Online Meeting with CHADEMA - Kuimarisha Upinzani na Kuleta Maendeleo - No 1

Allien, hoja zako ni nzuri sana na CHADEMA wanatakiwa wazifanyie kazi. Kwa maoni yangu si vizuri mtu kukimbilia kwenye chama kutafuta uongozi. Inakuwa vizuri kama unajiunga na chama kutoa mchango wako katika jambo ambalo chama hicho kinalisimiamia na endapo wewe unaliamini (towards attaining a common goal). Lakini mtu anayefika mahali na siku hiyo anataka ukubwa ni hatari. Ni bahati mbaya kwamba watu wengi tunapenda sana kutumikiwa kuliko kutumikia. Hii ni hali ya hatari sana na nadhani ndio chanzo cha wakulu wetu kudai kwa nguvu kuitwa waheshimiwa!! Ni upuuzi mtupu!

Ila kama mtu anataka kuongoza basi awashawishi wanachama kwanza kwa kuwatumikia ili wampime na si kuanza kunadi rekodi zake za huko alikotoka katika mtindo wa hadithi na ngonjera za paukwa pakawa.

Pia nakuunga mkono kwamba CHADEMA watafute jambo ambalo litawatofautisha na vyama vingine hapa TZ ikiwemo CCM. Na jambo rahisi la kutumia ila gumu kulitekeleza kwa hali TZ ya sasa ni UADILIFU. Kama wakiweza hilo na kuweka mikakati mizuri ya kuonyesha kuwa wana kitu kipya cha kuwapa Watz, sioni sababu kwa nini wananchi wasiwaami na kuwaunga mkono, na hatimaye kuwapa jukumu la kuongoza nchi yetu. Vinginevyo wataishia kutamani tu kuwakomboa WaTz lakini hawataweza kwa kuwa hawana mbinu za kufanya hivyo.

Mkuu, sasa tuko pamoja 100%! Umeongea kama Mwanamapinduzi na si kama Mwanasiasa.

Big up!
 
Mtanzania, I know hiyo statement ni vague kweli; bahati mbaya statements nyingi za kisiasa huwa ni vague :)

Nitatoa mchango wangu kwenye chadema, lakini sio kwa kugombea hivyo vyeo vizitovizito ambavyo vinanizidi uzito. Ahsante lakini kwa kunishawishi...

Aliens et al-hii thread ni muhimu sana, na mimi binafsi naisoma mara kadhaa kwa siku. Mtu kukupa ushauri ni kipimo muhimu sana cha kutambua kwamba anakupenda. Wote wanaotoa ushauri hapa kwa chadema mimi nachukulia kwamba wanaipenda na wanaitakia mema chadema.

Nakubaliana na hoja yenu kwamba kuna haja ya chadema kujipambanua kisera, kimkakati, etc. Haya mambo yameanza kufanyiwa kazi, na hiyo ya sangara operation ni moja ya namna ya kujipambanua kimkakati. Nakiri kwamba kwa upande wa kujipambanua kisera tu-bado. Bado tuna bidii ya kukosoa zaidi na kuibua kashfa kuliko kutoa alternative policies and strategies juu ya namna ya kuitoa nchi hapa tulipo. This is a challenge ambayo lazima tuifanyie kazi, maana wapiga kura hawatatuchagua tushike serikali kwa sababu tu mabingwa wa kuibua kashfa bali kwa kuwa na alternative sera, mikakati na mbinu za kuwatatulia matatizo yao ya msingi. Hili lazima lifanyiwe kazi sooner than later.

Kitila, sasa tuko pamoja Mkuu kama uliyoyaandika ndiyo what you mean.

Changamoto tunazozitoa hapa haina maana kuwa hatukubali ani na kazi nzuri ambayo imeendelea kufanywa na CHADEMA katika baadhi ya maendeo, wala haina maana kuwa tunatafuta vyeo huko, tunachotaka ni kuona CHADEMA inakubalika kuwa Chama Makini na Mbadala cha CCM.

