Online Meeting with CHADEMA - Kuimarisha Upinzani na Kuleta Maendeleo - No 1

Mkuu Nono;

Nadhani kiini cha hoja ya msingi bado hujakielewa . . .

Shida si kwa Watu Makini na uwezo mkubwa kujiunga CHADEMA na kupewa Uongozi. Shida ni viongozi wa namna gani wanatakiwa na je ni Waadilifu kiasi cha kuvuta Umma wa Tanzania kuwatambua kuwa wako serious?

Concept ya Watu Makini kuachiwa uongozi si suala jipya na limefanya kazi sana katika Historia ya Mabadiliko ingawa si wote wamefanikiwa kuleta mabadiliko ya kweli. Nyerere alifanya hivyo, CCM wao wana utaratibu wa Kung'atuka na hata kuchukua watu wanaohama Upinzani na kuwapa madaraka, Oliver Tambo alimwachia Nelson Mandela, Mabere Marando alimwachia Mzee wa Kilalacha n.k.

This issue if you look into the positive side, you will understand what I mean. Baadhi ya viongozi wa CHADEMA ambao ndiyo wenye nafasi kubwa ya kuleta Tranformation wamekuwa questioned sana juu ya uadilifu wao, matumizi mabaya ya pesa, upendeleo, na hata kwa baadhi ya maamuzi . . .

For sure these are not about constitution or about election procedures, it is about leadership. Wakati CCM wanaendelea kukumbatia Rushwa na hata Ufisadi, Makundi nk katika Chaguzi zao i.e UVCCM, UWT nk. CHADEMA inatakiwa ijisafishe . . .

Yote hayo kwa Ujumla wake ndiyo yanatakiwa yafanyiwe kazi. Na tunataka commitment yao . . . .

Mkuu Allien,
Mimi bado naendelea kuamini taratibu na sheria ndio kitu pekee ambacho kinaweza kuleta mabadiliko endelevu.
Ukitoa mfano wa ccm kuwa wanang'atuka sio kweli kwani aliyengatuka ni Nyerere pia baada ya kuona kuwa muda umekwenda na aliyokuwa anasimamia na kuyaamini yalikuwa hayaendi kwa dunia ya wakati ule (tunamshukuru sana kwa hilo). Kuwa wapinzani wanaojiunga na ccm wanapewa madaraka ni njia ya kuudumaza upinzani pamoja na kuwadumaza hao waliojiunga na ccm kwani vinafasi vyenyewe wanavyopewa ni vya kuwafunga midomo na baada ya muda hawasikiki tena.

Suala la msingi hapa nadhani ni je, vyama hivi vinafuata taratibu na demokrasia ya kweli ndani yake. Hili kama lipo, sioni haja ya kumpisha mtu, kwani cheo ni dhamana, utatumika leo na kesho mwenzio atapokea kijiti. Pale inapobidi nadhani chama husika kinaweza kuona umuhimu na baada ya kujihoji, kuridhika na kuondoa hofu na mashaka basi wanaweza kumpisha mtu katika nafasi ya juu ya uongozi hasa pale anapokuwa "Allien" (yaani ambaye alikuwa sio mwanachama) au wakiwa kama kina Mandela, amabo ni viongozi walikuwa walioachiwa huru, ila usisahau kufungwa kwao ndio kupandisha siasa kwenyewe!

Sheria na demokrasia ndani ya chama husika ikiwemo, basi akitokea kiongozi akavurunda, taratibu zilizopo zinatumika kumuwajibisha ikiwa ni pamoja na kusitisha nafasi yake ya uongozi pale inapobidi. Nadhani huu ndio msingi!

Kama demokrasia ya kweli ipo, basi wewe ukiwa mwanachama na wanachama wakikuona una sifa zinazostahili kwa nafasi yoyote, basi mazingira yatakuwa sawa kumpata kiongozi atakayekiongoza chama. Mimi nadhani tukisimama katika hili na vyama vikifanya mambo yake kama taratibu zilivyo na zinavyotakikana ziwe, huwezi kuwa na M/Kiti au Katibu mkuu kwa miaka 10-15 na idadi ya madiwani, wabunge na wanachama ni wawili wawili, labda kama hivyo vyama ni taasisi za watu binafsi! Unatakiwa upimwe kwa talanta zako.

Ahsante
 
Huwezi kaa nje ya uwanja halafu ukawa unapiga domo,wakati wenzako wanachangia soksi, na mambo mengine. Tunaweza toa lawama nyingi sana kwa chadema na uongozi wake ila wenye matatizo ni sisi ambao tupo nje ya chadema.
Ukiwa ni mtu na mtanzania mwenye uchungu wa nchi utaona kuwa Chadema wamejitahidi sana kuleta demokrasia angalau ya kweli na kutetea nchi. Mapungufu kweli yapo lakini hawana matatizo makubwa, ila tunatakiwa kuwaunga mkono na kutoa mawazo yetu kusaidia chama. Na ukiona unaweza uongozi na kutoa mchango chanya gombea uenyekiti, umoja wa vijana, tawi, wilaya , mkoa halafu leta mabadiliko.Chadema ndicho chama pekee cha upinzani kimebadilisha uongozi ndani ya chama tokea 1995 bila mikwaruzo.Sasa kulaumu eti kwanini fulani kawa kiongozi haisadii katiba iko wazi chukua fomu gombea unachaguliwa na wananchama. Akitokea kiongozi kachaguliwa kimizengwe hapo tutasema.
INGIENI CHADEMA LETENI CHANGAMOTO ZITAPOKELEWA NA CHADEMA KITAENDELEA KUTUMIKIA WANANCHI.
CHANGIA CHADEMA, MAWAZO ,FEDHA, NA TECHNOLOGIA.
IKULU 2010 NI LAZIMA, UKOMBOZI WA MTANZANIA.
TUSIPOBADILIKA SISI WATOTO WETU WATAKUWA WATUMWA.
 
