Onyo kwa CHADEMA na angalizo kwa Dr. Slaa - We are watching you!

Dr Matola PhD

JF-Expert Member
Oct 18, 2010
55,784
90,552
Kuna msemo wa kiswahili usemwao lisemwalo lipo na kama halipo laja ili sipendi lije kwa sababu halina tija kwa wapenda mabadiliko.

Ni wazi CCM sasa inatumia kila aina ya Propaganda ili kuhakikisha Taswira ya CHADEMA inaharibika katika umma au kuwagombanisha wenyewe kwa wenyewe kama inavyofanyika kwa Zitto Kabwe.

Kuna tetesi sasa hivi zimeenea kwamba Josephine anapiga jalamba kugombea Ubunge wa Kawe, kama tetesi hizi ni za kweli na zisipokanushawa basi moja kwa moja Dr Slaa hana sifa za kugombea Urais kwa kushindwa kuisimamia nyumba yake na kushindwa kumdhibiti Josephine katika harakati hizi haramu za kisiasa.

Ila nisiseme mengi kwa sababu hizi ni tetesi nawakaribisha wote waliozipata tetesi hizi ukweli wake ni upi? na kama si kweli ni kwa Josephine asiitishe Press Conference kukanusha hili officially? ni kichaa peke yake ndani ya CHADEMA anayeweza kugombea na Halima Mdee kura za maoni 2015 ili kufanya Halima Mdee asigombee tena.

Nakala kwa Molemo
 
Kuna ukweli wowote kuwa Josephine anataka kugombea Kawe? Angalieni msije mkawa mnaicheza ngoma inayopigwa na Magamba... Hizo taarifa za huyo Josephine kugombea zimetoka wapi?
Mkuu Nicas heading ya thread ni tetesi, na nimeziona zinasambaa kwa nguvu kwenye social media, ndio maana nikasema ni vizuri hizi habari kama si za kweli zikanushwe mara moja. sipendi ninapoona jina la Josephine likihusishwa sana na mambo ya Chadema hii inaharibu Image ya Chadema na tunavyomthamini Dr Slaa.
 
MKUU kwa nini unapenda JF wakusaidie hizi tetesi? Kwa nini usimuulize JOSEPHINE mwenyewe? Naona umetumwwa!!
 
Hivi Chadema hakuna anaefaa kuwa Katibu Mkuu zaidi ya Slaa? mbona kuna vijana hodari na wachapakazi wenye maadili kama Zito Kabwe?
Chadema kinahusishwa na udini na ukanda! Slaa ni Padre na mlei wa Kanisa aliesaini mkataba wa KIFISADI wa MOU 1992 akiwakilisha Kanisa na Edwad Lowasa kama Waziri ktk Serikali ya awamu ya Pili!

kama mnataka kufuta hisia za kidini Chadema hamna budi kumsimamisha Mgombea urais mwingine mwenye sifa za uongozi na asie na kashfa za kifisadi, kimaadili au za kidini!
Slaa ni msalaba wenu na mkiendelea kumlea na kumuenzi, basi mjue Chadema itafia mikononi mwake!

Asiejua kifo aangalie kaburi! NCCR iko wapi?
 
Nakumbuka hizi habari zililetwa na Ritz alitoa katika gazeti moja la magamba,bt kama ni uongo kwa nini Josephine hajakanusha hadi leo?Hima mama Junior hebu jibu tuhuma hii upesi maana nawe ni mwanachama active humu!
 
Mbona hata Dr.Lilian Mbowe naye naskia atagombea Ubungo kwa mnyika 2015!? Na hizi habar nilioma kwenye gazeti 1 la sauti huru, sasa ni vyema makamanda wakaweka clear hizi habari ili kuondoa propaganda za ajabu na kuvuruga taswira ya chama.
 
Kama anataka kugombea shida nini? Kama anaweza kwa nini asijitupe na asubiri vya mezani kama wama. Mwache Agombee sera zake ndizo zitamlinganisha na wengine, Tuache woga na tuache tabia kugombia bila kupingwa
 
Kama ni tetesi kwa nn uanzishe uzi bila kufanya utafiti japo kuuliza mhusika?kama si majungu yenu
 
Hivi Chadema hakuna anaefaa kuwa Katibu Mkuu zaidi ya Slaa? mbona kuna vijana hodari na wachapakazi wenye maadili kama Zito Kabwe?
Chadema kinahusishwa na udini na ukanda! Slaa ni Padre na mlei wa Kanisa aliesaini mkataba wa KIFISADI wa MOU 1992 akiwakilisha Kanisa na Edwad Lowasa kama Waziri ktk Serikali ya awamu ya Pili!

kama mnataka kufuta hisia za kidini Chadema hamna budi kumsimamisha Mgombea urais mwingine mwenye sifa za uongozi na asie na kashfa za kifisadi, kimaadili au za kidini!
Slaa ni msalaba wenu na mkiendelea kumlea na kumuenzi, basi mjue Chadema itafia mikononi mwake!

Asiejua kifo aangalie kaburi! NCCR iko wapi?

mkuu wewe si mwanaCUF lakin?
 
Na katika hili tupunguze mihemko kidogo ndugu matola

tujaalie ya kwamba tetesi hzo ni kweli kwani kuna ubaya gani kwa josephine kuonesha nia hiyo??