Hatuko ndani ya CHADEMA, lakini moja kato ya BITTER PILL ambayo CHADEMA mnaweza kuitumia ni kumwomba Mh. Mbowe kupisha uongozi wa juu kwa mtu ambaye ataunganisha chama na muadilifu. Kuendelea kijidanganya kisiasa kubaki mlipo badala ya kujisafisha ni kuwagawa wapenzi wa CHADEMA.

MBOWE akiamua kuachia ngazi, atakuwa amejijengea sifa kubwa sana kama wazee wake waliotangulia kuliko akisubiri malumbano ndani ya chama na hatimaye kukigawa.

Nitakutafuta Mkuu!
 
Hongera Ongara kwa kufafanua hoja kwa ukweli na uhakika!

Kama kweli tunataka siasa safi tujadilini kwa hoja za kimantiki na tuwe na correct data maana JF inasomwa na watu wengi na pia inatumika kama reference jamani.

I support you.
 
Now you are talking Kitila!

Mkiendelea na kuwekeza nguvu nyingi kwenye kuibua kashfa za watawala, mkishika dola mtaibua za nani? Na je hiyo ni kazi muhimu (central role) ya chama cha siasa kinachotakiwa kutoa sera mbadala kwa wananchi? Hata hivyo nawapongeza wote ambao mmeendelea kufanya kazi hasa katika mazingira yanayowakabili wapinzani hapa nchini. Inahitaji mtu kuwa na roho ya paka kubaki upinzani. Maadamu mumeweza hilo, basi songa mbele muibuie kitu cha maana kwa ajili ya kuwashawishi wapiga kura waipe CHADEMA nafasi ya kuongoza nchi. To me that's the main challenge now!

Dark City;

Umemaliza kila kitu, as if niliyokuwanayo na wewe ulikuwanayo.

We hope Bw. Kitila sasa tupo pamoja.

Tunaomba yote yafanyiwe kazi kwa vitendo isije ikawa siasa tena.

I have a lot of winning strategies, I am digesting what can be achievable . . . . Can't say anything for now.

I think we are done with CHADEMA now. We can now summon the next political party? Je, tuwaite CUF, TLP au NCCR or chama gani?
 
Dark City;

Umemaliza kila kitu, as if niliyokuwanayo na wewe ulikuwanayo.

We hope Bw. Kitila sasa tupo pamoja.

Tunaomba yote yafanyiwe kazi kwa vitendo isije ikawa siasa tena.

I have a lot of winning strategies, I am digesting what can be achievable . . . . Can't say anything for now.

I think we are done with CHADEMA now. We can now summon the next political party? Je, tuwaite CUF, TLP au NCCR or chama gani?


Kuna mtu kaniambia Lipumba huingia jamvini (sijui kwa jina gani), hivyo labda tuwaite CUF kwanza.
 
Kuna mtu kaniambia Lipumba huingia jamvini (sijui kwa jina gani), hivyo labda tuwaite CUF kwanza.

Peasant tuko pamoja . . . .

So, we close this thread now and call CUF. Na tunataka Mh. Lipumba atujibu kwa nini hawataki Kuungana. Siku CHADEMA na CUF Wanaungana, CCM hawana lao. Maana hakuna atakayezungumzia UDINI wala Ukabila katika vyama hivi. Pia CUF wana nguvu Visiwani CHADEMA bara, so itakuwa safi.

Here we go . . . now:

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...isha-upinzani-na-kuleta-maendeleo-no-2-a.html
 
Allien,
Unashauri Kitila na wenzake wamwombe Mbowe aachie uongozi wa juu kwa mtu atakayeunganisha chama na muadilifu, unaweza kutanabaisha ni vipi Mbowe si muadilifu? Kuhusu kuunganisha chama, nakushauri urudi nyuma kidogo wakati Mbowe anachukua uongozi, jaribu kulinganisha na hali ya chama sasa hivi, ukishindwa kutambua uwezo wa Mbowe katika hilo kutakiwa na matatizo mengine.
Mbowe anaweza kuwa na matatizo kama binadamu yeyote, lakini hili la kushindwa kuunganisha chama haliwezi kuwa moja yamatatizo yake. CCM wanalifahamu hili vizuri sana na linawakosesha usingizi.
 