Huwezi kaa nje ya uwanja halafu ukawa unapiga domo,wakati wenzako wanachangia soksi, na mambo mengine. Tunaweza toa lawama nyingi sana kwa chadema na uongozi wake ila wenye matatizo ni sisi ambao tupo nje ya chadema.
Ukiwa ni mtu na mtanzania mwenye uchungu wa nchi utaona kuwa Chadema wamejitahidi sana kuleta demokrasia angalau ya kweli na kutetea nchi. Mapungufu kweli yapo lakini hawana matatizo makubwa, ila tunatakiwa kuwaunga mkono na kutoa mawazo yetu kusaidia chama. Na ukiona unaweza uongozi na kutoa mchango chanya gombea uenyekiti, umoja wa vijana, tawi, wilaya , mkoa halafu leta mabadiliko.Chadema ndicho chama pekee cha upinzani kimebadilisha uongozi ndani ya chama tokea 1995 bila mikwaruzo.Sasa kulaumu eti kwanini fulani kawa kiongozi haisadii katiba iko wazi chukua fomu gombea unachaguliwa na wananchama. Akitokea kiongozi kachaguliwa kimizengwe hapo tutasema.
INGIENI CHADEMA LETENI CHANGAMOTO ZITAPOKELEWA NA CHADEMA KITAENDELEA KUTUMIKIA WANANCHI.
CHANGIA CHADEMA, MAWAZO ,FEDHA, NA TECHNOLOGIA.
IKULU 2010 NI LAZIMA, UKOMBOZI WA MTANZANIA.
TUSIPOBADILIKA SISI WATOTO WETU WATAKUWA WATUMWA.

Nakubaliana nawe kwamba ili ulete mabadiliko ya kweli katika chama chochote kama vision yako ilivyo basi chukua kadi na ingia katika chama kisha omba nafasi ya uongozi.
Mengine yote hapa yatabaki kama porojo tu.
Mimi nahitaji kugombea uenyekiti wa mtaa kupitia Chadema. Then nitagombea udiwani na siku ya siku nitagombea ubunge.
Shida ni kwamba sina kadi yao na huku ninakoishi sijui hata ofisi yao ilipo. Hapo ndipo matatizo yanapoanzia.
Jamani viongozi wa Chadema tutajieni ofisi zenu zilipo mikoani na wilayani ili tukachukue kadi.
 
Mkuu Allien,
Mimi bado naendelea kuamini taratibu na sheria ndio kitu pekee ambacho kinaweza kuleta mabadiliko endelevu.
Ukitoa mfano wa ccm kuwa wanang'atuka sio kweli kwani aliyengatuka ni Nyerere pia baada ya kuona kuwa muda umekwenda na aliyokuwa anasimamia na kuyaamini yalikuwa hayaendi kwa dunia ya wakati ule (tunamshukuru sana kwa hilo). Kuwa wapinzani wanaojiunga na ccm wanapewa madaraka ni njia ya kuudumaza upinzani pamoja na kuwadumaza hao waliojiunga na ccm kwani vinafasi vyenyewe wanavyopewa ni vya kuwafunga midomo na baada ya muda hawasikiki tena.

Suala la msingi hapa nadhani ni je, vyama hivi vinafuata taratibu na demokrasia ya kweli ndani yake. Hili kama lipo, sioni haja ya kumpisha mtu, kwani cheo ni dhamana, utatumika leo na kesho mwenzio atapokea kijiti. Pale inapobidi nadhani chama husika kinaweza kuona umuhimu na baada ya kujihoji, kuridhika na kuondoa hofu na mashaka basi wanaweza kumpisha mtu katika nafasi ya juu ya uongozi hasa pale anapokuwa "Allien" (yaani ambaye alikuwa sio mwanachama) au wakiwa kama kina Mandela, amabo ni viongozi walikuwa walioachiwa huru, ila usisahau kufungwa kwao ndio kupandisha siasa kwenyewe!

Sheria na demokrasia ndani ya chama husika ikiwemo, basi akitokea kiongozi akavurunda, taratibu zilizopo zinatumika kumuwajibisha ikiwa ni pamoja na kusitisha nafasi yake ya uongozi pale inapobidi. Nadhani huu ndio msingi!

Kama demokrasia ya kweli ipo, basi wewe ukiwa mwanachama na wanachama wakikuona una sifa zinazostahili kwa nafasi yoyote, basi mazingira yatakuwa sawa kumpata kiongozi atakayekiongoza chama. Mimi nadhani tukisimama katika hili na vyama vikifanya mambo yake kama taratibu zilivyo na zinavyotakikana ziwe, huwezi kuwa na M/Kiti au Katibu mkuu kwa miaka 10-15 na idadi ya madiwani, wabunge na wanachama ni wawili wawili, labda kama hivyo vyama ni taasisi za watu binafsi! Unatakiwa upimwe kwa talanta zako.

Ahsante

Kiongozi Nono;

Mimi naona kama tuko pamoja except for some approach hasa katika Siasa za Nchi yetu kama tunataka zizae matunda.

Napenda kuchangia yafuatayo:

Mimi bado naendelea kuamini taratibu na sheria ndio kitu pekee ambacho kinaweza kuleta mabadiliko endelevu.

Kwa maoni yangu mimi katika hali ya Tanzania ya sasa hivyo havitoshi peke yake. UADILIFU ni muhimu sana kuliko hivyo vingine na ndiyo linalotusumbua kwa sasa na ndiyo ninalojaribu kulisemea. Baada ya hilo ni lile suala la UMAKINI na uwezo wa kuleta MIKAKATI ya kuleta Ushindi na Maendeleo.

