Online Meeting with CHADEMA - Kuimarisha Upinzani na Kuleta Maendeleo - No 1

Allien

JF-Expert Member
Jul 6, 2008
5,546
1,861
Wana-CHADEMA mliomo humu, Karibuni katika Thread hii maalumu kwa ajili ya mambo muhimu ambayo tunataka myajibu.

Tunaanza na CHADEMA na tutawapima kutokana na maelezo yenu. Then tutaviita pia vyama vingine katika thread tofauti. So this is KITI MOTO!

Tunajua Mh. Mbowe, Dr. Slaa, Zitto, Mwanyika, nk wote mko humu, so tunataka majibu ya uhakika.

Watanzania tumechoka sana mwekeo wa nchi yetu.

Hakuna wa kututetea kikamilifu ndani ya Chama Tawala . . . .

Upinzani nao bado unasua sua na hauna mwelekeo wa kushika hatamu . . . .

Sasa baadhi ya wana JF na watanzania wengine makini ambo wako nje ya JF kwa hiari yetu tumeamua tunapenda kuona Nchi yetu ikiwa na mabadiliko na maendeleo ya kweli.

Tunapenda kuona mambo ya kimsingi ya kuleta mabadiliko ya kweli yafanyike na ikiwezekana CHADEMA ishike madaraka mwaka 2010 au 2015. Na wengi tuko tayari kuwaunga mkono na kujiandaa kufanya kweli endapo tu mtakidhi matakwa ya watanzania

Kujiridhisha mwanaweza kupitia thread hii kwanza: https://www.jamiiforums.com/complai...jamii-forums-kuwa-chama-tishio-cha-siasa.html

Kwa kuanzia tunaomba mtoe comment katika hili:

Sikonge:

Kumbe tuko kuipa mkono CHADEMA? Nilikuwa sijui. Na hata kama ni Chadema, basi huyo Mbowe basi aje hapa na kama kweli atakubali kupokea watu wengi kutoka JF, basi lazima vitu kadhaa viingizwe humo ndani. Kama amekuwa anaibeba Chadema kwa nguvu basi lazima aridhike kuwa sasa atakuwa na upinzani.

Kama nilivyosema mwanzo, itabidi hata wale ambao hawapo Dar kama mimi hapa, tuweze shiriki mkutano ONLINE. Tutachangia ila kwa makubalioano tuwe na SAY yetu. Kwa mtindo huo basi, Chadema kiwe chama cha kwanza kuanza kutumia INTERNET katika maswala yake mengi na hii inwe NYONGEZA katika maneno ya Nyerere kuwa "Ili tuendelee tunahitaji vitu vinne, Watu, Ardhi, Siasa safi, Uongozi bora na sisi tuseme TECHNOLOGY".

Chadema, njooni hapa, nendeni Tanzanet, nendeni kwa Michuzi nk ili muone jinsi Mtandao unavyovuta watu. Someni kutoka kwao na hapo anzisheni mtandao wenu. Ikibidi msaada wa kufungua kitu kama hiki basi nafikiri wapo watu wengi sana watakaokuwa tayari kuwachangua kwa mawazo, ufundi, fedha na vifaa kama mtaonyesha moyo wa kupokea hivyo vitu kutoka kwao na kuvitumia kwa faida ya Watanzania.

Ila cha muhimu ni "nini kitatokea kwa viongozi wataokiuka masharti na kuiba au kutumia vibaya hivyo vitu?" Hapa ndipo patakapotofautisha chama hiki na CCM.

Kazi kwenu Wana-CHADEMA
 
Allien,

Najua Ndoto yako toka wiki ianze ni kuona wewe Muungano wa Vyama Vya siasa na hasa Vya Upinzani.

Na lengo lako has ni kuona kuna hatu kubwa ya maendeleo infikiwa katika Nchi hii,Unataka wananchi wapewe Maisha Bora bila ya kuyasotea.

Muungano wa Upinzani ni Muhimu sana na ulikuwapo sana miaka ya Nyuma ila siku zote ulikuwa ukivunjiaka baada ya chama kimoja kujiona kipo juu ya vyama vingine.

