Open Source Intelligence: Mkandarasi wa "Stigla Goji" ana walakini?

Mzalendo_Mwandamizi

JF-Expert Member
Dec 12, 2007
1,117
4,764
Kinyume na imani iliyozoeleka kuwa intelijensia ni suala linalofanywa na mashushushu pekee, au watu wa vyombo vya dola, baadhi ya nyanja katika taaluma hiyo zinaweza pia kufanywa na wasiojihusisha na taaluma hiyo per se. Including you, or anybody else, kwa mfano, kwa kutumia "open source intelligence" kwa kifupi OSINT.

So, tuna kampuni moja kutoka Misri ambayo imekabidhiwa jukumu la kujenga "Stigla Goji" mradi unaotajwa kuwa wa kihistoria na ambao Jiwe anaamini kuwa utakuwa moja ya legacies zake. Lakini je kampuni hiyo ni safi?

Fanya urafiki na Google, kisha weka jina la kampuni hiyo plus neno "corruption." Let me not pre-empt matokeo ya "open source intelligence" yako, ila tu naomba kuamsha tafakuri yako kuhusu findings za uchunguzi huo mdogo, especially iwapo suala hilo zima halitokuwa na athari kwa mradi huo wa kihistoria.
 
Wadanganyika ni watu wa kuhurumiwa sana,kuna mtu kaamua kuwaswaga badala ya kuowaongoza, na wao wamekubali na kibaya zaidi, anakowapitisha wao hata hawatazami.

Bwana huyo kwa sasa kaamua kuelekeza "noti" nyingi kwenye sekta moja sekta ambayo ina-facilitate tu shughuli za maendeleo ili kukuza uchumi huku sekta ambazo zinatakiwa zi-take advantage ya sekta hiyo moja inayopewa kipaumbele kukuza uchumi, zikiwa zinaporomoka kwa kasi na bado wadanganyika waanaamini mtu atawafikisha mbali.So sad!

Mwisho wa siku, ataawachia structures zenye kupendeza na kuvutia machoni, lakini wao wakiwa hoi bin taabani kimaisha/kiuchumi huku wasio na ajira wakiongezeka, na mambo mengine mengi ama yakiwa yamedorora au kukwama kabisa.

Tutasonga mbele kwa fikra na vipaumbele vya mtu mmoja na hii iko dunia nzima!!!!!

Zidumu fikra za mwenyekiti!!
 
Back
Top Bottom