Ukitoa mfano wa ccm kuwa wanang'atuka sio kweli kwani aliyengatuka ni Nyerere pia baada ya kuona kuwa muda umekwenda na aliyokuwa anasimamia na kuyaamini yalikuwa hayaendi kwa dunia ya wakati ule (tunamshukuru sana kwa hilo). Kuwa wapinzani wanaojiunga na ccm wanapewa madaraka ni njia ya kuudumaza upinzani pamoja na kuwadumaza hao waliojiunga na ccm kwani vinafasi vyenyewe wanavyopewa ni vya kuwafunga midomo na baada ya muda hawasikiki tena.

Nyerere aling'atuka Urais na Uenyekiti wa CCM. Mwinyi na Mkapa wote waling'atuka uenyekiti wa CCM. Mandela, Tony Blair nk wote waling'atuka. Nasema tena si jambo geni pale ambapo mna uhakika kwa kufanya hivyo kunaweza kuleta mafanikio. Of course katika cases nyingine msipokuwa na uhakika na watu makini hasa walio na uchu wa madaraka then inakuwa vurugu tu.

Suala la msingi hapa nadhani ni je, vyama hivi vinafuata taratibu na demokrasia ya kweli ndani yake. Hili kama lipo, sioni haja ya kumpisha mtu, kwani cheo ni dhamana, utatumika leo na kesho mwenzio atapokea kijiti. Pale inapobidi nadhani chama husika kinaweza kuona umuhimu na baada ya kujihoji, kuridhika na kuondoa hofu na mashaka basi wanaweza kumpisha mtu katika nafasi ya juu ya uongozi hasa pale anapokuwa "Allien" (yaani ambaye alikuwa sio mwanachama) au wakiwa kama kina Mandela, amabo ni viongozi walikuwa walioachiwa huru, ila usisahau kufungwa kwao ndio kupandisha siasa kwenyewe!

Nakubaliana nawe kwa asilimia 100% ila nasema vigezo hivyo kwa saisa za kwetu havitoshi. CHADEMA wana maswali mengi ya kujibu juu ya upendeleo wa Madaraka, Ufujaji wa pesa nk. Nadhani sasa utakubali kuwa Sheria na Demokrasia bila Uadilifu hakutaleta hamasa itakiwayo. CHADEMA ukiondoa baadhi ya viongozi wachache wanaojitahidi kama Dr. Slaa na Zitto ambao wana ujasiri wa kutosha, wengine wana kazi ya ziada na changamoto kubwa. Tunataka CHADEMA ifanye vyema zaidi ya sasa na hilo linahitaji UADILIFU na Utashi wa Kweli wa Kisiasa.

Sheria na demokrasia ndani ya chama husika ikiwemo, basi akitokea kiongozi akavurunda, taratibu zilizopo zinatumika kumuwajibisha ikiwa ni pamoja na kusitisha nafasi yake ya uongozi pale inapobidi. Nadhani huu ndio msingi!

Nakubaliana na wewe kwa asilimia 100%. Ongeza Uadilifu. Maana Mbabe yeyote aliyechaguliwa kwa Njia ya Demokrasia au Mizengwe anaweza kuwa kikwazo kama hana UADILIFU au MIKAKATI HAI ya maendeleo. Rejea Bob Mugabe na Madai ya Mrehemu Chacha Wangwe (RIP) kwa CHADEMA.

Kama demokrasia ya kweli ipo, basi wewe ukiwa mwanachama na wanachama wakikuona una sifa zinazostahili kwa nafasi yoyote, basi mazingira yatakuwa sawa kumpata kiongozi atakayekiongoza chama. Mimi nadhani tukisimama katika hili na vyama vikifanya mambo yake kama taratibu zilivyo na zinavyotakikana ziwe, huwezi kuwa na M/Kiti au Katibu mkuu kwa miaka 10-15 na idadi ya madiwani, wabunge na wanachama ni wawili wawili, labda kama hivyo vyama ni taasisi za watu binafsi! Unatakiwa upimwe kwa talanta zako.

Nadhani hili linajibiwa na mengine hapo juu.

Mkuu, sisi wengine si Wanasiasa wala Wanachama wa Chama Chochote lakini tunapenda kuona mabadiliko ya kweli na kwa hili, tunajaribu kutoa changamoto ili zifanyiwe kazi. Ikishindikana tutaingia kazini wenyewe na kwa hili tunataka CHADEMA wayafanyie kazi mapungufu haya ambayo ndiyo yanawarudisha nyuma.
 
Huwezi kaa nje ya uwanja halafu ukawa unapiga domo,wakati wenzako wanachangia soksi, na mambo mengine. Tunaweza toa lawama nyingi sana kwa chadema na uongozi wake ila wenye matatizo ni sisi ambao tupo nje ya chadema.
Ukiwa ni mtu na mtanzania mwenye uchungu wa nchi utaona kuwa Chadema wamejitahidi sana kuleta demokrasia angalau ya kweli na kutetea nchi. Mapungufu kweli yapo lakini hawana matatizo makubwa, ila tunatakiwa kuwaunga mkono na kutoa mawazo yetu kusaidia chama. Na ukiona unaweza uongozi na kutoa mchango chanya gombea uenyekiti, umoja wa vijana, tawi, wilaya , mkoa halafu leta mabadiliko.Chadema ndicho chama pekee cha upinzani kimebadilisha uongozi ndani ya chama tokea 1995 bila mikwaruzo.Sasa kulaumu eti kwanini fulani kawa kiongozi haisadii katiba iko wazi chukua fomu gombea unachaguliwa na wananchama. Akitokea kiongozi kachaguliwa kimizengwe hapo tutasema.
INGIENI CHADEMA LETENI CHANGAMOTO ZITAPOKELEWA NA CHADEMA KITAENDELEA KUTUMIKIA WANANCHI.
CHANGIA CHADEMA, MAWAZO ,FEDHA, NA TECHNOLOGIA.
IKULU 2010 NI LAZIMA, UKOMBOZI WA MTANZANIA.
TUSIPOBADILIKA SISI WATOTO WETU WATAKUWA WATUMWA.