Mwaka 2000 Mrema alijiona yeye ndiyo baba wa vyama vyote hivyo TLP ilikuwa inastahili kupewa madaraka katika nchii hii na vyama vingine vya upinzani viunge mkono tu

2005 CHADEMA ilionekana ina Nguvu na kwa kutumia Viiongozi wa juu ambao walionehsa kuwa wao wanaweza kuliko Vyama vingine.

Ili ilisababisha vyama kama NCCR na CUF kuamua kujitoa katika Muungano ambao tayari ulishaasisiwa.

Tanzania inawezekana ila tatizo ni jambo Moja.Uroho wa Madaraka,Ubinafsi ambao umo miongoni mwa viongozi wa vyama vya Upinzani.

To make it clear ni kuwa Upinzani wa kwelli utaanza pale CCM itakapovunjika na kitokee Chama kingine..Inawezekana??
 
Last edited:
Allien,

Najua Ndoto yako toka wiki ianze ni kuona wewe Muungano wa Vyama Vya siasa na hasa Vya Upinzani.

Na lengo lako has ni kuona kuna hatu kubwa ya maendeleo infikiwa katika Nchi hii,Unataka wananchi wapewe Maisha Bora bila ya kuyasotea.

Muungano wa Upinzani ni Muhimu sana na ulikuwapo sana miaka ya Nyuma ila siku zote ulikuwa ukivunjiaka baada ya chama kimoja kujiona kipo juu ya vyama vingine.

Mwaka 2000 Mrema alijiona yeye ndiyo baba wa vyama vyote hivyo TLP ilikuwa inastahili kupewa madaraka katika nchii hii na vyama vingine vya upinzani viunge mkono tu

2005 CHADEMA ilionekana ina Nguvu na kwa kutumia Viiongozi wa juu ambao walionehsa kuwa wao wanaweza kuliko Vyama vingine.

Ili ilisababisha vyama kama NCCR na CUF kuamua kujitoa katika Muungano ambao tayari ulishaasisiwa.

Tanzania inawezekana ila tatizo ni jambo Moja.Uroho wa Madaraka,Ubinafsi ambao umo miongoni mwa viongozi wa vyama vya Upinzani.

To make it clear ni kuwa Upinzani wa kwelli utaanza pale CCM itakapovunjika na kitokee Chama kingine..Inawezekana??

Mzee wa masters, unaongea nini hebu tufafanulie sie vihiyo naona lugha yako ngumu sana
 
Allien,

Muungano wa Upinzani ni Muhimu sana na ulikuwapo sana miaka ya Nyuma ila siku zote ulikuwa ukivunjiaka baada ya chama kimoja kujiona kipo juu ya vyama vingine.

Tanzania inawezekana ila tatizo ni jambo Moja.Uroho wa Madaraka,Ubinafsi ambao umo miongoni mwa viongozi wa vyama vya Upinzani.

To make it clear ni kuwa Upinzani wa kwelli utaanza pale CCM itakapovunjika na kitokee Chama kingine..Inawezekana??

Mkuu Gembe;

Sitapumzika hadi kitu fulani cha Uhakika kitokee na pia napenda kuungana na maoni yako.

Kwa hiyo kazi tuliyonayo ni ya kuchuja hivyo vyma vyenye Uroho wa Madaraka na Ubinafsi. Ndiyo maana tunataka CHADEMA waje hapa tuwaweke kiti moto tuone kama wana hoja za kujibu.

Nimesha wa PM Mh. Zitto, Slaa, Mbowe, Mnyika waje Thread hii. Na naomba wanaoweza kuonana nao wawajulishe waje hapa kujibu hoja wakipata nafasi.
 
Wakuu,

Nimesha wa PM Wakulu wa CHADEMA ambao wako hapa JF waje kujibu hoja hapa.

Tunawasubiri . . .
 
