Operation Tokemeza Ujangili:Wanasiasa wasiguswe kwa namna yoyote

sungura1980

JF-Expert Member
May 20, 2013
1,909
1,210
Wapendwa wana JF
Kamati iliyoundwa kuchunguza yaliyojiri katika operation tokemeza Ujangili katika ripoti iliyowasilishwa jana bungeni aya ya 3:1:1 romans iii,Majibu ya kamati kuhusu majibu ya wizara ya maliasili na utalii.Kwamba kamati ilibaini kuwa kuna kauli na maelekezo yalitolewa na baadhi ya mawaziri kwenda kwa waliokuwa wakiendesha operation hiyo kuwa wanasiasa wasiguswe kabisa katika operation hiyo je ililenga kuwalinda nani na je kumbe operation hiyo ilikuwa ni kwa baadhi ya watu tu?
Binafsi nimesikitishwa sana na kipengele hicho na mshangao kwa nini watu na wabunge hawakuliongelea agizo hilo!

Ninaomba wana JF hapa tuiangalie na kuitafakari kauli hiyo tu kwanza"Wanasiasa wasiguswe",ni nani huyo alitoa kauli hiyo,nani walilengwa kulindwa na kauli hiyo,je kama wanasiasa hawakuguswa(kwa kutekeleza maagizo ya wasiguswe), wakati ripoti imebainisha wazi kuwa hata baadhi ya wabunge wanatuhumiwa je nini kifanyike?
Nawasilisha!
 
Wapendwa wana JF
Kamati iliyoundwa kuchunguza yaliyojiri katika operation tokemeza Ujangili katika ripoti iliyowasilishwa jana bungeni aya ya 3:1:1 romans iii,Majibu ya kamati kuhusu majibu ya wizara ya maliasili na utalii.Kwamba kamati ilibaini kuwa kuna kauli na maelekezo yalitolewa na baadhi ya mawaziri kwenda kwa waliokuwa wakiendesha operation hiyo kuwa wanasiasa wasiguswe kabisa katika operation hiyo je ililenga kuwalinda nani na je kumbe operation hiyo ilikuwa ni kwa baadhi ya watu tu?
Binafsi nimesikitishwa sana na kipengele hicho na mshangao kwa nini watu na wabunge hawakuliongelea agizo hilo!

Ninaomba wana JF hapa tuiangalie na kuitafakari kauli hiyo tu kwanza"Wanasiasa wasiguswe",ni nani huyo alitoa kauli hiyo,nani walilengwa kulindwa na kauli hiyo,je kama wanasiasa hawakuguswa(kwa kutekeleza maagizo ya wasiguswe), wakati ripoti imebainisha wazi kuwa hata baadhi ya wabunge wanatuhumiwa je nini kifanyike?
Nawasilisha!

Maagizo yatakuwa yametoka CCM siunajua katibu mkuu wa ndo anahusika sana na wasomali majangili wa tembo wetu!.Angalia jinsi kagasheki alivyopambana,wameshindwa kumsaidia wakapenyeza rushwa kwa watendaji wa opereshini tokomeza wakawa wanatesa watu na kupiga picha kama ushahidi,mi ningemshauri Rais amrudishe Kagasheki na Mathayo hawa wengine waende.Kagasheki majangili hawataki hata kumsikia alikuwa ana waweka roho juu sana hivi sasa wanafanya sherehe
 
Ukiwa mkweli kama Kagasheki, mwenye nia ya dhati ya kufanya kazi ya Wananchi kama yeye, wanafiki na mafisadi ndani ya system hawatakukubali! Nangojea niona nani atateuliwa kuongaza ile wizara! Akikubali kula pamoja na ajangili itaonekana ni shwari kumbe ndo majanga! Ningekuwa raisi singekubali kujiuzulu kwa Kagasheki bali ningemsaidia kumwongezea uwezo kwani pamoja na Kampeni kuwa na dosari hazikusababishwa na yeye!
 
Maagizo yatakuwa yametoka CCM siunajua katibu mkuu wa ndo anahusika sana na wasomali majangili wa tembo wetu!.Angalia jinsi kagasheki alivyopambana,wameshindwa kumsaidia wakapenyeza rushwa kwa watendaji wa opereshini tokomeza wakawa wanatesa watu na kupiga picha kama ushahidi,mi ningemshauri Rais amrudishe Kagasheki na Mathayo hawa wengine waende.Kagasheki majangili hawataki hata kumsikia alikuwa ana waweka roho juu sana hivi sasa wanafanya sherehe

Ni wazi kuwa hayo maagizo yalitoka kwa wana CCM maana ingekuwa sio kamati isingesita kuwataja majina!Sasa swali ni kwamba ni akina nani hao waliokusudiwa kulindwa wasiguswe?
 
Ni wazi kuwa hayo
maagizo yalitoka kwa wana CCM maana ingekuwa sio kamati isingesita
kuwataja majina!Sasa swali ni kwamba ni akina nani hao waliokusudiwa
kulindwa wasiguswe?

Swali zuri. Tuanzie hapa.
Ni kiongozi gani mwenye mamlaka ya kumuamrisha waziri kuwa viongozi wa siasa wasiguswe, kiasi cha yeye kutoa maagizo kwa watekelezaji wa Operation Tokomeza (OT)?

Je askari (washiriki ktk OT) waliokamatwa wakisindikiza magari yenye nyara za serikali, tena kwa kutumia magari ya Serikali walisema ni viongozi gani waliowatuma?
 
Swali zuri. Tuanzie hapa.
Ni kiongozi gani mwenye mamlaka ya kumuamrisha waziri kuwa viongozi wa siasa wasiguswe, kiasi cha yeye kutoa maagizo kwa watekelezaji wa Operation Tokomeza (OT)?

Je askari (washiriki ktk OT) waliokamatwa wakisindikiza magari yenye nyara za serikali, tena kwa kutumia magari ya Serikali walisema ni viongozi gani waliowatuma?

Hilo nalo neno!Kwa mujibu wa ripoti hiyo ni kwamba kuna mawaziri walitoa maagizo kuwa wanasiasa wasiguswe!Je ni mawaziri gani hao?Wana nguvu gani hadi kutoa maagizo hayo kukwamisha operation ambayo mheshimiwa raisi amebariki?Je wanamzidi mheshimiwa raisi nguvu hadi kuweza kutoa maagizo ya kukwamisha kazi yake?
 
Hilo nalo neno!Kwa mujibu wa ripoti hiyo ni kwamba kuna mawaziri walitoa maagizo kuwa wanasiasa wasiguswe!Je ni mawaziri gani hao?Wana nguvu gani hadi kutoa maagizo hayo kukwamisha operation ambayo mheshimiwa raisi amebariki?Je wanamzidi mheshimiwa raisi nguvu hadi kuweza kutoa maagizo ya kukwamisha kazi yake?

Mmh hapo kazi ipo,nafikiri aliyetoa maagizo alikuewa anamlenga katibu wa ccm Kinana ila asingeweza kumtaja mojakwamoja.Siunakumbuka ile kashfa ya kampuni yake kuwa wakala wa meli yenye conteiner za meno ya tembo?Sasa ili kumlinda wakawapa hadidu rejea kwamba mwisho hapa!,si unaona jinsi tz tulivyo?kila kitu siasa kwanza na ndio maana wanasiasa wanalipwa vzr kuliko wataalam mf madaktari
 
Back
Top Bottom