Kamanda Kinepi Nepi;

Peace to you man! Unaonekana Mwana CHADEMA hasa. Big Up!

Hoja zangu ni kama ifuatavyo:

Huwezi kaa nje ya uwanja halafu ukawa unapiga domo,wakati wenzako wanachangia soksi, na mambo mengine. Tunaweza toa lawama nyingi sana kwa chadema na uongozi wake ila wenye matatizo ni sisi ambao tupo nje ya chadema.

Mkuu, kuleta mabadiliko katika nchi si lazima uwe ndani ya chama. Mawazo mazuri na Changamoto pia yanaleta maendeleo kama yakifanyiwa kazi. Ungekuwa katika Uendeshaji wa makampuni SWOT analysis inaweza ikakusaidia kuleta mafanikio makubwa katika makampuni. Si lazima uwe ndani ya CHADEMA ili mambo yaende. Tunataka kuja huko sasa lakini tunataka mjisafishe kama mtakubali. Marehemu Wangwe alikuwa na baadhi ya hoja za kweli, hatutaki kuzileta hapa tena. Zifanyieni kazi kujijengea umakini mbele ya WaTZ.

Kuna wa TZ Million40, je wote ni Wanachama? Mandela alileta mabadiliko SA, je, alikuwa kwenye active Politics? Mkuu, kubali changamoto na zifanyieni kazi.

Ukiwa ni mtu na mtanzania mwenye uchungu wa nchi utaona kuwa Chadema wamejitahidi sana kuleta demokrasia angalau ya kweli na kutetea nchi. Mapungufu kweli yapo lakini hawana matatizo makubwa, ila tunatakiwa kuwaunga mkono na kutoa mawazo yetu kusaidia chama. Na ukiona unaweza uongozi na kutoa mchango chanya gombea uenyekiti, umoja wa vijana, tawi, wilaya , mkoa halafu leta mabadiliko.Chadema ndicho chama pekee cha upinzani kimebadilisha uongozi ndani ya chama tokea 1995 bila mikwaruzo.Sasa kulaumu eti kwanini fulani kawa kiongozi haisadii katiba iko wazi chukua fomu gombea unachaguliwa na wananchama. Akitokea kiongozi kachaguliwa kimizengwe hapo tutasema.

Nakubaliana na wewe kwa kiasi kikubwa. Sina mgogoro na baadhi ya makamanda wa CHADEMA kama Slaa, Zitto, Mwanyika nk. Shida ni kwa baadhi ambao si waadilifu ndani ya CHADEMA. Jisafisheni. Ukivaa suti nyeupe kama inadoa lazima ulitoe vinginevyo itakuharibia unadhifu wako, na haya ndiyo mawazo tunayotaka myafanyie kazi. Mkiyafanyia kazi, nina uhakika wengi tutakuja huko. Msipoyafanyia kazi, tutatafuta Chama kitakachokubali kuwa makini na adlifu na tutakwenda huko. Tunapenda kwaza kuwapa nafasi CHADEMA kwa kuwa kuna baadhi wamefanya kazi nzuri. Ikikubalika, tunauntangazia UMMA wa JF kuwa mmekubali na wale wana JF makini tutawaambia waje huko kuongeza nguvu. Mimi sitaki uongozi wa juu, nitaomba nafasi maalumu ya kuwa STRATEGIST maana udhaifu wa Siasa za Tanzania nazijua na nini cha kufanya nafahamu na ndiyo maana napiga kelele.

So, ukisikia napiga domo kama unavyosema, basi lifanyie kazi. Sina uchu wa Madaraka lakini natka maendeleo na kuona mabadiliko.
 
Nakubaliana nawe kwamba ili ulete mabadiliko ya kweli katika chama chochote kama vision yako ilivyo basi chukua kadi na ingia katika chama kisha omba nafasi ya uongozi.
Mengine yote hapa yatabaki kama porojo tu.
Mimi nahitaji kugombea uenyekiti wa mtaa kupitia Chadema. Then nitagombea udiwani na siku ya siku nitagombea ubunge.
Shida ni kwamba sina kadi yao na huku ninakoishi sijui hata ofisi yao ilipo. Hapo ndipo matatizo yanapoanzia.
Jamani viongozi wa Chadema tutajieni ofisi zenu zilipo mikoani na wilayani ili tukachukue kadi.

Mkuu;

Post no. 24 na 25 hapo juu zina maelezo ya kutosha.

Peace to you!
 
Mkuu Kitila;

Kwanza tunashukuru kwa kuitikia wito wa kutembelea thread hii. Ingawa naona umejibu kwa haraka haraka na kuacha maswali ya msingi yaliyoulizwa na wadau katika post zao.

Kwanza, CHADEMA wako tayari kupokea Wanamapinduzi kutoka JF na kwingineko ambao wataleta changamoto ya kweli?

Je, mko tayari kufanya marekebisho ya kiuongozi na mfumo wa uongozi kukidhi Demokrasia ya kweli kivitendo katika uendeshaji wa chama?

Je, kwa wale watu makini na ambao ni rasilimali ya Taifa wakija CHADEMA je, viongozi wa sasa wako tayari kutoa nafasi za uongozi kwa wadau hawa?