Nchi yetu ikipata vichwa kumi tu kama huyu Allien basi tunaweza kuelekea kwenye neema ya asali na maziwa
 
Allien,
Unashauri Kitila na wenzake wamwombe Mbowe aachie uongozi wa juu kwa mtu atakayeunganisha chama na muadilifu, unaweza kutanabaisha ni vipi Mbowe si muadilifu? Kuhusu kuunganisha chama, nakushauri urudi nyuma kidogo wakati Mbowe anachukua uongozi, jaribu kulinganisha na hali ya chama sasa hivi, ukishindwa kutambua uwezo wa Mbowe katika hilo kutakiwa na matatizo mengine.

Mbowe anaweza kuwa na matatizo kama binadamu yeyote, lakini hili la kushindwa kuunganisha chama haliwezi kuwa moja yamatatizo yake. CCM wanalifahamu hili vizuri sana na linawakosesha usingizi.

Mkuu Gagnija;

Sijasema Mbowe si Muadilifu kwa kuwa mpaka sasa hakuna prooof yoyote. Lakini Mbowe ameshakuwa questined sana juu ya Uadilifu wake hasa yanapokuja masuala ya Matumizi ya Pesa, Ukabila, Upendeleo wa Vyeo n.k. Najua kisisa ni rahisi kujibu hoja hizi kwa kuwa tutaambiwa kuwa taratibu zilifuatwa.

Hakuna haja pia ya kurejea yale Marehemu Chacha Wangwe aliyokuwa anapigania ndani ya CHADEMA.

Ushauri tunaoutoa kwa CHADEMA ni kuwa lazima mkubalike kwa Wananchi kuwa nyie ni WAADILIFU, na kama Wananchi wengi wa Tanzania ambao wao ndiyo wapiga kura wataanza kuwa na mashaka na maswali kwa baadhi ya viongozi, then hilo ni doa tosha la kuonekana kuwa hamko tofauti na CCM.

Tungependa kuona moja ya mitaji mikubwa ya CHADEMA inakuwa UADILIFU, na kwa hili lazima mkubali kunywa MWAROBAINI.

Vinginevyo mimi sina ugomvi na Mbowe wala si Mwanasiasa. Ni watu tunaoitakia mema nchi hii.
 
Ni bahati mbaya kwamba watu wengi tunapenda sana kutumikiwa kuliko kutumikia. Hii ni hali ya hatari sana na nadhani ndio chanzo cha wakulu wetu kudai kwa nguvu kuitwa waheshimiwa!! Ni upuuzi mtupu!

Dark,
Mie napendekeza kwanza CHADEMA waanze na neno Mheshimiwa. Waanza kukataa kuitwa waheshimiwa na warudishe neno NDUGU. Hili lilikuwa na maana kubwa sana kwa Watanzania miaka hiyooo.

Allien :- Hadi sasa tuko pamoja. Ila ningependa kupishana kidogo kwenye swala la MBOWE. Kubadilisha hili jambo katika kipindi hiki sidhani kama itakuwa ni vizuri na rahisi. Kwangu mie ningependa kuona Mbowe akichagua kati ya haya mawili. Wakati akichagua haya mawili, itakuwa tayari ni HOMEWORK kwake kwamba inabidi AJIFANYIE yeye mwenyewe kama MBOWE mabadiliko. Kama akilifanya hili basi itakuwa ni hatua kubwa sana mbele.
1. Mbowe akubali kubaki MWENYEKITI wa Chadema (ila kwenye uchaguzi wa Rais amwachie mtu mwingine). Hii itakuwa inaleta sura kwamba Chadema hawajilundikii madaraka.
2. Mbowe aachie Umwenyekiti na abaki kama Mgombea wa Urais. Hii itakuwa na hatari kubwa kwake kwamba kama akishindwa Urais, basi ajue anabaki ni kiongozi wa kawaida Chadema. Ila machoni mwa Watz italeta sura moja nzuri sana kuwa MABADILIKO YA KWELI YANALETWA NA CHADEMA.