Yap, tuwasubiri tusikie watasema nini.
Gembe, ni kweli vyama vya siasa ni vingi sana na vingi vinachemsha. Tatizo havina misingi imara na sheria kali na kuwa na watu wa kulinda sheria hizo zisivunjwe na watu kuanzia Mwenyekiti hadi wanachama wa kawaida. Wanaweka sheria ambazo wao itakuwa rahisi kuzikivunja na wasichukuliwe hatua yoyote. Kama hii kitu ikianza CHADEMA, basi itakuwa mwanzo mzuri sana kuitofautisha na vyama vingine hasa kilichoko madarakani.
Ona sasa hivi kwenye uchaguzi wa UWT. Wenyewe wanasema kabisa LIVE kuwa UFISADI umetawala uchaguzi. Hayo anayasema Anna Abdallah na anaambiwa mwenyekiti wa chama. Ila unashangaa hakuna hatua yoyote imechukuliwa katika wale walioshinda kwa gia hiyo. Hayo ni moja ya mambo yanayotakiwa kuthibitiwa.
Gembe, tofauti na NYANI anavyosema, kuwa MIAFRIKA NDIVYO TULIVYO, mie naona kidogo anakosea. Inatakiwa kusema "Binadamu ndiyo tulivyo". Ila wenzetu hujiwekea sheria kali kwao wote hadi viongozi na atakayevunja basi cha moto atakiona. Hii ikianzishwa katika chama chochote na kuwa inafuatwa, basi ujuwe maneno ya Nyerere tutawahi kidogo. Kunaweza kutokea upinzani mkali sana kwa CCM na hadi Mwalimu huko aliko atasema "I'm proud with my Childrens, they've proved me wrong...."
Zamani USA ilikuwa inajulikana kuwa ili ushinde inabidi upewe pesa na Matajiri au makampuni makubwa. Obama amekuja na njia mpya. Inawezekana CCM ina MAFISADI na pesa nyingi za EPA, Deepgreen, Meremeta, madini nk, ila kama una nia, unaweza kushinda ki-David Vs Goloati.
Bado nina OMBI la MWISHO kabla sijachukua kadi ya CHADEMA. Hii itahusu UONGOZI wa chama. Ila hili naliweka mwisho kabisa. Wakiniridhisha kwa hili, basi kweli ntanunua na kuchangia chama.
 
Unapozungumzia uongozi wa chadema usimsahau na Kitila ambaye naona yuko online hapa jamvini. Naye aje ajibu maswali!
 
Yebo yebo,
Ni swali lililokaa kama pendekezo. Wakikubali, tumo. Wakikataa sisi hatumo. Wakikubali na baadaye wakatae maoni yetu, pia sisi hatumo. Ni simple sana. Hii itakuwa ni TEST ya kwanza kwao kujua wanaweka mbele UTAMU wa madaraka au nchi yao kwanza.
 
Allien,

Najua Ndoto yako toka wiki ianze ni kuona wewe Muungano wa Vyama Vya siasa na hasa Vya Upinzani.

Na lengo lako has ni kuona kuna hatu kubwa ya maendeleo infikiwa katika Nchi hii,Unataka wananchi wapewe Maisha Bora bila ya kuyasotea.

Muungano wa Upinzani ni Muhimu sana na ulikuwapo sana miaka ya Nyuma ila siku zote ulikuwa ukivunjiaka baada ya chama kimoja kujiona kipo juu ya vyama vingine.

Mwaka 2000 Mrema alijiona yeye ndiyo baba wa vyama vyote hivyo TLP ilikuwa inastahili kupewa madaraka katika nchii hii na vyama vingine vya upinzani viunge mkono tu

2005 CHADEMA ilionekana ina Nguvu na kwa kutumia Viiongozi wa juu ambao walionehsa kuwa wao wanaweza kuliko Vyama vingine.

Ili ilisababisha vyama kama NCCR na CUF kuamua kujitoa katika Muungano ambao tayari ulishaasisiwa.

Tanzania inawezekana ila tatizo ni jambo Moja.Uroho wa Madaraka,Ubinafsi ambao umo miongoni mwa viongozi wa vyama vya Upinzani.

