizoni na wataalamu walipojaribu kufuatilia waligundua ni kompyuta ya Mina ndio imetoa taarifa na tulipojaribu kifuatilia kwa Sattelite ilionesha ipo kwenye msitu wa Ndeko magharibi mwa Butembo!!” Brigedia Hawa Maiga alisema huku akichomoa picha mbili kutoka kwenye makabrasha yaliokuwa karibu na mikono yake..
Picha zile alimrushia Kamishina Zenge wa Zenge.
Zenge wa Zenge alizichukua picha zile na kuzitazama.
Picha zote zilikuwa ni za mtu mmoja ila isipokuwa picha moja ilikuwa ni ya mtu akiwa na mavazi ya jeshi la wananchi huku juu kidogo ya bega lake la kushoto kukiwa kuna mchoro wa ndege aliechanua mabawa hewani.
Hiyo ilimaanisha yule mtu alikuwa ni komando wa daraja la juu sana akiwa amefuzu hatua zote za ujasusi na ukomando. Na picha ya pili ilikuwa ni ya mtu yuleyule ila akiwa amevaa kanzu nyeupe na baragashia; lakini mtu yule alievaa kanzu alikuwa amevaa na kiziba jicho cha rangi nyeusi na mikanda ilionekana kupita kushoto na kulia ili kushikilia kizibo kile.
“Hii ina maana gani!!” Kamishina aliuliza baada ya kutoelewa kinachoendelea..
“Huyo ndie Chepe Mazonge; ambae ndie kiongozi mtendaji wa kikundi cha waasi nchini Congo!!”Bi Hawa alifafanua.
“Muasi Congo? Sa mbona anamavazi ya jeshi letu?” Zenge wa Zenge alihoji.
“Aliwahi kuwa hapa na pia nimemlea mimi hadi alipofikia kuasi na kukimbilia msituni huko Congo hivyo anatujua vizuri sana huyu jamaa!!” Bi Hawa alifafanua tena kuhusu picha zile.
Kamishina alijikuna kichwa kwa kidole cha mwisho huku akili yake ikicheza sombolo bila kupata majibu..
“Usitake kunambia kambi zetu zilizokuwa zinavamiwa aliongoza yeye!!” Kamishina alitoa hoja kwa wasiwasi.
“Ndo yeye huyo na kubwa anaua kila mtanzania anaehisi ni shushu bila kuwa na hakika!!” Bi Hawa alijibu.
.
“Ajabu hii!!” Kamishina alishangaa.
“Kwa hiyo unasemaje labda!!” Kamishina alihoji.
“Zedi na Mina kuwa chini ya Chepe ni kuliangamiza taifa,mi nadhani tupeleke huko kikosi maalumu kuwakomboa na ikibidi kumchakaza huyu jamaa.” Bi Hawa alimwambia Kamishina.
“Una hisi hilo ni wazo sahihi katika kipindi hiki?” Kamishina alihoji.
“Hakuna namna tena ya kupeleka jasusi wakati kila anaetia maguu kwenye anga za Chepe anarudi akiwa mbali na Dunia!!” Hawa Maiga alimwambia Zenge wa Zenge.
“Afu huyu Chepe ni mtu ambae alifanya kazi ya ujasusi kwa kiwango kikubwa sana, hivyo anajua ABC za kazi hii na kupeleka jasusi wengine ni kuwauza tu bila kuwahurumia.” Brigedia alimwambia Kamishina.
Kamishina alifikiria kidogo kisha akasema
“Na kwa nini huyu jamaa anawagundua vyema majasusi wetu kiasi hicho?”
“Hujuma Kamishina;tunahujumiwa kuanzia mamlakani hadi huko Duniani!” Brigedia Hawa Maiga alimwambia Kamishina Zenge wa Zenge.
“Kama tuhujumiwa kuanzia hapa basi tuna kazi kubwa sana ya kufanya.” Kamishina alisema huku akichukua simu yake na kutazama muda.
“Nadhani tunapaswa pia kufanya jambo ili kuondoa hujuma hizi!” Kamishina alisema.
“Unadhani tutaweza vipi?” Brigedia jenereli Hawa Maiga alihoji.