Mwisho, narudia tena au kusisitiza neno MAADILI YA UONGOZI. Na hii lazime kiwepo kitengo ndani ya CHADEMA ambacho kitasimamia na kuhakikisha maadili yanafuatwa. Hiki kipengere cha mwisho kikifanyika, najiunga ila kugombea uongozi si leo wala kesho.
 
Ndugu wa JF,

Samahanini kwa kutokuwepo kwenye hii online meeting. Kwa miezi mingi nilikuwa sijaingia JF hususani kwenye PM na hata kwenye visitors page ambapo Allien aliniewekea mwaliko.

Naomba wakati mwingine kukiwa na kikao kama hiki nijulishwe kupitia mnyika@yahoo.com au mnyika@chadema.net au nitumiwe ujumbe kwenye simu 0754694553 niweze kupata mwito kwa wakati.

Mubarikiwe

JJ
 
Hapa patazuka kama ile maoni iko kusema Kikwete anapendwa , sijaona msukumo wowote ambao unaonyeshwa Chadema ina nguvu ,jamani tusemeni ukweli ,nguvu gani ambazo Chadema inazo,mimi sijaziona kabisa zaidi ya makelele ya kumfukuza mwizi halafu mwizi wenyewe msimpate ,hivi mtakuwa na nguvu hapo ? Na ikitokea habari mwizi amekamatwa nyie hamhusishwi kabisa ,wengine ndio wanajisifu na kujisifia kuwa ndio waliomkamata mwizi.Chadema mnaachwa mnahema na mawe mikononi ,mkiulizwa mnajibu tumemuona...!Mbona hamjamkamata..mnabaki sie ndo wa mwanzo kumwona.

Kwa wakati huu tulionao tusidanganyane ,mimi nasema Chama chochote ambacho kitafanikiwa kuibua hisia za wananchi na kuungana katika kudai Katiba mpya ya Nchi hii ,Chama hicho ndicho kitakachofanikiwa kuwa na nguvu ,Ingawa Chadema wanasema kuwa CHama chao ndio Chenye nguvu lakini ukweli uliopo ni kuwa bado CUF ni Chama nambari mbili Tanzania hilo halina ubishi ,na hili inatokana na kuwa wanachama wa CUF hawafi moyo ,hilo tu,na hiyo ni akiba ya Chama ,wanachama wa CUF wamekaa kama mazezeta ambao msimamo wao haubadiliki,imani waliyo nayo ni kuwa Chaguzi zilizopita wameibiwa kura ,matokeo yamebadilishwa ,hivyo hazina ile ipo pale pale naweza kusema wanachama wa CUF inakuwa kama wanakisasi wanaposhindwa na kila uchaguzi ukija kura yao haibadiliki inakuwepo pale pale ,hiyo ni silaha ambayo Chama cha CUF kinabaki na mhimili ,ona Tambwe ametoka chama lakini hakuna mwanachama ambae umemsikia akimsifu Tambwe kila unaemuuliza anamlaani Tambwe ,ikimaanisha wanachama wa CUF ni wanachama wenye msimamo mkubwa sana usio tetereka.

Mimi huwaga sipendi kubishana sana kuhusu vyama vya upinzani .kwa sababu najua hakuna mpinzani wa kweli wa serikali hii zaidi ya CUF na hakuna Chama kilichotulia kama CUF ,kusema kweli kimevuka mambo mengi ukilinganisha na vyama vingine ,kwa mfano katika uongozi wa Chadema naamini kabisa watu au wananchi wengi hawawatambui wengi zaidi ya Slaa na Mbowe na kidogo Zitto katika uongozi wa Chadema,tuzungumzeni ukweli na tuondoe jazba ,nazungumzia wananchi na sio waishio humu JF na hata humu ndio hivyo hivyo ,mnazungumzia mtandao hivi ni asilimia ngapi ya wapiga kura waTanzania wanauwezo wa kuwepo na kutumia mtandao ,zaidi mtajikuta mnazungushana nyie kwa nyie mtu mmoja ana majina zaidi ya matatu ,mtu huyo huyo mmoja anajivalisha vyama vyote.

