Luteni
JF-Expert Member
- Jan 9, 2010
- 2,274
- 301
Nguvu zile zile na ari ile ile kwa kasi ile ile ya Operation Sangara iliyotumika kuhamasisha wananchi kujua haki na wajibu wao, sambamba na kufanya mabadiliko ya mfumo wa utawala, sasa itumike kuhamasisha wananchi hao hao umuhimu wa kuwa na katiba mpya kupitia slogan ya 'Operation Katiba'.
Suala la katiba lichukuliwe kwa mapana yake lisije likaonekana ni suala la viongozi au watu wachache tukarudia makosa ya zamani ya kutoshirikisha wananchi na kujikuta tunaanza kutia viraka baada ya kipindi kifupi, tuwapelekee wenye nyumba ambao ni wananchi.
Naamini kabisa kwa kutumia slogan hii mpya baada ya miezi sita watu watakuwa wamehamasika na kuwa na uelewa mpana wa nini umuhimu wa kuwa na katiba mpya, mbona Operation Sangara ilifanikiwa.
Napendekeza jina hilo kwa vile limebeba ujumbe ulio wazi kabisa unaotakiwa kufikishwa kwa walengwa kwa vile neno lake ni simple and easy to remember, 'OPERATION KATIBA'
Naomba kuwasilisha.
Suala la katiba lichukuliwe kwa mapana yake lisije likaonekana ni suala la viongozi au watu wachache tukarudia makosa ya zamani ya kutoshirikisha wananchi na kujikuta tunaanza kutia viraka baada ya kipindi kifupi, tuwapelekee wenye nyumba ambao ni wananchi.
Naamini kabisa kwa kutumia slogan hii mpya baada ya miezi sita watu watakuwa wamehamasika na kuwa na uelewa mpana wa nini umuhimu wa kuwa na katiba mpya, mbona Operation Sangara ilifanikiwa.
Napendekeza jina hilo kwa vile limebeba ujumbe ulio wazi kabisa unaotakiwa kufikishwa kwa walengwa kwa vile neno lake ni simple and easy to remember, 'OPERATION KATIBA'
Naomba kuwasilisha.