“Siku za karibuni nitamhitaji Honda Makubi ambae yupo masoni Israel lakini pia ni mtu anaeifahamu sana Congo,nadhani anafaa kuanza na hili jambo!!” Kamishina alimwambia Hawa Maiga.
“Ni sawa mawazo yako lakini kuna kitu tunasahau Kamishina.” Hawa Maiga alimwambia Kamishina Zenge wa Zenge.
“Jambo gani!!” Kamishina aliuliza.
“Alienyuma ya Chepe ni nani na anatokea nchi gani au ni nchi gani ilioko nyuma ya Chepe na Chepe kikundi chake kinaitwaje na kwa nini hadi sasa wanafanya kazi nyuma ya migongo ya waasi wengine?” Bi Hawa Maiga alimfafanulia Zenge wa Zenge.
“Yes!! Inafikirisha hii.” Kamishina aliitikia.
“Ni lazima tujue nguvu anatoa wapi na ni wapi anapata taarifa nyeti za uwepo wa madini kwenye sehemu vinapoweka mahema vikosi vya kulinda amani kutoka Tanzania!!” Bi Hawa alimwambia Kamishina.
“Kuna tatizo sehemu Brigedia na hatuna namna zaidi ya kujua ni wapi tunapopigiwa!!” Kamishina alimwabia Hawa Maiga.
“Hakuna kungoja inabidi operesheni kubwa ifanyike ili tuwakomboe Mina na Zedi.” Hawa aliendelea kusisitiza lengo lake.
“Sawa fanya kile kinachostahili kufanywa!” Kamishina alijibu huku akisimama na kisha wakapigiana saluti na kila mmoja akaendelea na shuguli zake.
Baada ya kamishina Zenge wa Zenge kutoka ofisini kwake; Brigedia jenerali Hawa Maiga alichukua ramani moja iliokuwa mezani kwake kisha akaelekea kwenye chumba cha mkutano katika ofisi ile na kisha akaandika ujumbe kwenye simu yake na kuusambaza kwa watu sita aliowahitaji muda huo.
Haukuchukua hata dakika arobaini, tayari chumba kilikuwa kimetimia wanaume sita huku mtu wa saba na akiwa ni mwanamke pekee akiwa ni Bi Hawa Maiga mwenye cheo cha Brigedia Jeneral.
Wanaume wale walikuwa wamejazia vyema miili yao huku nyuso zao zikionesha ukomavu wa hali ya juu katika medani za kivita.
Wanaume wote walikuwa na alama ya ndege akipaa kwenye mabega yao huku chini yake kukiwa kuna michoro ya jambia zilizopishana.
Ilimaanisha Bi Hawa alikuwa amekutana na timu ya makomando walio chini ya kitengo chake anachokiongoza cha Military intelligence na special operations.
Brigedia Hawa Maiga akawatazama wote baada ya kila mmoja kutoa saluti kwake na kukaa.
Aliwatizama mmoja mmoja huku akijaribu kuona kama nyuso zao zinaweza kuwa tayari kwa kile alichowaitia pale.
Bi Hawa Maiga alihitaji kufanya operesheni ya siri nchini Congo huku lengo lake likiwa ni kuwakomboa Zedi Wimba na Mina; watu ambao aliwathamini kuliko ngozi yake na aliamini wakibanwa wanaweza kutoa mengi kwa Chepe ambae hakuna anaejua uasi wake kama utaishia huko Congo ama utaibuka hadi hapa nchini mana ni yeye pekee aliejua kwa nini Chepe aliamua kuasi jeshi na mabishano yao yalikuwa ni nini hadi Chepe akamua kuvunja mkeka.
Bi hawa aliita Roger Team 6. Kikosi maalumu kwa kazi maalumu na hakijawahi kushindwa huku operesheni yao ya kukumbukwa ni ile ya kumkomboa Waziri wa ulinzi Kenya aliekuwa anazuiliwa na kikundi cha waasi wa Al shabaab huko Somalia na timu hii ikapewa kazi moja tu kuhakikisha waziri anarudi salama nchini mwake huku kazi ile ikiwa inajulikana na Rais wa Kenya na watu wachache nchini ili kuondoa hujuma ambazo Rais wa Kenya alizigundua kwenye baraza lake la mawaziri.