Maswali haya na mengine katika post yanatakiwa yajibiwe. Tutayapima majibu yako kwa hiyo ni vema majibu yakiwa detailed with facts.

Sana tu mkuu. Wana mapinduzi kutoka JF na kwingineko wanakaribishwa sana chadema. In fact wana mapinduzi wengi hapa nchini sasa hivi wamejiunga na chadema. Nadiriki kusema kuwa watu wengi wanaona haja ya mabadiliko katika nchi hii wanaiona chadema ndio agent pekee kwa sasa. Kuna wimbi kubwa la mabadiliko katika fikra za watu kwa sasa, na kama wana mapinduzi wa hapa JF watajiunga katika wimbi hili tunaweza kuleta ukombozi mapema kuliko tulivyotarajia.

So karibuni sana. Bahati nzuri kuna uchaguzi unaendelea ndani ya chama, hii ndio nafasi nzuri zaidi kushiriki kuleta mabadiliko kwa kujitokeza kugombea na/au kuchagua viongozi makini. Sasa hivi uchaguzi upo katika ngazi ya kata na by March/April utakuwa katika ngazi ya Taifa.
 
Sana tu mkuu. Wana mapinduzi kutoka JF na kwingineko wanakaribishwa sana chadema. In fact wana mapinduzi wengi hapa nchini sasa hivi wamejiunga na chadema. Nadiriki kusema kuwa watu wengi wanaona haja ya mabadiliko katika nchi hii wanaiona chadema ndio agent pekee kwa sasa. Kuna wimbi kubwa la mabadiliko katika fikra za watu kwa sasa, na kama wana mapinduzi wa hapa JF watajiunga katika wimbi hili tunaweza kuleta ukombozi mapema kuliko tulivyotarajia.

So karibuni sana. Bahati nzuri kuna uchaguzi unaendelea ndani ya chama, hii ndio nafasi nzuri zaidi kushiriki kuleta mabadiliko kwa kujitokeza kugombea na/au kuchagua viongozi makini. Sasa hivi uchaguzi upo katika ngazi ya kata na by March/April utakuwa katika ngazi ya Taifa.

Mkuu Kitila, naunga mkono hoja yako mia kwa mia!!

Siungi mkono hata kidogo hoja kwamba wanamapinduzi wakifika kwenye chama wapewe nafasi za uongozi papo kwa papo. Waje, wafanye kazi ili kuonyesha kwamba wanafaa na wanastahili kupewa uongozi. Staili ya kukurupuka na kupewa uongozi wa papo kwa papo kama Mrema alivyokuwa anafanya baada ya kuhama vyama ina matatizo makubwa. Pia staili hiyo hiyo inawavuruga CCM kwa kuwapa mamluki vyeo baada ya kuwavua toka upinzani. Hii haitendi haki, kwani kuna wanachama wazuri sana ambao wamesaidia chama na ndio hao wanastahili kupewa nafasi ya kukiongoza chama. Si busara, na kwa maoni yangu ni upuuzi na ujinga kumpa mtu cheo eti kwa sababu kakubali kujiunga na chama. Mtu aje afanye kazi kuhalalisha cheo anachotaka kukigombea. Haya mambo ya offer ni hatari na sumu ya demokrasia. CHADEMA isimamie katiba yake na isijiingize kwenye mbwembwe za kijinga.
 
Nakuunga mkono Dark City.

Watu waenda chama cha siasa kukijenga kwa nafasi yoyote iwayo. mchango wako katika chama ukionekana kwa wanachama basi itakuwa muda muafaka kugombea nafasi yoyote ya uongozi.

Muhimu ni kuwa watu wasiwe na mawazo ya kugombea nafasi za juu tuu, si mbaya kuanzia ngazi za chini, kama serikali za mitaa, udiwani na hatimaye ubunge.

Chama tawala chochote kikikaa madarakani muda mrefu hata kama kinafanya vyema hufika muda vikaishiwa mawazo mapya na kuanza kufanya kazi kwa mazoea. Hujiona kwamba wao ndiyo wao na bila wao nchi haiendi. Hujawa na kiburi na wala hawawatii na kuwaogopa acha kuwaheshimu wapiga kura. Ni muda muafaka changamoto ya kweli iwafikie watawala kwa cha upinzani serious kujitokeza - na kwa sasa ni CHADEMA kwa Tanzania bara na CUF kwa Zanzibar.
 
Dark City,
Umegonga penyewe. Nilishangaa sana Guninita alipopokelewa na kupewa ukatibu mwenezi bila hata kutaka kuangalia kama kauli ya Marecela kuwa Guninita alidanganya kwenye elimu yake ilikuwa na ukweli. Akaja Akwilombe, akapewa unaibu katibu mkuu. Baadaye wote hawa walirudi ccm na wote wana nyadhifa huko. Guninita alikuwa mwalimu daraja C, siasa ikampandisha hadi kuwa mkuu wa wilaya. Ukimwambia aachane na siasa maana yake arudi kufundisha shule ya msingi kitu ambacho ni kigumu sana. Watu wa aina hii wamegeuza siasa kuwa ajira, na hawa ndio vyama inabidi viwe na umakini sana vinapokuwa nao.
 
Dark City,
Umegonga penyewe. Nilishangaa sana Guninita alipopokelewa na kupewa ukatibu mwenezi bila hata kutaka kuangalia kama kauli ya Marecela kuwa Guninita alidanganya kwenye elimu yake ilikuwa na ukweli. Akaja Akwilombe, akapewa unaibu katibu mkuu. Baadaye wote hawa walirudi ccm na wote wana nyadhifa huko. Guninita alikuwa mwalimu daraja C, siasa ikampandisha hadi kuwa mkuu wa wilaya. Ukimwambia aachane na siasa maana yake arudi kufundisha shule ya msingi kitu ambacho ni kigumu sana. Watu wa aina hii wamegeuza siasa kuwa ajira, na hawa ndio vyama inabidi viwe na umakini sana vinapokuwa nao.