Chadema ili kuuteka umma wa Tanzania ni lazima ienee mikoa yote kama ilivyo enea CUF ,maana CUF sio mchezo hakuna kona ya Tz utakayotembelea usiione bendera yake ikipepea ,ni true story wandugu ,ndani vijijini huko makolokoloni utaikuta bendera ya CUF,japo juu ya mti.

Chadema lazima wajitambulishe zaidi ya Slaa na Mbowe ,hivi chama hiki kina viongozi wawili tu ? Viongozi wengine watumike wasikike waonekane wakiandikwa kwenye magazeti ,wapewe hoja nzito kuhutubia wananchi ,hapo itaweza kupiga hatua lakini kujikusanya wapiga debe hapa JF na kurapu ,itakuwa kama mpo stendi ya basi mkisubiri abiria wakati wengine wanakusanya abiria kwa njia za mkato wala hawaikaribii stendi.
 
Dark,
Mie napendekeza kwanza CHADEMA waanze na neno Mheshimiwa. Waanza kukataa kuitwa waheshimiwa na warudishe neno NDUGU. Hili lilikuwa na maana kubwa sana kwa Watanzania miaka hiyooo.

Allien :- Hadi sasa tuko pamoja. Ila ningependa kupishana kidogo kwenye swala la MBOWE. Kubadilisha hili jambo katika kipindi hiki sidhani kama itakuwa ni vizuri na rahisi. Kwangu mie ningependa kuona Mbowe akichagua kati ya haya mawili. Wakati akichagua haya mawili, itakuwa tayari ni HOMEWORK kwake kwamba inabidi AJIFANYIE yeye mwenyewe kama MBOWE mabadiliko. Kama akilifanya hili basi itakuwa ni hatua kubwa sana mbele.
1. Mbowe akubali kubaki MWENYEKITI wa Chadema (ila kwenye uchaguzi wa Rais amwachie mtu mwingine). Hii itakuwa inaleta sura kwamba Chadema hawajilundikii madaraka.
2. Mbowe aachie Umwenyekiti na abaki kama Mgombea wa Urais. Hii itakuwa na hatari kubwa kwake kwamba kama akishindwa Urais, basi ajue anabaki ni kiongozi wa kawaida Chadema. Ila machoni mwa Watz italeta sura moja nzuri sana kuwa MABADILIKO YA KWELI YANALETWA NA CHADEMA.

Mwisho, narudia tena au kusisitiza neno MAADILI YA UONGOZI. Na hii lazime kiwepo kitengo ndani ya CHADEMA ambacho kitasimamia na kuhakikisha maadili yanafuatwa. Hiki kipengere cha mwisho kikifanyika, najiunga ila kugombea uongozi si leo wala kesho.

sidhani kama hili ni tatizo, cha maana kazi ya mwenyekiti iwe defined. mfano uk leader of the party ni gordon brown, lakini chairman ni mtu mwingine na anachaguliwa na leader of the party. ata marekani chairman wa democrats ni mtu mwingine. chairman wa vyama uk & us unakuta mara nyingi ni watu ambao hawana nia ya kuwa rais au waziri mkuu na ni wazee.

ushauri wangu: kutokana na siasa za TZ na uchu wa madaraka, CHADEMA wakifanya hivi watakua wamejitegea bomu ambalo litawalipukia wenyewe. kutokana na demokrasia ndogo ya TZ na upeo mdogo chairman anaweza akataka kushika hatamu na hii ikaleta mvutano kati ya chairman na kiongozi(mgombea urais), chama kikawa hakina discpline na matatizo yakatokea kibao.

kukiwa na mwenyekiti na mgombea urais kutapunguza media coverage ya mgombea urais, ni shida sana kupata media coverage TZ. bado democrasia yetu ni ndogo.