Kwa sababu ana mahusiano ya kimapenzi na wilbroad peter slaa au kwa sababu zipi??

Me naamin dada josephine ile ni haki yake kikatiba kugombea ubunge na kuonesha nia hiyo kupitia chama chake cha cdm,kwani kavunja katiba ya cdm??

Na kwa kuonesha kwake nia hiyo josephine kuna m-disco vipi slaa na uhalali wake wa kuwa mgombea pendwa wa chadema??
 
Hivi Chadema hakuna anaefaa kuwa Katibu Mkuu zaidi ya Slaa? mbona kuna vijana hodari na wachapakazi wenye maadili kama Zito Kabwe?
Chadema kinahusishwa na udini na ukanda! Slaa ni Padre na mlei wa Kanisa aliesaini mkataba wa KIFISADI wa MOU 1992 akiwakilisha Kanisa na Edwad Lowasa kama Waziri ktk Serikali ya awamu ya Pili!

kama mnataka kufuta hisia za kidini Chadema hamna budi kumsimamisha Mgombea urais mwingine mwenye sifa za uongozi na asie na kashfa za kifisadi, kimaadili au za kidini!
Slaa ni msalaba wenu na mkiendelea kumlea na kumuenzi, basi mjue Chadema itafia mikononi mwake!

Asiejua kifo aangalie kaburi! NCCR iko wapi?
The way unaongelea CDM ni kama wewe sio mwanachama wao.
Kama kweli wewe si mwanachama kwanini unaingilia mambo yao?
Acha chama kiamue nani awasimamie. Kila mtu ana historia, kila mtu ana dini.
Kama chama na wanachama wameridhika na Dr. Slaa, basi watampigia kura
Haijalishi kama alikua padre, coz hatowakilisha kanisa katoliki, atawakilisha CDM

On the other hand, kusema Dr. Slaa hafai ila Zitto Kabwe ndie anafaa ni uchochezi
Zitto mwenyewe kasema atatii maamuzi ya chama, na amesema wengi wanafaa
halafu wewe unakuja kusema hivo na unajua that is a hot question in CDM
Nahisi mchango wako ni wa kuchochea zaidi, sio wa kuleta mwangaza.
That said, naheshim hatua yako ya ku-express mtazamo wako hata kama sikubaliani nayo.

BTT: I think itakua vema Josephine akanushe, au aeleze kwanini anagombea
after all, she is a Tanzanian citizen, CDM member, ana haki ya kugombea
hasa kama anahisi ana uwezo wa kuwakilisha Kawe kuliko mbunge wa leo.
 
Kwanini inachukua mda Josephina kukanusha habari hizi???????
 
CCM waalitumia mbinu ya kuwabambikizia viongozi wa CHADEMA kesi katika maeneo mbalimbali, wamegundua hiyo haijawezekana, maana CHADEMA bado imeendelea kuwabana, CCM wamekuja na mbinu mpya ya kuanzisha propaganda za kitoto ili viongozi wawe busy kujibu. CCM watakuwa wamefanikiwa sana kama propaganda wanazoanzisha CHADEMA Wanahangaika kujibu, kwa sababu lengo lao ni kuwasumbua ili viongozi wa CHADEMA wasijikite katika kuelezea ugumu wa maisha ya watanzania, unaopaswa kujibiwa na CCM kwa wananchi. VIONGOZI WA CHADEMA, Wananchi wanajua kipi cha kweli na kipi cha Uongo. Mada hii ni ya uwongo na haiwezekani kwa akili ya kawaida kitu kama hicho kutokea.
 
Kamanda Matola na wewe umeingia kwenye huu mchezo wa upuuzi wa kina Mchambuzi?
Please Matola usiwaamini hao ni wanafiki, hivi leo tena ukisikia Zitto anataka kugombea Arusha jimbo la Lema utaamini?na Msigwa wa Iringa anampisha mwakalebela ili aje kugombea Ubungo kwa Mnyika,

Mgamba wameona issue ni kututibua ovyo ovyo tu, kutuchanganya na mkuu kama wewe kuuanza kurudi nyuma,(nakutambua kama mteteze mkubwa wa CDM hapa JF)
anyway Kamanda Josephine, atajitokeza kwa njia hii ya social media, asifanye kuwa official sana!
 
Last edited by a moderator:
Kwanini inachukua mda Josephina kukanusha habari hizi???????
Inategemea anakanusha nini? Nasikitika wakuu wangu mmeingia kwenye mtego wa kitooto, hivi chadema ikae kila siku inakanusha tuu kutokana na habari za JF? kwa nini usifuatilie? na kwani Muda wa kutafuta wagombea umefika?
 
Mie binafsi ni mkazi wa Kawe hakuna ubaya wowote Josephine, kugombea ubunge Kawe kama mwanachama wa Chadema ni haki yake ya kikatiba.

Msitake kubaka demokrasia Halima Mdee hana hati miliki ya jimbo la Kawe.
 
Last edited by a moderator:
Wacha Josephine agombee, mimi naona huyu bi Halima jimbo limeshamshinda kabisa.

Yupo bize kweli na kesi ya Lulu kuliko kufuatilia mambo ya jimboni kwake kula kukicha malalamiko.
 
15 Reactions
Reply
Back
Top Bottom