Very well said!
 
Sana tu mkuu. Wana mapinduzi kutoka JF na kwingineko wanakaribishwa sana chadema. In fact wana mapinduzi wengi hapa nchini sasa hivi wamejiunga na chadema. Nadiriki kusema kuwa watu wengi wanaona haja ya mabadiliko katika nchi hii wanaiona chadema ndio agent pekee kwa sasa. Kuna wimbi kubwa la mabadiliko katika fikra za watu kwa sasa, na kama wana mapinduzi wa hapa JF watajiunga katika wimbi hili tunaweza kuleta ukombozi mapema kuliko tulivyotarajia.

So karibuni sana. Bahati nzuri kuna uchaguzi unaendelea ndani ya chama, hii ndio nafasi nzuri zaidi kushiriki kuleta mabadiliko kwa kujitokeza kugombea na/au kuchagua viongozi makini. Sasa hivi uchaguzi upo katika ngazi ya kata na by March/April utakuwa katika ngazi ya Taifa.

Kitila,

Asante sana Mkuu, I hope wana JF wataitikia ukaribisho wako . . .

Tunatumaini pia maoni yote ya msingi na manufaa yatafanyiwa kazi.

Maini yangu ni kuwa tusibweteke sana na hamasa ya sasa bali ni muhimu kuweka mfumo imara na uongozi adilifu. Na hili mliangalie sana katika chaguzi zinazoendelea . . .

Kumbuka wimbi na Mrema alipotoka CCM kwenda NCCR au hata TLP, walijiona wao ndiyo zaidi kwa kuwa kulikuwa na hamasa . . . . lakini leo NCCR na TLP wako wapi . . . .

Wenye nia nzuri na mabadiliko ya kweli bado tunawapa changamoto mpaka hapo mtakapozifanyia kazi vinginveyo baada ya muda CHADEMA nao watajikuta pabaya . . . .
 
Mkuu Kitila, naunga mkono hoja yako mia kwa mia!!

Siungi mkono hata kidogo hoja kwamba wanamapinduzi wakifika kwenye chama wapewe nafasi za uongozi papo kwa papo. Waje, wafanye kazi ili kuonyesha kwamba wanafaa na wanastahili kupewa uongozi. Staili ya kukurupuka na kupewa uongozi wa papo kwa papo kama Mrema alivyokuwa anafanya baada ya kuhama vyama ina matatizo makubwa. Pia staili hiyo hiyo inawavuruga CCM kwa kuwapa mamluki vyeo baada ya kuwavua toka upinzani. Hii haitendi haki, kwani kuna wanachama wazuri sana ambao wamesaidia chama na ndio hao wanastahili kupewa nafasi ya kukiongoza chama. Si busara, na kwa maoni yangu ni upuuzi na ujinga kumpa mtu cheo eti kwa sababu kakubali kujiunga na chama. Mtu aje afanye kazi kuhalalisha cheo anachotaka kukigombea. Haya mambo ya offer ni hatari na sumu ya demokrasia. CHADEMA isimamie katiba yake na isijiingize kwenye mbwembwe za kijinga.

Mkuu, naukubaliana na wewe 100%

Lakini nasisitiza bado kuwa kiongozi bila uadilifu haina maana yoyote kwa kuwa mabadiliko hayatakuja hata kama watachaguliwa kwa kura nyingi. Itakuwa ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu.

Tujifunze kutoka CCM . . . Si wanaendesha serikali sasa? Si walichaguliwa? Ubunge, udiwani, nk. Lakini je kuchaguliwa kwao kumeleta tija yoyote?

UADILIFU UADILIFU UADILIFU na MIKAKATI ndiyo mbinu pekee ya kuleta msukumo. Na hayo CHADEMA inabidi myafanyie kazi.

Of course common sense ni muhimu katika maamuzi, unafikiri Watanzania waliowapigia kura Mafisadi walifahamu kuwa ni mafisadi? Ni nini kifanyike kuwatambua mapema?

Kama nikiamua kujiunga CHADEMA binafsi sitotaka Cheo chochote, nitapenda kuwa mbunifu wa mikakati na kama hilo halikubaliki eti mpaka nigombee katika mitaa, au nafasi nyingine yoyote, then I am sorry to say, wengi mtatukosa bado.

Haya mambo si ya kuongea kwa jazba, tunapenda kuona reasoning, ukisoma post zangu zinajieleza kikamilifu unless kama tunataka kuleta ule ubishi wa kisiasa usio na Tija.

Mwenye macho haambiwi Tazama wala mwenye masikio haambiwi Sikia.
 
Nakuunga mkono Dark City.

Watu waenda chama cha siasa kukijenga kwa nafasi yoyote iwayo. mchango wako katika chama ukionekana kwa wanachama basi itakuwa muda muafaka kugombea nafasi yoyote ya uongozi.

Muhimu ni kuwa watu wasiwe na mawazo ya kugombea nafasi za juu tuu, si mbaya kuanzia ngazi za chini, kama serikali za mitaa, udiwani na hatimaye ubunge.

Chama tawala chochote kikikaa madarakani muda mrefu hata kama kinafanya vyema hufika muda vikaishiwa mawazo mapya na kuanza kufanya kazi kwa mazoea. Hujiona kwamba wao ndiyo wao na bila wao nchi haiendi. Hujawa na kiburi na wala hawawatii na kuwaogopa acha kuwaheshimu wapiga kura. Ni muda muafaka changamoto ya kweli iwafikie watawala kwa cha upinzani serious kujitokeza - na kwa sasa ni CHADEMA kwa Tanzania bara na CUF kwa Zanzibar.