Timu hii haijawahi kumuangusha Bi Hawa Maiga na haijawahi kupoteza mpiganaji wake hata mmoja.
Roger Team 6 ilikuwa inaongozwa na Luteni Rambo (code name) ambae jina lake halisi aliitwa Zuri Sanadi.
Rambo hakuwahi kufeli katika misheni zote alizowahi kuziongoza.
Rambo mara nyingi hakupenda kikosi kiitwe timu 6 wawapo kazini bali alipenda kuita kikosi chake “BAMBADIKA” ikiwa na maana ya Shimo la Mamba; msemo maarufu sana huko Gambia na wao walijiona ni sawa na shimo hilo kwa kuwa adui kwao hajawahi kupona kila walipomweka kwenye rada za kuingia kwenye shimo hilo.
Bambadika chini ya Rambo walikuwa kimya kungojea maelezo toka kwa Brigedia Jeneral Hawa Maiga.
Wakati Bi Hawa akiweka akili sawa kutuma kikosi chake nchini Congo; Kamishina Zenge wa Zenge nae alikuwa anamalizia kuwasiliana na Komando na Jasusi Honda Makubi aliekuwa Israel kwa mafunzo maalumu baada ya kuwa ametoka kuuguza majeraha yake alioyapata huko Somalia katika mkasa wa Urithi wa Gaidi.
Ujio wake ilikuwa ni kawaida kwake yeye na Kamishina ila ilikuwa ni taharuki kwa majahili na wazandiki waliokuwa wanacheza na kitengo cha kazi maalumu “Special operations”.
NA; BAHATI MWAMBA
SIMU; 0758573660
SEHEMU YA SITA
--EAGLE WING HOUSE-DAR—
Mwanamke aliependeza kwenye sare zake za jeshi alishusha mkonga wa simu ya mezani huku uso wake ukiwa umejikunja na mdomo wake akiwa ameupeleka mbele kama kalambishwa konyagi.
Akakalia kiti chake cha kuzunguka na kuweka miguu juu ya meza iliokuwa mbele yake huku mikono yake akiufumbata pamoja na kuilaza juu kidogo ya kinena kisha macho yake yakatua juu ya ukuta na kukutana na picha ya rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania.
Mwanamama yule mabegani mwake alikuw na kola yenye ngao (bibi na bwana) kisha nyota tatu kumaanisha cheo chake kilikuwa Brigedia Jeneral na juu kidogo ya mfuko wa vazi lake la juu kulikuwa kuna jina lake.
Alikuwa ni Brigedia Jeneral Hawa Maiga.
Muda huo alikuwa ametoka kuwasiliana na simu mbili huku simu ya kwanza ikiwa ni kutoka nchini Congo kwenye vikosi vya umoja wa mataifa na kuarifiwa kuwa mkubwa wa waasi Chepe alikuwa amegoma kuzungumza nao hivyo walikuwa hawajui ni nini shida yake kwa waandishi wale.
Bi Hawa Maiga alishindwa kuelewa kama Chepe alishindwa kuzungumza ni kwa kuwa amejua aina ya watu aliowateka ama anahisi tu.
Bi. Hawa Maiga alimtambua vyema Chepe kuliko mtu yeyote na alijua ni lazima Chepe atakuwa amejua wale ni Zedi na Mina kutoka kwenye kitengo chake cha MI chini ya mwamvuli wa special operations..
“Lakini nimekutengeneza mimi Chepe na huwezi kushindana na mimi hata kidogo, uliowaua wanatosha, familia zao zimelia vya kutosha nisingependa tena damu imwagike ni lazima nikutie mikononi hata kwa kuingia mi mwenyewe” Brigedia Jeneral Hawa Maiga alijisemea huku akitikisa mguu wake wa kulia na kwa waliomfahamu hapo walijua yupo kwenye kiwango cha mwisho cha hasira na hata ukimzingua unaweza kuchezea risasi ama mbata za kutosha.
Bi Hawa pia alikuwa amepiga Simu kwa Kamishina Zenge wa Zenge ambae nae alikuwa ni msimamizi wa operesheni maalumu upande wa jeshi la polisi huku yeye akiwa ni msimamizi wa operesheni maalumu upande wa jeshi yani Military intelligence (MI).
