Onyo la kutokunywa pombe latolewa, watu kulikaribisha kwa "party"

Richard

JF-Expert Member
Oct 23, 2006
14,939
20,399


Watu wenye tabia ya kubeba makopo ya pombe ndani ya garimoshi za chini ya ardhi katika jiji la London, watasheherekea onyo lililotolewa na Meya wa London la kukataza tabia hiyo.

Wameamua kunywa usiku wa Jumamosi kukaribisha onyo hilo ambalo linaanza kutumika Jumapili,tarehe 7.

Watu zaidi ya 4,000 wamejiorodhesha katika orodha hio ya walevi ambao watakwenda na pombe zao katika treni inayopita njia iitwayo "circle line" ambayo kwa kawaida ni ya mzunguko katikati ya jiji la London au "Central London".

Meya mpya wa jiji la London bwana Boris Johnson ambe ni wa chama cha conservative ametimiza ahadi ya kutoa onyo hilo ili kuzuia tabia ya ajabu ya baadhi ya abiria kubeba pombe zao za makopo na kuwa wanakunywa kidogokodogo huku wakitoa maneno ya kejeli na matusi kwa abiria wengine.

Hii sijawahi kuona kabisa na kwa maana hio watu hawatatumia circle line siku ya Jumamosi jioni.

Je kuna yeyote ambae amepata kuona mambo haya ya ajabu mahali alipo ughaibuni?

Source: Evening Standard
 
...mie ninapoishi usafiri wa subway na mabasi unaitwa "T"...very well established and one of the oldest in USA if not the whole world!! ni marufuku kunywa pombe ktk sehemu yeyote public in the US, let alone ktk treni!! lakini kuna walevi mbwa ambao wanapiga tungi kama kawa na kutukana watu, pia wapo wale wanaolewa mouthwash kwikwikwikwikwi ni vituko sana kwenye subway...lakini "wastoni" wakimnyaka ni faini ya $$ 100 au lupango kwa mwezi mzima!!
...jamaa wa "T" wana polisi wao, ila kusema kweli hizi arrests zipo kidogo sana....fegi, kuna watu wanavuta illegally kwenye vituo na ndani ya treni. Sheria zipo lakini zinavunjwa, usije kushangaa hapo kwenu kuendelea kuwepo vichwa ngumu ambao wataendeleza libeneke la tabia yao chafu ya kunywa "kinywaji kikongwe..second to water" kwenye mabehewa kama kawa......ndio dunia hiyo!! LOL.

Bwahahahaaaa....unajua sana mambo ya pombe wewe.....kwikwikwiiiiii
 
...

Je kuna yeyote ambae amepata kuona mambo haya ya ajabu mahali alipo ughaibuni?

Boris Johnson kaja na moto, lakini sidhani kama 'atayetaka' kuvunja sheria atashindwa!

...acha ughaibuni, bongo bwana... nilikuwanashangaa shangaa 'vijana' wengi wao wamekamata chupa za maji ya 'kilimanjaro' zile za 300ml, nikawa najisemea moyoni mnh, hawa jamaa wamegundua nini kunywa maji kwa wingi hivi, Kumbeee...!

si wamemimina Konyagi bwana ndani ya hizo chupa!

damn!...

sitashangaa 'wajanja' wachache wakaamua 'kumimina' hayo maji yao ya shaba kwenye chupa za juice, na bia inavyofanana na apple juice ndio kabisaa...


haitawezekana?
 
Back
Top Bottom