Thanks and well written . . . .

Na hapa ndiyo tunataka CHADEMA wajiunde with CONTROLS and CHECKS & BALANCES kwa viongozi wote ili chama kiwe cha Ukombozi wakati wote hata wakija kushika madaraka. Sasa hivi CHADEMA hakuna hicho . . .

Unajua ndugu zangu, sisi tunang'ang'ania tu kuingia kushinda Uchaguzi bila kuwa na Ubunifu makini na hoja zote za kuwaambia muwe WAADILIFU na KUJISAFISHA zote mnazikwepa. Tuwaelewaje? Mmeng'ang'ania tu ALIENS wasipewe uongozi mpaka wagombee . . . . kuna katiba inayoruhusu uongozi wa kupewa? Hata hao Watu makini ambao tunasema wakije CHADEMA wapokelewe, lazima muwe na vigezo vya kuwatambua kuwa ni watu makini. Naweza kuwa FISADI na bado nikagombea CHADEMA na kuchaguliwa, is that what CHADEMA wants?
 
Dark City,
Umegonga penyewe. Nilishangaa sana Guninita alipopokelewa na kupewa ukatibu mwenezi bila hata kutaka kuangalia kama kauli ya Marecela kuwa Guninita alidanganya kwenye elimu yake ilikuwa na ukweli. Akaja Akwilombe, akapewa unaibu katibu mkuu. Baadaye wote hawa walirudi ccm na wote wana nyadhifa huko. Guninita alikuwa mwalimu daraja C, siasa ikampandisha hadi kuwa mkuu wa wilaya. Ukimwambia aachane na siasa maana yake arudi kufundisha shule ya msingi kitu ambacho ni kigumu sana. Watu wa aina hii wamegeuza siasa kuwa ajira, na hawa ndio vyama inabidi viwe na umakini sana vinapokuwa nao.

Mkuu, asante sana kwa post hii, ina mengi ya kujifunza . . . .

Ni vema CHADEMA wakawa na vigezo makini vya kupokea wanachama na kuwapa uongozi. Mtu hata kama ana hamasa vipi lakini hana UADILIFU aachwe. With TIME watu wakigundua hivyo, mtaheshimiwa.
 
Sana tu mkuu. Wana mapinduzi kutoka JF na kwingineko wanakaribishwa sana chadema. In fact wana mapinduzi wengi hapa nchini sasa hivi wamejiunga na chadema. Nadiriki kusema kuwa watu wengi wanaona haja ya mabadiliko katika nchi hii wanaiona chadema ndio agent pekee kwa sasa. Kuna wimbi kubwa la mabadiliko katika fikra za watu kwa sasa, na kama wana mapinduzi wa hapa JF watajiunga katika wimbi hili tunaweza kuleta ukombozi mapema kuliko tulivyotarajia.
.

Mkuu Kitila,
Ni kweli hayo? Mbona kama umekuja na vague statements ambazo kikawaida kama msomi inatakiwa uzikwepe? watu wengi hao wangapi?
So karibuni sana. Bahati nzuri kuna uchaguzi unaendelea ndani ya chama, hii ndio nafasi nzuri zaidi kushiriki kuleta mabadiliko kwa kujitokeza kugombea na/au kuchagua viongozi makini. Sasa hivi uchaguzi upo katika ngazi ya kata na by March/April utakuwa katika ngazi ya Taifa.

Asante kwa taarifa, nilikuwa najiuliza CHADEMA watafanya lini uchaguzi? Wakati wanamwondoa Chacha walisema ungelikuwa November/December 2008 kwa uchaguzi ngazi ya taifa. Kweli ni nafasi kwa wana CHADEMA kufanya mabadiliko kwa faida ya chama chao na nchi. Nitafurahi Kitila hata ukiukwaa japo umakamu Mwenyekiti au naibu katibu. 2010 sio mbali na inabidi muanze mapema kutengeneza sera za kuwasaidia kuwashinda CCM.
 
Mkuu, naukubaliana na wewe 100%

Lakini nasisitiza bado kuwa kiongozi bila uadilifu haina maana yoyote kwa kuwa mabadiliko hayatakuja hata kama watachaguliwa kwa kura nyingi. Itakuwa ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu.

Tujifunze kutoka CCM . . . Si wanaendesha serikali sasa? Si walichaguliwa? Ubunge, udiwani, nk. Lakini je kuchaguliwa kwao kumeleta tija yoyote?

UADILIFU UADILIFU UADILIFU na MIKAKATI ndiyo mbinu pekee ya kuleta msukumo. Na hayo CHADEMA inabidi myafanyie kazi.

Of course common sense ni muhimu katika maamuzi, unafikiri Watanzania waliowapigia kura Mafisadi walifahamu kuwa ni mafisadi? Ni nini kifanyike kuwatambua mapema?

Kama nikiamua kujiunga CHADEMA binafsi sitotaka Cheo chochote, nitapenda kuwa mbunifu wa mikakati na kama hilo halikubaliki eti mpaka nigombee katika mitaa, au nafasi nyingine yoyote, then I am sorry to say, wengi mtatukosa bado.

Haya mambo si ya kuongea kwa jazba, tunapenda kuona reasoning, ukisoma post zangu zinajieleza kikamilifu unless kama tunataka kuleta ule ubishi wa kisiasa usio na Tija.

Mwenye macho haambiwi Tazama wala mwenye masikio haambiwi Sikia.

