zitto junior
JF-Expert Member
- Oct 7, 2013
- 19,036
- 28,679
- Thread starter
- #321
Mkuu hoja yako naielewa ingawa inajipinga kabisa.Narudia tena huwezi elewa kwanini Savimbi alikufa kifo cha aibu... Na jeshi lake lenye nguvu...
Una andika usicho elewa... Au una elewa lakini tayari una starring wako hutaki kusikia habari za kushindwa kwake...
Hakuna kikundi cha waasi kinacho weza shindana na dola, hakuna... Narudia tena hakuna... Na ingekuwa ina wezekana basi kila nchi kungekuwa na makundi ya waasi...
Waasi unao waona au kuwasikia ni propaganda... Na ndio maana mwisho wao Mara nyingi sio mzuri hata kama watashinda mapigano wao wanabaki ni maroboti...
Ongeza madesa zaidi hachana na hivyo viPDF viwili unavyo viita marejeo au sources... Soma source nyingi zaidi zenye kusifu na kuponda...
Nimeshasema kama Huyo Savimbi ni roboti wa mataifa mengine basi leo ufahamu hata Dos Santos naye alikua kibaraka wa Urusi kwahyo hapo wote ni walewale unless useme na Serikali nazo ni propaganda tu maana zinatumika pia.
2. By the time savimbi anakufa jeshi lake lilishapungua nguvu sana na wanaomsaidia hawakuona ana input tena. Lakini vilevile kuna serikali halali kabisa pia huwa zinatumika na pamoja kuwa na majeshi makubwa ila huwa marais wanauawa na mifano iko mingi sasa sijui kwanini unataka ionekane ni rebep groups pekee ndio zinapokea orders za mabeberu.
3. Vikundi vya waasi vipo vinavyoishinda dola kabisa. Ukiona dola imezidiwa ujue support ya beberu wake ni ndogo. Hata hapo DRC as much as rebels walipewa support na mabeberu ila pia serikali nayo ilipata msaada huo huo kww mataifa makubwa kwahyo labda useme BEBERU mwenye nguvu ndio hushinda bila kujalisha ni serikali au muasi.
Source zipo nyingi hizo nmeweka sababu ni fupi ila ukisoma kitabu cha Gerard prunier kuhusu Congo war au Conflagration of great lakes region imeelezea kwa undani zaidi suala hili ila watanzania hawawezi soma page 300+ ya vita moja!!
NB: Main point hapa ni kuwa wote wanatumika tu so uache bias dhidi ya waasi kuwa ni maroboti pekee