1. chama kiwe kina update website yake ili ku recruit young and new generation, kiwe kinajiunga na sehmu kama facebook na kwingineko.
2. chama kianzishe online donation system.
 
wakuu nadhani ingekuwa vema next time mjiandae vizuri na mpange muda na siku na tarehe kamili iliwatu wengi watambue meeting yenu, otherwise itaonekana kwa watu wachache waliobahatika kuwa online siku iyo. Hata ivo nimeushangaa mchango wa mmoja wetu akimuuliza dr. kitila mkumbo kama wako tayari kuwapokea makamanda kutoka jf na kuhaidi kuwapa vyeo!!!! hapa ndo mwanzo wa chama kufa ktk harakati za kusaka nafasi na kulipana fadhira, hapa hapana. Kama kweli si wpiganaji wa kweli tuwepo chamani na jf kwa ujumla ili cheo kije kutokanma na wawe kuhitajika zaidi chamani wala si kugawana vyeo, ingekuwa ivo vyeo visingetosha. Mi siendi cdm kutafuta cheo,hapana ni uzalendo wangu tu. Ni maoinii yangu.
 
Sana tu mkuu. Wana mapinduzi kutoka JF na kwingineko wanakaribishwa sana chadema. In fact wana mapinduzi wengi hapa nchini sasa hivi wamejiunga na chadema. Nadiriki kusema kuwa watu wengi wanaona haja ya mabadiliko katika nchi hii wanaiona chadema ndio agent pekee kwa sasa. Kuna wimbi kubwa la mabadiliko katika fikra za watu kwa sasa, na kama wana mapinduzi wa hapa JF watajiunga katika wimbi hili tunaweza kuleta ukombozi mapema kuliko tulivyotarajia.

So karibuni sana. Bahati nzuri kuna uchaguzi unaendelea ndani ya chama, hii ndio nafasi nzuri zaidi kushiriki kuleta mabadiliko kwa kujitokeza kugombea na/au kuchagua viongozi makini. Sasa hivi uchaguzi upo katika ngazi ya kata na by March/April utakuwa katika ngazi ya Taifa.

Dr. Mkumbo
Mimi nimejaribu sana ku-inquire kupitia website ya chadema (nimechukua address hapo) nikauliza maswali tele kuhusu namna ya kujiunga na CDK kwa sisi tulio nje. Lkn mara zote sijajibiwa. Sijui hapa vp.
 
Mkuu;

Kuna mambo kadhaa wa kadhaa ya kimsingi yanayohitaji mabadiliko kuhusu CHADEMA kama suala la Ubinafsi, Ukabila, Upendeleo, Ubadhirifu wa pesa nk. Tunataka CHADEMA waje hapa kama baadhi ya viongozi watakubali kuyaacha.

Pia kuwe na mfumo ambao hayo mambo hayata ruhusiwa kutokea . . . . Kuna maswali mengi ya kuwauliza. waje tu wasiogope. Waanze na post kuu hapo juu.

Toa evidence ya hizo kauli zako kwanza au utakua umetumwa wewe. kwanza hao watu wanaotaka kuingia chama kimasharti hawafai na ikiwa masharti yenyewe sio ya kikatiba, kwanza omba katiba ya chadema then ikikuridhisha ujiunge na sio hizo porojo zako. kujiunga kwa vyama kwanza inaanza na kutunga katiba ambayo itaongoza au kuridhiana na vyama vyote so, ni makubaliano na ili ni ngumu kokote duniani ukizingatia hata hicho chama tawala hakiwezi kwa sababu ya ruzuku zaidi ni kwa serikali kuchuja na kubakiza vichache vyenye nguvu na majimbo mengi au katiba hii tunayoitarajia tolimit vyama aidha mwisho viwe vitatu au viwili kwa idadi ya majimbo iliyotwaa ili kodi zetu zisichezewe


(2. Kuna mambo kadhaa wa kadhaa ya kimsingi yanayohitaji mabadiliko kuhusu CHADEMA kama suala la Ubinafsi, Ukabila, Upendeleo, Ubadhirifu wa pesa nk.)