To make it clear ni kuwa Upinzani wa kwelli utaanza pale CCM itakapovunjika na kitokee Chama kingine..Inawezekana??


Huu ni upotoshaji uliovuka mipaka! Hakukuwa na ushirikiano mwaka 2005 kisha CHADEMA ikajitoa! Kulikuwa na majadiliano ila waliokuwa wanajiona chama kikubwa walikuwa ni CUF amabao walikuwa wanataka waachiwe kila kitu!

Lazima ikumbukwe kuwa mwaka 95 CHADEMA haikusimamisha mgombea wa Uraisi ili muunga mkono Mrema alie kuwa mgombea wa NCCR. Mwaka 2000 CHADEMA ilimuunga mkono Lipumba.

Kwa hiyo mpaka sasa chama ambacho kimedhihirisha dhahiri kuwa kina nia njema na kuwa tayari kuunga mkono wenzake ni CHADEMA Pekee!CUF, TLP NA NCCR ni lini wamemuunga mkono mgombea wa chama kingine katika nafasi ya uraisi? Hata hivyo kuunga mkono huku hakuleta manufaa kwa CHADEMA kutokana na ubinafsi wa vyama vilivyoungwa mkono.

Mwaka 2005 CHADEMA ilisimamisha mgombea wake wa uraisi, ili kuwa kama inajitambulisha kitaifa kuwa imeingia rasmi katika siasa za kitaifa na mapambano ya moja kwa moja! Jambo ambalo limeta hamasa na mvuto wa aine yake na kukisogeza CHADEMA kuelekea kuwa chama kikuu cha Upinzani nchini kabla ya kuchukua madaraka kamili mwaka 2015, ila mahesabu ya kikosewa wanaweza kuingia 2010 kabla ya mda wao! Mda utasema.

Tuitendee haki CHADEMA. Ndio pekee wamewahi kumuunga mkono wenzao, NCCR ilikuwa na nguvu mwaka 95 CHADEMA walikubali kuiunga mkono na ndivyo ilivyokuwa mwaka 2000 kwa CUF, Leo CHADEMA ina nguvu zaidi, CUF, NCCR na TLP waiunge mkono! Ni kivipi sasa tunasema CHADEMA ndio wana uroho wa madaraka?
 
Sidhani kama "maswali" mnayo..!!

Mkuu;

Kuna mambo kadhaa wa kadhaa ya kimsingi yanayohitaji mabadiliko kuhusu CHADEMA kama suala la Ubinafsi, Ukabila, Upendeleo, Ubadhirifu wa pesa nk. Tunataka CHADEMA waje hapa kama baadhi ya viongozi watakubali kuyaacha.

Pia kuwe na mfumo ambao hayo mambo hayata ruhusiwa kutokea . . . . Kuna maswali mengi ya kuwauliza. waje tu wasiogope. Waanze na post kuu hapo juu.
 
Huu ni upotoshaji uliovuka mipaka! Hakukuwa na ushirikiano mwaka 2005 kisha CHADEMA ikajitoa! Kulikuwa na majadiliano ila waliokuwa wanajiona chama kikubwa walikuwa ni CUF amabao walikuwa wanataka waachiwe kila kitu!

Lazima ikumbukwe kuwa mwaka 95 CHADEMA haikusimamisha mgombea wa Uraisi ili muunga mkono Mrema alie kuwa mgombea wa NCCR. Mwaka 2000 CHADEMA ilimuunga mkono Lipumba.

Kwa hiyo mpaka sasa chama ambacho kimedhihirisha dhahiri kuwa kina nia njema na kuwa tayari kuunga mkono wenzake ni CHADEMA Pekee!CUF, TLP NA NCCR ni lini wamemuunga mkono mgombea wa chama kingine katika nafasi ya uraisi? Hata hivyo kuunga mkono huku hakuleta manufaa kwa CHADEMA kutokana na ubinafsi wa vyama vilivyoungwa mkono.