Kwa nini walishirikiana?
Kwa sababu vijana wa special operations walikuwa ni wale wale huku wakijigawa kimajukumu kulingana na uzito wa kazi kila pande hivyo wakiwa chini ya Zenge wa Zenge walipaswa kufanya kazi za kipolisi na wakiwa chini ya Hawa Maiga wanafanya kazi za jeshi kikamilifu kwa kuwa wote walikuwa ni makomando waliofuzu kila idara na pia walikuwa wameiva kwenye mafunzo ya ujasusi na upelelezi.
Simu aliopiga ilimhitaji Kamishina afike makao makuu yao wote kwa kikao chao cha dharura kuhusu jambo lile.
Na kikao kile ndicho kilizaaa balaa na kizaaa zaa kikubwa ndani ya Dar na nchini Congo na ikawa ni operesheni kufa kupona iwe jua iwe mvua.
****
Kamishina Zenge wa Zenge aliingia kwenye ofisi ya Bi Hawa Maiga zikiwa zimebaki sekunde chache kutimia saa moja tangu alipopokea simu ya wito kutoka kwa Bi Hawa Maiga wa kitengo cha special operations ndani ya idara ya MI katika jeshi la wananchi.
Alikaa kwenye kiti bila kukaribishwa huku akitupa bareti yake karibu na miguu ya Brigedia Jenerali Hawa Maiga.
“Usiniambie kama hii ni priority Red!!” Kamishina Zenge wa Zenge alianzisha mazungumzo huku salamu ikiwa si kipaumbele chao wakati huo.
“Yes!! Ni priority red Kamishina!!” Hawa alijibu huku akishusha miguu kwenye meza na kumtazama Kamishina Zenge wa Zenge.
“So!!” Zenge alihoji hivyo..
“Rescue team!! Nadhani ndo kipaumbele chetu kwa sasa kwa sababu spies are blacked!!” Brigedia Hawa Maiga alimwambia Kamishina Zenge wa Zenge.
“Why!?” Kamishina aliuliza.
“Kila wanaokanyaga maguu kule Beni wanarudi vichwa chini kwa kifo ama vilema,idara ipo hoi sasa!!” Brigedia alijibu.
“Unataka kusema nini juu ya Mina na Zedi?” Kamishina aliuliza huku akiwa ametoa jicho kuashiria hakupenda kusikia habari mbaya kuwahusu.
“Mitambo ilitoa taarifa ya kuwa wao wapo matatizoni na ni ngumu kupona!!” Hawa Maiga alijibu.
“What!!!” Zenge wa Zenge alishangaa.
“Kompyuta ya malkia ilitoa mlio kuashiria moja ya vijana wa special op,yupo matatizoni na wataalamu walipojaribu kufuatilia waligundua ni kompyuta ya Mina ndio imetoa taarifa na tulipojaribu kifuatilia kwa Sattelite ilionesha ipo kwenye msitu wa Ndeko magharibi mwa Butembo!!” Brigedia Hawa Maiga alisema huku akichomoa picha mbili kutoka kwenye makabrasha yaliokuwa karibu na mikono yake..
Picha zile alimrushia Kamishina Zenge wa Zenge.
Zenge wa Zenge alizichukua picha zile na kuzitazama.
Picha zote zilikuwa ni za mtu mmoja ila isipokuwa picha moja ilikuwa ni ya mtu akiwa na mavazi ya jeshi la wananchi huku juu kidogo ya bega lake la kushoto kukiwa kuna mchoro wa ndege aliechanua mabawa hewani.
Hiyo ilimaanisha yule mtu alikuwa ni komando wa daraja la juu sana akiwa amefuzu hatua zote za ujasusi na ukomando. Na picha ya pili ilikuwa ni ya mtu yuleyule ila akiwa amevaa kanzu nyeupe na baragashia; lakini mtu yule alievaa kanzu alikuwa amevaa na kiziba jicho cha rangi nyeusi na mikanda ilionekana kupita kushoto na kulia ili kushikilia kizibo kile.
“Hii ina maana gani!!” Kamishina aliuliza baada ya kutoelewa kinachoendelea..
“Huyo ndie Chepe Mazonge; ambae ndie kiongozi mtendaji wa kikundi cha waasi nchini Congo!!”Bi Hawa alifafanua.