Tunaitaji ushaidi wa kitaaluma please can you count with evidence? jf sio janvi la bla,bla or ndio propaganda mnazokujanazo hapa jf?
3. Naongeza hapo mlikuja na chadema inavunja amani, chadema inafadhiliwa pesa na mataifa ya nje ili iondewe serikali madarkani, chadema na maandamano so, tueleze na kama wapo hao UWT waeneza uongo watueleze kwa evidence

Magamba wanavyofanya maandamano ya kujisifia kuwa tumejivua magamba! na kutumia msululu wa magari ya kifahari bila kutueleza wananchi kwanini tuu maskini ivi na huu mfumuko wa bei juu kila kukicha, ubadhirifu wa kodi zetu,mikataba ya kuneemesha wachache, vijana kufanya vibaya mashuleni, migomo kila kona dowan+richmond nk embu tujuze na wewe ni vipi chadema walichokosea wao wanaenda kwa raia kuwaelimisha na sasa wamewafungua macho wananchi kuhusu katiba je hao Magamba wanawaelimisha nini wazalendo uko kwenye mikutano yao?

Na sasa Mmefanikiwa kuvibana vyombo vya habari jamani nchi aiendishwi kijinga namna hii
Spika wa bunge na ujinga wake
Magamba kudakia sera za chadema mfano katiba wanasema wao ndio wameanzisha huu mswada wakati wamelazimishwa na ukikumbuka kwenye campaign hii ilikua ni ilani ya chadema wakati Magamba uko ilani yao aikuwepo. mengi na mengi......

Mtoa mada tuache upotoshaji wa mambo na naomba ujibu hoja zangu.
 
Huwezi kaa nje ya uwanja halafu ukawa unapiga domo,wakati wenzako wanachangia soksi, na mambo mengine. Tunaweza toa lawama nyingi sana kwa chadema na uongozi wake ila wenye matatizo ni sisi ambao tupo nje ya chadema.
Ukiwa ni mtu na mtanzania mwenye uchungu wa nchi utaona kuwa Chadema wamejitahidi sana kuleta demokrasia angalau ya kweli na kutetea nchi. Mapungufu kweli yapo lakini hawana matatizo makubwa, ila tunatakiwa kuwaunga mkono na kutoa mawazo yetu kusaidia chama. Na ukiona unaweza uongozi na kutoa mchango chanya gombea uenyekiti, umoja wa vijana, tawi, wilaya , mkoa halafu leta mabadiliko.Chadema ndicho chama pekee cha upinzani kimebadilisha uongozi ndani ya chama tokea 1995 bila mikwaruzo.Sasa kulaumu eti kwanini fulani kawa kiongozi haisadii katiba iko wazi chukua fomu gombea unachaguliwa na wananchama. Akitokea kiongozi kachaguliwa kimizengwe hapo tutasema.
INGIENI CHADEMA LETENI CHANGAMOTO ZITAPOKELEWA NA CHADEMA KITAENDELEA KUTUMIKIA WANANCHI.
CHANGIA CHADEMA, MAWAZO ,FEDHA, NA TECHNOLOGIA.
IKULU 2010 NI LAZIMA, UKOMBOZI WA MTANZANIA.
TUSIPOBADILIKA SISI WATOTO WETU WATAKUWA WATUMWA.
sahihisha badala ya 2010 iwe 2015 na undoe neno LAZIMA kwa maana ya kutoviza demokrasia hii changa ya TANGANYIKA yetu.
 
Good post. Kumbe ni kweli Jf ni ya Chadema. Utaona kila post CDM good. Tuwe kitaifa zaidi. Hii ni kawaida kwa Post za kibongo kushabikia hata jambo lisilo na tija kwa Taifa.
Jf take care. Kuna blog nyingi zimefungwa kwa ajili ya uchochezi. I am sure if you do not change your trend soon or later it will be blocked. I am sure 100%. Bye
 
Back
Top Bottom