Mwaka 2005 CHADEMA ilisimamisha mgombea wake wa uraisi, ili kuwa kama inajitambulisha kitaifa kuwa imeingia rasmi katika siasa za kitaifa na mapambano ya moja kwa moja! Jambo ambalo limeta hamasa na mvuto wa aine yake na kukisogeza CHADEMA kuelekea kuwa chama kikuu cha Upinzani nchini kabla ya kuchukua madaraka kamili mwaka 2015, ila mahesabu ya kikosewa wanaweza kuingia 2010 kabla ya mda wao! Mda utasema.

Tuitendee haki CHADEMA. Ndio pekee wamewahi kumuunga mkono wenzao, NCCR ilikuwa na nguvu mwaka 95 CHADEMA walikubali kuiunga mkono na ndivyo ilivyokuwa mwaka 2000 kwa CUF, Leo CHADEMA ina nguvu zaidi, CUF, NCCR na TLP waiunge mkono! Ni kivipi sasa tunasema CHADEMA ndio wana uroho wa madaraka?

Mkuu;

Asante sana kwa kutupa analysis ya huko nyuma, ingawa kama tukitaka kuwa realistic, CHADEMA bado nao wana mapungufu yao.

Hapa si mahali pa kulaumiana. Kinachoongelewa hapa ni kuwa, je CHADEMA wako tayari kujiunda upya na kwenda katika misingi inayotarajiwa na Wananchi wengi ili hatimaye ichukue Nchi?

Tunapenda kuona mapungufu yote yanafanyiwa kazi na kunakuwa na marekebisho makubwa katika mfumo wa Uongozi na Uwajibikaji ambao unatakiwa uvunje Umimi na matabaka yote ili kuleta maendeleo ya kweli.

Wakiwa Serious, kuna baadhi ya wana JF waliomo humu na wengine walio nje, watakubali kujiunga CHADEMA na kuleta msukumo wa Ki-OBAMA kufanya kweli.

Kama hawawezi tunatafuta chama kingine ambacho kitakuwa tayari. Kama hakuna, tutaunda chetu.

Ni hayo tu yanayotaka maelezo kwa kuanzia.
 
Ni kweli CHADEMA ni chama chenye muelekeo ila mapungufu bado yako. wakiweza kujipanga vizuri waweke ubinafsi pembeni wengi tunaweza shawishika kujiunga nao. Inatakiwa kuwe na mpinzani wa kweli wa CCM hadi sasa wapo ila hakuna mwenye dalili ya kuchukua nchi 2010, 2015 ni mbali mimi ningefurahi kwa kipindi kilichobaki 2010 tuone kuna uwezekano wa CCM kuwa mpinzani. vitu kama JF ni moja ya changamoto kubwa kwa watu wa mijini ila ibuniwe aina kama hii kwa watu ambao mtandao hawapati.

asante kwa mada nzuri
 
Nimewasoma, mengi ni maoni mazuri yanayostahili kufanyiwa kazi na mengi tayari yameshafanyiwa kazi.
 
Nimewasoma, mengi ni maoni mazuri yanayostahili kufanyiwa kazi na mengi tayari yameshafanyiwa kazi.

Mkuu Kitila;

Kwanza tunashukuru kwa kuitikia wito wa kutembelea thread hii. Ingawa naona umejibu kwa haraka haraka na kuacha maswali ya msingi yaliyoulizwa na wadau katika post zao.

Kwanza, CHADEMA wako tayari kupokea Wanamapinduzi kutoka JF na kwingineko ambao wataleta changamoto ya kweli?

Je, mko tayari kufanya marekebisho ya kiuongozi na mfumo wa uongozi kukidhi Demokrasia ya kweli kivitendo katika uendeshaji wa chama?

Je, kwa wale watu makini na ambao ni rasilimali ya Taifa wakija CHADEMA je, viongozi wa sasa wako tayari kutoa nafasi za uongozi kwa wadau hawa?

Maswali haya na mengine katika post yanatakiwa yajibiwe. Tutayapima majibu yako kwa hiyo ni vema majibu yakiwa detailed with facts.
 