“Muasi Congo? Sa mbona anamavazi ya jeshi letu?” Zenge wa Zenge alihoji.
“Aliwahi kuwa hapa na pia nimemlea mimi hadi alipofikia kuasi na kukimbilia msituni huko Congo hivyo anatujua vizuri sana huyu jamaa!!” Bi Hawa alifafanua tena kuhusu picha zile.
Kamishina alijikuna kichwa kwa kidole cha mwisho huku akili yake ikicheza sombolo bila kupata majibu..
“Usitake kunambia kambi zetu zilizokuwa zinavamiwa aliongoza yeye!!” Kamishina alitoa hoja kwa wasiwasi.
“Ndo yeye huyo na kubwa anaua kila mtanzania anaehisi ni shushu bila kuwa na hakika!!” Bi Hawa alijibu.
.
“Ajabu hii!!” Kamishina alishangaa.
“Kwa hiyo unasemaje labda!!” Kamishina alihoji.
“Zedi na Mina kuwa chini ya Chepe ni kuliangamiza taifa,mi nadhani tupeleke huko kikosi maalumu kuwakomboa na ikibidi kumchakaza huyu jamaa.” Bi Hawa alimwambia Kamishina.
“Una hisi hilo ni wazo sahihi katika kipindi hiki?” Kamishina alihoji.
“Hakuna namna tena ya kupeleka jasusi wakati kila anaetia maguu kwenye anga za Chepe anarudi akiwa mbali na Dunia!!” Hawa Maiga alimwambia Zenge wa Zenge.
“Afu huyu Chepe ni mtu ambae alifanya kazi ya ujasusi kwa kiwango kikubwa sana, hivyo anajua ABC za kazi hii na kupeleka jasusi wengine ni kuwauza tu bila kuwahurumia.” Brigedia alimwambia Kamishina.
Kamishina alifikiria kidogo kisha akasema
“Na kwa nini huyu jamaa anawagundua vyema majasusi wetu kiasi hicho?”
“Hujuma Kamishina;tunahujumiwa kuanzia mamlakani hadi huko Duniani!” Brigedia Hawa Maiga alimwambia Kamishina Zenge wa Zenge.
“Kama tuhujumiwa kuanzia hapa basi tuna kazi kubwa sana ya kufanya.” Kamishina alisema huku akichukua simu yake na kutazama muda.
“Nadhani tunapaswa pia kufanya jambo ili kuondoa hujuma hizi!” Kamishina alisema.
“Unadhani tutaweza vipi?” Brigedia jenereli Hawa Maiga alihoji.
“Siku za karibuni nitamhitaji Honda Makubi ambae yupo masoni Israel lakini pia ni mtu anaeifahamu sana Congo,nadhani anafaa kuanza na hili jambo!!” Kamishina alimwambia Hawa Maiga.
“Ni sawa mawazo yako lakini kuna kitu tunasahau Kamishina.” Hawa Maiga alimwambia Kamishina Zenge wa Zenge.
“Jambo gani!!” Kamishina aliuliza.
“Alienyuma ya Chepe ni nani na anatokea nchi gani au ni nchi gani ilioko nyuma ya Chepe na Chepe kikundi chake kinaitwaje na kwa nini hadi sasa wanafanya kazi nyuma ya migongo ya waasi wengine?” Bi Hawa Maiga alimfafanulia Zenge wa Zenge.
“Yes!! Inafikirisha hii.” Kamishina aliitikia.
“Ni lazima tujue nguvu anatoa wapi na ni wapi anapata taarifa nyeti za uwepo wa madini kwenye sehemu vinapoweka mahema vikosi vya kulinda amani kutoka Tanzania!!” Bi Hawa alimwambia Kamishina.
“Kuna tatizo sehemu Brigedia na hatuna namna zaidi ya kujua ni wapi tunapopigiwa!!” Kamishina alimwabia Hawa Maiga.
“Hakuna kungoja inabidi operesheni kubwa ifanyike ili tuwakomboe Mina na Zedi.” Hawa aliendelea kusisitiza lengo lake.
“Sawa fanya kile kinachostahili kufanywa!” Kamishina alijibu huku akisimama na kisha wakapigiana saluti na kila mmoja akaendelea na shuguli zake.