Allien, hoja zako ni nzuri sana na CHADEMA wanatakiwa wazifanyie kazi. Kwa maoni yangu si vizuri mtu kukimbilia kwenye chama kutafuta uongozi. Inakuwa vizuri kama unajiunga na chama kutoa mchango wako katika jambo ambalo chama hicho kinalisimiamia na endapo wewe unaliamini (towards attaining a common goal). Lakini mtu anayefika mahali na siku hiyo anataka ukubwa ni hatari. Ni bahati mbaya kwamba watu wengi tunapenda sana kutumikiwa kuliko kutumikia. Hii ni hali ya hatari sana na nadhani ndio chanzo cha wakulu wetu kudai kwa nguvu kuitwa waheshimiwa!! Ni upuuzi mtupu!

Ila kama mtu anataka kuongoza basi awashawishi wanachama kwanza kwa kuwatumikia ili wampime na si kuanza kunadi rekodi zake za huko alikotoka katika mtindo wa hadithi na ngonjera za paukwa pakawa.

Pia nakuunga mkono kwamba CHADEMA watafute jambo ambalo litawatofautisha na vyama vingine hapa TZ ikiwemo CCM. Na jambo rahisi la kutumia ila gumu kulitekeleza kwa hali TZ ya sasa ni UADILIFU. Kama wakiweza hilo na kuweka mikakati mizuri ya kuonyesha kuwa wana kitu kipya cha kuwapa Watz, sioni sababu kwa nini wananchi wasiwaami na kuwaunga mkono, na hatimaye kuwapa jukumu la kuongoza nchi yetu. Vinginevyo wataishia kutamani tu kuwakomboa WaTz lakini hawataweza kwa kuwa hawana mbinu za kufanya hivyo.
 
Mtanzania, I know hiyo statement ni vague kweli; bahati mbaya statements nyingi za kisiasa huwa ni vague :)

Nitatoa mchango wangu kwenye chadema, lakini sio kwa kugombea hivyo vyeo vizitovizito ambavyo vinanizidi uzito. Ahsante lakini kwa kunishawishi...

Aliens et al-hii thread ni muhimu sana, na mimi binafsi naisoma mara kadhaa kwa siku. Mtu kukupa ushauri ni kipimo muhimu sana cha kutambua kwamba anakupenda. Wote wanaotoa ushauri hapa kwa chadema mimi nachukulia kwamba wanaipenda na wanaitakia mema chadema.

Nakubaliana na hoja yenu kwamba kuna haja ya chadema kujipambanua kisera, kimkakati, etc. Haya mambo yameanza kufanyiwa kazi, na hiyo ya sangara operation ni moja ya namna ya kujipambanua kimkakati. Nakiri kwamba kwa upande wa kujipambanua kisera tu-bado. Bado tuna bidii ya kukosoa zaidi na kuibua kashfa kuliko kutoa alternative policies and strategies juu ya namna ya kuitoa nchi hapa tulipo. This is a challenge ambayo lazima tuifanyie kazi, maana wapiga kura hawatatuchagua tushike serikali kwa sababu tu mabingwa wa kuibua kashfa bali kwa kuwa na alternative sera, mikakati na mbinu za kuwatatulia matatizo yao ya msingi. Hili lazima lifanyiwe kazi sooner than later.
 
Hongera Ongara kwa kufafanua hoja kwa ukweli na uhakika!

Kama kweli tunataka siasa safi tujadilini kwa hoja za kimantiki na tuwe na correct data maana JF inasomwa na watu wengi na pia inatumika kama reference jamani.
 
Mtanzania, I know hiyo statement ni vague kweli; bahati mbaya statements nyingi za kisiasa huwa ni vague :)

Nitatoa mchango wangu kwenye chadema, lakini sio kwa kugombea hivyo vyeo vizitovizito ambavyo vinanizidi uzito. Ahsante lakini kwa kunishawishi...

Aliens et al-hii thread ni muhimu sana, na mimi binafsi naisoma mara kadhaa kwa siku. Mtu kukupa ushauri ni kipimo muhimu sana cha kutambua kwamba anakupenda. Wote wanaotoa ushauri hapa kwa chadema mimi nachukulia kwamba wanaipenda na wanaitakia mema chadema.

Nakubaliana na hoja yenu kwamba kuna haja ya chadema kujipambanua kisera, kimkakati, etc. Haya mambo yameanza kufanyiwa kazi, na hiyo ya sangara operation ni moja ya namna ya kujipambanua kimkakati. Nakiri kwamba kwa upande wa kujipambanua kisera tu-bado. Bado tuna bidii ya kukosoa zaidi na kuibua kashfa kuliko kutoa alternative policies and strategies juu ya namna ya kuitoa nchi hapa tulipo. This is a challenge ambayo lazima tuifanyie kazi, maana wapiga kura hawatatuchagua tushike serikali kwa sababu tu mabingwa wa kuibua kashfa bali kwa kuwa na alternative sera, mikakati na mbinu za kuwatatulia matatizo yao ya msingi. Hili lazima lifanyiwe kazi sooner than later.

Now you are talking Kitila!

Mkiendelea na kuwekeza nguvu nyingi kwenye kuibua kashfa za watawala, mkishika dola mtaibua za nani? Na je hiyo ni kazi muhimu (central role) ya chama cha siasa kinachotakiwa kutoa sera mbadala kwa wananchi? Hata hivyo nawapongeza wote ambao mmeendelea kufanya kazi hasa katika mazingira yanayowakabili wapinzani hapa nchini. Inahitaji mtu kuwa na roho ya paka kubaki upinzani. Maadamu mumeweza hilo, basi songa mbele muibuie kitu cha maana kwa ajili ya kuwashawishi wapiga kura waipe CHADEMA nafasi ya kuongoza nchi. To me that's the main challenge now!
 
Back
Top Bottom