Mkuu Allien,

FYI
Hebu jaribu kubofya hapo chini, kuna nasaha, na majibu mengi tu kuhusu CHADEMA mafikirio yangu yatakusaidia...

'Focus 2010'-'The Road towards 2010 Elections'-'Chadema Must Reform'

Kama sijakosea hizo hapo juu ziliunganishwa.



Hili hapa chini lilikuwa swali mojawapo kwa JJ kutoka kwa Rev. Kishoka...

Hapa si mahali pa kulaumiana. Kinachoongelewa hapa ni kuwa, je CHADEMA wako tayari kujiunda upya na kwenda katika misingi inayotarajiwa na Wananchi wengi ili hatimaye ichukue Nchi?


Na kuhusu hapo juu, ninamnukuu JJ akimjibu Rev. Kishoka...


Rev. Kishoka

Samahani kwa kukuelewa vivyo sivyo.

Hayo mengine nimekupata, tuendelee kuyajadili kule kwenye "CHADEMA must reform"

Mtanzania wa kawaida anachojua tu ni kwamba waCHADEMA wanapinga ufisadi na kutetea rasilimali za Taifa; wanachojua ni Mbowe wa Helikopta anayekemea rushwa ya CCM kwa kuwaapiza, Zitto Kabwe aliyefukuzwa Bungeni kwa sababu ya Dili la Karamagi la Buzwagi, Dr Slaa ambaye ameshika pabaya Balali kwenye BOT na Tundu Lissu ambaye ameshirikiana na Slaa kutaja orodha ya mafisadi. Hizo ndio stori za vijiweni! Ukiwauliza kuhusu falsafa na itikadi hawayajui mambo hayo, changamoto ni CHADEMA kuweza kueleza zaidi sera zake mpaka watanzania wajue kwamba ni chama cha itikadi ya mrengo wa kati chini ya falsafa ya "Nguvu ya Umma", taratibu tutafika. Hatua ya kwanza ambayo tumeanza nayo ni kutoa mafunzo kwa viongozi wetu ngazi za chini, taratibu tutafika. Safari ya maili mia huanzia na moja!

Elimu ya bure tunayoipata hapa inapenya katika akili zetu na tunaitoa tunapokaa katika vikao vya chama ama vya ushirikiano wa vyama ama tunapoandaa rasimu ya nyaraka mbalimbali za kutoa mwelekeo. Tunaitumia pia tunavyopanda jukwaani kuhutubia wananchi ikiwemo huko vijijini. Kwa hiyo, chukulia kila unachoandika hapa kinasadia katika kujenga demokrasia na maendeleo nchini. Sisi ni watumishi na wawakilishi, vyama vya siasa ni taasisi za umma!

CHADEMA ina kurugenzi mbalimbali ambazo zinawataalamu wa fani mbalimbali, lakini hawa pekee hawawezi kutosha kusambaa maeneo mbalimbali nchini. Tunahitaji wataalamu mbalimbali, hata kama wanakazi zao huo mawilayani ama kwenye taasisi mbalimbali watenge japo siku moja kwa mwezi huko walipo kujitolea utaalamu wao kwa ajili ya kusaidia mikakati ya kuleta demokrasia na maendeleo nchini. Vinginevyo, usomi wao utakuwa ni wa kibinafsi kama yule aliyechangiwa chakula chote kijijini avuke jangwa akalete chakula kwa waliobaki wenye njaa, huyo asiporudi ni msaliti! Kadhalika, wasomi wetu wakishindwa kuchukua japo muda mchache kukumbuka wajibu wao kwa wasiosoma na taifa kwa ujumla, nao ni wasaliti. Kama tunaweza kukaa kwenye pub masaa kadhaa tukipiga soga, tujue kuwa tunaweza kabisa kuwa na muda kwa ajili ya hii noble course tukitaka.