Baada ya kamishina Zenge wa Zenge kutoka ofisini kwake; Brigedia jenerali Hawa Maiga alichukua ramani moja iliokuwa mezani kwake kisha akaelekea kwenye chumba cha mkutano katika ofisi ile na kisha akaandika ujumbe kwenye simu yake na kuusambaza kwa watu sita aliowahitaji muda huo.
Haukuchukua hata dakika arobaini, tayari chumba kilikuwa kimetimia wanaume sita huku mtu wa saba na akiwa ni mwanamke pekee akiwa ni Bi Hawa Maiga mwenye cheo cha Brigedia Jeneral.
Wanaume wale walikuwa wamejazia vyema miili yao huku nyuso zao zikionesha ukomavu wa hali ya juu katika medani za kivita.
Wanaume wote walikuwa na alama ya ndege akipaa kwenye mabega yao huku chini yake kukiwa kuna michoro ya jambia zilizopishana.
Ilimaanisha Bi Hawa alikuwa amekutana na timu ya makomando walio chini ya kitengo chake anachokiongoza cha Military intelligence na special operations.
Brigedia Hawa Maiga akawatazama wote baada ya kila mmoja kutoa saluti kwake na kukaa.
Aliwatizama mmoja mmoja huku akijaribu kuona kama nyuso zao zinaweza kuwa tayari kwa kile alichowaitia pale.
Bi Hawa Maiga alihitaji kufanya operesheni ya siri nchini Congo huku lengo lake likiwa ni kuwakomboa Zedi Wimba na Mina; watu ambao aliwathamini kuliko ngozi yake na aliamini wakibanwa wanaweza kutoa mengi kwa Chepe ambae hakuna anaejua uasi wake kama utaishia huko Congo ama utaibuka hadi hapa nchini mana ni yeye pekee aliejua kwa nini Chepe aliamua kuasi jeshi na mabishano yao yalikuwa ni nini hadi Chepe akamua kuvunja mkeka.
Bi hawa aliita Roger Team 6. Kikosi maalumu kwa kazi maalumu na hakijawahi kushindwa huku operesheni yao ya kukumbukwa ni ile ya kumkomboa Waziri wa ulinzi Kenya aliekuwa anazuiliwa na kikundi cha waasi wa Al shabaab huko Somalia na timu hii ikapewa kazi moja tu kuhakikisha waziri anarudi salama nchini mwake huku kazi ile ikiwa inajulikana na Rais wa Kenya na watu wachache nchini ili kuondoa hujuma ambazo Rais wa Kenya alizigundua kwenye baraza lake la mawaziri.
Timu hii haijawahi kumuangusha Bi Hawa Maiga na haijawahi kupoteza mpiganaji wake hata mmoja.
Roger Team 6 ilikuwa inaongozwa na Luteni Rambo (code name) ambae jina lake halisi aliitwa Zuri Sanadi.
Rambo hakuwahi kufeli katika misheni zote alizowahi kuziongoza.
Rambo mara nyingi hakupenda kikosi kiitwe timu 6 wawapo kazini bali alipenda kuita kikosi chake “BAMBADIKA” ikiwa na maana ya Shimo la Mamba; msemo maarufu sana huko Gambia na wao walijiona ni sawa na shimo hilo kwa kuwa adui kwao hajawahi kupona kila walipomweka kwenye rada za kuingia kwenye shimo hilo.
Bambadika chini ya Rambo walikuwa kimya kungojea maelezo toka kwa Brigedia Jeneral Hawa Maiga.
Wakati Bi Hawa akiweka akili sawa kutuma kikosi chake nchini Congo; Kamishina Zenge wa Zenge nae alikuwa anamalizia kuwasiliana na Komando na Jasusi Honda Makubi aliekuwa Israel kwa mafunzo maalumu baada ya kuwa ametoka kuuguza majeraha yake alioyapata huko Somalia katika mkasa wa Urithi wa Gaidi.
Ujio wake ilikuwa ni kawaida kwake yeye na Kamishina ila ilikuwa ni taharuki kwa majahili na wazandiki waliokuwa wanacheza na kitengo cha kazi maalumu “Special operations”.