Wapinzani wanafanya nini kuchukua tuzo za siasa na ujamaa na kujitegemea? Tunafanya. Mimi na Profesa Baregu tulikuwa kwenye kamati ya kufanya mapitio ya itikadi ya CHADEMA kutenganisha bayana itikadi na falsafa ya CHADEMA katika muktadha wa malengo, sera za CHADEMA na mwelekeo wa Taifa kwa ujumla. Hatimaye katiba ikafanyiwa mabadiliko 2006- nimeweka kwenye "CHADEMA must reform" nakala ya Katiba ya CHADEMA- ukisoma 'itikadi ya CHADEMA ya mrengo wa kati" na falsafa ya CHADEMA ya "Nguvu ya umma" utaona kwamba imechota baadhi ya tunu za Ujamaa na kujitegemea ikachanganya na baadhi ya manufaa ya ubepari. Mchanyato uliopatikana utawezesha CHADEMA ikichukua dola- kuendesha nchi bila dola kuhodhi nyanja zote, lakini kuhakikisha pia uchumi unamilikiwa na wananchi waliowengi na si uchumi unaomilikiwa na kunufaisha kwa kiasi kikubwa tabaka la watu wachache ama wawekezaji kutoka nje chini ya ubepari wa kimataifa wa ukoloni mamboleo.

JJ

Matarajio yangu ni kuwa hili litakufungulia wigo.

Aksante
 
Kwanza tunashukuru kwa kuitikia wito wa kutembelea thread hii. Ingawa naona umejibu kwa haraka haraka na kuacha maswali ya msingi yaliyoulizwa na wadau katika post zao.

Kwanza, CHADEMA wako tayari kupokea Wanamapinduzi kutoka JF na kwingineko ambao wataleta changamoto ya kweli?

Je, mko tayari kufanya marekebisho ya kiuongozi na mfumo wa uongozi kukidhi Demokrasia ya kweli kivitendo katika uendeshaji wa chama?

Je, kwa wale watu makini na ambao ni rasilimali ya Taifa wakija CHADEMA je, viongozi wa sasa wako tayari kutoa nafasi za uongozi kwa wadau hawa?

Maswali haya na mengine katika post yanatakiwa yajibiwe. Tutayapima majibu yako kwa hiyo ni vema majibu yakiwa detailed with facts.

He, hapa kweli naona unatoka Sayari ya MBALI.
Haya maswali yako unategemea watu wakujibu ndio au wakujibu hapana?

Ninachoamini ni kuwa vyama vyote vya siasa vinahitaji wanachama waaminifu na wenye nia thabiti kufikia malengo chama kiliojiwekea.

Naamini kuna taratibu na sheria za kuendesha chama ikiwa ni pamoja na kupata viongozi wake. Naamini nawe unafahamu kuwa viongozi wote waliopo ndani ya chadema sio walionza, ila hawa ni wa awamu ya 3 kama sikosei. Swali, ni je walipatikana kwa mtindo unaooujadili wewe au ni kwa kufuata katika ya chama?

Unataka, leo ukijiunga upewe uenyekiti, ukatibu, ukurugenzi hapo hapo? ipo wapi nafasi ya kupimwa na kuujua uzalendo wako? Je watajuaje kuwa sio miongoni mwa waliotumwa kukiangamiza chama chao?

Jiweke kwenye nafasi yao halafu ujaribu kujibu maswali yako.

#NB. HUU NI MTIZAMO WANGU NA WALA HAUHUSIANI NA CHADEMA, NA WALA MIE SIO MWANACHAMA.
 
Mkuu Allien,

FYI
Hebu jaribu kubofya hapo chini, kuna nasaha, na majibu mengi tu kuhusu CHADEMA mafikirio yangu yatakusaidia...

'Focus 2010'-'The Road towards 2010 Elections'-'Chadema Must Reform'

Kama sijakosea hizo hapo juu ziliunganishwa.



Hili hapa chini lilikuwa swali mojawapo kwa JJ kutoka kwa Rev. Kishoka...




Na kuhusu hapo juu, ninamnukuu JJ akimjibu Rev. Kishoka...




Matarajio yangu ni kuwa hili litakufungulia wigo.

Aksante

Ndugu yangu Sura ya Kwanza;

Mimi mgogoro wangu mkubwa na hivi vyama si kwenye Sera au falfasa ya vyama. Ukisoma hata Katiba na falfasa za CCM au TLP kama kuna mapungufu ni machache sana. Wote wanadai kuwaletea maendeleo Wananchi kama wakishika hatamu . . .

Do I need to explain what is happening at CCM, or CHADEMA or TLP nk now?

Mgogoro uliopo kwa sasa ni Viongozi kijifanyia yale wanayotaka wao. Hawana Utashi wa kweli na wamejawa na Ubinafsi, n.k. Mambo haya mabaya yanafuta uzuri wa aina yoyote wa Kisera au falfasa . . . .

People Power . . . Kasi Mpya Nguvu Mpya n.k. vyote hivyo ni hadithi. Tunachosema ni kuwa CHADEMA wanaweza kuwa na nafasi nzuri kama uongozi utakuwa adilifu . . . na hicho ndo tunataka watuambie kama kweli wako tayari kwa reforms. Wameshaanza kujijengea sifa kwa mambo fulani fulani . . . Lakini je, hiyo yatosha kuwapa dhamana ya kuongoza nchi?
 
He, hapa kweli naona unatoka Sayari ya MBALI.
Haya maswali yako unategemea watu wakujibu ndio au wakujibu hapana?

Ninachoamini ni kuwa vyama vyote vya siasa vinahitaji wanachama waaminifu na wenye nia thabiti kufikia malengo chama kiliojiwekea.

Naamini kuna taratibu na sheria za kuendesha chama ikiwa ni pamoja na kupata viongozi wake. Naamini nawe unafahamu kuwa viongozi wote waliopo ndani ya chadema sio walionza, ila hawa ni wa awamu ya 3 kama sikosei. Swali, ni je walipatikana kwa mtindo unaooujadili wewe au ni kwa kufuata katika ya chama?

Unataka, leo ukijiunga upewe uenyekiti, ukatibu, ukurugenzi hapo hapo? ipo wapi nafasi ya kupimwa na kuujua uzalendo wako? Je watajuaje kuwa sio miongoni mwa waliotumwa kukiangamiza chama chao?

Jiweke kwenye nafasi yao halafu ujaribu kujibu maswali yako.

#NB. HUU NI MTIZAMO WANGU NA WALA HAUHUSIANI NA CHADEMA, NA WALA MIE SIO MWANACHAMA.

Mkuu Nono;

Nadhani kiini cha hoja ya msingi bado hujakielewa . . .

Shida si kwa Watu Makini na uwezo mkubwa kujiunga CHADEMA na kupewa Uongozi. Shida ni viongozi wa namna gani wanatakiwa na je ni Waadilifu kiasi cha kuvuta Umma wa Tanzania kuwatambua kuwa wako serious?

Concept ya Watu Makini kuachiwa uongozi si suala jipya na limefanya kazi sana katika Historia ya Mabadiliko ingawa si wote wamefanikiwa kuleta mabadiliko ya kweli. Nyerere alifanya hivyo, CCM wao wana utaratibu wa Kung'atuka na hata kuchukua watu wanaohama Upinzani na kuwapa madaraka, Oliver Tambo alimwachia Nelson Mandela, Mabere Marando alimwachia Mzee wa Kilalacha n.k.

This issue if you look into the positive side, you will understand what I mean. Baadhi ya viongozi wa CHADEMA ambao ndiyo wenye nafasi kubwa ya kuleta Tranformation wamekuwa questioned sana juu ya uadilifu wao, matumizi mabaya ya pesa, upendeleo, na hata kwa baadhi ya maamuzi . . .

For sure these are not about constitution or about election procedures, it is about leadership. Wakati CCM wanaendelea kukumbatia Rushwa na hata Ufisadi, Makundi nk katika Chaguzi zao i.e UVCCM, UWT nk. CHADEMA inatakiwa ijisafishe . . .

Yote hayo kwa Ujumla wake ndiyo yanatakiwa yafanyiwe kazi. Na tunataka commitment yao . . . .
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom